Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuna habari kuwa kuna wabunge wanajiandaa kuihama CCM kwa mkupuo wa pamoja au mmoja mmoja ,kitu ambacho kipo kwenye mashauriano.
Habari zimezidi kutonya kuwa wabunge hao ambao wameamua kulinda maslahi na malengo yaliowapeleka hapo Bungeni badala ya kukaa na kuwalinda watu wasio kuwa na uchungu wa Inchi hii ,wana imani kubwa kuwa WaTanzania walio wengi watawaunga mkono katika kitendo hicho ambacho wamekiita ni cha Kishujaa na utii kwa wananchi na pia wana imani kuwa wananchi waliowachagua kuwapeleka Bungeni watawachagua tena hata wakiwa ni wagombeaq binafsi kwa vile msimamo wao ni kulinda maslahi ya wananchi na kutowaonea haya wezi wa fedha ya Nchi hii na mali zake.
Wabunge hao wamezidi kuipa msonyo CCM kuwa ni Chama kinachoendeshwa kidikiteta na zaidi wengine kujiona wao ni wa Mjini na wanaweza kufanya lolote bila ya huruma kwa wananchi,na kuwafanya wabunge wawe na hali ngumu kurudi kuomba kura tena pale ufikapo msimu wa harakati za kujinadi ili wachaguliwe tena.
Wakizidi kutoa mchapo kuwa CCM kumejaa vigogo ambao wanatumia fedha nyingi kwa kulinda maslahi binafsi na kusahau kama wao wapo hapo kwa ajili ya maslahi ya Taifa na wananchi wake ,ndio ukaona jinsi wanavyoiba fedha ya umma bila ya huruma ..mmoja wao aliongezea.
Wabunge hao ambao wengi wao huwa wanaonekana wakimya ndani ya bunge wamezidi kutonya kuwa safari hii CCM magome watafahamu kuwa mizizi ndio muhimu kwa mti.

Tuna muomba Mungu muweza yote, hata kama hizi ni tetesi ziwaingie na kuwasuka suka, wakumbuke wajibu wao na waweze kutenda hivo kwa ajili ya kuinusuru nchi yetu Tanzania iliyo tekwa na mafisadi.
 
Nani kakuambia haya Mkuu? ama ndiyo hadithi za arinacha? pale ccm hawabanduki, labda kuna kamuuhujiza katendeke
 
What we all need sio wao wahame tu wahame na wawe mstari wa mbele kutetea maslahi ya nchi hii. Watu wanahitaji kuamka kutoka usingizini na wajue kwamba wakati wa mabadiliko umefika and there is nothing they can do about it.
 
Nani kakuambia haya Mkuu? ama ndiyo hadithi za arinacha? pale ccm hawabanduki, labda kuna kamuuhujiza katendeke

Stage tuliyofika sasa miujiza inaweza kutokea, watu wameumia sana na sidhani kama Mungu hajasikia vilio vya wana wake wa Tz.
 
Bado hawajachelewa,ila wasisubiri hukumu ya waTz itakapo anza kumla mmoja baada ya mwingine.

Vipi mafisadi nao wakihamia huko wanakohamia hawa wabunge?
 
Bado hawajachelewa,ila wasisubiri hukumu ya waTz itakapo anza kumla mmoja baada ya mwingine.

Vipi mafisadi nao wakihamia huko wanakohamia hawa wabunge?

Waliofuatwa na Mafisadi wahame tena!
 
Kuna habari kuwa kuna wabunge wanajiandaa kuihama CCM kwa mkupuo wa pamoja au mmoja mmoja ,kitu ambacho kipo kwenye mashauriano.
Habari zimezidi kutonya kuwa wabunge hao ambao wameamua kulinda maslahi na malengo yaliowapeleka hapo Bungeni badala ya kukaa na kuwalinda watu wasio kuwa na uchungu wa Inchi hii ,wana imani kubwa kuwa WaTanzania walio wengi watawaunga mkono katika kitendo hicho ambacho wamekiita ni cha Kishujaa na utii kwa wananchi na pia wana imani kuwa wananchi waliowachagua kuwapeleka Bungeni watawachagua tena hata wakiwa ni wagombeaq binafsi kwa vile msimamo wao ni kulinda maslahi ya wananchi na kutowaonea haya wezi wa fedha ya Nchi hii na mali zake.
Wabunge hao wamezidi kuipa msonyo CCM kuwa ni Chama kinachoendeshwa kidikiteta na zaidi wengine kujiona wao ni wa Mjini na wanaweza kufanya lolote bila ya huruma kwa wananchi,na kuwafanya wabunge wawe na hali ngumu kurudi kuomba kura tena pale ufikapo msimu wa harakati za kujinadi ili wachaguliwe tena.
Wakizidi kutoa mchapo kuwa CCM kumejaa vigogo ambao wanatumia fedha nyingi kwa kulinda maslahi binafsi na kusahau kama wao wapo hapo kwa ajili ya maslahi ya Taifa na wananchi wake ,ndio ukaona jinsi wanavyoiba fedha ya umma bila ya huruma ..mmoja wao aliongezea.
Wabunge hao ambao wengi wao huwa wanaonekana wakimya ndani ya bunge wamezidi kutonya kuwa safari hii CCM magome watafahamu kuwa mizizi ndio muhimu kwa mti.

Wabunge wa CCM hawana ujasiri huo, sahau hilo labda mpaka baada ya kuvunjwa bunge.

Hat hao wanaopiga kelele ukienda kuwachunguza mpaka chini unagundual deals mbovu kibao. Ila kwasisi wananchi kwasasa furaha yetu ni hiyo vita vya panzi, furaha ya kunguru. Kadri wanavyogombana na kuumbuana ndivyo tunavyozidi kujua ukweli juu ya hawa viongozi wetu. Nchi ina majambazi badala ya viongozi.
 
Namkubuka sana Julius K.Nyerere...angelikuwepo najuaa Chama kingepasuka ili kuleta ushindani zaidi....nazidi kuona utabiri wake...RIP JKN...
 
Sitashangaa kama watafanya hivyo wakiongozwa na Anna Kilango.

Ukikaa karibu na ua ridi utanukia ua ridi, vivyo hivyo ukikaa karibu na uvundo huwezi kunukia marashi asilani.Watimke wakaungane na wazalendo wa kweli wana wa nchi hii
 
Sitashangaa kama watafanya hivyo wakiongozwa na Anna Kilango.

Ukikaa karibu na ua ridi utanukia ua ridi, vivyo hivyo ukikaa karibu na uvundo huwezi kunukia marashi asilani.Watimke wakaungane na wazalendo wa kweli wana wa nchi hii

KWA HIYO MBUNGE AKIWA STRONG HAFAI CCM....?
KILANGO KAA HAPO HAPO PIGA KAZI....!
WANAOHAMA CCM NI WALE WALIOISHIWA....! (mtei,mapalala,sharif hamad)
WANAOHAMIA CCM NI STRONG...........!
(japo kuna strong ambao bado hawajahamia....SLAA, NDESA)
I SUBMIT
 
ushauri wangu kuwa wasihame, bali waipiganie haki hapo hapo kwenye ccm. kufanya hivyo kutampatia ushindi zaidi mwananchi kuliko kwa kujiengua chama.
 
Whatever the case will b, we need strong leader,upright and focused for betterment of this country.
To quit sometimes is not an answer,why dont stay there costly,courageous while exchanging blows and mash dodgy member within?
I dont think if they failed while inside that they will accomplish it when outside rather than deceitful speeches to b made.
 
mkuu la umeme limeisha sasa umekuja na hili.

yale yale ya kunudihana tumbaku.


mtegemea mkono ukatike ni fisi binaadam anajua hio ni ya guju.
 
Yes they are there but kama wataweza basi itakuwa poa kwani taifa hili linazamishwa na mafisadi waliojiwekea kichaka kule CCM na kudai kuwa ni watetezi wa wakulima na wafanyakazi
 
Sitashangaa kama watafanya hivyo wakiongozwa na Anna Kilango.

Ukikaa karibu na ua ridi utanukia ua ridi, vivyo hivyo ukikaa karibu na uvundo huwezi kunukia marashi asilani.Watimke wakaungane na wazalendo wa kweli wana wa nchi hii


annakilango.jpg



unakusudia huyu?
never mkuu hizo ni njozi za wale ambao daima huota bila ya kufumba macho
 
Watende walivyo nena....Tunawaomba waje upinzani kwa nguvu mpya.
 
Isije Ikawa Mafisadi Ndo Wanataka Kuhama, Baada Ya Kuhisi Moto Wa Epa Hautawaacha, Wasubiri Hukumu Zao Huko Huko Ccm
 
Kuna habari kuwa kuna wabunge wanajiandaa kuihama CCM kwa mkupuo wa pamoja au mmoja mmoja ,kitu ambacho kipo kwenye mashauriano.
Habari zimezidi kutonya kuwa wabunge hao ambao wameamua kulinda maslahi na malengo yaliowapeleka hapo Bungeni badala ya kukaa na kuwalinda watu wasio kuwa na uchungu wa Inchi hii ,wana imani kubwa kuwa WaTanzania walio wengi watawaunga mkono katika kitendo hicho ambacho wamekiita ni cha Kishujaa na utii kwa wananchi na pia wana imani kuwa wananchi waliowachagua kuwapeleka Bungeni watawachagua tena hata wakiwa ni wagombeaq binafsi kwa vile msimamo wao ni kulinda maslahi ya wananchi na kutowaonea haya wezi wa fedha ya Nchi hii na mali zake.
Wabunge hao wamezidi kuipa msonyo CCM kuwa ni Chama kinachoendeshwa kidikiteta na zaidi wengine kujiona wao ni wa Mjini na wanaweza kufanya lolote bila ya huruma kwa wananchi,na kuwafanya wabunge wawe na hali ngumu kurudi kuomba kura tena pale ufikapo msimu wa harakati za kujinadi ili wachaguliwe tena.
Wakizidi kutoa mchapo kuwa CCM kumejaa vigogo ambao wanatumia fedha nyingi kwa kulinda maslahi binafsi na kusahau kama wao wapo hapo kwa ajili ya maslahi ya Taifa na wananchi wake ,ndio ukaona jinsi wanavyoiba fedha ya umma bila ya huruma ..mmoja wao aliongezea.
Wabunge hao ambao wengi wao huwa wanaonekana wakimya ndani ya bunge wamezidi kutonya kuwa safari hii CCM magome watafahamu kuwa mizizi ndio muhimu kwa mti.

..habari hii inaukweli?

..fmes?

..kuhani mkuu?
 
Back
Top Bottom