Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Kifo cha Wangwe: Shuhuda atoa taarifa mpya polisi


* Adai Mbunge Wangwe hakuendesha gari lililopata ajali

Na Faraja Jube, Dodoma


UTATA umejitokeza iwapo marehemu Chacha Wangwe aliyefariki katika ajali ya gari Jumatatu usiku alikuwa akiendesha gari hilo ama la.


Kwa mujibu wa mtu aliyefika katika eneo la tukio dakika chache baada ya ajali hiyo, Mwiguni George, alimkuta marehemu Wangwe akiwa katika kiti cha mbele cha abiria huku sehemu ya kichwa chaki kikiwa kimebanwa ubavuni mwa kiti hicho na mlango wa nyuma.


Akizungumza juzi mbele ya Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishina Msaidizi wa Polisi, Peter Kivuyo, Kamanda wa Usalama Barabarani wa Mkoa wa Dodoma, Vitus Nikata na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kongwa, Ramadhan Kalowa, Georgr alieleza kwamba alikuta mwili wa marehemu Wangwe ukiwa umebanwa ubavuni mwa kiti na mlango wa nyuma huku mkanda wa usalama katika gari hilo ukiwa bado upo mwilini mwake.


''Nilikuwa nyumbani nasikiliza kipindi cha michezo, muda ya saa mbili na nusu usiku, nikasikia kishindo kikubwa, nikakimbilia eneo la ajali. Nilipofika katika eneo la ajali nilimkuta kijana mmoja akiwa analizunguka gari huku akipiga kelele za kuomba msaada,'' alieleza George.


Hata hivyo, mtu huyo alieleza mashaka yake kuwa kulikuwa na watu watatu katika gari hilo na siyo wawili kamba ambavyo ilitangazwa katika vyombo vya habari.


Juzi Deus Francis Mallya alikaririwa mara mwili wa marehemu ulipofikishwa katika hospitali ya Mkoa ya Dodoma, akisema kwamba walikuwapo wawili katika safari hiyo na kwamba marehemu Wangwe ndiye aliyekuwa akiendesha gari.


''Nilisikia katika taarifa ya habari kuwa walikuwa wawili. Marehemu ndiye aliyekuwa akiendesha gari na kwamba mmoja amepona. Mimi nina mashaka, kwani nahisi kuwa na mtu wa tatu na kwamba marehemu hakuwa anaendesha gari wakati wa tukio,'' alisema George na kuongeza.


''Nilipofika katika eneo la ajali kulikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa akiwatawanya watu walioanza kufika kwa ajili ya kutoa msaada wasilikaribie gari. Hata hivyo, tulianza kuutoa mwili wa marehemu uliokuwa katika kiti cha abiria upande wa mbele,'' alieleza George.


''Nilimvua mkanda wa usalama katika gari ambao bado ulikuwapo mwilini mwake, kisha tukamtoa kupitia mlango wa dereva kwani mlango upande aliokuwa amekaa haukuweza kufunguka,'' alisema.


Kwa mujibu wa Goerge, mtu huyo wa tatu alielekeza kutolewa kwa fedha alizokuwa nazo marehemu ndani ya mfuko wa koti, jambo ambalo lilimfanya shuhuda huyo kuhisi kuwa alikuwa pamoja nao.


''Tulianza kutoa vitu vya marehemu na mtu huyo alielekeza kuwa kuna fedha ndani ya mfuko wa koti,'' alieleza na kuhoji: ''Sasa mie nikajiuliza kama hakuwa nao alijuaje kuwa marehemu aliweka fedha ndani ya mfuko wa koti?''


Hata hivyo, shuhuda huyo alieleza kuwa wakati pilikapilika zilipokuwa zikiendelea, hakuweza tena kumuona mtu huyo wa tatu, ambaye alitoweka.


Maelezo hayo ya George yalipelekea Kamanda Kivuyo kuagiza askari waliokuwapo katika eneo hilo kuchukua maeleo ya shuhuda huyo kwa

ukamilifu.


''Kwanza nakupongeza sana kwa ujasiri wako na moyo wa kizalendo wa kutoa msaada kwa marehemu,'' Kamanda Kivuyo alimweleza shuhuda huyo.


Maelezo hayo yanaleta mkanganyiko kutokana na taarifa za awali kuwa marehemu Wangwe alikuwa akiendesha gari na kwamba walikuwapo watu wawili katika gari hilo.
source:MWANANCHI

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=6189

sasa hapo inabidi uchunguuzi ufanyike tupate ukweli juu ya kifo chake
 
nakusoma

nakushukuru kwa mawazo.mie nawakilisha mawazo yangu. bush ni nick name yangu kutokana na kutokubali mawazo potofu. napenda ona watu wanaojenga hoja hasa wakiangalia pande zote za shilingi.

jamii yetu inabadilika na kila kitu kinaangalia katika upande wa ubaya tu bila hata kuangalia uzuri wa jambo lenyewe.
 
Wanandugu Mambo Yanzidi Kunoga Hivi Majuzi Bwana Mmoja Aneitwa Deus Mallya Aliekuwepo Kwenye Gari Moja La R.i.p Wangwe Alisema
Hajui Kuendesha Gari Kabisa ..hivi Jana Wanahabari Wakiwa Na Mshushu Wameenda Sehemu Ya Ajali Na Kukutana Na Mzee Aliekuwa Wakwanza Kumtoa Marehemu Wangwe Na Kusema Marehemu Alikuwa Kiti Cha Mwisho Nyuma Na Alikuwa Kama Amebanwa Na Wala Akuendesha Gari ..mzee Mwingule Katika Kuwahakikishia Hilo Amesema Wakaangalie Gari Damu Ilikuwa Kwenye Kiti Cha Nyuma Kushoto.....na Wala Si Vinginevyo Mwisho Akaomba Kupelekwa Kumwangalia Huyo Deus Kujua Kama Alikuwepo Kwenye Ajali Au La Maana Amesema Anawakumbuka Wote Waliopo.na Pamoja Na Aliekuwepo Mbele!!!!1
R.i.p Wangwe Mungu Akulaze Pema Peponi
Wote Walioshiriki Kukuua Mungu Aawaadhibu Wote Pamoja Na Chama Husika

Mkuu,

Hao witnesses kwenye ajali popote duniani wanaongoza kwa kuwa unreliable.

Kama ni msomaji mzuri wa magazeti au hata msikilizaji wa TV hasa huku nje kwa wenzetu ambako wanajua kuchambua mambo, hao wanaojifanya wameona ajali huwa wanachemsha mno na baada ya muda hata wao huwa wanakiri hawana uhakika.

Sisemi huyo mzee anadanganya, ila tu tusiamini kwa asilimia 100 wanachosema watu kama hao. Kwanza kufika tu kwenye ajali unachanganyikiwa kabisa kiasi kwamba kukumbuka mambo yote hayo ni kitu cha mwisho.

Kumbukumbu inayokumbukwa ni ile ambayo inatokana na mazungumzo baada ya ajari. Watu wanakaa na kuongea nini kimetokea, baadaye hiyo ndio kumbukumbu inayobaki kichwaji.

Mimi niliwahi kupata ajali na SCANDINAVIA kule Morogoro, baada ya kutoka nje, watu wengi tu walianza kusema wameona kwa macho yao abiria 7 wamekufa. Hata magazeti karibu yote siku ya pili yaliandika abiria saba wamekufa, lakini ukweli ni kwamba abiria watatu tu ndio walikufa.

Aidha inaelekea watu wengi hawajui ajali zinavyotokea na madhara yake. Kwa ajali kama hiyo hata siku moja usitegemee kumkuta abiria pale pale alipokuwa amekaa. Gari likipata ajali likiwa katika mwendo wa 120km/h yaani balaa tupu.

Hapo ndipo umuhimu wa technology, ingelikuwa kama huku Europe hayo maswali ya walikuwa wangapi kwenye gari na nani alikuwa anaendesha, yangelijibiwa kirahisi kwasababu ya camera za barabarani. Kutoka Dodoma mpaka kwenye ajali, wangelikuwa wamenaswa na kamera nyingi tu.

Kuna uwezekano huyo kijana alikuwa anaendesha gari. Ni kawaida kwa wanaoendesha gari bila kuwa na leseni au sababu zingine, hudanganya pale kunapotokea ajali.

Any way lets hope ukweli kamili utajulikana mapema kwa faida ya familia ili wasiendelee kuongezewa majonzi zaidi ya waliyo nayo.
 
