Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
1.

2.


3.

Mkuu heshima yako, nilijua kuwa nimekukamata pabaya na ujanja wako wako mwingi, sasa hizi ndio akili zako nyingi ambazo sasa karibu watu wote hapa wameanza kuzielewa ukishikwa pabaya basi ni unageuka kinyonga unabadili rangi na kuwa nyoka, najua ulifikiri utaweza kui-control hii forum na hiyo janja yako lakini unajua kuwa kwangu umekwama!

Kwa taarifa yako tu ni kwamba viongozi wa CCM kwa niaba ya CCM waliiomba radhi rasmi familia ya Kolimba kwa kitendo cha kumkatalia mtoto wake asiingie kwenye kile kikao, na hata kum-offer ndugu yake kugombea ubunge wa ndugu yake,
Naona unateseka sana na dataz zangu, maana unajaribu sana kui-control hii forum, kwa kutuchezea vichwa watu hapa lakini ni mimi peke yangu ndiye ninakukwamisha, na ninakuhakikishia kuwa as long as nipo hapa, utabadilika na ukinyonga wako mapaka uwe kufutu, lakini nipo nyuma yako bro, mpaka kieleweke!

Right on!!!!
 
Hata madai ya kuhusishwa RA ktk Habari hizo ama kuhusishwa RA kuwa ni mwajiri wangu nayo hayana uthibitisho na mnayaacha yapite free.

Lakini mimi nikikuhusisha wewe na Mbowe waja juu.Hapo ndipo unaona hakuna UHURU humu ndani.Na lazima kuhakikisha kila taasisi ya MTZ inakua huru,Hiyo ni moja ya wajibu wangu.

Ama UHURU uliomo humu mtu yeyote akipinga maada zenu lazima awe wa RA na anayehusishwa na MBOWE basi uhuru unakua umeingiliwa??

Kungekuwa hakuna uhuru usingeweza kuongea unayoongea sasa wala usingeona post zako.

Uhuru wanatunyima hao wanaoandika habari moja katika magazeti matano katika vichwa tofauti. hapa kuna uhuru wa kweli unachosoma ndicho kilocho andikwa sio kilichopikwa.

somo
]mtu anakuwa huru pale anapokuwa na uwezo wa kuutumia uhuru anaopewa wewe hapa JF unapata uhuru wa kutoa mawazo yako. lakini unakuwa huru zaidi pale unapokuwa na mawazo yakutoa. kama hauna mawazo yakutoa then huo uhuru haukuhusu wala haukusaidii chochote maana you have nothing to say.
 
Mkama,

Ndiyo kusema RA alirudi Tanzania kuja kwenye msiba kwa kukusanya wahariri na kufanya nao kikao cha siri Dar?

Magazeti yake yametuhumiwa kuwa na majina tofauti ya waandishi walioripoti habari ile na pia yana wahariri tofauti, lakini habari ile inafanana. Nadhani mtu anaweza kusema wording imefanana, je, hata jina la James Mbatia magazeti yote yatakosea? Kumbuka ni waandishi tofauti na pia yana wahariri tofauti, ina maana kuna ka-ukweli kwenye tuhuma za RA kukutana na wahariri na ndiyo maana kukawa na habari ambayo imeitwa ni ya kupika.

Msiba ulikuwa Tarime, kama RA alirejea nchini kushiriki msiba wa best yake ilikuwaje asifike Tarime?

Wewe nadhani unafahamu mengi, tujulishe ushiriki wa RA kwenye msiba. Maana kama ni kutuma rambi rambi angeweza kutuma toka huko alikokuwa. Lakini kama alirejea nchini maalum kwa ajili ya msiba basi lazima angeenda mpaka Tarime kwenda kushiriki kwenye mazishi.
 
Mkuu FMES,

Nimecheka kweli kweli hiyo ya Kolimba. Naamini hapa tuna madaktari, si ajabu na wao wanacheka kama mimi. Sikujua siku hizi kuna dawa ya ugonjwa wa moyo inafanya kazi kama dawa ya kisukari kwi kwi kwi!!!!!

Huu mjadala mimi nimejitoa kuchangia, ila hii ya mbeba dawa pembeni imenichekesha mno, sikuweza kujizuia tena.


Mkuu,

Duh, are you OK !!! Bila shaka utarudi tena kwenye mjadala utakapopata nafuu kwi kwi kwi!!!!
 
Kungekuwa hakuna uhuru usingeweza kuongea unayoongea sasa wala usingeona post zako.

Uhuru wanatunyima hao wanaoandika habari moja katika magazeti matano katika vichwa tofauti. hapa kuna uhuru wa kweli unachosoma ndicho kilocho andikwa sio kilichopikwa.

somo
]mtu anakuwa huru pale anapokuwa na uwezo wa kuutumia uhuru anaopewa wewe hapa JF unapata uhuru wa kutoa mawazo yako. lakini unakuwa huru zaidi pale unapokuwa na mawazo yakutoa. kama hauna mawazo yakutoa then huo uhuru haukuhusu wala haukusaidii chochote maana you have nothing to say.


Kwa hiyo UHURU wenu unawahusu ninyi ni ule tu anaye pingana na mawazo yako ni mwajiriwa wa RA.

Na uhuru wenu ni halali tu kila jambo mbaya lazima lifanywe na RA.Huu uhuru wenu ni BUTU yani kuanzia UHURU wa fikra hadi haki za binadamu .
 
Kwa hiyo UHURU wenu unawahusu ninyi ni ule tu anaye pingana na mawazo yako ni mwajiriwa wa RA.
Na uhuru wenu ni halali tu kila jambo mbaya lazima lifanywe na RA.Huu uhuru wenu ni BUTU yani kuanzia UHURU wa fikra hadi haki za binadamu .

Mimi sijaongelea uhuru kuhusiana na yote unayoyasema hapo juu. mimi nachosema ni nini haswa maana ya uhuru. Mtu asiyejua kuimba kwa mfano, uhuru wa kuimba kwake hauna maana yoyote kuwepo kwake au kutokuwepo kwa uhuru huo haumdhuru kwa aina yoyote.

vile vile hapa JF uhuru wa kutoa mawazo upo, hilo ndio la msingi ninalosema. wewe unasema hakuna uhuru, jambo ambalo sio sahihi hata kidogo. Mtu anayeona hapna uhuru, kuna mawili moja hajui nini maana ya uhuru anao ongelea, pili hayuko disposed kufaidika na huo uhuru sasa mwenzagu sijui uko wapi wewe mwenyewe ujiweke katika hayo mawili.

Jamani tuendelee na mijadala yenye manufaa
 
Mkama,

Ndiyo kusema RA alirudi Tanzania kuja kwenye msiba kwa kukusanya wahariri na kufanya nao kikao cha siri Dar?

Magazeti yake yametuhumiwa kuwa na majina tofauti ya waandishi walioripoti habari ile na pia yana wahariri tofauti, lakini habari ile inafanana. Nadhani mtu anaweza kusema wording imefanana, je, hata jina la James Mbatia magazeti yote yatakosea? Kumbuka ni waandishi tofauti na pia yana wahariri tofauti, ina maana kuna ka-ukweli kwenye tuhuma za RA kukutana na wahariri na ndiyo maana kukawa na habari ambayo imeitwa ni ya kupika.

Msiba ulikuwa Tarime, kama RA alirejea nchini kushiriki msiba wa best yake ilikuwaje asifike Tarime?

Wewe nadhani unafahamu mengi, tujulishe ushiriki wa RA kwenye msiba. Maana kama ni kutuma rambi rambi angeweza kutuma toka huko alikokuwa. Lakini kama alirejea nchini maalum kwa ajili ya msiba basi lazima angeenda mpaka Tarime kwenda kushiriki kwenye mazishi.

KEIL
Safi sana mkuu
Kwanza kabisa hizo RA kufanya Mkutano na waandishi nayo yawezekana ni mwendelezo wa speculation ya watu .
wewe umeamini vipi na nini kimekuaminisha kua alifanya mkutano na waandishi wake? tupe picha ama record mliyomrekodi kafanya mkutano wa siri ili tuamini mnachosema ,vinevyo wewe unadhani tuwaiteje hawa?

Kuna mambo mengine hayahitaji hata kua mtu mwenye HEKIMA kutambua speculations ,yani ya kwamba kama hayo magazeti ni ya RA kunahaja gani ya RA kufanya mkutano badala ya kutoa agizo tu habari hii iandikwe ktk kila gazeti lake.

Na kuhusu Habari kufanana yawezekano wa kudesa upo mkubwa,mimi mwenyewe nimeshaona maranyingi habari zimekopiwa kama zzilivyo na magazeti ya TZ kutoka magazeti ya kenya na bbc,hii yawezekana ni wavivu ama hawajiamini ama waandishi hawaendi eneo la tukio na hiyo posho wanatia ndani.Ama kwavile ni kampuni moja RA walitumia mwandishi mmoja wakijaribu kuserve gharama.

Wangapi tumepewa fedha za research kwenda kufanya research na badala yake eneo ya research hufiki ila unakusanya ma paper ya watu ama unakaa ktk internet unaanza KUDESA fedha yote night zote,nauli,maradhi unatia ndani.Mbona hamjiulizi hilo?
 
Mkuu FMES,

Nimecheka kweli kweli hiyo ya Kolimba. Naamini hapa tuna madaktari, si ajabu na wao wanacheka kama mimi. Sikujua siku hizi kuna dawa ya ugonjwa wa moyo inafanya kazi kama dawa ya kisukari kwi kwi kwi!!!!!

Huu mjadala mimi nimejitoa kuchangia, ila hii ya mbeba dawa pembeni imenichekesha mno, sikuweza kujizuia tena.

Zipo mkuu, mfano buccal NTG for angina pectoris ina kick within 2 minutes..........

Inategemea mtu ana aina gani ya cardiac issues na dawa gani anayotumia mfano Calcium blockers (cardizem), beta blockers (atenolol) n.k OPD yake ni tofauti...lakini hapa ninapoishi protocol ya "code blue" ya li impending or actual infarct ni "MONA" from MONALISA na hiyo N inasimama kwa Nitroglycerin ambayo kama nilivyosema huko juu depending na application inaweza kukick within 2 min na kuokoa maisha........LOL

hiyo ni kwenye "nutshell" ki-layman...

kwahiyo mkulu FMES hakuwa kachekesha.... na yapo madawa mengine kedekede ya kimarekani yanafanya kazi chapchap hasa kwa ER!! kama unashida sana ni PM (lakini kuna fees ina apply) bwahahahahahahaha.

tuwe tunajaribu ku-research kidogo kabla ya kudhalilisha au kujidhalilisha....na hiyo ndio kisa cha Wangwe (RIP), anasema kweli watu wanamgeuza kichekesho na kumpandikizia uadui usio na maana...kwani ni uongo kwamba mapesa mengi yanaishia HQ ya chadema? kwani ni uongo kwamba wabunge wengi wa kuteuliwa wa chadema aidha ni wachagga au wananasaba za kichagga..........tuwe makini sana na kuacha maushabiki yasio ya lazima.

wkend njema!!.
 
na hata JF Very Senior members ambao mara nyingi kutokana na utashi na ushawishi mkubwa credibility ya 'source of info' na posting 'zao/zetu/zenu' zinaaminiwa na wengi.

Mkuu wangu Nyani, kumbe na wewe umemshitukia jamaa, si unamuona nilifikiri niko peke yangu tu kumbe na wewe umemshitukia saafi sana,

JF Experts wote wako sawa mkuu, hakuna anayezusha hapa kwa sababu hupewi hicho cheo bila ya kuwa na uwezo nacho, halafu kama unatuona hapa JF ni wazushi Mkulu Wangu MMJ ameshasema mara nyingi sana, kwa nini usende mbele kusikouwa na wazushi?
 
Wakuu.... naomba tuorodheshe majina ya magazeti yote ambayo yalitumia hii story iliyopikwa.
1. MAJIRA
 

JF Experts wote wako sawa mkuu, hakuna anayezusha hapa kwa sababu hupewi hicho cheo bila ya kuwa na uwezo nacho, halafu kama unatuona hapa JF ni wazushi Mkulu Wangu MMJ ameshasema mara nyingi sana, kwa nini usende mbele kusikouwa na wazushi?

...Nothing personal bro, heshima mbele kwa kuzingatia uhuru wa maoni.
 
Hawa wahariri wananifanya nizidi kujivunia kuwa mtanzania. Inanipa matumaini kwamba uchuro wa watu waliopo serikalini sio kiwakilishi cha uchuro wa sisi watanzania, ni uchuro wa watu wachache kabisa waliopo kwenye CCM na pengine na kikundi fulani ndani ya hicho chama. Kwa utaratibu huu tutafika.

Nawatakia uchunguzi mwema sana kamati hii, yenye wajumbe makini kabisa.
 
Nimekupata mkuu, mimi sio dakitari wala sina idea kabisa kuhusu haya magonjwa, lakini ninajua for fact kuwa yuela kijana alikwua akifuatana na baba yake akiwa akiwa na hizo dawa, inaweza kwua zilikuwa dawa za something else, lakini viongozi wengi walithibitisha kuwa sio mara moja wala mbili Kolimba aliwahi kuzidiwa wakiwa kwenye shughuli zao siasa, na huyu kijana akatoa hizo dawa, kama zilikuwa za moyo au kisukari siwezi ku-argue maana sijui lolote lakini ndivyo kijana alivyonithibitishia,

Na niaamini zaidi kwa sababu, aliyekuwa katibu wa Kolimba akiwa msaidizi wa Sokoine, aliwahi kuhamishiwa ofisi moja na ndugu yangu mmoja, naye nikaamuuliza vipi Kolimba na hii ishu, akanihakikishia kuwa ni kweli mara kwa mara alipokuwa akimfanyia kazi alikuwa na hayo matatizo na huyu mtoto wake alikuwa mara nyingi ndiye anakuja na hizo dawa,

Kama ni za moyo au za kisukari sina uhakika, na wala siwezi ku-argue on that,
Ahsante Mkuu!

bwana eeeenh hukuwa umekosea wala nini! hukuwa na haja ya kuomba radhi au kutoa maelezo zaidi juu ya position yako!

Ushauri wa bure FMES, kuomba omba msamaha na kujielezea sana kila unapobishiwa ni dalili kubwa sana ya weakness, ukimwona "shrink" kwa mahali ulipo sasa na tatizo hili wallahi lazima atakuweka kwenye medication au a serious counselling...STOP IT!! wewe wa-ignore watu wanaobisha kila kitu bila kuwa na facts.

Huyo mwingine ana act kama wale lecturers wa college writing mambo ya EN 101 na EN 102 kazi kukosoa bila kutoa njia mbadala.....mie nahisi ni "pandikizi" lipo hapa kuvuruga utaratibu, achana nae na asikuumishe kichwa!

atalegea na kushundwa siku si nyingi!!

have a nice wkend.
 
Mchongoma,

Mkuu suifanye mzaha ama utani hii issue yetu inachanganya sana akili. Huyu kijana wetu kweli alikuwa katika ajali hiyo (kulingana na madai yake) lakini katoka msafiiii wakati hiyo ya Blonde accident ni joke tu hufanywa kuhusiana na visa vya hawa Ma blondie..
Picha ya accident hiyo huyu bibie ni mtu alikwenda kuangalia accident kabla Polisi hawajafika..
Sasa badala ya ya yeye kusaidia alionekana akijali sana nywele zake, uzuri wake akifanya miondoko kama modeling, unajua tena hawa mabinti wetu kumbe jamaa walikuwa wakimchukua ktk Video visa vyake vyote....
Huyu wa kwetu inashangaza sana kuona nguo hazina hata vumbi mkuu!
 
Mkama,

Mfano wako wa magazeti kudesa ninaweza kukubaliana na wewe kama gazeti husika ama chombo cha habari kilichoripoti ni cha nje na baadaye gazeti la Tanzania likaripoti habari ile ile. Lakini siyo udesaji kutoka kwenye gazeti la hapa hapa na tena kwa tukio lile lile ambalo kila gazeti limepeleka mwandishi wake.

Unawezaje kudesa habari ambayo haijatoka gazetini? Vyumba vya habari vya magazeti ya Majira na Mtanzania viko mbali mbali. Kimoja kiko Mjini na kingine kiko Sinza, walideseana saa ngapi kiasi kwamba asubuhi magazeti yote yawe na habari zinazofanana?

Kumbuka kuna wahariri wa habari ambao huzipitia habari zote kabla hazijachapwa, na pia kuna wahariri wakuu ambao pia hupitia habari hizo hizo zote ama gazeti lote kwa ujumla. Ina maana na hao wahariri walideseana na wao walikubali kwamba Mwenyekiti wa NCCR ni Joseph Mbatia? Hii ni aibu kubwa sana!

Hata kama ni kudesa huwa watu wanadesa kwa akili japo unabadilisha hata wording. Lakini habari hiyo Sakina Datoo anasema ni neno kwa neno!

HEKIMA uliyosema mtu anaweza kuitumia sijaiona. RA ni mmiliki wa New Habari Corp., hayo magazeti mengine ni kwamba aidha ana hisa kiasi fulani ama amenunua wahariri wa hayo magazeti na ndiyo maana hawezi kutoa command kwa kuwa Mhariri hayuko responsible kwa RA peke yake bali yuko responsible kwa wenye hisa wote na hivyo lazima kuwe na maelezo ya kina na siyo kutoa amri peke yake. Kwa hiyo hapo bado sijaona HEKIMA. Nadhani kama ingekuwa ni gazeti la Mtanzania pekee ndiyo limeripoti habari hiyo wala watu wasingeshangaa sana au kujiuliza maswali, lakini magazeti manne yanaporipoti tukio lile lile na same wording lazima mtu uende ana extra mile ili ujue kulikoni?

Sidhani kama kikao cha siri kinaweza kuwa recorded na ndiyo maana kinaitwa ni kikao cha siri. Lakini siri ya kikao inaweza kuvuja, kwani hao wahariri wakiitwa hawaagi kwamba wanakwenda wapi? Na wakitoka huko hawasemi walikuwa wapi na walikuwa wanafanya nini? Siri zinavuja kwa kuwa kuna mambo ambayo yanapofanyika lazima watu wengine wahusike. Habari ikitumwa na mwandishi haipokelewi na Mhariri, na lazima waandishi wengine wajiulize kulikoni habari hii itoke kwa mwandishi huyu wakati gazeti lina mwakilishi wake?
 
Wahariri kuchunguza waandishi walioripoti msiba wa Wangwe
Na Kizitto Noya

UTATA wa kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe bado, umezidi kutanda baada ya Jukwaa la Wahariri Tanzania, kuunda tume kwa ajili ya kuchunguza matukio kadhaa yaliyojitokeza kabla na baada ya mazishi.


Wahariri hao walifikia uamuzi huo jana katika mkutano wao uliofanyika jijini Dar es Salaam baada ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuvilalamikia baadhi ya vyombo vya habari kwamba vilipotosha umma katika kuripoti msiba wa Wangwe kwa kueleza kuwa ulitawaliwa na vurugu zilizohatarisha maisha ya viongozi wa chama hicho.


Naibu Katibu Mkuu Chadema, Zitto Kabwe alisema katika mkutano huo kuwa vyombo hivyo vya habari (sio vya kampuni ya Mwananchi Communications), vilitumika vibaya na wanasiasa kuiua Chadema na kumchafua Mwenyekiti wake Freeman Mbowe.


"Suala hilo sio dogo, tumeshtushwa sana na ripoti ya Tarime kabla na baada ya mazishi na tunaamini kwamba taarifa hizo zilikuwa na lengo la kuua Chadema na kumchafua mwenyekiti wake," alisema Zitto kwa hisia kali na kuongeza:


"Sitaki kusema mliandika uongo kwa sababu neno hilo ni kali sana lakini mlichoripoti sio cha kweli. Sisi (Chadema) tuna mkanda wa video wa matukio yote unaoonyesha ukweli lakini kama kuna mtu mwenye mkanda mwingine alete tulinganishe,"


Awali, akisoma baadhi ya magazeti, Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Sakina Datoo alionyesha kushangazwa na jinsi taarifa hiyo ilivyoripotiwa kwani iliandikwa na magazeti manne tofauti ikiwa ifanana neno kwa neno.


Sakina alihoji sababu za kufanana hivyo na usahihi wa kilichoandikwa na kuwataka wahariri kutoa maoni yao jinsi ya kubaini ukweli wa suala zima na sababu za maandishi hayo kufanana.


Wakichangia hoja hiyo wahariri hao walishindwa kupinga wala kukubali hoja ya Chadema kwamba haikutendewa haki badala yake walishauri kuundwa tume itakayochunguza suala hilo kabla ya katoa tamko lake.


"Editors Furum ifanye uchunguzi wa kina kabla ya kujiingiza kwenye mgogoro huo na kutoa tamko, iunde tume kuchunguza vyanzo mbalimbali vya habari na kubaini ukweli," alisema Said Kubenea Mhariri na Mmiliki wa magazeti ya Mwanahalisi na Mseto.


Kauli ya Kubenea iliungwa mkono na Mhariri wa gazeti la Majira, Joseph Kulangwa aliyeonyesha wasiwasi juu ya madai ya Chadema kwa kuitaka ieleze sababu za Mbowe kutohudhuria mazishi ya Wangwe kama sio kwa sababu za vurugu hizo.


"Mimi naunga mkono hoja kwani Chadema inaweza kuelezaje sababu za Mbowe kutohudhuria mazishi? Pili mimi nimekaa Tarime, ni kawaida kabisa kwa Wakurya kwenda msibani wakiwa na zana hizo hivyo kwa waandishi ambao hawalifahamu hilo lazima hisia ziwapeleke huko," alisema.


Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya The Guardian, Kiondo Mshana alisema haamini kwamba waandishi wa habari wameanza kutumika vibaya kwa maslahi ya wasiasa na kuunga mkono kwamba suala hilo lina utata unaohitaji uchunguzi na tamko la jukwaa la Wahariri.


Katika maelezo yake, Zitto alisema Chadema ina ushahidi kutoka vyanzo mbalaimbali kwamba vyombo hivyo vya habari vilitumiwa na wanasiasa kukichafua Chadema na kuleta mgogoro ndani ya chama hicho na kuonya kuwa tabia hiyo inahatarisha usalama wa taifa.


"Chadema hatutoi 'demand notice' kwa chombo chochote isipokuwa niseme tu kwa TBC1 ambayo inaendeshwa kwa kodi zetu suala hilo sitalikalia kimya, nitadeal nao ipasavyo kwani walichochea na kuligawa taifa wakati wa mazishi ya Wangwe," alisema na kueleza kuwa atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia suala hilo baadaye.

Source: Mwananchi
 
YournameisMINE YournameisMINE is hakuna matata
JF Senior Expert Member

Re: Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake


1.
Quote:Originally Posted by Mtanzania

Mkuu FMES,

Nimecheka kweli kweli hiyo ya Kolimba. Naamini hapa tuna madaktari, si ajabu na wao wanacheka kama mimi. Sikujua siku hizi kuna dawa ya ugonjwa wa moyo inafanya kazi kama dawa ya kisukari kwi kwi kwi!!!!!Huu mjadala mimi nimejitoa kuchangia, ila hii ya mbeba dawa pembeni imenichekesha mno, sikuweza kujizuia tena.

Zipo mkuu, mfano buccal NTG for angina pectoris ina kick within 2 minutes..........

Inategemea mtu ana aina gani ya cardiac issues na dawa gani anayotumia mfano Calcium blockers (cardizem), beta blockers (atenolol) n.k OPD yake ni tofauti...lakini hapa ninapoishi protocol ya "code blue" ya li impending or actual infarct ni "MONA" from MONALISA na hiyo N inasimama kwa Nitroglycerin ambayo kama nilivyosema huko juu depending na application inaweza kukick within 2 min na kuokoa maisha........LOL

hiyo ni kwenye "nutshell" ki-layman...

kwahiyo mkulu FMES hakuwa kachekesha.... na yapo madawa mengine kedekede ya kimarekani yanafanya kazi chapchap hasa kwa ER!! kama unashida sana ni PM (lakini kuna fees ina apply) bwahahahahahahaha.

tuwe tunajaribu ku-research kidogo kabla ya kudhalilisha au kujidhalilisha....na hiyo ndio kisa cha Wangwe (RIP), anasema kweli watu wanamgeuza kichekesho na kumpandikizia uadui usio na maana...kwani ni uongo kwamba mapesa mengi yanaishia HQ ya chadema? kwani ni uongo kwamba wabunge wengi wa kuteuliwa wa chadema aidha ni wachagga au wananasaba za kichagga..........tuwe makini sana na kuacha maushabiki yasio ya lazima.

wkend njema!!.

Mkuu YNMSN,

Heshima mbele sana mkuu kwa kuiweka hii sawa, mimi mkuu kwenye medicine sina idea kabisa, kwa mfano nina mshikaji wangu mmoja wa karibu sana, ambaye ninapokuwa naye, ninajua kuwa anakuwa na kidude flani hivi kama yeye anakiita pump, anakuwa nacho mfukoni na kingine kwenye gari kwa hiyo nikiwa naye ninajua kuwa mara kwa mara hupatwa na ugonjwa mmoja hivi na kama hakukiwahi kile kijitu na kujipulizia mdomoni basi ana-pass out mara moja, kwa hiyo akichelewa tu basi ninakitafuta ninampulizia mdomoni anapata fahamu tena, sasa guess what ukiniuliza leo anaumwa nini sijui na wala sijawahi kumuuliza, na hata kile kijitu sijui kinaitwa nini zaidi tu ya pump!

Kwa hiyo hata hii ya Kolimba ndio maana sikuuliza sana ni ugonjwa gani lakini ni viongozi na watu wengi sana waliokuwa karibu na Kolimba walithibitisha kuhusu hii ya mtoto wake na dawa, anyways ninashukuru kwa kuiweka sawa hii ndio uzuri wa JF siku zote wapo watu wanaoelewa ishus, saafi sana.

Ahsante Mkuu!
 
Nafikiri ni inhaler hiyo!

Zipo dawa nyingi ambazo zinahitaji kuzila mara kwa mara, ukiacha kula umekwenda na maji, na sitashangaa kama hivi ndivyo ilivyokuwa kwa Kolimba. Hata hivyo huyu mtoto wake na yeye mwenyewe walikuwa wazembe kidogo kukubali kuingia kwenye kikao bila hizo dawa na kukubali huyu kijana asiingie kama kweli ndiye alikuwa anashikilia uhai wake!
 
Mkama,

Mfano wako wa magazeti kudesa ninaweza kukubaliana na wewe kama gazeti husika ama chombo cha habari kilichoripoti ni cha nje na baadaye gazeti la Tanzania likaripoti habari ile ile. Lakini siyo udesaji kutoka kwenye gazeti la hapa hapa na tena kwa tukio lile lile ambalo kila gazeti limepeleka mwandishi wake.

Unawezaje kudesa habari ambayo haijatoka gazetini? Vyumba vya habari vya magazeti ya Majira na Mtanzania viko mbali mbali. Kimoja kiko Mjini na kingine kiko Sinza, walideseana saa ngapi kiasi kwamba asubuhi magazeti yote yawe na habari zinazofanana?

Kumbuka kuna wahariri wa habari ambao huzipitia habari zote kabla hazijachapwa, na pia kuna wahariri wakuu ambao pia hupitia habari hizo hizo zote ama gazeti lote kwa ujumla. Ina maana na hao wahariri walideseana na wao walikubali kwamba Mwenyekiti wa NCCR ni Joseph Mbatia? Hii ni aibu kubwa sana!

Hata kama ni kudesa huwa watu wanadesa kwa akili japo unabadilisha hata wording. Lakini habari hiyo Sakina Datoo anasema ni neno kwa neno!

HEKIMA uliyosema mtu anaweza kuitumia sijaiona. RA ni mmiliki wa New Habari Corp., hayo magazeti mengine ni kwamba aidha ana hisa kiasi fulani ama amenunua wahariri wa hayo magazeti na ndiyo maana hawezi kutoa command kwa kuwa Mhariri hayuko responsible kwa RA peke yake bali yuko responsible kwa wenye hisa wote na hivyo lazima kuwe na maelezo ya kina na siyo kutoa amri peke yake. Kwa hiyo hapo bado sijaona HEKIMA. Nadhani kama ingekuwa ni gazeti la Mtanzania pekee ndiyo limeripoti habari hiyo wala watu wasingeshangaa sana au kujiuliza maswali, lakini magazeti manne yanaporipoti tukio lile lile na same wording lazima mtu uende ana extra mile ili ujue kulikoni?

Sidhani kama kikao cha siri kinaweza kuwa recorded na ndiyo maana kinaitwa ni kikao cha siri. Lakini siri ya kikao inaweza kuvuja, kwani hao wahariri wakiitwa hawaagi kwamba wanakwenda wapi? Na wakitoka huko hawasemi walikuwa wapi na walikuwa wanafanya nini? Siri zinavuja kwa kuwa kuna mambo ambayo yanapofanyika lazima watu wengine wahusike. Habari ikitumwa na mwandishi haipokelewi na Mhariri, na lazima waandishi wengine wajiulize kulikoni habari hii itoke kwa mwandishi huyu wakati gazeti lina mwakilishi wake?


Mkuu vipi tena
Unaongelea Sinza ni mbali yani unasahau kabisa wewe na mimi tunaongea live tena tukiwa umbali wa maelfu ya mail.INTERESTING sana.

Wewe unasema kudesa wakati watu wana desa mstari kwa mstari na wanakusanya pepa hiyo kwa PROF mmoja.

Mhariri wa gazeti anapohariri gazeti anakua hana magazeti mengine ya kufaninasha na kubaina ,umenipata.

Hawa waandishi wahabari mara nyingi wamekua wakifanya hivyo kama umekua makini toka siku nyingi wenda hua wanabana posho na wanawakilishwa na mmoja wao kazi yake ni KUDESA.

Tuseme basi RA kawanunua na huko kuna maana waandishi wetu hawana elimu.Sasa hapo nani mnafiki Mnafiki ni BAADHI ya MEMBER wa JF.
SERIKALI imeshasema waandishi hawana taaluma waende shule WATU humu JF minafiki ya kutupwa yaja juuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu .Hao hao waandishi wameleta habari feki hiyoo hiyo minafikiiii yaja juuuuuuuuu tena Hawa waandishi hawana elimu wala taaluma eti hata Habari washindwa badirisha,
Eti Ndg yangu KEIL mnafiki mkubwa ni nani?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom