Kumekucha TTCL wateja sasa bwerere!

Kumekucha TTCL wateja sasa bwerere!

mtumishi wa umma asietumia line ya TTCL afukuzwe kazi, serikali haiwezi kukupa mshahara mtumishi wa umma, halafu unaenda kununua vocha ya tigo au vodacon, huko ni kukosa uzalendo!
Vocha za TTCL hazipo kila mahali.
Naona hujielewi kununua vocha ya TtCL unahitaji kuwa na Tigo pesa yako au mpesa!!!! Vocha za Tigo na vodacom haiepukiki
 
Wewe ni sehemu ya TTCL,usijione kama uko mbali sana na TTCL.Kumbuka kwamba ukii-support TTCL unaisaidia serikali kupata fedha kupitia gawio,na hivyo indirectly unaisaidia serikali kukulipa wewe mshahara.Usione kama TTCL iko mbali sana na wewe no.Jitafakari.
TTCL wababaishaji vocha jiji tu la dar es salaam kupata shida.
 
Ok TTCL hapo wana changamoto ya kuhakikisha vocha zao zinapatikana Hadi kwa shemeji yangu nyasa vijijini waliko mabwana shamba na mabibi shamba na watendaji wa vijiji na kata na walimu wa shule za msingi za porini waajiriwa wa serikali.Vocha za TTCL Ni changamoto.
Siku hz watu hatununui vocha..tunanunua kwa tigopesa , mpesa, aitel money, simbanking n.k
 
Haina shida TTCL imejiandaaje kupeleka vocha zake za muda wa maongezi kwa walimu wa shule za msingi mfano walioko maporini vijijini ambako hawajafika na hawana wakala.Vocha za TTCL dar es salaam tu ukitoka nje ya mji kuzipata shida.Haina tatizo wamefunguliwa soko je wamejiandaa kulimudu? Kwa usambazaji vocha na usajiri wa line hasa maeneo remote vijijini kuliko na wafanyakazi wa serikali?

Taasisi zote za umma huwa zina ufanisi duni. Tena hao TTCL ndio wako vizuri ukilinganisha na taasisi nyingine za umma.
 
Kama TTCL wako serious hizo line watoe bure na wawekeze Kwa vijana wa vyuo kwa kuwapa muda wa hewani na bundle kuanzia saa 4 usiku mpaka saa 2 asubuhi.
 
Siku hz watu hatununui vocha..tunanunua kwa tigopesa , mpesa, aitel money, simbanking n.k
Kwa mtandao husika . Mfano tigo pesa iko Kila kona ya nchi.Nikitaka vocha nina uhuru nikitaka ya kukwangua napata .Nikitaka ya kununua tigopesa naweka pesa mfano elfu Moja kwa wakawa wa tigo pesa nanunua vocha ya elfu Moja exactly.Tuje upande wa TTCL vocha zao kupata shida , TTCL pesa shida sehemu nyingi za nchi hazipo kabisa ikiwemo Dar es salaam.Unachoongea wewe unakijua mwenyewe .Hiyo TTCL vocha ukinunua kwa kutumia tigopesa,mpesa,airtel money,simbanking kuna extra charge unayochajiwa kama service fee . Wakati nikinunua mfano nina line ya Tigo nikinunua vocha ya kampuni yao ya Tigo sichajiwi extra charge ya service fee.Hivi kwa akili yako unategemea Mimi mitume mtandao wa TTCL unaoniongezea gharama kwa matumizi ya simu kwa hizo extra charges Kila ninunuapo vocha? Mitaani wengi hawatumii TTCL line si kwa sababu hawaitaki bali vocha hamna na hizo TTCL pesa hamna!!!!! TTCL kiukweli biashara ya simu za mkononi wako zero sio siri.
 
HIVI: WATUMISHI WANGAPI WA VODA, TIGO AU HALOTEL WANAOPEWA VOCHA ZA SIMU NA MWAJRI WAO HALAFU HIZO VOCHA ZIKATOKEA KUWA ZA KAMPUNI NYINGINE??
 
Kwa mtandao husika . Mfano tigo pesa iko Kila kona ya nchi.Nikitaka vocha nina uhuru nikitaka ya kukwangua napata .Nikitaka ya kununua tigopesa naweka pesa mfano elfu Moja kwa wakawa wa tigo pesa nanunua vocha ya elfu Moja exactly.Tuje upande wa TTCL vocha zao kupata shida , TTCL pesa shida sehemu nyingi za nchi hazipo kabisa ikiwemo Dar es salaam.Unachoongea wewe unakijua mwenyewe .Hiyo TTCL vocha ukinunua kwa kutumia tigopesa,mpesa,airtel money,simbanking kuna extra charge unayochajiwa kama service fee . Wakati nikinunua mfano nina line ya Tigo nikinunua vocha ya kampuni yao ya Tigo sichajiwi extra charge ya service fee.Hivi kwa akili yako unategemea Mimi mitume mtandao wa TTCL unaoniongezea gharama kwa matumizi ya simu kwa hizo extra charges Kila ninunuapo vocha? Mitaani wengi hawatumii TTCL line si kwa sababu hawaitaki bali vocha hamna na hizo TTCL pesa hamna!!!!! TTCL kiukweli biashara ya simu za mkononi wako zero sio siri.
Ngoja nikupe siri.unaweza nunua aitime ya ttcl kwa kutumia tigopesa, mpesa ata airtel money mjomba. Vile vile unaweza nunua airtime ya tigo kupitia mpesa charges utakayotozwa ni sawa tu naungenunua hyo aitime ya mtandao husika. Siku hizi maisha si magumu
 
Ngoja nikupe siri.unaweza nunua aitime ya ttcl kwa kutumia tigopesa, mpesa ata airtel money mjomba. Vile vile unaweza nunua airtime ya tigo kupitia mpesa. Siku hizi maisha si magumu
Kuna extra charges unachajiwa na hizo kampuni ukinunua vocha kwa njia hiyo kama hujui . TTCL waache ubabaishaji.
 
Kwa nini Mfanyakazi wa TiGo kuwa na line ya tiGo, Vodacom kuwa na laini ya Vodacom, AirTel kuwa na line ya Airtele , Zantel kuwa na line ya Zantel (mwajiri) , nk siyo issue, ila Mfanya kazi wa Serikali kuwa na line ya mwajiri (Shirika la Mawasiliano la Taifa (TTCL) inaonekana ni issue?! Naomba kujua.
Wafanyakazi wa hizo kampuni za simu za Tigo,vodacom,nk uliowataja hupewa vocha na kampuni zao kama marupurupu au posho.Kila mfanyakazi huwekewa vocha kwenye simu Kila mwezi ndio maana Kila mfanyakazi wa hizo kampuni ana line ya kampuni yake.
 
Ok TTCL hapo wana changamoto ya kuhakikisha vocha zao zinapatikana Hadi kwa shemeji yangu nyasa vijijini waliko mabwana shamba na mabibi shamba na watendaji wa vijiji na kata na walimu wa shule za msingi za porini waajiriwa wa serikali.Vocha za TTCL Ni changamoto.
Kweli,vocha za Ttcl mikoani ni za kutafuta kwa tochi
 
Asante kwa kutambua kuwa elimu yangu haijanisaidia.

TTCL wakiwa wabunifu na huduma zikiwaridhisha watu, wateja watakuja tu bila kutumia nguvu na kejeli kama hizi.

Madhara ya kutegemea watumishi wa umma ni shirika kubweteka then kushindwa ktk soko.

Ukiamua kufanya biashara, fanya biashara. Usitafute huruma za wazalendo.

Niliwahi kuwa na TTCL line nikaitupa kule. Hela yangu halafu nipate shida ya huduma kisa nini?
Laiti ungejua biashara kijana.Mafinikio katika biashara yanategea mambo mengi ikiwa ni pamoja na mtaji,uwezo wa ku-attract customers,lakini pia friends,ndugu na wengine walio tayari kuku-support kwa sababu moja au nyingine.Tunayo base kubwa ya wafanyakazi,"the others," base ambayo nayo eventualy ita-benefit moja kwa moja through the TTCL investiment.I had thought that this base,would be willing to support TTCL without being forced to do it,because the investment is theirs,unfortunately that is not the case.Why?To me it seems their is silent resistance on the part of the civil service because of the various steps taken to streamline it.But remember,that was necessary,the previous system was just unsustainable.It is however important to realize that these steps are not isolated to Tanzania only,several countries do it.
 
Mkuu Kilatha asante kwa mchango wako.
Ni kweli lazima kufanya mikakati ya masoko, lakini tusisahau pia TTCL iliwahi kuhujumiwa sana huko nyuma na mashirika haya , ikiwemo kutumiwa kwa miundombinu yake kuinua kampuni hizi, kunyimwa vibali nk enzi zile za ufisadi , hivyo ipo haja kuwasaidia kuinuka, lakini na wao LZIMA WA STRUGLE KISAYANSI KUSIMAMA KWA MIGUU YAO. TTCL ikipata faida inabaki na kusaidia ndani ya Nchi yetu, je wengine wakipata faida zainaenda wapi?!
Kuna namna mbili za kumsaidia mtu

Mpe msaada wa mahitaji yake kila siku kama vile mlemavu, siku ukiondoka na yeye arudi kwenye hali yake ya shida

Au muwezeshe kwa mbinu kusudi ajitegemee kwa muda mrefu ata usipokuwepo bado atazimudu changamoto

Magufuli ataiongoza Tanzania kwa miaka kumi, hata kama mtu alikuwa si shabiki wa ndege zipo na zishanunuliwa busara ni kuona wanapata faida, same applies to TTCL anayotaka kuiewezesha na yenyewe aliikuta na ataondoka ataicha.

Raisi anaweza fanya anavyoweza kwa jitihada zake kuyasaidia mashirika ya umma lakini kama yenyewe hayana mbinu za biashara akitoka hali yao itarudi kuwa vile vile.

Kama watanzania tunataka kuona haya mashirika yanapata faida na wanakuwa washindani sokoni bila ya Magu ni lazima wawe wabunifu kama washidani wao walivyo.

Wenzao wanaelewa mafanikio kwenye soko la ushindani ni kujua gap ilipo ya wateja, kuelewa consumer expectations kwenye huduma zao, kuzindua huduma kutokana na ushahidi, kushindana kwa value na wengine na kutoa huduma yenye kiwango.

Ngoja nikupe mfano miaka mitatu/minne nyuma kupitia humu humu JF Halotel ilivyofunguliwa walikuja na clever entry strategy na ilikuwa kila ukifungua kule jukwaa la habari kuna thread halotel mkombozi sijui bei zake nafuu, hatolel sijui package fulani ni bora kushinda Voda in short habari ya mjini ilikuwa Halotel. Aikuchukua muda thread zikaanza kubadilika hawa Halotel wameanza kuwa wezi etc with malalamiko ya watanzania.

Plan hapo ilikuwa ni kuvutia wateja kwanza walipopata wa kutosha taratibu wakawarudisha kwenye uhalisia wa gharama za kuzalisha huduma na kuanza kutoza kwa bei za uhalisia kwa kuzingatia value competition leo wanawateja 10 million wakati TTCL ina laki tano.

Point yangu ni kwamba haya mashirika ya serikari hawana jitihada za kupata wateja na awajali kuona washindani wao wanafanya nini kusudi watengeneze competitive edge sokoni.

Matokeo yake results zao ni mbovu wote, sasa awawezi endelea na kuwa watoa gawio wazuri mbeleni kwa kupewa kila kitu. Magu akitoka na wao wanarudi kule kule ni bora kuwapa ukweli kama tunataka kuona wanakuwa na sustainable businesses sio kuendelea kuona wanalelewa vibaya na mlezi aliepo wanakuwa kama spoilt brats who cant fend for themselves wote iwe Posta, TTCL, ATCL, TANAPA. Airport Authorities, Bandari etc wote ni below the capacity of their potential na hawana pressure kwa sababu sisi wenyewe atutoi kasoro zao.
 
mtumishi wa umma asietumia line ya TTCL afukuzwe kazi, serikali haiwezi kukupa mshahara mtumishi wa umma, halafu unaenda kununua vocha ya tigo au vodacon, huko ni kukosa uzalendo!
Naomba pia kupata ukweli je ukiwa Vodacom, tIGO, AIrtel, Zantel,Halotel etc je unayo hiari ya kutumia mtandao wao au ni LAZIMA?!
 
Wafanyakazi wa hizo kampuni za simu za Tigo,vodacom,nk uliowataja hupewa vocha na kampuni zao kama marupurupu au posho.Kila mfanyakazi huwekewa vocha kwenye simu Kila mwezi ndio maana Kila mfanyakazi wa hizo kampuni ana line ya kampuni yake.
Ok, Nashukuru kwa taarifa hizo. Napenda pia kujua kutumia mtandoa wa mwajiri ni LAZIMA au HIARI?!
 
Ok, Nashukuru kwa taarifa hizo. Napenda pia kujua kutumia mtandoa wa mwajiri ni LAZIMA au HIARI?!
Kampuni za simu hazilazimishi wafanyakazi wao kutumia simu za kampuni zao ila mfanyakazi haoni umuhimu wa kutotumia simu ya kampuni yake wakati kuna kujaziwa vocha kibao bure.Anaona ni ujinga kwa nini.akanunue vocha za mitandao mingine wakati za kampuni yake anapata bure.Hawalazimishi.
 
Back
Top Bottom