I'm going to sleep.. I'll leave you with this:

a. Ni kweli huyo Malya alikuwa kiti cha nyuma
b. Ni kweli Chacha alikuwa abiria (kiti cha kushoto)
c.
d. Na aliyekuwa dereva aidha alikuwa anajulikana na Wangwe, au Malya au wote wawili na mtu wa kuaminika hadi kuachiwa gari la Mbunge.
e. Huyo/hao abiria wengine walipewa usafiri huo kati ya Dodoma na eneo la ajali.

Na mwisho kabisa: this is my biggest "what if of the night"

what if Chacha had no choice but to leave with those people and at that particular day or time hata kama alijua ni mgonjwa na familia walimtaka apumzike. What if that was not an option? Clue... one of my post earlier yesterday.

check KLHN for my own take.

Hiyo C ni bahati mbaya au unampango wa kuielezea baada ya kuamka?????????
 
Mapya yaibuka ajali ya Wangwe




na Waandishi Wetu, Dodoma na Dar



UTATA unazidi kuongezeka kuhusu namna ajali iliyosababisha kifo cha Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe (CHADEMA) ilivyotokea usiku wa Jumatatu wiki hii.

Kuongezeka kwa utata huo kunatokana na mahojiano ya ana kwa ana ambayo Tanzania Daima imeyafanya jana na mmoja wa wazee wa Kijiji cha Pandambili ambaye alikuwa miongoni mwa watu wa mwanzo kufika katika eneo la ajali.

Mzee huyo, George Mwigunde ambaye anasema yeye ndiye aliyemtoa marehemu kutoka ndani ya gari kwa msaada wa wakazi wengine wa kijiji hicho kilicho katika Wilaya ya Kongwa, karibu kilomita 120 kutoka Dodoma mjini, alisema Wangwe alikuwa amekaa katika kiti cha abiria cha mkono wa kushoto wakati ajali hiyo ikitokea.

Mwigunde ambaye alijitambulisha kuwa ni mkulima wa kijiji hicho alisema, kabla ya kumtoa kutoka kitini, yeye mwenyewe ndiye aliyelazimika kumfungua mkanda wa gari kutoka katika kiti chake hicho alipokuwa ameketi.

Hata hivyo, alisema kutokana na namna mlango wa mbele wa abiria ulivyokuwa umeharibika walishindwa kumtoa upande huo, hali iliyowalazimisha wampitishie mlango wa dereva.

'‘Mimi ndiye niliyemfungua mkanda akiwa amekaa kiti cha mbele cha abiria, na kisha tukasaidiana na watu wengine kumtoa kutoka garini. Ingawa alikuwa akionekana kuwa na joto mwilini, alionekana akiwa ameshafariki dunia," alisema Mwigunde.

Mzee huyo ambaye alikuwa akizungumza wakati makachero kadhaa wa polisi wakiwa eneo la tukio hadi majira ya saa 6:00 mchana jana, alisema hata yeye na wenzake walishangazwa na maelezo waliyoyapata kutoka kwa Deus Mallya aliyekuwa katika gari hilo lililopata ajali, aliyewaeleza kuwa Wangwe ndiye aliyekuwa akiendesha gari.

'‘Nilisikia breki kali za gari na muda mfupi baadaye kishindo kikubwa kilifuatia, hali iliyosababisha niache shughuli zangu nyumbani kwangu na kukimbilia barabarani, nikijua kuwa kulikuwa na ajali iliyotokea.

'‘Nilipofika hapa nikiwa na mke wangu (anamuonyesha mwanamke aliye pembeni yake) tulimkuta kijana akizunguka zunguka kando ya gari akilalamika kuomba baada ya kupata ajali.

'‘Maelezo aliyotueleza kwamba marehemu ndiye aliyekuwa akiendesha gari yalinishtua. Kwanza marehemu alikuwa amekaa kiti cha abiria akiwa amefunga mkanda na mimi ndiye niliyemfungua," alisema mzee huyo na kisha akatoa maelezo kama hayo hayo kwa makachero wa polisi waliokuwa wakiendelea na uchunguzi wa ajali hiyo.

Miongoni mwa watu ambao walikuwapo eneo la tukio hilo jana, alikuwa ni mwanamke ambaye jina lake halikutambulika mara moja, aliyejitambulisha kuwa ni mke wa Profesa Samuel Wangwe ambaye ni kaka wa marehemu Chacha.

Mbali ya hilo, Mwigunde alisema kulikuwa na mtu mwingine wa tatu ambaye hakumtambua, aliyefika katika eneo la tukio muda mfupi baada baadaye, na akaanza kufanya kazi ya kuwazuia watu kusogelea eneo hilo la ajali huku akitoa maelezo ya kutaka mwili wa marehemu ukaguliwe iwapo ulikuwa na vitu vya thamani na kuvihifadhi.

Maelezo hayo ya Mwigunde yalisababisha Tanzania Daima ilazimike kurudi tena katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kufanya mahojiano zaidi na Mallya ili kumuuliza ukweli kuhusu nani aliyekuwa akiendesha gari wakati wa tukio.

Mallya kwa mara nyingine tena alisisitiza kwamba yeye hakuwa akiendesha gari hilo kwani hajui kuendesha kabisa na hajawahi kufanya kazi hiyo.

"Mimi sijui kuendesha gari dada, na wala sina utaalam wowote wa kuendesha magari, nimeshangazwa sana na taarifa za watoto wa marehemu zilizopo magazetini kwamba tulipotoka nyumbani nilikuwa namuendesha baba yao.

"Ninayaogopa sana magari, lakini niliwahi kujifunza gari mwaka 2004, nikiwa Nairobi, yupo rafiki yangu mmoja alinishawishi kujifunza, lakini niliacha, wakati najifunza niligonga ukuta, nikaumia vibaya na sikujifunza tena mpaka leo, hivyo sijui kabisa kuendesha," alisema Mallya.

Alisema kuwa walipoanza safari aliketi kiti cha mbele cha pembeni ya dereva huku akiwa anasinzia, Wangwe akamwambia ahamie kiti cha nyuma ili apumzike kwani si vizuri kusinzia akiwa kiti cha mbele.

Kwa mujibu wa Deus, walipofika eneo lenye maduka walisimama, Wangwe akanunua vocha kwa ajili ya simu yake ya mkononi na yeye akapata wasaa wa kuhama kutoka mbele na kwenda kukaa kiti cha nyuma.

Alisema alipokaa nyuma alifunga mkanda na kuendelea kusinzia wakati Wangwe akiwa anaendesha gari kabla ya ajali kutokea, maelezo ambayo yanapingana na yale yaliyotolewa na watoto wawili wa marehemu, Zakayo (17) na Bob (16) ambao wote walidai kuwa Mallya ndiye aliyekuwa akiendesha gari wakati wakitoka nyumbani.

"Wakati baba anaondoka nyumbani, alikuwa anaumwa na alionekana wazi kwamba ni mgonjwa, hivyo hakuwa anaendesha gari, aliyekuwa anaendesha gari ni rafiki yake anayeitwa Deus (Mallya) ambaye alikuwa amefikia hapa nyumbani tangu juzi," alisema Zakayo alipohojiwa na Tanzania Daima juzi.

Mallya katika maelezo yake ya jana alieleza kusikitishwa kwake na kauli za watoto wa marehemu, na kusema kwamba yeye hajui kuendesha gari na hajawahi kugusa usukani wa gari la Wangwe kwa lengo la kuendesha.

Aliwaomba watoto wa marehemu Wangwe kusimamia ukweli kwani kifo cha baba yao si mwisho wa urafiki wao, na amesema kwamba wapo huru kwenda kumuomba ushauri, atashirikiana nao kama kaka yao.

Alisema atasimamia ukweli na hayupo tayari kuongea uongo, kwani kifo cha rafiki yake Chacha kimemgusa sana kama kilivyowagusa wao.

"Nitaendelea kusema ukweli daima hata kama itanigharimu maisha yangu, sioni sababu ya kudanganya umma kufuatia kifo cha rafiki yangu kipenzi, na rafiki mzuri ni yule anayesimamia ukweli," alibainisha.

Utata huo kuhusu nini kilitokea hata kumsababishia umauti Wangwe, umesababisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilazimike kuandika barua kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema kikitaka kufanyika kwa uchunguzi wa kina.

CHADEMA katika tamko lake hilo lililotolewa jana, inasema imefikia uamuzi huo kutokana na kuwapo kwa taarifa zinazoonyesha kuwapo kwa utata katika tukio zima.

'‘Ninalazimika kukuandikia rasmi kuhusiana na taarifa ambazo zimekuwa zikiripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini, juu ya utata ambao umekigubika kifo hicho na haswa mazingira ya ajali yenyewe," ilisema taarifa hiyo ya CHADEMA iliyosainiwa na Naibu Katibu Mkuu wake, John Mnyika.

Chama hicho kimemtaka IGP kumchunguza Mallya na kubainisha ni mtu wa namna gani, ikiwa ni kufuatilia shughuli zake na uhusiano aliokuwa nao na marehemu Wangwe.

CHADEMA pia imemtaka IGP kuchunguza ukweli kuhusu maelezo ya Mallya na kujua ni wapi alikuwa amekaa wakati ajali ikitokea, na kuchukua hatua zinazopaswa baada ya uchunguzi huo.

'‘Tunapendekeza hatua hizo zichukuliwe mara moja kwani tunaamini kuwa kifo hiki kimegubikwa na utata mkubwa sana, na haswa kutokana na maelezo ambayo yamekuwa yakitolewa na aliyeshuhudia ajali (Deus Mallya) pamoja na watoto wa marehemu," alisema Mnyika katika tamko hilo la kwanza rasmi kutolewa na CHADEMA.
 
Huwa tunafanya hivi,
-Ukisha maliza kazi na pandikizi lako basi kinachofuatia ni kuliua hilo ili kupoteza ushahidi.ingekuwa mapandikiza hayauawi basi leo hii Balali angekuwepo au kungekuwa na maelezo mauuuri ya kifo chake toka serikalini.
Mfano:-ukiwa jambazi mkuu (fisadi),ukamtuma mtu wako kuua mtu A na kuchukua pesa,basi baada ya kufa huyo mtu A itafuatia mpango wa kuua huyo mtu wako.Na ndio maana katika trend ya mauaji huwa haiishi coz utaua hadi kuua.

-Kwa wale wanaobisha kuwa watu wa tarime siyo wagomvi basi wakaulize iliyokuwa ze comedy wao walipata wapi ujasiri na uhakika wa kuwaigiza watu hao kwa tabia yao ya ugomvi.Naamini ili haliitaji mjadala kwani hakuna hasiyejua hulka na silka ya sisi watu wa mkoa wa Mara aka Musoma.Yaani siku hizi wewe malibe unatukemea kuwa sisi siyo wagomvi???Aisee nitake radhi kwani mimi hili kwangu ilikuwa SIFA kubwa mno na nilijivunia kwa hilo kuwa mtu akiniudhi mimi ni kumgacha tu na kwa kutumia fahari hii niliweza kuishi pale Sekei (Idara ya Maji) Arusha swafi kabisaaa enzi zileeee na kwa jina tu la kuitwa mkurya nilipeta.Sasa leo kumbe tumekuwa wapole na wanasiasa kama watani zangu wahaya??hahahahahahaha hihihihikwkikwikwikwi

Acheni mambo ya ajabu kama wakurya tunapenda kupigana tuacheni tupigane, wengi nyie humu wajita na mnawaongelea wakurya vitu viwili tofauti. Na hiyo ccm yenu wameanza kueneza chuki huko tarime ole wao watu wauane tena kama damu za watu huko kihongera na korotambe hazijawatosha wamenyamaza kimya na sasa wanataka kuona damu zinamwagika zaidi in the name of msiba wa wangwe mshindwe.
 
"Mimi sijui kuendesha gari dada, na wala sina utaalam wowote wa kuendesha magari, nimeshangazwa sana na taarifa za watoto wa marehemu zilizopo magazetini kwamba tulipotoka nyumbani nilikuwa namuendesha baba yao."


my take---Hii inahashiria kwamba huyu kijana hakuwa na leseni wakati anendesha hivyo anaoogopa sheria kumbana kwa kuendesha gari bila leseni. kumbe masikini ndo anajiponza zaidi, bora aseme ukweli
 
By the way leo ni siku ya tano mapigano ya koo yanaendelea huko, i hope watasimama kwanza wakamzike wangwe and yet we have sirikali, polisi na jeshi na rais na mawaziri kibao ambao wala hawajali. naandika haya kwa uchungu coz i know what they are going through, na kila kukicha watu wanaimba tanzania kuna amani, nonsense.Kuna mtu anafikiria wajane na mayatima wanavyoongezeka huko? I repeat again serikali haioni? Ni kweli haiwezi kufanya kitu? kasehemu kadogo hako ka nchi kamewashinda kucontrol? au ndo mnawachunia kwa sabau tu walichagua chadema, now that chacha is gone are you going to do something? I wont be suprised that you will act now as a part of campaign mlichukue hilo jimbo. And he died thinking of helping his people out of those terribal tribal wars, may his soul rest in peace.
 
Nimemuona leo asubuhi Mallya TBC 1 kwa kweli yule kijana namuona kama amechanganyikiwa kabisa .....wamuache kwanza akitulia ndio ataweza kujibu vizuri....kwa sasa bado ana maluwe luwe....ukweli utajulikana tu...ila kwa sasa no way ..muda wake wa kumuhukumu badoo.....
 
Hivi wenye majina hawafi vifo vya kawaida bila "mkono" wa mtu? Ajali, magonjwa,... ni kwetu sisi tu!
 
Nimemuona leo asubuhi Mallya TBC 1 kwa kweli yule kijana namuona kama amechanganyikiwa kabisa .....wamuache kwanza akitulia ndio ataweza kujibu vizuri....kwa sasa bado ana maluwe luwe....ukweli utajulikana tu...ila kwa sasa no way ..muda wake wa kumuhukumu badoo.....

..sahihi,

..huyu kijana kwasasa anajiona kuwa yeye ndio atahukumiwa kwa mauaji. hayuko katika akili ya kawaida. in fact,anahitaji msaada wa kisaikolojia kwanza kabla hajasema lolote la maana.

..kwa kiasi fulani kwasasa watu wanaomhoji wanakuwa kama wanaongea na chizi tu.
 
Deus Fransis Mallya, mwanachama wa CCM na CHADEMA wakati huo huo. Deus Mallya yule kijana ambaye nusu ya siku huitumia pembeni ya mtaa wa Ufipa na nusu ya siku huitumia Mtaa wa Lumumba. Deus Mallya, kabla ya tukio hilo alitafuta namba za viongozi wote wakuu wa CHADEMA na waasisi wake na kuwapigia simu za kuwadodosa wiki moja kabla. Deus Mallya, wiki moja kabla ya tukio alimpigia pia Rostam Aziz. Anyway, tutaona mengi mwaka huu. Sitasema mengine, mpaka marehemu atakapopumzika mbele ya haki.

PM

Duh, mimi nazidi kuogopa. Ukiongeza habari za shahidi aliyenukuliwa na gazeti mojawapo la leo na hii ya kwako PPRZ nazidi kuogopa. Afadhali nikae kimya na kusikiliza kinachoendelea.
 
Hivi wenye majina hawafi vifo vya kawaida bila "mkono" wa mtu? Ajali, magonjwa,... ni kwetu sisi tu!

Mbona last week walikufa mtoto wa mbunge na dereva kwa ajari maeneo ya dodoma huko huko lakini hawakusema kuwa kuna mkono wa mtu? tukubali tu kuwa mungu amempangia kila mtu njia yake.
 
Adai Mbunge Wangwe hakuendesha gari lililopata ajali

Na Faraja Jube, Dodoma


UTATA umejitokeza iwapo marehemu Chacha Wangwe aliyefariki katika ajali ya gari Jumatatu usiku alikuwa akiendesha gari hilo ama la.


Kwa mujibu wa mtu aliyefika katika eneo la tukio dakika chache baada ya ajali hiyo, Mwiguni George, alimkuta marehemu Wangwe akiwa katika kiti cha mbele cha abiria huku sehemu ya kichwa chaki kikiwa kimebanwa ubavuni mwa kiti hicho na mlango wa nyuma.


Akizungumza juzi mbele ya Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishina Msaidizi wa Polisi, Peter Kivuyo, Kamanda wa Usalama Barabarani wa Mkoa wa Dodoma, Vitus Nikata na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kongwa, Ramadhan Kalowa, Georgr alieleza kwamba alikuta mwili wa marehemu Wangwe ukiwa umebanwa ubavuni mwa kiti na mlango wa nyuma huku mkanda wa usalama katika gari hilo ukiwa bado upo mwilini mwake.


''Nilikuwa nyumbani nasikiliza kipindi cha michezo, muda ya saa mbili na nusu usiku, nikasikia kishindo kikubwa, nikakimbilia eneo la ajali. Nilipofika katika eneo la ajali nilimkuta kijana mmoja akiwa analizunguka gari huku akipiga kelele za kuomba msaada,'' alieleza George.


Hata hivyo, mtu huyo alieleza mashaka yake kuwa kulikuwa na watu watatu katika gari hilo na siyo wawili kamba ambavyo ilitangazwa katika vyombo vya habari.


Juzi Deus Francis Mallya alikaririwa mara mwili wa marehemu ulipofikishwa katika hospitali ya Mkoa ya Dodoma, akisema kwamba walikuwapo wawili katika safari hiyo na kwamba marehemu Wangwe ndiye aliyekuwa akiendesha gari.


''Nilisikia katika taarifa ya habari kuwa walikuwa wawili. Marehemu ndiye aliyekuwa akiendesha gari na kwamba mmoja amepona. Mimi nina mashaka, kwani nahisi kuwa na mtu wa tatu na kwamba marehemu hakuwa anaendesha gari wakati wa tukio,'' alisema George na kuongeza.


''Nilipofika katika eneo la ajali kulikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa akiwatawanya watu walioanza kufika kwa ajili ya kutoa msaada wasilikaribie gari. Hata hivyo, tulianza kuutoa mwili wa marehemu uliokuwa katika kiti cha abiria upande wa mbele,'' alieleza George.


''Nilimvua mkanda wa usalama katika gari ambao bado ulikuwapo mwilini mwake, kisha tukamtoa kupitia mlango wa dereva kwani mlango upande aliokuwa amekaa haukuweza kufunguka,'' alisema.


Kwa mujibu wa Goerge, mtu huyo wa tatu alielekeza kutolewa kwa fedha alizokuwa nazo marehemu ndani ya mfuko wa koti, jambo ambalo lilimfanya shuhuda huyo kuhisi kuwa alikuwa pamoja nao.


''Tulianza kutoa vitu vya marehemu na mtu huyo alielekeza kuwa kuna fedha ndani ya mfuko wa koti,'' alieleza na kuhoji: ''Sasa mie nikajiuliza kama hakuwa nao alijuaje kuwa marehemu aliweka fedha ndani ya mfuko wa koti?''


Hata hivyo, shuhuda huyo alieleza kuwa wakati pilikapilika zilipokuwa zikiendelea, hakuweza tena kumuona mtu huyo wa tatu, ambaye alitoweka.


Maelezo hayo ya George yalipelekea Kamanda Kivuyo kuagiza askari waliokuwapo katika eneo hilo kuchukua maeleo ya shuhuda huyo kwa

ukamilifu.


''Kwanza nakupongeza sana kwa ujasiri wako na moyo wa kizalendo wa kutoa msaada kwa marehemu,'' Kamanda Kivuyo alimweleza shuhuda huyo.


Maelezo hayo yanaleta mkanganyiko kutokana na taarifa za awali kuwa marehemu Wangwe alikuwa akiendesha gari na kwamba walikuwapo watu wawili katika gari hilo.
 
Nimpongeze Mh. Zitto kwa namna ya pekee kabisa kwa kubeba MSALABA uliokuwa umelitangulia JENEZA bila kujali kuwa yeye ni MWISLAMU. Msalaba ni alama muhimu sana kwenye UKRISTO na ni Waislamu wachache sana wanaweza kuushika licha ya kuubeba kama alivyofanya Mh. Zitto.
 
5.JPG


Gari lililohitimisha maisha ya Chacha likiwa
limeharibika vibaya, watu wanajiuliza kumbe
huyu mtu hakuwa Fisadi alitumia tu kataksiii
wakati wengine wana mashangingi!!!!!!!!


Nimelitazama kwa makini hilo gari lilipata ajali lakini upande wa kulia anapokaa dereva halijaumia sana ila upande wa mbele kushoto anapokaa abiria ndiyo limeumia sana na kioo kimingia ndani. Hii inaongeza mashaka kuwa huenda Wange alikua ni abiria tu na si dereva na hii inaongeza mashaka zaidi kwa kuzingatia kauli ya shahid aliyenukuliwa na mojawapo ya magazeti ya leo kuwa kulikuwa na mtu mwingine.​
 
Mimi "my take" yangu baada ya kusoma magazeti mbalimbali na yale yaliyoandikwa humui JF ni kwamba;

1. Marehemu Chacha Wangwe alikuwa akiendeshwa na dereva ambae yeye marehemu Wangwe alim-recruit ili amfikishe Dar katika muda muafaka.

2. Hapo hapo palikuwa na kijana Malya ambae aliomba kusafiri na marehemu Wangwe kwenda Dar.

3. Gari hio kutokana na kuharibika vibaya, basi lilikuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kasi kubwa na zaidi ya hio 120km/hr anayosema Malya kwamba ndio anafikiri.

4. Huyo dereva kwa kuwa ni mtu wa Dodoma basi inawezekana baada ya ajali hio amerudi zake Dodoma na hatapatikana na pia inawezekana Malya hamkumbuki tena.

7. Wananchi wanajua ukweli na kama hawakuhusika na kifo cha marehemu Wangwe kwa kummalizia katika harakati za kumwibia basi wajitokeze kusaidia polisi kwani mahali ilipotokea ajali panaonekana pana watu wengi tu.

6. Chadema hawahusiki na lolote lile.

7. Polisi watakuja na majibu kwamba ilikuwa ni ajali kama zingine na gari lilikuwa kwenye mwendo wa kasi kubwa kabla ya kupatwa na ajali.

Jimbo la Tarime lijiandae kwa uchaguzi mdogo ambao ndio utatoa jibu la kama upinzani bado upo Tarime au umekwisha.

"my take" yako imekaa positive sana

ngoja tuendee kusubiria
 
5.JPG


Nimelitazama kwa makini hilo gari lilipata ajali lakini upande wa kulia anapokaa dereva halijaumia sana ila upande wa mbele kushoto anapokaa abiria ndiyo limeumia sana na kioo kimingia ndani. Hii inaongeza mashaka kuwa huenda Wange alikua ni abiria tu na si dereva na hii inaongeza mashaka zaidi kwa kuzingatia kauli ya shahid aliyenukuliwa na mojawapo ya magazeti ya leo kuwa kulikuwa na mtu mwingine.

...ndio hapo sasa, yaani wala haihitaji rocket science kulijibu hilo, wala kutafsiri kushoto kwa huyo mzee, au kwanini kiti chake (sababu ya impact) kilisukumwa mpaka nyuma upande wa abiria.

...
Kwa mujibu wa Goerge, mtu huyo wa tatu alielekeza kutolewa kwa fedha alizokuwa nazo marehemu ndani ya mfuko wa koti, jambo ambalo lilimfanya shuhuda huyo kuhisi kuwa alikuwa pamoja nao.

''Tulianza kutoa vitu vya marehemu na mtu huyo alielekeza kuwa kuna fedha ndani ya mfuko wa koti,'' alieleza na kuhoji: ''Sasa mie nikajiuliza kama hakuwa nao alijuaje kuwa marehemu aliweka fedha ndani ya mfuko wa koti?''

Hata hivyo, shuhuda huyo alieleza kuwa wakati pilikapilika zilipokuwa zikiendelea, hakuweza tena kumuona mtu huyo wa tatu, ambaye alitoweka.

...na hili wala halihitaji elimu ya unajimu kuwatambua vibaka wa aina hii kila ajali zikitokea Bongo siku hizi. Huyo mzee kama kawaida ya wanakuwa kwenye tukio kama hilo ali- assume huyo mtu wa tatu ni mmoja wa abiria, kumbe.... watu kazini!
 
Kwa historia iliyoletwa hapa JF kuhusu Deus, sio kijana mjinga aliyechanganyikiwa kama muonavyo. Ni kijana mjanja ajuaye anachokifanya, tatizo lake upeo wake wa kupanga hoja za uongo kama alivyoelekezwa sio mkubwa kwahiyo anachanganya na matokeo zinaonekana kama pumba. Mkimpa nafasi baadaye ataongea mambo ambayo hamtayaamini hata kidogo.

Sasa yenyewe anaonekana kuwakana watoto wa marehemu, lakini kuna ukweli mkubwa kwamba yeye ndio aliondosha gari nyumbani maana walipoondoka ni Deus alilazimisha kwakuwa Marehemu alikuwa hoi tena mnyonge na alikuwa ndani ya dozi. Isingewezekana Marehemu aendeshe halafu Deus ndio alale tena siti ya nyuma.

Deus angekuwa amechanganyikiwa angejikuta anasema ukweli kwa asilimia kubwa, hajachangikiwa ila hana upeo wa kupanga hoja za kukwepa ukweli.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom