Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Katika Tanzania nimejifunza kitu kimoja nacho ni matapeli/mafisadi ni wa kuogopa sana. Migogoro ilipo anza Chadema wengi wetu waligawanyika sana. Na baadhi ya watu tuliowaamini sana hata hapa JF walikuwa hawaoni tena mbali. Wakati nipo JKT waliniambia kwamba wakati unasonga mbele ni vizuri kujua adui wako vizuri na anatumia mbinu gani.

Watanzania wanapigana hawajui maadui wanatumia mbinu gani. Na hilo tutaedelea kulalamika milele. Kuna watu ambao leo wanapigana lakini adui akitokea nyuma yao wanaweza kuweka maswali kwamba huyo si adui bali ni mwenzao tu. Kwa haya Jmushi anayesema hana haja tena na bongo na mimi namsapoti kwa kusema tumepoteza nchi, anayekubalina na mimi akubali asiyekubali na aendelee kuamini.

Tumeanzia ujambazi, tukaenda UFISADI tumekuja na watu wa madini na hawa wote ni watu ambao wana pesa. Haijalishi wewe uko wapi hawa watu wanaweza hata kubadili aliye rafiki yako leo akawa adui yako kesho(kuwa makini na hili). Ni kuomba tu maana mimi kuna hata baadhi ya watu hapa hapa JF sihamini kama mawazo waliyokuwa wakitoa kama kweli ni mawazo huru.

Bado wengine wakati mwingine huwa tunasoma mawazo ya watu lakini kupoteza watu huwa pia tunaona. Atakayetaka kuona spin angalia mawazo yaliyotolewa hata na watu tunaowajua sana. Huwezi kuwa unapigana na adui na wakati huo huo hauwezi kujua adui atatokea wapi au atatumia mbinu gani.

Ukisikiliza vizuri taarifa ya habari ya TBC1 ya jana huna haja ya kujua walikuwa wanasema nini na huna haja ya kujua walitumiwa katika hii issue.

Suala linakuja huyo aliye weza kuandaa waandishi mpaka wakafika TARIME, TBC1, JF(maamuruki) nk alitoka wapi na hiyo kazi ilifanyika lini? Je alijua Kuna mtu atakufa?

Nafikiri ukisikiliza taarifa/magazeti mbali mbali nategemea watu wafungue kesi nyingi maana ushahidi upo kuwa hizo information hakuna mtu ambaye ni mataaluma anaweza kuzitoa. Anyway hiyo inaweza kufanyika tu tanzania mabayo inaelekea kupoteza mwelekeo.

Mwisho Tanzania yetu ya amani na utulivu itatoweka kama hatutaweza kusimama na sheria zetu na kuwa na viongozi wanaoweza kusimamia sheria kikamilifu.
 
Kuanzia mwanzo wa mjadala wa tukio hili la Wangwe nimejaribu kuonesha clues kadhaa (tatu hadi sasa) kati ya sita hivi. Kutokana na udadisi wangu tangu muda mfupi baada ya kupata habari ya msiba nimeamini kwa moyo wote kuwa suala hili siyo la CCM na Chadema tu bali lina maslahi makubwa sana ya Taifa. Hivyo kuna clues chache ambazo naamini zinahiji kuangaliwa kwa karibu ili hatimaye kuleta sense kwenye mambo kadha wa kadha.

Mengine nimeyaandika kwa kirefu kwenye gazeti kesho nikito msaada kwa Polisi baada ya kuombwa kufanya hivyo na Manumba. Aliomba wale wenye kuona utata basi wasaidie Polisi kuonesha utata huo. Katika makala hiyo sikujaribu kuelekeza kidole mahali popote au kwa mtu yeyote isipokuwa kuwaambia mkijibu maswali haya mtajua ni ajali ya kawaida au la. Hivyo clue zilizosalia:

(za kwanza, ni muda, gari, mwili);

4: Simu ya kwanza na simu ya mwisho

. Ni nani ambaye Bw. Mallya alimpigia simu kwanza. Bahati mbaya sidhani tunaweza kupata jibu la swali hili hasa baada ya SIM card kutolewa kwenye simu ya huyo kijana. Siamini kama hadi hivi sasa kuna uwezekano wa kupata taarifa za simu hiyo. Uchunguzi wa upande wangu unaonesha pasipo shaka kuwa watu wa kwanza kupigiwa simu hawakuwa Chadema na hawakuwa watu tu wa CCM; bali mtu fulani mahsusi. Huyo mtu ndiye ambaye anaufunguo wa kuunganishwa kati ya yeye na Malya.

Je yawezekana mtu wa mwisho kupigiga simu kwa malya/chacha ndiye alikuwa mtu wa kwanza kupigiwa simu? Na baadaye ni nani wengine waliopigiwa simu na Malya eneo la ajali kujulishwa kuhusu msiba?

5. Fedha
Wengi wetu wamekubali kuwa Chacha alirudi (baada ya kuanza safari) nyumbani kuchukua Charger baada ya gari kuharibika/kufanyiwa matengenezo. Je alikuwa anataka charger ya nini wakati Deus alikuwa na simu na walikuwa wanalala tu Morogoro kuwahi msiba Dar, na angeweza kupata charger eneo lolote Dar?

Je yawezekana kuwa aidha alirudi nyumbani kuleta fedha/ kuchukua fedha. Sentensi inayofuatia nitaiandika taratibu sana na uisome hivyo; Kulikuwa na jaribio la kumshawishi Wangwe asilete hoja yake na ushawishi huo ulifanywa kwa fedha na kuna zaidi ya mtu mmoja anayejua juu ya hilo na walimsihi Wangwe asifanye hivyo. Hata hivyo (sijui kama hela zilichukuliwa au la) lakini vyovyote ilivyokuwa Wangwe alikuwa afanye anachotaka kufanya (kuleta hoja).

6. Hoja ya Wangwe:
Hii inatokana na hicho hapo juu (namba tano); Wangwe alikuwa amepanga baod kuwasilisha hoja yake lakini kwa sababu fulani hakuweza kufanya hivyo hata walipomtafuta siku hiyo. Je, aliyekuwa anamtafuta Wangwe alijua kuwa Wangwe hayupo Dodoma na ameshaondoka na hiyo kutumika kama geresha? Kama Wangwe alikuwapo Dodoma kutwa nzima, na kushindwa kupata muda wa kuwasilisha hoja yake kwa Spika ilikuwaje nafasi imefunguka baada ya yeye kuondoka?

Baadhi ya kinachohisiwa na ka "nzi" ni kuwa sehemu ya hoja hiyo inahusiana na madini kule Tarime.

Hii hoja ya nini na nani ananakala yake? Jibu la swali hili ni jepesi. Hoja ya Wangwe imepotea. (Haikuwasilishwa kwa Spika) na nyaraka na mabegi vimeibwa eneo la ajali. Na hivyo ni almost impossible kupata nakala hiyo isipokuwa kama kuna mtu atajitokeza na kusema anayo nakala. Je kiongozi wa kambi ya upinzani alikuwa na nakala; je kiongozi mwingine wa Chadema ana nakala? (sidhani) Hata hivyo sitoshituka kama nakala hiyo itakuja kupatikana baada ya siku kadhaa hivi. You can guess why na haitatolewa na watu wa Chadema; labda familia wanayo nakala nyingine nyumbani.

Ukiyasoma haya yote, ongeza na yatakayotoka kesho; na utakubaliana na mimi kuwa suala la "risasi" it was a waste of time, but a deliberate diversion ya watu and resources toka Dodoma kwenda Tarime na hivyo kununua muda kitu ambacho kilikuwa ni muhimu sana na kinachohitajika kuliko kurundikana Tarime. Wakati wao wanaenda Tarime, vya kutengenezwa vimetengenezwa, vya kusafishwa vimesafishwa, na wa kufundishwa amefundishwa.
 
Naona wakuu wemgi mmeanza kukata tamaa na ukweli kupatikana, lakini msisahau kuwa uchunguzi wa ishu ngumu kama hii, hauwezi kukamilika in one day, na siamini kuwa the truth, yaani nothing but the truth, ungeweza kupatikana kutoka kwenye huu mkoroganyo unaoendelea huko Tarime, kati ya serikali na Familia ya marehemu,

Pamoja na minong'ono mingi na theory nyingi zilizokwisha tolewa tayari kuhusiana na hiki kifo, na ambazo zote zimefuatiliwa kwa makini na kina, bado tunaifutilia kwa makini zaidi, theory inayoongoza kuelekea kwenye kampuni ya madini ya Barrick, kwa kushirikiana na kikundi cha baadhi ya viongozi/kiongozi mmoja wa taifa,

Inaonekana kuwa na uzito sana, kwa sababu pamoja na kwamba ni ndefu sana nitaiweka kwa ufupi tu, habari zinasema kuwa marehemu, alishwakilisha hoja yake nzito kwa Spika, against Barrick ambayo alikuwa akisubiri tu kuiweka wazi kwenye kikao cha bunge, Barrick katika kipindi cha miezi michache iliyopita wamekuwa wakijihusisha sana na local politics katika kujaribu kuuzima mjadala wa kamati ya madini, ambao in private Marehemu, alikuwa ameuvalia njuga sana kuusimamia tena kwa nguvu sana, sasa kinachoshitua sana ni kwamba ukiwauliza wnaohusika kuhusu hii theory wanashituka sana, sasa swali lnakuwa Why?

Sasa ninarudia tena kuwa uchunguzi wa ishu nzito kama hii hauwezi kufanyika kwa siku moja, wengi inaonekana kuwa tulitegemea a knockout punch kutokana na uchunguzi wa mtaalamu wa mwili wa marehemu, sasa kitendo cha serikali kukataa kutoa ruhusa kufanyika, peke yake kinaonyesha kuwa aliyefanya uchunguzi huu ni yule anyekubalika na serikali, sasa huu haukuwa uchunguzi independent kuna some ubabaishaji hapa na matokeo,

Kwa wale mliokta tamaa sawa ni haki yenu, lakini kuna sisi wengine bado tunaendelea na uchunguzi mpaka tuone mwisho wake unakuwaje, ukweli na uongo uko wapi, na tutausema wazi hapa JF, kwa sababu mafisadi wanaweza kulala usingizi mzuri sana kusikia kuwa tumekata tamaa, hasa hapa JF among all the places, ninasema katika vita hii na mafisadi, ni lazima tuwe tayari kwenda nao hata kama ni mabli kidogo kuliko inavyotegmewa, kwa sababu tuki-give up kirahisi namna hii tunakuwa tunawapa nguvu ya kuamini kuwa next time itakuwa hivi hivi, hapana mimi ninasema kuwa bado tunaendelea na uchunguzi, hii ishu ni bado kabisaa!

Ahsante Wakuu
 
Naona wakuu wemgi mmeanza kukata tamaa na ukweli kupatikana, lakini msisahau kuwa uchunguzi wa ishu ngumu kama hii, hauwezi kukamilika in one day, na siamini kuwa the truth, yaani nothing but the truth, ungeweza kupatikana kutoka kwenye huu mkoroganyo unaoendelea huko Tarime, kati ya serikali na Familia ya marehemu,

Pamoja na minong'ono mingi na theory nyingi zilizokwisha tolewa tayari kuhusiana na hiki kifo, na ambazo zote zimefuatiliwa kwa makini na kina, bado tunaifutilia kwa makini zaidi, theory inayoongoza kuelekea kwenye kampuni ya madini ya Barrick, kwa kushirikiana na kikundi cha baadhi ya viongozi/kiongozi mmoja wa taifa,

Inaonekana kuwa na uzito sana, kwa sababu pamoja na kwamba ni ndefu sana nitaiweka kwa ufupi tu, habari zinasema kuwa marehemu, alishwakilisha hoja yake nzito kwa Spika, against Barrick ambayo alikuwa akisubiri tu kuiweka wazi kwenye kikao cha bunge, Barrick katika kipindi cha miezi michache iliyopita wamekuwa wakijihusisha sana na local politics katika kujaribu kuuzima mjadala wa kamati ya madini, ambao in private Marehemu, alikuwa ameuvalia njuga sana kuusimamia tena kwa nguvu sana, sasa kinachoshitua sana ni kwamba ukiwauliza wnaohusika kuhusu hii theory wanashituka sana, sasa swali lnakuwa Why?

Sasa ninarudia tena kuwa uchunguzi wa ishu nzito kama hii hauwezi kufanyika kwa siku moja, wengi inaonekana kuwa tulitegemea a knockout punch kutokana na uchunguzi wa mtaalamu wa mwili wa marehemu, sasa kitendo cha serikali kukataa kutoa ruhusa kufanyika, peke yake kinaonyesha kuwa aliyefanya uchunguzi huu ni yule anyekubalika na serikali, sasa huu haukuwa uchunguzi independent kuna some ubabaishaji hapa na matokeo,

Kwa wale mliokta tamaa sawa ni haki yenu, lakini kuna sisi wengine bado tunaendelea na uchunguzi mpaka tuone mwisho wake unakuwaje, ukweli na uongo uko wapi, na tutausema wazi hapa JF, kwa sababu mafisadi wanaweza kulala usingizi mzuri sana kusikia kuwa tumekata tamaa, hasa hapa JF among all the places, ninasema katika vita hii na mafisadi, ni lazima tuwe tayari kwenda nao hata kama ni mabli kidogo kuliko inavyotegmewa, kwa sababu tuki-give up kirahisi namna hii tunakuwa tunawapa nguvu ya kuamini kuwa next time itakuwa hivi hivi, hapana mimi ninasema kuwa bado tunaendelea na uchunguzi, hii ishu ni bado kabisaa!

Ahsante Wakuu
 
Nimeangalia tena picha ya ile gari ya marehemu na jinsi ilivyopondekapondeka. Ilipopinduka ilibiringika mara ngapi? Ilikuwa inakwenda kasi ya speed gani?
 
Kuanzia mwanzo wa mjadala wa tukio hili la Wangwe nimejaribu kuonesha clues kadhaa (tatu hadi sasa) kati ya sita hivi. Kutokana na udadisi wangu tangu muda mfupi baada ya kupata habari ya msiba nimeamini kwa moyo wote kuwa suala hili siyo la CCM na Chadema tu bali lina maslahi makubwa sana ya Taifa. Hivyo kuna clues chache ambazo naamini zinahiji kuangaliwa kwa karibu ili hatimaye kuleta sense kwenye mambo kadha wa kadha.

Mengine nimeyaandika kwa kirefu kwenye gazeti kesho nikito msaada kwa Polisi baada ya kuombwa kufanya hivyo na Manumba. Aliomba wale wenye kuona utata basi wasaidie Polisi kuonesha utata huo. Katika makala hiyo sikujaribu kuelekeza kidole mahali popote au kwa mtu yeyote isipokuwa kuwaambia mkijibu maswali haya mtajua ni ajali ya kawaida au la. Hivyo clue zilizosalia:

(za kwanza, ni muda, gari, mwili);

4: Simu ya kwanza na simu ya mwisho

. Ni nani ambaye Bw. Mallya alimpigia simu kwanza. Bahati mbaya sidhani tunaweza kupata jibu la swali hili hasa baada ya SIM card kutolewa kwenye simu ya huyo kijana. Siamini kama hadi hivi sasa kuna uwezekano wa kupata taarifa za simu hiyo. Uchunguzi wa upande wangu unaonesha pasipo shaka kuwa watu wa kwanza kupigiwa simu hawakuwa Chadema na hawakuwa watu tu wa CCM; bali mtu fulani mahsusi. Huyo mtu ndiye ambaye anaufunguo wa kuunganishwa kati ya yeye na Malya.

Je yawezekana mtu wa mwisho kupigiga simu kwa malya/chacha ndiye alikuwa mtu wa kwanza kupigiwa simu? Na baadaye ni nani wengine waliopigiwa simu na Malya eneo la ajali kujulishwa kuhusu msiba?

5. Fedha
Wengi wetu wamekubali kuwa Chacha alirudi (baada ya kuanza safari) nyumbani kuchukua Charger baada ya gari kuharibika/kufanyiwa matengenezo. Je alikuwa anataka charger ya nini wakati Deus alikuwa na simu na walikuwa wanalala tu Morogoro kuwahi msiba Dar, na angeweza kupata charger eneo lolote Dar?

Je yawezekana kuwa aidha alirudi nyumbani kuleta fedha/ kuchukua fedha. Sentensi inayofuatia nitaiandika taratibu sana na uisome hivyo; Kulikuwa na jaribio la kumshawishi Wangwe asilete hoja yake na ushawishi huo ulifanywa kwa fedha na kuna zaidi ya mtu mmoja anayejua juu ya hilo na walimsihi Wangwe asifanye hivyo. Hata hivyo (sijui kama hela zilichukuliwa au la) lakini vyovyote ilivyokuwa Wangwe alikuwa afanye anachotaka kufanya (kuleta hoja).

6. Hoja ya Wangwe:
Hii inatokana na hicho hapo juu (namba tano); Wangwe alikuwa amepanga baod kuwasilisha hoja yake lakini kwa sababu fulani hakuweza kufanya hivyo hata walipomtafuta siku hiyo. Je, aliyekuwa anamtafuta Wangwe alijua kuwa Wangwe hayupo Dodoma na ameshaondoka na hiyo kutumika kama geresha? Kama Wangwe alikuwapo Dodoma kutwa nzima, na kushindwa kupata muda wa kuwasilisha hoja yake kwa Spika ilikuwaje nafasi imefunguka baada ya yeye kuondoka?

Baadhi ya kinachohisiwa na ka "nzi" ni kuwa sehemu ya hoja hiyo inahusiana na madini kule Tarime.

Hii hoja ya nini na nani ananakala yake? Jibu la swali hili ni jepesi. Hoja ya Wangwe imepotea. (Haikuwasilishwa kwa Spika) na nyaraka na mabegi vimeibwa eneo la ajali. Na hivyo ni almost impossible kupata nakala hiyo isipokuwa kama kuna mtu atajitokeza na kusema anayo nakala. Je kiongozi wa kambi ya upinzani alikuwa na nakala; je kiongozi mwingine wa Chadema ana nakala? (sidhani) Hata hivyo sitoshituka kama nakala hiyo itakuja kupatikana baada ya siku kadhaa hivi. You can guess why na haitatolewa na watu wa Chadema; labda familia wanayo nakala nyingine nyumbani.

Ukiyasoma haya yote, ongeza na yatakayotoka kesho; na utakubaliana na mimi kuwa suala la "risasi" it was a waste of time, but a deliberate diversion ya watu and resources toka Dodoma kwenda Tarime na hivyo kununua muda kitu ambacho kilikuwa ni muhimu sana na kinachohitajika kuliko kurundikana Tarime. Wakati wao wanaenda Tarime, vya kutengenezwa vimetengenezwa, vya kusafishwa vimesafishwa, na wa kufundishwa amefundishwa.

Swadakta mkuu hapa umenena. Toka mwanzo wa hili suala sikuona mantiki ya Chacha kuuwa na CCM ama Chadema. Kwa hili suala la madini linalowahusu Barick company ni possibility kubwa ya kusababisha kifo hiki.

Na pia kama ulivyosema simu ya mwanzo na ya mwisho ya Deus Mallya ni mwanga mkubwa sana katika hili. Huu ni ukweli usiopingika.

Nami pia ningependa kuongeza kwamba kumpata yule mtu wa tatu aliyekuwepo katika ajali ambaye aliweza kuwazuia watu kusogelea ajali na kuwakumbusha kumsachi marehemu pia ingesaidia kujua nini hasa chanzo cha kifo hiki.

Kitu kikubwa kwa sasa ambacho kitatupa ukweli ni ripoti ya uchunguzi unaofanywa na mtaalamu wa familia na kumbana mbavu kwa hali na mali huyu kijana Mallya. Kama Chacha alipigwa risasi basi mtaalamu huyo atatueleza na tukila sahani moja na Mallya lazima atamwaga ukweli ingawa pia ni very possible tukasikia Mallya naye amefariki ili kuzima kila kitu.
 
Kidatu, hakuna cha risasi; hili lilijulikana tangu siku aliyofanyiwa uchunguzi pale Dodoma. Mazingaombwe ni lazima yawe na distraction. Jana ilikuwa ni distraction ya kile kilichokuwa kinaendelea Dodoma.
 
Fellow Tanzanians I write the following with a heavy heart for we are being played just like puppets on a string. Someone, somewhere knows our weakness and so is always one step ahead of most of us. Our weakness in responding to stimuli has become our undoing and this has given them a chance to take advantage of us and so know our every move. They will throw us a bait and behold while we are scrambling for the pieces, they will move to safer grounds.

Our vulnerability gives them the opportunity to thrive on their evil ways and suppress our liberties even further. Lack of unity in our resolve for a better Tanzania, helps then build the kind of confidence that makes them act with unimaginable impunity. Our impotence to face them head-on, lets even the most evil among them roam the streets treading on our poor toes. Our despair will only give them a sense self satisfaction that they have won and we have lost. But have they ?

What follows is a rule of fear and intimidation and woe to him that challenges the status quo for the reward is capital punishment. Traitors of the masses will be compromised and like we are witnessing in JF right now their numbers will grow. They will ridicule genuine efforts to seek fairness and spin and twist falsehood as truth to justify their bootlicking and lampoon all those that seek justice. No enough is enough and if we cannot take action for ourselves, lets do it for the sake of our children and grand children.

Fellow Tanzanians, do we let them ? Like Zig Ziglar said, "People often say that motivation doesn't last. Well, neither does bathing - that's why we recommend it daily". Do we have motivation ? Of course we do, If you don't go after what you want, you'll never have it. If you don't ask, the answer is always no. If you don't step forward, you're always in the same place. Since we dont want to remain where we are, let's all begin but with the end in mind. Ndugu zangu how many of us are ready to step forward - today.


Am I off-topic ? No, tradition has always been on our side. Tough decisions were often made at burial ceremonies. Again RIP Comrade Wangwe, long live our aspirations and desires for better life while here on earth.
 
Moderators, nafikiri ingekua ni busara zaidi kama tungeunganisha topic hii na ile nyingine iliyokuwemo tangu zamani..
 
Jana nilishauri ile thread ya Wangwe ifungwe (isimamishwe).....Watu wakashambulia freedom of speech. Sasa freedom of speech hata hatujui kuitumia.Duuh!!
I also said hindsight is a great foresight......go figure!!
If only people learn to sit back and watch......
The spinning on that thread is unbelieavable.....
 
Moderators, nafikiri ingekua ni busara zaidi kama tungeunganisha topic hii na ile nyingine iliyokuwemo tangu zamani..

Usually threads are left to flourish for a while to accommodate new upshots on a particular matter, but with time are merged with previous ones accordingly to help the flow. Thanks for your concern and have a nice day !


 
Last edited:
MKJJ Ushauri wangu ni kuwa waweke ukweli la sivyo huu ni ujumbe wangu kwa Manumba....Msitake kutuletea matatizo hapa USA!

Nyie mnajuwa Wangwe alikuwa anapingana na BARRICK...Na BARRICK ina wabunge wanaoisapoti...!

Na BARRICK BUSH YUMO...SASA SI BALAA MNATAKA KUTULETEA WATU TULIOKO USA?

Sasa kitendo cha kufa huko ama kuuwawa huko kwa Wangwe si ni sawa na kusema Bush kamwua Wangwe kama tukiamuwa kuhusisha BARRICK na mauwaji hayo?

Sasa na sisi tulioko USA TUKISEMA WANGWE NI SHUJAA NA WAKATI ALIKUWA KINYUME NA BARRICK SI NI SAWA NA KUWASHUTUMU WAMAREKANI kwamba kampuni ambaye rais wao msataafu ana share imesababisha mbunge kuuwawa?


Kwa watanzania waelewa...Ni bora mnge reach out na sisi mtuambie ili tujuwe namna ya kubehave...La sivyo mnahatarisha maisha yetu bila sababu za msingi.

Sasa na hivi mko na wachina...Halafu tena mko na Bush...Jamani!

Halafu haya mambo yanatokea na mkorogo wa waarabu na warusi humo...Na mcanada...Yani UTAJIRI WETU WAAFRIKA UMEGEUKA BALAA!

Kama mnataka kufuta vyama vingi ni bora mfanye hivyo....Na muweke wazi msitutafutie matatizo..Kama kweli tunaheshimiana kama watanzania ni heri tuelezane kwa maslahi ya TAIFA ili tuwe kama wananchi wa maana na si mbumbu wa kupiga kelele na huku mauwaji yakiendelea.

Na hao BARRICK..SIO KWAMBA TUNAWAPINGA...NO!

TUNATAKA WANANCHI WANUFAIKE PIA NA MADINI HAYO KWANI HATUTAKI WANANCHI WAFE KWA NJAA WALA MAGONJWA NA UKOSEFU WA MAJI SAFI...!

Na pia narudia kuwa ni heri wamarekani wamchaguwe Obama la sivyo mambo haya si mazuri kabisa.

Tunajuwa issue ya EPA wala mimi binafsi sijisumbuwi nayo tena kwa sasa...Lakini kabla ya kufanya hivyo...Serikali itafute namna ya kuwaeleza wananchi na wale wahusika wote wasiruhusiwe kujihusisha na siasa tena...!

Wale walioinjinia...Kama wanataka suluhu waweke ukweli wazi,waombe msamaha..Hiyo pesa irudishwe na itumike kwa wananchi,maelezo na negotiations ziendelee na wamarekani...Na kuwe na tume ya ukweli na maridhiano...Hiyo tume nipenda niwemo hiyo..Kwani kwenye kunegotiate huko tunakoelekea ni muhimu kwani tumechoshwa na vita kila siku kwani vinatuletea umasikini!

Ni kama vita ya Kagera ambayo kwa kweli kama tusingepigana vita ile basi labda tungekuwa mbali sana!

Na sijui kwanini ilimlazimu mwalimu kupiga ile vita kwa nguvu zake zote na kuivalia njuga kama alikuwa hana kashinikizo flani ka kimaslahi!

Sasa tuko na Kabila ambaye na yeye naona kalipiza kisasi cha Baba yake kuuwawa wakati majeshi ya Mugabe yakimsaidia kupigana na majeshi yaliyokuwa yakipewa sapoti na mganda ambaye si shaka alikuwa kipenzi cha USA!

Na kwasababu Mkapa ali align na Kabila kwa siri..Maofisa flani flani waliwezesha kupitisha URANIUM KUTOKA ZAIRE KWA KABILA KWENDA IRAN.

Sasa mkorogo kama huo namna ya kuushughulikia ni namna mnayofanya!

Mimi mwenyewe sasa hivi naionea serikali HURUMA kwani matatizo hayo ya kimaamuzi si madogo!

Ila kwa upande mmoja ni wazi kuna direction ya namna ya kudeal na mambo haya inamezwa na mahusiano mengine.

Na ndio maaana nikasema ni heri maridhiano na haki itendeke na hao watu wasijiusishe na siasa tena hiyo ikiwa ni kama sharti la kusamehewa!

Lakini UHURU KWANZA...THEN UKWELI NA MARIDHIANO KWASABABU SI KWELI KWAMBA WANANCHI WOTE HAWAHUJUI UKWELI.

Kuna uwezekano wa kuwa na taifa la kitumwa siku za mbeleni kama tusipokuwa makini.

Hivyo kwasababu tumeshajuwa kuwa tuna utajiri..Basi mje pamoja na kulijenga TAIFA...

ILA MAFISADI NI LAZIMA WATOKE KWENYE SIASA KWA HIYARI LA SIVYO HATUNA HABARI TENA NA MAMBO YENU NA MUWE SALAMA NA TANZANIA YENU!

Hivyo basi majadliano yaendelee na kama kweli Manumba haujuwi ukweli...Basi tunadanganyana.

Tulisema wazi kama kweli wanataka ukweli..Tokea mwanzo nilisema...Waseme kijana alitumwa na nani...Marehemu alikuwa akutane na nani...Alikuwa ana wasiliana na nani?

Vigezo gani vilitumika kumruhusu kijana huyo kuwa karibu na Wangwe..Je alikuwa mwakilishi wa nani?

Taarifa kuwa alikuwa nje ya nchi mara kwa mara akiandamana na watu mashuhuri ni za kweli?

Na habari hiyo ya kijana huyo kuponea kwenye ajali kama hiyo ni za kweli?
Hilo gari ambalo linaonekana kama ni corrolla ni lile lile?
Hapo garage walipoenda labda kuna jambo lilifanyika...Je ile assumption ya Fildi Marshall kuwa gari ni kama limepondwa...Kuna uwezekano wa kuwa na gari kama hilo hapo garage?
Nani aliwapa service hapo garage?

Ni garage wanayopenda kuitumia ama ni mara ya kwanza?

Nani fundi wanayependa kumtumia?

Aliona watu wangapi?

Wangwe na Deus walikuwa katika hali gani??

Je gari lilipopelekwa hapo garage bado walikuwa wote?
Hiyo garage haina camera?

Kijana anasema walisimama wapi na wapi?

Nini hasa kilichomwua marehemu?

Maana kwenye uchunguzi kama huo huwezi tu kusema ni ajali...Bali ni lazima useme ni nini kimepelekea umauti wake..Either ni internal bleeding...Kama ni sharp metal ili penetrate...Ni kivipi alipata majeraha hayo ilihali alikuwa amefunga mkanda?

Ni kwanini kuna taarifa tatanishi kwenye kuhusu nani alikuwa mwendeshaji...Nani alikuwa passenger..Kama kulikuwa na mtu mwingine nk.

Pia kwenye simu nadhani kampuni ya simu inaweza kutowa msaada kama wakiombwa na serikali na wanaweza kutrace ni namba gani alikuwa akipigiwa na ni nani alikuwa akipigiana naye simu.

Kama ni simu za vocher then labda inaweza kuwa shida hapo wataalam wake waseme.

Lakini maswali ni mengi labda kama wana nia kweli waanze na hayo machache kabla ya kuget even deeper.
 
acha Hizo Usimuingize Kabisa Mungu Kwenye Uuwaji Na Ujangili Na Unyama Huu!

Si Mapenzi Ya Mungu Wangwe Afe..unless Proven Otherwise.

Na Wewe Mkumbo Kama Ni Chadema Ni Heri Uache Propaganda Sasa Hivi...sitokubali Hadi Munieleze Ni Kivipi Wakibosho Ni Wasaliti Kwasababu Ya Sina Na Deus Mallya...na Pia Unieleze Usafi Huo Unaouzungumzia Wa Chadema Tukianzia Na Epa.

Huyu Dogo Si Alikuwa Ana Print Mambo Ya Both Ccm Na Chadema Kama Alivyokuwa Wangwe Akideal Na Issues?

Mkumbo Tunaomba Urekebishe Kauli Zako Na Utowe Mchango Ambao Hautajaza Thread Hapa...semeni Kama Uhusiano Wenu Uko Vipi Na Huyo Gaidi Deus...tena Inawezekana Umeshawahi Kukutana Naye...tafadhali Usiseme Deus Ni Ana Upendeleo Kutoka Kwa Bwana....sema Ana Upendeleo Kutoka Ccm Na Chadema.
Tunataka Mgombea Huru!
Mushi Leo Upo? Ngoja Nikusome Kwanza Au Ulikuwa Unasubiri Ripoti Ya Daktari?
 
Kuchomolewa kwa Simcard si tatizo kubwa
Record zote za simu nani kampigia nani, saa gapi, wameongea muda gani, na huyo nanii alimpigia nani baada ya kupokea simu toka kwa Malya hizo zote zipo katika mitambo ya simu ya mashirika husika.
Mtu asijifanye kujaribu kuzifuta taarifa hizo.
On demand zinapatikana tu.

Technology haina usiri hata kidogo.
Hilo gari la Marehemu Wangwe likikaguliwa na Magwiji wa Scotland Yard kuna mengi yatasikika.
Tunaweza pata picha nzima ya kilichotokea isipokuwa kumrudisha Marehemu Wangwe katika uhai wake tu.
 
Biko (Steve) was arrested by police in 1977 and died in detention, naked and manacled, from extensive brain damage, six days later. His death caused international protest and a UN arms ambargo. An inquest in the late 1980s found no one responsible for his death, BUT in 1997 former five policemen adamitted being involved.

Chacha Wangwe Movement!!!!!
Tanzania Liberation Movement!!!!
Tuungane hapa ndio pa kuanzia, Hoja Binafsi ya wangwe, alafu taarifa ya kamati ya madini ya Raisi

Jawabu lipo tunaweza kulifikia
 
Duh JMushi unaongea mengi ndugu ,Miruzi mingi humpoteza mbwa!

But all in all time will tell.Lets allow time things 'll be open .
 
Duh JMushi unaongea mengi ndugu ,Miruzi mingi humpoteza mbwa!

But all in all time will tell.Lets allow time things 'll be open .

Jmushi ana machungu na hasira kutokana na mambo yanayoendelea huko, sio siri leo kazini nimewaza sana kuhusu kifo cha jamaa, ingawa simfahamu hivyo ila inatia machungu na hasira sipati picha familia yake. Mungu pleaseee! wape adhabu watu waliofanya haya mambo.
 
ikiwa barrick waliweza kumtuma balozi wa nchi kuwafanyia lobbying......watashindwa na kitu kidogo kama hicho? na hasa kutokana na kujua kuwa tanzania hakuna vyombo vya usalama vya kutosha.

tuombe mungu iwe mafile hayo ya data yawe na copy iliyohifadhiwa na wana fammilia au kambi ya upinzani pahala salama
 
Kuhani.. jaribu kunielewa ninachosema, ama sivyo nitakuwa na kazi kweli ya kufafanua kila kitu. Kuna wakati natumia irony, sarcasm, etc. Itabidi unisome vizuri au itabidi niwe nafafanua kila kauli ili kuianisha iko kundi gani.

Unajua katika blog za marekani huwa wanaweka kwenye mabano [snark] kuonyesha kwamba ni sarcasm. Labda ungetumia mbinu hii ili baaadhi ya watu wasichanganyikiwe, maana sarcasm ni high level literary tool, not everyone has mastered it! Kwikwikwi
 
Malya ndie mwenye kujua kama si kila kitu, basi ni sehemu ubwa ya issue hii.

jee polisi watamhoji kiasi cha kupatikana ukweli? hilo ni suala jengine kabisa ambalo nafikiri only time will tell
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom