Jambo kubwa na ambalo ningetaka wenzangu humu mulijadili kwa kina na kuangalia kinachoendelea ni kuwa ukisoma magazeti yote ya leo isipokuwa Tanzania daima na Mwananchi ambayo yaliripoti taarifa hiyo utaona ya kuwa mwandishi wa habari hiyo alikuwa ni mtu mmoja.
Ukianza kusoma Nipashe,majira,mtanzania,kulikoni,uhuru na habari leo utaona hiki ninachosema ,kwani kuna paragrafu tatu zinafanana kila sentensi na ni zile zinazohusiana na Mbowe jinsi alivyowasili Kemakorere.
Nimefanya uchunguzi wangu tangu asubuhi leo na nimeweza kujua kuwa habari hiyo ilitumwa na Mwandishi mmoja ambaye naomba kumtaja baadae huyu mwandishi ni mwandishi wa IPP Media,na yuko based Mkoa wa Mara.
Nowashuri muweze kusoma hicho ninachosema kwenye magazeti niliyotaja ,na kisha mtaweza kuupata ukweli wenyewe jinsi ulivyo, haiwezekani waandishi tofauti wakaandika kitu kile kile kwa maneno yaleyale na paragrafu zilezile,na kila penye koma,nukta na hata mkato pakawa ni pale pale.
Nimegundua kuwa Rostam Aziz jana amekutana na wahariri na wale ambao hawakwenda aliwapigia simu kuanzia saa tisa na dakika 26 jioni na kuanza kufanya kazi yake,na ilipofikia jioni akakutana na wahariri wa habari na kuwapa bahasha maalum kwa ajili ya kuitumia story hiyo, na kuwaahidi kuwapatia donge nono na hizi nina uhakika nazo nasubiri muda wa kuziweka hadharani .
Tatu, waandishi ambao majina yao yametumika kwenye magazeti niliyotaja hawapo na kwa vile vyombo vilivyoandika majina ni majina ya kutungwa kwani waliokuwepo huko leo wamekaa na kutoa msimamo kuwa ni kwanini habari zao hazikutumika kama walivyotuma .
Prof. Wangwe anategemewa kutoa tamko jioni hii kuhusiana na habari zilizoandikwa kuhusiana na Mbowe kutimuliwa kwa mapanga,marungu n.k. ila alikuwa anashauriwa na watu watatu waliokuwa naye kuwa asifanye hivyo ila yeye anaonekana kuwa na msimamo wa kutaka kusema kilichojiri na kutoa tamko rasmi la familia .
Naenda tena kupata habari nyingine za kina kwani imebidi nikaweka watu maalum huko kwa ajili ya kuhakikisha kuwa napata habari za kweli na kuna siku nitajitambulisha rasmi kuwa mimi ni nani ,na haya maandishi yangu yataendelea kuwa ni ukweli, nakumbuka jana niliandika na kuna mtu aliniuliza humu kama ninayoandika kuhusiana na magazeti yataripoti nini kama ni ukweli nami nilimjibu kuwa ni ukweli..Ndugu,Mtanzania unakumbuka ni wewe uliniuliza jana majira ya mchana saa za huku ila ilikuwa majira ya jioni huko nyumbani kama sio usiku.