afu na mtoa mada nae, talaka haidaiwi chumbani! huyo bidada si aondoke talaka itamfuata huko aliko? mi nakasirika kweli mwanamke kushindwa kujitambua!
Kuna dada etu kaolewa dom lakini tangu kaolewa miaka 3 iliyopita amekuwa akichezea kichapo sana tokakwa mumewe ambaye ni mlevi na mkorofi sana ameshamvunja mkono dada mara mbili kwa kipigo..nipo dom kwa mapumziko na nilienda kumtembelea dadangu ambae ana p.o.p mkono wakushoto kwa kipigo cha mumewe nilipo muuliza ni kwa nini iwe hivo na ndugu wanasemaje akasema ndugu washachoka kuamua mana wakati mwingine nao huambulia vitisho kama si kipigo toka kwa njemba hiyo...mbaya zaidi jamaa amegoma hata kutoa talaka...sasa wakati tukizungumza na dada mara shem kaingia na kuanza na kejeli na dharau zake kwangu eti tunamfatilia sana na maisha yake n mke wake mara ooh ntaoa uko mzima nilipomwambia ajiheshimu ndo kama kapata sababu nilikua nakunywa chai akachukua ile chai na kunimwagia na maneoo kibao ya kashfa dada kuona vile akaingilia kati maskini kunitetea dah! Alisukumwa na kukanyagwa vibaya aisee nilipata hasira mbaya nilichomfanya huyo jamaa sasa hivi yupo moi nilivunja mguu na mkono....sasa kimbembe kimekuja ndugu wa huyo ***** na wangu kuna bifu kubwa na kibaya zaidi baadhi ya ndugu upande wangu wanaunga mkono upande wa pili eti kwa nini naingilia ndoa za watu...kesi iko polisi na kesho kuna kikao hapa hom kizito....hebu nambieni waungwana nisimamie wapi' na je nilichokifanya ni kosa?
safi kabisa, uje uchukue juice yako...
Dodoma mbali halafu leo nimekuota tunapita milima na mabonde halfu kuna maua meeeeeeeeeeeengi ya rangi nyekundu na njano yaani we acha tu ukimaliza kusoma futa MJ1 asione maana muda kitambo najua TF atanitumia ila advance ya mahari ya Loner.
hahahahaha! Umeanza uchokozi heartbreaker. Ngoja nimwamshe MJ1 nikusemee.
ubaya haulipwi kwa ubaya sangara. Kwani hakukuwa na namna nyingine ya kumaliza tatizo?
ishu ni kwamba uwepo wake pale umesababisha kwa kiasi kikubwa hayo yote yatokee. Kwanini huyu kaka asingetulia kwake? Dada mtu ameshajichagulia hayo maisha ya u-tyson. Jamaa anaona amemdhibiti shemeji lakini hiyo haitorejesha amani katika ndoa hata kidogo. Kifupi jamaa, shemeji na dada wote wana makosa. Sioni haja ya kumpongeza jamaa alichokifanya otherwise aje mwanasheria aniambie kisheria sister wako akidundwa kumvunja mguu na mkono shemeji inaruhusiwa.
Ngoja nitafute na watu wa imani waniambie.
hapa nadhani kuna mlolongo wa matukio yanayohusu zaidi ya wanandoa (namaanisha ndugu) na inaonekana jamaa alipoenda kumsalimia dada yake mwanaume alihisi kuna uchochezi unaendelea au yawezekana jamaa anamjua kaka mtu jinsi alivyo kwa hiyo akaamua kuanza kumshambulia kwa kujua au kwa kujaribu kulinda nyumba yake ..
mkuu kwa hali ya namna hii ulitakiwa kutimka uwaachie wanandoa .. leo hii umemvunja shemejio mkono kesho ukimkuta amemshika dada yako kiuno na wanateta utachukua hatua gani??? kumbuka wewe ni ndugu na yule ni mme wa dadayo hivyo kila mmoja ana nafasi yake kwa wakati wake
Ifike mahali wanawake tuwe tunajitetea
inafikia unavunjwa mkono mara mbili bado
unaishi na katili kisa nimefunga nae ndoa.
Mkuu ulivyofanya ni sawa na kwenye kikao ukienda
usibabaike, eleza kilichotokea mpaka kufikia kuvunjana
mkono na mguu ulokataa kujiunga tena.
Niliposoma heading nilidhani inazungumzia mtu ninayemfahamu, lakini seems matatizo yanafanana.
Shemeji yangu wa kike amenasa kwenye tundu bovu, na ndoa haina hata nusu mwaka lakini jamaa yake anamtenda kama msimuliaji anavyobainisha kwa dada yake. Ila shemeji yangu ameamua kufa na tai shingoni ( Jamaa anapiga wala hajali kama mkewe ana kiumbe tumboni)
Tatizo lililopo kwenye jamii ni namna hawa akina mama wanavyojua kuficha maovu ya watesaji wao ambapo huishia either kujeruhiwa ama kufa ama kupata ulemavu kabisa. Sheria ya ndoa ipo wazi kabisa kuhusu hizi brutality zinazoendelea kwenye bedrooms zetu. Women (and men) you must step out and speak it loud ili muweze kuokoa ndoa zenu na maisha yenu.
Asee Paw pamoja na kusoma kwa woga woga hii post yako (haikawii kuwa ya kumpa mtu ban) unamaanisha kuwa anyefanya izo mambo ni kaka yako au ndugu wa damu? hebu fanya mpango bana umtoe huko kuzimu shemeji yako na hatakusau!
u mean kutimka na kumwacha dada akipata kichapo pengine kufa eti kisa ni wanandoa?? Ina mana unaweza kaa ukishangilia mwanao akichezea kichapo wewe....