Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 98,011
- 142,701
Mimi siku hizi mbona siipati kabisa KLH News? Kulikoni....nimepewa indefinite ban nini? I miss podomatic...ile ilikuwa haina mizengwe....
Hold on a minute... huyu kijana alihusika na ajali nyingine nairobi (sources zinasema hivyo) ambapo gari ilichakaa nyang'anyang'a hadi kulazimu kukatwa ili kumtoa; hata hivyo alitoka mzima kama alivyotoka kwenye hii nyingine. Just that you should know.
Hivi Hizi Romours Kuwa Marehe Chacha Wangwe Amekuwa Murdered Zinatoka Wapi Na What Is The Reason Behind People To Speculate Like That, Sielewi Kwa Nini Watu Wanashindwa Kuamini Kuwa Ajili Huwa Zinatokea Na Baadhi Ya Watu Wanapona Na Wengine Kupoteza Maisha!
Siku Hizi Kumekua Na Hulka Mtu Yoyote Maarufu Akifariki Kunakuwa Na Rumours Nyingi Juu Ya Kifo Chake, Jamaa Ya Watanzania Imeanza Kujengwa Na Hofu Na Kutoaminiana, Kitu Ambacho Kinaweza Kuleta Maafa Makubwa Sana.
Tafadhali Wana Forum Wenzangu Naomba Ufafanuzi Wa Kina Kwa Wale Wote Wanao Speculate Kuwa The Guy Was Assassinated Or Something?
Let Us Be Realist!
Basi mwenzetu huyu ana upendeleo maalumu kutoka kwa "Bwana"!
Hold on a minute... huyu kijana alihusika na ajali nyingine nairobi (sources zinasema hivyo) ambapo gari ilichakaa nyang'anyang'a hadi kulazimu kukatwa ili kumtoa; hata hivyo alitoka mzima kama alivyotoka kwenye hii nyingine. Just that you should know.
watu Huwa Wanauawa Kimitindo, Executive, Na Ku Speculate Sio Vibaya.
The Thing Is, Nadharia Zilizoletwa So Far - Tlp Na Nccr Wameua Ili Wapate Kiti, Au Ccm Wameua Ili Kuwagombanisha Chadema, N.k - Zote Ni, Well, Ngoja Nisema Tu Nyepesi Nyepesi, Japo Kuna Namna Sahihi Zaidi Ya Kuzi Describe Kwa Jinsi Ambayo Inaweza Kuwakatisha Watu Tamaa Wakaacha Kujaribu Kuleta Nadharia Nyingine Na Shinikizo Kwa Officials, Halafu Tukazika Marehemu Kumbe Ana Risasi Kichwani.
Hatimaye Chacha Wangwe azikwa kwao Tarime
Frederick Katulanda, Tarime
Mbunge wa Tarime (Chadema), Chacha Wangwe ambaye kifo chake kimezua utatanishi, hatimaye amezikwa jana kwenye makaburi ya kijijini kwao Kimakorere baada ya familia kuridhika na uchunguzi uliofanyika na daktari wao.
Wangwe alizikwa jana majira ya saa 12:00 jioni huku kukiwa na hali tata, wakati baadhi ya ndugu wakigoma na wengine kukubali.
Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa nchini ambao pia walikuwapo katika uchunguzi uliofanyika kabla.
Akizungumza kabla ya mazishi kwa niaba ya familia muda mfupi baada ya kutoka ndani ya chumba cha uchunguzi, Prof Samwel Wangwe alisema jana kuwa uchunguzi walioutaka familia umekamilika na kwamba sasa wameridhika kuwa mbunge huyo alikufa kwa ajali na si vinginevyo.
Prof Wangwe alisema kutokana na kuridhika na uchunguzi huo, sasa wameamua kufanya mazishi ya marehemu huyo nyumbani kwake na kusema kuwa taarifa kamili itatolewa na daktari baada ya kukamilika na kukabidhiwa jeshi la polisi.
"Baada ya uzushi mwingi tuliamua kama familia kufanya uchunguzi ambao umefanyika leo. Ingawa taarifa kamili itaandikwa na daktari sisi tunasema tumeridhika kuwa marehemu alikufa kwa ajali na sasa tunakwenda kuzika," alieleza.
Uchunguzi huo ambao ulifanywa katika hospitali ya Wilaya ya Tarime kuanzia saa 5: 27 hadi 9:40, ulimuhusisha daktari wa serikali Charles Shija kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara, maofisa wa Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa, Mbunge Zitto Kabwe kwa niaba ya Chadema na daktari wa familia ambaye mpaka sasa familia imesema haitamtangaza.
Hata hivyo Zitto alichelewa kufika hospitali na kukuta uchunguzi umeanza lakini baadaye aliruhusiwa kuingia baada ya kuruhusiwa na maofisa wa Jeshi la Polisi.
Majira ya saa 9: 42 Zito alikuwa wa kwanza kutoka ndani ya chumba hicho na kuzungumza na waandishi wa habari kuwa kwa niaba ya chama chake kwamba ameridhika na uchunguzi huo.
"Mimi kwa niaba ya chama changu ambacho nilikuwa nawakilisha, nimeridhika na uchunguzi huo" alisema Zitto.
Awali Samson Chacha toka Tarime aliripoti kuwa baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani walijikusanya katika hospitali hiyo wakisubiria taarifa ya uchunguzi wa mwili wa marehemu Wangwe.
Waliokuwapo ni Augustino Mrema wa TLP, Joseph Mbatia wa NCCR-Mageuzi, Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF, ambao walisema hawawezi kuondoka kabla ya mazishi ya mpiganaji mwenzao huyo.
Profesa Lipumba aliwaomba wananchi na wafiwa kuwa na msikamamo wasiyumbishwe na baadhi ya wanasiasa wanaotaka kusambaratisha vyama vya upinzani kupitia kifo cha shujaa huyo kwani ukweli utabainika tu.
Haya ma- Spin Doctor tuleteeni spinning nyingine ...
Masatu, kwanini unafikiri kwa sababu haikuonekana risasi basi kifo cha Wangwe ni cha kawaida na ajali yake ni ya kawaida? Walichochunguza kwenye mweli ni ajali na wakaweza kuielezea kuwa ni ya kawaida; au walikuwa wanachunguza nini?
Kwa sababu ninaamini aliyeleta hoja ya "risasi" kuwa kapigwa risasi amefanikiwa kuyumbusha mjadala kwa sababu kama walijua hakuna risasi, basi watu wataamini kuwa hakuuawa kwa risasi; je waliangalia sumu? je waliangalia ajali yenyewe ilivyotokea? Je kutokukuta risasi ina maana hakuuawa?
No sir, walichojaribu ni kuspin mjadala tu, lakini kesho tunawarudishia wao squarely.
Masatu, kwanini unafikiri kwa sababu haikuonekana risasi basi kifo cha Wangwe ni cha kawaida na ajali yake ni ya kawaida? Walichochunguza kwenye mweli ni ajali na wakaweza kuielezea kuwa ni ya kawaida; au walikuwa wanachunguza nini?
Kwa sababu ninaamini aliyeleta hoja ya "risasi" kuwa kapigwa risasi amefanikiwa kuyumbusha mjadala kwa sababu kama walijua hakuna risasi, basi watu wataamini kuwa hakuuawa kwa risasi; je waliangalia sumu? je waliangalia ajali yenyewe ilivyotokea? Je kutokukuta risasi ina maana hakuuawa?
No sir, walichojaribu ni kuspin mjadala tu, lakini kesho tunawarudishia wao squarely.
Hapa tunawaletea dondoo chache za siku ya kifo chake ambayo ni Jumatatu, Julai 28, 2008, ambacho kimsingi kimeacha maswali mengi kuliko majibu.
Saa 12 asubuhi
Anaamka na kutaka kwenda kuoga lakini anashindwa, hivyo inawalazimu watoto wake kumpelekea maji bafuni. Hii ni kutokana na hali yake kutokuwa nzuri kwa muda wa siku tatu.
Saa 2:10
Wangwe anaingia katika Jengo la Bunge na kumuuliza Naibu Spika, Anna Makinda kama atapata nafasi ya kuwasilisha hoja yake binafsi. Makinda anamuomba amsubiri Spika wa Bunge, Samuel Sitta kwani yeye ndiye anayeweza kumpa muda wa kuwasilisha.
Saa 8 mchana
Anarudi katika makazi yake Dodoma na kumwambia mtoto wake Zakaria Chacha (18) kwamba ameshindwa kuwasilisha hoja yake binafsi, hivyo ameamua kusitisha ili aweze kuendelea na shughuli nyingine.
Mwanaye anampa maji anakunywa lakini hayamezi, ikabidi achukue vidonge na kumnywesha, alimeza kisha akala matunda na kuamua kwenda kulala huku akitaka aamshwe majira ya jioni.
Saa 11 jioni
Anaamshwa na kuiambia familia yake anakwenda Dar es Salaam kwenye mazishi ya Bhoke Munanka.
Saa 12 jioni
Anaanza safari ya kwenda Dar es Salaam akifuatana na rafiki yake Deus Mallya, lakini wakati yuko safarini maofisa wa Bunge wanahaha kumsaka katika eneo lote la Bunge ili aje awasilishe hoja yake binafsi lakini jitihada za kumpata zinashindikana.
Saa 12.10 jioni
Anaipigia simu familia yake na kuwaambia analazimika kurejea Dodoma kwani walipofika eneo la Ihumwa gari yao ilipata matatizo hivyo inabidi arudi mjini ili kulipeleka gereji liweze kutengenezwa.
Saa 12.30 jioni
Baada ya gari lao kutengemaa anapitia nyumbani kwake ili kuchukua chaja ya simu aliyokuwa ameisahau, huku gari likiwa linaendeshwa na rafiki yake.
Saa 1 usiku
Safari ya kuelekea Dar es Salaam ikaanza, huku akipanga kulala Morogoro mjini kwani alihofu wataingia usiku sana ili kesho yake alfajiri waanze tena safari ya kuelekea jijini humo.
Saa 2.55 usiku
Chacha Wangwe anafariki baada ya gari linalodaiwa alikuwa akiliendesha kupinduka zaidi ya mara tano ikiwa ni baada ya kuserereka umbali wa mita 50 kutoka barabarani.
Mkuu rekebisha kauli yake hakuna mahala nimesema nafikiri kwa kuwa hawakuona risasi then hajauawa.
Nimeweka bandiko hapo juu linalo wakariri msemaji wa familia Prof Wangwe na mwakilishi wa Chadema Mh Zitto wakisema kutokana na uchunguzi "wanaridhika" kuwa amekufa kwa ajali ya kawaida na si vinginevyo!
Ni vizuri kuanzia sasa kuja na sera inayokataza uchunguzi wa vifo vyenye utata. Tukubali yaishe.
Kama kuna wakati ambapo uchunguzi huru kweli unahitajika ni kwenye hiki kifo cha Mhe. Wangwe. Hakuna kitu kitakachosemwa na serikali au taasisi ambacho watu watakikumbatia na kukubali na bila ya shaka vitakavyosemwa na familia au jamaa zake na Chadema nacho kitakuwa na utata. Nimeandika kwa urefu "utata" huo kwenye gazeti la kesho, na kwa makini sijahusisha suala la risasi hata kidogo kwa sababu siamini kuwa ilikuwa ni risasi. Walipogeuza kuwa ni suala la risasi wamebadilisha mjadala kabisa kwa sababu kwa makosa watu wanaweza kuhitimisha kuwa "no bullet, no assassination" kitu ambacho kinaweza kuwa kosa kubwa sana.
Suala la madai ya kifo cha risasi ni kupoteza lengo sana; Tangu juzi nimeitisha kuwa kuna haja ya Kikosi cha Scotland Yard kuitwa kufanya uchunguzi huru kwani uchunguzi wa serikali si huru na ule wa familia si huru kwani vyote viwili vimeangalia mwili kitu ambacho kinafanywa katika ajali nyingi.
Suala zima ni mazingira ya safari na ajali yenyewe kwani kufanya kitu kibaya kwa mtu siyo lazima utumie risasi.
Kuhusisha kifo hiki na CCM au Chadema ni kosa kubwa na kwa yeyote anayesoma maandishi yangu sijaelekeza tuhuma kwa Chama chochote kile au mtu isipokuwa kuonesha utata uliopo na ya kuwa ufunguo wa utata huo Malya na ushahidi uliopo.
Naamini kama wabunge wa CCM na wa Upinzani na viongozi wao wakiungana kuitisha NSY waje kufanya uchunguzi kama walivyoitwa kwenye kifo cha Ouko, Bhutto, au hivi karibuni huko Antigua naamini ndio njia pekee ya kuonesha ukweli na kuondoa utata.
Yule ambaye hatotaka NSY kuja na kupewa ushirikiano wote mara moja; huyu ndiye nitamshuku. Sasa nani atakuwa wa kwanza kuitisha kwa NSY na hana kitu cha kuficha na yuko tayari NSY kufanya uchunguzi wote na yeye kutoa ushirikiano wote?
Miye nasema tuitishe NSY kama hakuna cha kufichwa na ni kweli na tukubaliane lolote watakalosema lifunge mjadala au lianze criminal procedure. Vinginevyo tukubali tu yaishe, tusubiri mwingine aondoke kwa ajali ya baiskeli.