Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Hata Mbowe naye alikua NJE.Ni nini kilimfanya Mbowe ahairishe mikutano yake Afrika kusini??

Mambo mengine hayahitaji kwenda darasani kupata utambuzi. Hukujua kuwa Marehemu C. Wangwe amefariki akiwa Mbunge wa Chadema?? Daaa. Hapa napo unahitaji darasa kuelewa connection ya Mbunge wa chama pamoja na Mwenyekiti wa Chama. Mkamap, hivi ni kweli unahitaji kuelewa hiyo connection au ni moja ya mikakati ya kuongeza posts.
 
Je kuna uwezekano wa kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria waliohusika ? au bado ni mapema na inategemea na wahusishwa yaani Mbowe na wenziwe.Tumezoea kuona magazeti mengine yakitishiwa au kutakiwa kuomba radhi tena kwenye ukarasa wa mbele kwa kusema mambo ya mafisadi na kuwataja majina.
Naona waheshimiwa wajitayarishe kudai mabilioni kwa kuchafuliwa majina yao.Yaani wakilipwa basi kitita kingine watukatie hapa JF ili kulipa kodi.
 
Heshima yenu wakuu? Inaonekan leo baraza lina wajumbe wachache sana. Naomba mtu ani-update kama Jukwa la wahariri lililokuwa likae leo limesha kaa na je wametoka na tamko gani?
 
Mkuu YNMSN,

Heshima mbele sana mkuu kwa kuiweka hii sawa, mimi mkuu kwenye medicine sina idea kabisa, kwa mfano nina mshikaji wangu mmoja wa karibu sana, ambaye ninapokuwa naye, ninajua kuwa anakuwa na kidude flani hivi kama yeye anakiita pump, anakuwa nacho mfukoni na kingine kwenye gari kwa hiyo nikiwa naye ninajua kuwa mara kwa mara hupatwa na ugonjwa mmoja hivi na kama hakukiwahi kile kijitu na kujipulizia mdomoni basi ana-pass out mara moja, kwa hiyo akichelewa tu basi ninakitafuta ninampulizia mdomoni anapata fahamu tena, sasa guess what ukiniuliza leo anaumwa nini sijui na wala sijawahi kumuuliza, na hata kile kijitu sijui kinaitwa nini zaidi tu ya pump!

Kwa hiyo hata hii ya Kolimba ndio maana sikuuliza sana ni ugonjwa gani lakini ni viongozi na watu wengi sana waliokuwa karibu na Kolimba walithibitisha kuhusu hii ya mtoto wake na dawa, anyways ninashukuru kwa kuiweka sawa hii ndio uzuri wa JF siku zote wapo watu wanaoelewa ishus, saafi sana.

Ahsante Mkuu!

jamaa yako possibly ana asthma na hiyo pump inaitwa MDI (metered dose inhaler)! anaweza kuwa yupo kwenye beta blockers kama albuterol, anticholinergics kama Ipratropium Bromide au combination ya madawa kama Advair!!

nakuelewa mzee, lakini sometimes achana na watu wanaobisha bila sababu kwani ndivyo tulivyo....wengine hapa wanataka masifa ya kuonekana wanajua kutoa watu nishai kumbe ni mabwege wa kutupwa!!.
 
Nafikiri ni inhaler hiyo!

Zipo dawa nyingi ambazo zinahitaji kuzila mara kwa mara, ukiacha kula umekwenda na maji, na sitashangaa kama hivi ndivyo ilivyokuwa kwa Kolimba. Hata hivyo huyu mtoto wake na yeye mwenyewe walikuwa wazembe kidogo kukubali kuingia kwenye kikao bila hizo dawa na kukubali huyu kijana asiingie kama kweli ndiye alikuwa anashikilia uhai wake!

true, jamaa huenda alikuwa na angina/ischemic attacks..huenda ilikuwa unstable na hivyo unpredictable!! angina ikiachiwa bila udhibiti inaweza ku-develop kuwa Myocardial Infarction (MI)...good news ni kwamba dawa zake hasa NTG unaweza kuchukua prophylactically, sasa sijui Kolimba alikuwa na HD ya aina gani na dawa gani alikuwa anatumia kiasi kwamba akupata dose prophylactically kama alijua anaenda kwenye gauntlet!!?? au pengine hakujua, walimstukiza!?....vyovyote vile, hawa jamaaz itakuwa waliua bila kukusudia!! siku tukichukua nchi watajibu na hili.
 
Mimi binafsi nisingependa kuona inafungwa. Angalau hapa majibu ya uzushi wa vyombo vya habari nyumbani yatajibiwa. Ikifungwa, wale wote wenye kubeza na kueneza habari za uchochezi kwa wakazi wa Tarime kwenye vyombo vya habari Tanzania (wakioongozwa na TBC) wataendelea tu bila majibu yoyote yale au kupata upande mwingine wa kinachotokea Tarime.

Asante.

Kaka MAGABE,

Tanzania inakuhitaji. Rudi nyumbani haraka tuendeleze jukumu tulilolianza mwaka 2000. Tafadhali kaka, rudi nyumbani....

Tanzanianjema
 
huyu jamaa alipigwa risas kichwani kisha dereva akaigongesha gari kwenye mti. na sijui watasema nini baada ya majibu ya kukuta risas kichwani kupatikana, sijui kama polis watakanusha taarifa ya awali ya jeraha tupu kichwani?? hapa cha msingi alie andaa haya mauaji ajisalimishe mapema mwenyewe, sababu huku alikogusa sio kwa mcheso!
asari amangána mona bhoke!

Mhhhhhhhh......

Ndio Tanzania yetu hiyo...
 
Unaweza kupitia tena na tena gazeti la majira la leo www.majira.co.tz kujua kuwa kwako uongo ni jadi yako, nusura wamuue Mwenyekiti wa Chadema na wametoa tamko ni marufuku kwake kuhudhuria mazishi ya Wangwe.

ana mtihani mkubwa kwani yeye anataka kuhudhuria mazishi ili kuondoa tetesi kwa vyombo vya sheria pindi vikianza kutafuta chanzo na kifo cha Wangwe,itakuwa kichekesho kama hatahudhuria mazishi ya mwenyekiti wa mkoa wa mara na Mbunge aliyekuwa masaidizi wake kama makamu mwenyekiti huo upande mmoja, lakini upande wa pili wana Tarime wameapa asihudhurie mazishi.

Na hawa ndiyo selfmade opinion makers wa TANZANIA.....MAJIRA ya ufisadi ndio reference.....

Tuna safari ndfu na ya hatari kubwa.....

Tanzanianjema
 
Polisi wanaweza kuishurutisha kampuni ya simu, ikibidi kwa mamlaka ya mahakama (subpoena) itoe rekodi za simu za mteja fulani ili kuendesha uchunguzi.

My concern is, if the players are big enough, the right person's palm at the telephone company can be oiled, the records deleted in time and by the time a slopoke police comes to ask nothing controversial will be found.

Pundit,

What if Malya and Wangwe phones were Vodacom phones? will we be able to at least get near the truth if it is alleged.......
 
Mambo mengine hayahitaji kwenda darasani kupata utambuzi. Hukujua kuwa Marehemu C. Wangwe amefariki akiwa Mbunge wa Chadema?? Daaa. Hapa napo unahitaji darasa kuelewa connection ya Mbunge wa chama pamoja na Mwenyekiti wa Chama. Mkamap, hivi ni kweli unahitaji kuelewa hiyo connection au ni moja ya mikakati ya kuongeza posts.


Kwanini pia wewe unashindwa kuona connection ya RIP CHACHA na RA hadi kukutan HOTEL sijui ya KEMPSik au nalo mlimzushia marehemu ??
 
Invisible na wengine,

Msilifanye suala hili kuwa la kisiasa,nilishasema toka jana..Ole wenu CHADEMA,kwa vyovyote vile bado mnalo...hata kama,kuna kosa lillishafanyika na lazima watu walinywe sasa nomatter who did but it will be like it is.Poleni coz mmeshikwa pabaya

Kwa Mtanzania anayedhani hili ni la CHADEMA ama Mbowe tu namuonea huruma. Kwani hata kama unaweza kuwa ni mfaidika wa MFUMO FISADI tulionao, ni wazi mwisho wa siasa hizi ni kuvunjika kwa taifa letu.

Kuanguka kisiasa kwa CHADEMA ni kuanguka kwa vuguvugu la maendeleo ya demokrasia ya vyama vingi nchini. Kuanguka ama kuharibikiwa kwa MBOWE sio tu kuwapa maadui wa maendeleo ya demokrasia nafasi ya kujidai zaidi na vi-EPA kedekede bali pia ni kustawisha chuki dhidi ya ndugu zetu WACHAGA. By the time tunazinduka tutakuwa tumeshatengeza adui mwingine...sijui itakuwa ni watu wa Nyanda za Juu ama Waswahili ama .......

Tanzanianjema
 
Kabla Amina Chifupa hajafariki hapa JF kuna watu walishatabiri na ikatokea kweli, the matter of fact hata kifo cha Balali, kilishatabiriwa mapema hapa, halafu ninaomba nikuhakikishie kuwa nimewahi kuongea sana watoto wa Mwaikambo, Kolimba, na Kombe, niliyoyapata ni Kolimba peke yake ndiye aliyefariki kifo cha Mungu, kwa ugonjwa aliokuwa nao, kwa sababu kila siku ya Mungu, alikuwa akifuatana na mtoto wake aliyekuwa akimshikia dawa zake maalum za moyo, alipoitwa kwenye kikao maalum cha CC, mtoto wake hakuruhusiwa kuingia, akaamua kwenda kupumzika hotelini ndilo hasa kosa lilopelekea baba yake kufa, kwa sababu alipoanza kuumwa, wakanza kumtafuta huyu kijana, by the time wamekuja kugundua kuwa yupo hotel, it was too late, na besides kaka yake Kolimba alihusishwa kwa 100% na uchunguzi wa mwili wa ndugu yake na kuridhika na kila step kuwa hakukuwa na faulo, Lakini sio vifo vya hao wengine wawili ninam-challenge kiongozi yoyote wa taifa bongo anayeamini kuwa hawakuuliwa kwa makusudi, tuzichambue facts chini,

FMES,

Nashukuru kwa hii Nondoz, lakini nauliza swali kwa jamii, ni nini kilichotokea mpaka Kolimba akapata shinikizo au mshtuko wakati wa Kikao nyeti cha Kamati Kuu/NEC? Kama katibu mkuu wa chama na kiongozi, alikuwa anajulikana kuwa ni mgonjwa, ikiwa kijana alikatazwa kukaa pale kwenye jengo akaamua kurudi Hotelini, alirudi kwa miguu bila kupelekwa na gari la CCM au bila baba yake au wasaidizi kujua amekwenda wapi hasa ukizingatia alikuwa na dawa za Baba yake?

Je kuchelewa huku kubaini kuwa Kijana alikuwa amerudi hotelini kulifanywa makusudi ili kilivhotokea kihalalishwe kuwa ni kifo cha kawaida kwa kuwa alikosa dawa?

Jee, mganga wa Rais na hospitali walikuwa wapi na umbali gani kugundua kuwa Kolimba alikuwa na ugonjwa mbaya ambao unahitaji dawa na tiba ya haraka?

Je ulikuwa ni usiri wa namna gani kwa kiongozi mkubwa kama Kolimba kuficha ugonjwa wake kwa viongozi wenzake, watu wa Usalama na wasaidizi wake?

My point hapa ni kuwa pamoja na appearance ya natural death kutokana na mshituko wa moyo au blood presure, mazingira yote yanaonyesha kana kwamba kulikuwa na delibarate efforts kuhakikisha kuwa Kolimba haponi tena alipopata ule mshituko.

Hivyo kuhitimisha, naomba urudishe jina la Kolimba katika listi ya vifo vya utata!
 
Je kuna uwezekano wa kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria waliohusika ? au bado ni mapema na inategemea na wahusishwa yaani Mbowe na wenziwe.Tumezoea kuona magazeti mengine yakitishiwa au kutakiwa kuomba radhi tena kwenye ukarasa wa mbele kwa kusema mambo ya mafisadi na kuwataja majina.
Naona waheshimiwa wajitayarishe kudai mabilioni kwa kuchafuliwa majina yao.Yaani wakilipwa basi kitita kingine watukatie hapa JF ili kulipa kodi.

Hiyo Mkuu ndio suluhu tu nasi kupiga propaganda .

Mbowe Amezushiwa kua alitolewa bunduki ktk mazishi basi awapeleke ktk vyombo vya sheria huo ndio utaratibu halali na si vinginevyo.

Huko ikionekana alizushiwa yeye ndiye anaweza amau alipwe ama asilipwe huo ndio utaratibu wa msingi.
akiamua naye kulipwa mabilioni ili aje awapige cha juu hapa hiyo ni uamuzi wake.
 
Mkama,

Nadhani sasa tunaweza kukubaliana kwamba aliyeandika habari ni mtu mmoja na ilitumika kwa magazeti yote yaliyoweka habari hiyo na wala hakuna swala la kudeseana. Swali la kujiliuliza ni kwamba je, kwanini walikubali kufanya hivyo?

Madai yako kwamba waandishi huwa wanadeseana kwa kuwa huwa wanabana posho, hilo sikubaliani na wewe hata kidogo. Kwanza hapo mwandishi ana risk kufukuzwa kazi kwa kuwa habari ile ikileta mushkeli kwa jamii, mhariri ndiyo huwa anakuwa responsible.

Kazi ya mhariri ni ku-proof read ile habari na ku-cross check kama habari aliyotumiwa ni ya kweli. Kuna sources nyingi za kufanya hivyo na kama mwandishi katuma habari bila ya kuwepo kwenye tukio basi wakati wa ku-cross check lazima atagundulika na hasa kwa news sensitive ambayo ilikuwa imevuta hisia za watu kama ilivyokuwa kwenye huo msiba. Kama wahariri wangefanya kazi hiyo sidhani kama kuna mtu angelalamika. Kinachotakiwa ni mtu kuwa fair kwenye analysis yake na pale mhariri anapo-detect chumvi basi lazima ajiulize na na kuifanyia kazi.

Siku nyingine habari huwa zinafanana lakini siyo neno kwa neno. Sometimes hata heading zinaweza kufanana lakini contents zikawa tofauti.

Kama ni swala la elimu, wahariri wote wana elimu na tena ya chuo kikuu lakini wametuambia Joseph Mbatia ni Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi. Hivi ili kujua kwamba Mwenyekiti wa NCCR ni nani lazima uwe na gazeti jingine la kulinganisha??

Mnafiki na yule ambaye anaandika habari kwa malengo tofauti. Mtu anaweza kuwa na PhD lakini bado akawa mnafiki, na kuna wengine ambao hawajasoma hata darasa moja na siyo wanafiki.

Kununuliwa kwa waandishi hakutokani na kuwa naa elimu duni. Unadhani kwanini watu wanasema kwamba RA kanunua wahariri? Mhariri ndiye anayeidhinisha habari itoke gazetini na anaweza kuibadilisha kwa jinsi yeye anavyoona inafaa na yeye ndiyo anakuwa responsible just in case habari ikiwa ina matatizo. Lini uliona mwandishi wa habari anaomba radhi? Wanao omba radhi huwa ni wahariri kwa kuruhusu kuchapa habari ambayo haikuwa na ukweli ama ili-ripotiwa kimakosa.

Tatizo letu ni kwamba tunawaangalia waandishi wa habari as if kile walichoandika ndicho ambacho huwa kinatoka gazetini kama kilivyo.

Waandishi waliotuhumiwa kununuliwa na mafisadi (RA) wote wamesoma na wana degree zao. Kila siku watu wanamtaja Balile na Muhingo Rweyemamu kwamba walinunuliwa na RA, na wote wana degree. Je, bado una hoja kwamba mwandishi kama hajasoma basi itakuwa rahisi kumnunua?
 
miongoni mwa waliopigiwa simu mara ya kwanza na Malya si mwengine bali ni..... yes you guessed it!
 
Kwa taarifa yako tu ni kwamba viongozi wa CCM kwa niaba ya CCM waliiomba radhi rasmi familia ya Kolimba kwa kitendo cha kumkatalia mtoto wake asiingie kwenye kile kikao, na hata kum-offer ndugu yake kugombea ubunge wa ndugu yake,

FMES,

Then my opinion above kuwa Kolimba's death was not natural but appeared to be natural due to delibarate efforts to rid of him are true!

Nilichojifunza kutoka siasa za Tanzania na hasa hiki kifo cha Wangwe kama vile vya kina AC, Mbatia, Ballali, hata ukirudi nyuma kwa Kombe na Mwaikambo, posibly even Akukweti, utagundua kuwa kuna utata wa hali ya juu ambao huambatana na rumours kibao halafu mwisho wa safari, kama Taifa kwa shingo upande, tunaendelea na maisha bila kupata majibu au ufumbuzi wa kweli kuhusiana na kilichotokea.

Serikali yetu imejenga tabia ya kusema Watanzania ni wavumilivu, they will get by and forget about it! There is not truth coming out, dubious and circumstantial news rule the airwaves and business as usual!

This is SCARY S H I T!
 
Nyie kubalini tu vifo vya viongozi wenu, na siku zaidi ya mmoja watakufa kwa wakati mmoja na mtaambiwa ni mapenzi ya Mungu. Endeleeni tu kukubali maelezo ya watawala siku moja watatoa maelezo ambayo hayaingii kichwani na mtajikuta mnakubali kwa sababu hamtaki to rock the boat.
 
Kingine ni kuwa Mallya alikuwa na funguo za gari mkononi alizichukua wakati gani?kama ni baada ya ajali je?inawezekana kuwa eneo la funguo halikuumia?ziliwezaje kutoka?je?alichukua funguo kabla ya ajali?na kama ni kabla maana yake ni kuwa gari haikupata ajali kwani ilikuwa imesimama?

Angalieni tena picha za ajali, juzi na jana walifanikiwa kuhamisha mjadala badala watu kuangalia chanzo cha ajali tulijikita kuangalia kama ni risasi ama sio risasi na hapo tukapotea njia moja kwa moja.

Huu mjadala wa risasi ulitokea wapi? ni kwanini ulisemwa hivyo?aliyeanzisha mjadala wa risasi ni nani?
Naambiwa kuwa aliyeanzisha mjadala huo sasa kaanzisha mwingine kuwa kuna rushwa ilitolewa jana kwa familia na daktari ili wakubaliane na uchunguizi ,sasa hapa lazima sisi kama tunatafuta ukweli tuende hatua moja mbele na kuwa mbele yao na kuwa independent ili kuweza kuangalia chanzo cha ajali .



Cha ajabu aliyemwaga sumu hii ya RISASI ana jukumu la kuwafundisha vijana wa kitanzania kazi nyeti ya UDAKTARI.....No wonder watu wanapasuliwa vichwa badala ya miguu....

Tukumbuke kuwa aliyeshupalia hii story na hata kunyanyua BANGO linalouliza swali kama NI RISASI AMA AJALI ni yuleyule aliyehakikisha kuwa Marehemu Chacha Rasta anafungwa jela wakati yeye akiwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime akiwa kada mzuri wa CCM.

My respects to Prof Wangwe...usomi kweli ni dawa maana bila ya busara zake tungekuwa tunasema mengine kutokana na juhudi za ma-oppurtunists wa ndani na nje ya familia.

Sasa nimeamini kuwa ni kweli FISADI hana SONI....

Tanzanianjema
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom