Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Kuna hali ya vurugu huko na polisi wamefukuzwa pamoja na viongozi wote waliokuwepo huko.

Wananchi kwa kuwa walishajengwa kisaikolojia kuwa amepigwa risasi walikuwa wanatarajia kuona kuambiwa kuwa ndivyo ilivyokuwa ,sasa baada ya taarifa hiyo kuwa sivyo wamekuwa wakali sana.

Wananchi wengi ni walevi sana na ukweli ni kuwa wamefika wakiwa na mapanga na kuna baadhi wana mishale eneo hilo.

Wananchi hao ambao ni wapo hapo wanalazimisha kuwa lazima CHADEMA inahusika kwenye msiba huo na wamefikia mahali pa kuwatishia wanachama wa CHADEMA kuwa chama kinahusika .

Wamemaliza kuzika na hali imetulia sasa ,baada ya kikundi cha vijana wale kuondoka.

TBC hawaonekani tena huko na huenda wameamua kuondoka nalifuatilia hilo pia kuwa kwa nini wameamua kuondoka huko.
 
mmmmh .....watanzania tumezidisha ...msiba tumeufanya kama movie! hatari hasa!

nilisema hapa......watu tunapewa taarifa vipande pande ndio maana watu wanalazimisha hayo mambo ya risasi!

serikali inapokuwa haipo wazi, ndio mambo kama haya hutokea.
 
jmushi nilifikiri utakuwa umekoma kukurupuka na maneno ya vitisho ndugu yangu....kumbe ndo kwanza mkoko!
Acha upumbavu wewe!

Kama bado una bifu kwasababu ya issue ya NYALANDU NA MISS TZ UACHE UPUUZI KWANI HII ISSUE NI NYETI!

Hakuna haki hapa...Hii ni jamii forums na ina refelct jamii yetu ambayo ni CORRUPT! Nimenyanyaswa hata mtandaoni ndiyo ije kuwa live mtaani?

Marehemu alikuwa anjuwa siri za ccm na chadema...Na ccm na chadema wote walikuwa kwenye EPA...Taitizo ni kwamba kama mgombea binafsi angepitishwa basi ccm na chadema walikuwa hawana cha kumwambia RASTA!

Sasa tatizo pesa hizo za EPA zinaweza kuwa za URANIUM ambayo ilikwenda IRAN...Na kwasababu chadema nao kuna waliohusika..Basi hata wao wakishinda urais bado watakuwa na tatizo la kuhusika na pesa chafu...Hivyo hakuna wa kumshughuliia mwenzake hapo...WANGWE PEKEE ALIKUWA HURU KAMA MIMI!

Uhuru wa kutosikiliza ORDER ZA VIONGOZI WAZEMBE WASIOONA MBELE.

Lakini tatizo ni kuwa...Aliyempiga risasi ya mdomo ni ISHARA YA KUMFUNGA MDOMO...Na aliyemuuwa marehemu ni mtu ambaye marehemu anamfahamu na inawezekana pia walimtesa kabla..Either kwa raha zao...Ama kwa kutafuta habari flani flani...Pia kizungu zungu unaweza kuta alishawekewa sumu na HUYO NYOKA na ilikuwa afe anyways...Lakini labda wakataka ku retreave more INFO from him.

nAKUBALIANA NA MAONI YA SUSUVIRI PIA.

Pia inawezekana kuwa Jasusu Deus ni mtu aliyekuwa akijuwa part ya deal..Ndio zakimafia hizo...Unaweza kuta eye alishuhudia mauwaji ama alipewa bastola amuuwe yeye na bastola hiyo kuachwa hapo ili fingerprints zioneshe kuwa ni mchagga mkibosho huyo aliyemuuwa wangwe.

Tatizo mapengo ni mengi na hawawezi kuyaziba yote.
Na kwa taarifa yako hawa chadema na ccm wasipokuwea kweupe basi machafuko yanaweza kutokea...Lakini kwa mtizamo wangu...RASTAFARIANS WOTE KAMA NI WAKWELI ANZISHENI MAPINDUZI HAPO BONGO...LA SIVYO TUNARUDI ccm ILI KUILINDA AMANI.
 
The very latest: Hizi nimezipata kwa wadau waliopo Dar na Tarime muda mfupi uliopita, naripoti kama zilivyo, kila mtu achambue mchele na pumba:

  1. Post Morterm imefanyika. matokeo: hakuna risasi wala kitu kingine, bali ni ajali iliyomuua Wangwe.
  2. Marehemu ameshazikwa.
  3. Mbowe hakufanyiwa fujo yoyote. Kilichofanyika, Rostam na akina Balile na George Marato, wameandaa stori kwa malengo ya kisiasa.
  4. Kesho Jukwaa la Wahariri linakaa kufanya uchambuzi wa kitaalamu wa stori hiyo (ambayo ilisambazwa vyombo vya habari kadhaa); na watatoa tamko kali dhidi ya ufisadi uliofanyika.
  5. Kuna wazalendo walienda kamera za video kwenye msiba.. Picha zinaonyesha halihalisi ya matukio yote. Zitatumika katika kueleza umma kilichotokea.
  6. Tunaambiwa mkakati uliokuwepo ni kama ule uliotumika na utakaoendelea kutumika kummaliza Sumaye na Malecela kisiasa
  7. Wahariri wa vyomboa vya habari kesho wanakaa kuweka mambo sawa. Inasemekana kutakuwa na kuvuana nguo sio mchezo

8. Dogo Deus Mallya ametinga courting kujibu mashitaka ya kuendesha gari bila lesseni.
Udhibitisho
- Mtoto wa marehemu
- Garage, Deus ndiye aliyepeleka gari na wakati wa kuondoka alimwona yeye
- Yule mzee wa Kwanza kumtoa marehemu kwenye kiti cha Abiria
 
jamani wana JF nimepitia kona zote juu ya hii ishu lkn bado nina pata wasi wasi

mbona cjaona post yoyote iliyotoka kwa JMUSHI au ndio niamini kwamba DEUS MALLYA ni JMUSHI?

Hiyo ndiyo plan yao na ccm...Ya kuhusisha watu wenye kufanan kwa kila hali na jmushi...HALAFU MAMLUKI chadema...Wakaja na kauli kuwa wakibosho ni wasaliti kwa kutumia mfano wa mangi SINA...Mangi huyu ambaye ni babu yangu alikuwa ni shujaa..Licha ya vita kati ya wamachame na wakibosho...Bado nilidhani kuwa migawanyiko imekwisha...Lakini kauli ya chadema inayoongozwa na mmachame kuwa wakibosho ni wasaliti...Imepelekea mimi kuingilia kati kwani wachagga si wote wabaguzi.
 
jmushi is back!! ....twende baba ....wote wapumbavu ....mwerevu na huru ni wewe peke yako!
 
Hivyo basi kama tunataka mjadala wa kistaarabu...Twende na ushahidi na discussions za kitaalam na kisayansi kama watu wenye kuelimika na tusianze kwanza mambo ya chama...Kwani MAFISADI WAKO KOTE KOTE NA KAMA WAKISHIRIKIANA MTAPATA SHIDA!
Nimesema kabla hatujapigia kelele kuhusu uhuru wa vyombo vya habari...Tuanze kwanza na UHURU WA JF!
Kwasasa I am OUT.
Nasubiri maelezo ya usaliti wa mkibosho dhidi ya MKURYA na USAFI WA MMACHAME!
 
Acha ushabiki jmushi si huyo post 1467?

JMushi asipoandika ni shughuli akiandika ni kesi jamani hata kama ni kijana mdogo haruhusiwi?Tunajua huwa anaandika mada ndefu wakati mwingine zenye hasira na lugha kali lakini msisahau excessive nationalism and patriotism aliyonayo JMushi ambayo akina Hitler na Mussolini waliita CHAUVINISM ndio inamtuma kufanya hivi.Maana nimesoma mahali watu wanaulizana eti JMushi yuko wapi ina maana mada yoyote humu lazima JMushi achangie na asipochangia ahojiwe?
Grow up!
 
Lakini tatizo ni kuwa...Aliyempiga risasi ya mdomo ni ISHARA YA KUMFUNGA MDOMO
Kumbe alipigwa risasi ya mdomo?.....Mushi tuambie vizuri
 
Hapa pasiwe sehemu ya kuhamisha mada ,tunapeana taarifa serious hapa kama kuna mtu anabeef lake basi aanzishe sehemu nyingine please ,kuna watu serious hapa wanafuatilia kujua nini kinaendelea Tarime.

Kuna kikao kimepangwa kufanyika kwenye hoteli moja jioni hii mjini Msoma ,ninaweka mtoa habari pale kama kitafanywa ntaweza kuwajulisha , ila hali ya wananchi kwa sasa wametulia na huenda nyumbani ndio pawaka na kizaazaa ......nafuatilia kwani sitaki kusema kitu kisichokuwepo.
 
JMushi asipoandika ni shughuli akiandika ni kesi jamani hata kama ni kijana mdogo haruhusiwi?Tunajua huwa anaandika mada ndefu wakati mwingine zenye hasira na lugha kali lakini msisahau excessive nationalism and patriotism aliyonayo JMushi ambayo akina Hitler na Mussolini waliita CHAUVINISM ndio inamtuma kufanya hivi.Maana nimesoma mahali watu wanaulizana eti JMushi yuko wapi ina maana mada yoyote humu lazima JMushi achangie na asipochangia ahojiwe?
Grow up!

Kevo

Hii posti unai-direct kwangu?
 
Hii thread vipi, mara ya mwisho nilisoma post ya 152. Nashangaa sasa ni post ya 149. Kunani hapa ........... au JF imeshatupiwa "vijiunga unga" nini???

Sidhani kama mtandao ninaoutumia unanidanganya ..... msaada tafadhali ...
 
nadhani mwiba ukirudi kurasa chache utaweza kuona sikumbuki ni wapi lakini nilishazibandika hapa.
 
Kama hizo habari mnaweza kuziweka hapa tukaziona kwani wengine hatuna njia ya kupata magazeti yote na kuanza kupitia mstari kwa mstari,nahisi itakuwa vizuri sana kuweka vipande hivyo na gazeti lililochapisha.

Pitia magazeti ya uhuru,majira,mtanzania,habari leo,nipashe, na uzuri ni kuwa haya magazeti yote yapo online, utaweza kuona kinachosemwa hapa.

Hapa nitawaletea habari zaidi na za kina kuhusu kikao cha jana ,nimeamua kujitosa kwenye hili potelea mbali kwani mchezo wa Rostam Azizi utawaumiza wengi kama tukiendelea kukaa kimya haswa wenye kuweza kujua ,na ajue kabisa kuwa nitasema ukweli mtupu na ukweli daima.
 
nimeshangaa hivyo hivyo; kumbe mada zinazohusu waandishi wa habari na ripoti zao zimehamishwa na kuunganishwa. Angalia kuna thread yake.
 
Kevo

Hii posti unai-direct kwangu?

I did not direct it to any one my friend.Nimeona tu watu wanakuwa unfair kwa huyu mchangia mada mwenzetu kwa hiyo mimi ku quote post yako did not mean you.
Please dont misunderstand me.
Nothing personal.
Cheers
 
Hivyo basi kama tunataka mjadala wa kistaarabu...Twende na ushahidi na discussions za kitaalam na kisayansi kama watu wenye kuelimika na tusianze kwanza mambo ya chama...Kwani MAFISADI WAKO KOTE KOTE NA KAMA WAKISHIRIKIANA MTAPATA SHIDA!
Nimesema kabla hatujapigia kelele kuhusu uhuru wa vyombo vya habari...Tuanze kwanza na UHURU WA JF!
Kwasasa I am OUT.
Nasubiri maelezo ya usaliti wa mkibosho dhidi ya MKURYA na USAFI WA MMACHAME!


Jmushi kwani nani wewe amesema mkibosho kasaliti? wewe waja kweli ndugu yangu.
 
Hii thread vipi, mara ya mwisho nilisoma post ya 152. Nashangaa sasa ni post ya 149. Kunani hapa ........... au JF imeshatupiwa "vijiunga unga" nini???

Sidhani kama mtandao ninaoutumia unanidanganya ..... msaada tafadhali ...

Kunachujwa pumba ,maana haijulikani kuhusu uchunguzi kama ulifanyika au haukufanyika ni nani alifanya ,jee wandugu wameukubali au bado wamekubali shingo upande ? huwezi kujua ila tusubiri kubwa lijalo maana udikteta unaonyesha haufanywi na raisi Kikwete ila kuna walioiteka hii nchi na wanaiendesha wanavyotaka wao.Kiasi wazenji wadai Nchi yao na hawaambiliki ,maana huku mambo yameshakuwa hayatibiki tena.
 
Mungu saidia..tusifike kwenye chuki za ukabila..CCM hawajui outcome ya hili wanalotaka kulifanya.... mola epushia mbali hili na naomba uwaumbue hadharani.....Let us cross our fingers..!!
 
Habari nilizozipata,

Marehemu amezikwa jioni hii, Wakuu wa vyama vyote vya siasa walikuwepo isipokuwa Mhe. Mbowe ambaye ameondoka na kurudi Dar es salaam.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom