na hata JF Very Senior members ambao mara nyingi kutokana na utashi na ushawishi mkubwa credibility ya 'source of info' na posting 'zao/zetu/zenu' zinaaminiwa na wengi.
Mkuu Heshima yako, sina uhakika kama ninakuelewa vizuri lakini unaonekana kukimbia kivuli cha serikali yao, au chako mwenyewe either kwa sababu hujui historia au unajua ila umeamua kuikwepa, JF tuna sifa moja kubwa sana mbele ya jamii na hasa kwa viongozi karibu wote wa juu, nayo ni accuracy ya information zetu,
Ninajua kua wananchi wengi hapa hamlijui hili kwa sababu viongozi hao hawajaja hapa na kusema wazi, lakini kwa wale wachache ambao tuna access nao tunajua fika kuwa hata wao hapa ni mahali muhimu sana pa kupata habari zilizochambuliwa, ndio maana ukiona tunag'aka na habari fulani ujue kuna something tunajua, kwa mfano kwenye kifo cha Balali, viongozi wetu walikuwa wakisema kwa public kuwa amefariki katika hospitali ya Boston, ukweli ukawekwa hapa kuwa hakuwepo huko,
Sasa cha ajabu ni kwamba viongozi wale wale waliokuwa wanalihakikishia taifa kuwa amefariki, walikuwa wakitafuta watu hapa kuwathibitishia kama ni kweli, serikali yetu haikuwa inajua kuwa Balali alikua na permanent resident permit ya kuishi US, ukweli ni kwamba kuna kiongozi mmoja mkubwa sana kutoka Zanzibar, ambaye nilimfahamisha dakika ya mwisho anataka kuingia kwenye kikao cha NEC Butiama, ikabidi arekebishe hotuba yake na kunishukuru sana,
Kabla Amina Chifupa hajafariki hapa JF kuna watu walishatabiri na ikatokea kweli, the matter of fact hata kifo cha Balali, kilishatabiriwa mapema hapa, halafu ninaomba nikuhakikishie kuwa nimewahi kuongea sana watoto wa Mwaikambo, Kolimba, na Kombe, niliyoyapata ni Kolimba peke yake ndiye aliyefariki kifo cha Mungu, kwa ugonjwa aliokuwa nao, kwa sababu kila siku ya Mungu, alikuwa akifuatana na mtoto wake aliyekuwa akimshikia dawa zake maalum za moyo, alipoitwa kwenye kikao maalum cha CC, mtoto wake hakuruhusiwa kuingia, akaamua kwenda kupumzika hotelini ndilo hasa kosa lilopelekea baba yake kufa, kwa sababu alipoanza kuumwa, wakanza kumtafuta huyu kijana, by the time wamekuja kugundua kuwa yupo hotel, it was too late, na besides kaka yake Kolimba alihusishwa kwa 100% na uchunguzi wa mwili wa ndugu yake na kuridhika na kila step kuwa hakukuwa na faulo, Lakini sio vifo vya hao wengine wawili ninam-challenge kiongozi yoyote wa taifa bongo anayeamini kuwa hawakuuliwa kwa makusudi, tuzichambue facts chini,
Kama una tatizo na habari za uchochezi, basi wakaripie magazeti wanaolipwa na viongozi sometimes kuandika ukanjanja, halafu kwa nini usimlaumu Tido Mhando, kwa kuwadanganya wananchi na taifa letu kwa ujumla kuwa polls za BBC zinaonyesha kuwa Mtandao ndio wanaotakiwa kutawala, ni info kama zile ndio zinaweza kuleta maafa kwa taifa, looking at waht is going on now na uongozi wa Tanzania,
JF huwa tunachambua ishus kwa kutumia ushahidi mbali mbali ambao unakubalika kwa siasa za online, na siku zote huwa tuko wazi kujibu maswali yanayohusu hoja zetu hapa, huenda hufahamu kuwa kuna watu hapa ambao huwa wanaulizwa maswali mazito sana na serikali kulingana na ishus za hapa, tena kila siku ya Mungu, na serikali huwa inajibiwa na kuelewa, kwa hiyo mkuu mimi sipendi kuzunguka mbuyu, ni mmoja wa Senoir Expert hapa na JF na huwa niko mstari wa mbele sana kwenye kuchambua ishus na ku-speculate kwa kutumia ushahidi wa ground zero na wa online, na ninaomba nirudie kuwa mpaka nitakapopata majibu ya maswali mawili ndio nitaamini kuwa ile ilikwa ni ajali tu:-
1. Mallya alitokaje kwenye lile gari bila kuchubuka wala tone la damu.
2. Lile gari exactly lilipata ile ajali wapi? Mimi ni mwenyeji wa mkoa wa Dodoma na pale ajali ilipotokea ninapajua vizuri sana, hakuna mawe wala vyuma vya kuweza kuiumiza ile gari kiasi kile, na wala lile gari halikugonga jiwe wala vyuma vizito, sasa ni nini hasa kilichojiri na tena kulikoni mpaka gari kuwa noma kiasi kile?
So far nimewauliza karibu viongozi wengi wanaohusika na handling ya hii ajali hakuna mwenye jibu, kama unalo ninaliomba mkuu na nitaacha hapo hapo kuchangia tena hii ishu,
Otherwise A luta Continua!
Ahsante Mkuu.