Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
5.JPG


Gari lililohitimisha maisha ya Chacha likiwa
limeharibika vibaya, watu wanajiuliza kumbe
huyu mtu hakuwa Fisadi alitumia tu kataksiii
wakati wengine wana mashangingi!!!!!!!!


3.JPG


Mallya, jamaa aliyekuwa na Chacha katika gari lililopata ajali
.

2.JPG


Gari alilokula nalo mzinga likiwa linaondolewa
barabarani maeneo ya Pandambili, Dodoma jana.


1.JPG


Chacha enzi za uhai wake baada yakunyoa rasta!

Pictures Credit: http://mpoki.blogspot.com/
 

Nchini Tanzania kumejengeka tabaka hatari linalotumia siasa kama kivuli cha kuhalalisha kuwepo kwake, linatumia ushindi haramu kwenye uchaguzi kama pasipoti ya ufisadi, linatumia dola kutoa hukumu haramu (kama kifo) na mwisho linatumia ukondoo wa wananchi kama ngazi ya kujikita kwenye maovu yao. Ole wako ukipingana na hili kundi - orodha ya waliojaribu ni kubwa....
 
Mimi "my take" yangu baada ya kusoma magazeti mbalimbali na yale yaliyoandikwa humui JF ni kwamba;

1. Marehemu Chacha Wangwe alikuwa akiendeshwa na dereva ambae yeye marehemu Wangwe alim-recruit ili amfikishe Dar katika muda muafaka.

2. Hapo hapo palikuwa na kijana Malya ambae aliomba kusafiri na marehemu Wangwe kwenda Dar.

3. Gari hio kutokana na kuharibika vibaya, basi lilikuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kasi kubwa na zaidi ya hio 120km/hr anayosema Malya kwamba ndio anafikiri.

4. Huyo dereva kwa kuwa ni mtu wa Dodoma basi inawezekana baada ya ajali hio amerudi zake Dodoma na hatapatikana na pia inawezekana Malya hamkumbuki tena.

7. Wananchi wanajua ukweli na kama hawakuhusika na kifo cha marehemu Wangwe kwa kummalizia katika harakati za kumwibia basi wajitokeze kusaidia polisi kwani mahali ilipotokea ajali panaonekana pana watu wengi tu.

6. Chadema hawahusiki na lolote lile.

7. Polisi watakuja na majibu kwamba ilikuwa ni ajali kama zingine na gari lilikuwa kwenye mwendo wa kasi kubwa kabla ya kupatwa na ajali.

Jimbo la Tarime lijiandae kwa uchaguzi mdogo ambao ndio utatoa jibu la kama upinzani bado upo Tarime au umekwisha.
 
tusimshuku huyu kijana kuwa alihusika moja kwa moja.. ila ni mtu pekee ambaye akiulizwa vizuri atakuwa ni ufunguo wa kuelewa nini kilichotokea.
 
Kuna anaefahamu au yeyote yule ambae amefanikiwa kupata "profile" ya huyu Deus Malya?.

Nauliza hivi kwa sababu kwa sasa vijana wengi wenzangu hawana kazi wanaweza kuzurura mpaka Dodoma na kurudi Masaki.

Ni vizuri akajulikana zaidi ya wale ambao wamekwishawahi kuelezwa kuhusika na hizi ajali ambazo zinahisiwa kuwa na utata.
 
cha Wangwe: Shuhuda atoa taarifa mpya polisi





Mkazi wa eneo la Pandambili, Mwiguni George, aliyefika dakika chache katika eneo la Pandambili baada ya kutokea ajali iliyosababisha kifo cha Mbune Chacha Wangwe, akieleza hali ilivyokuwa kwa Kamanda wa Polisi, Peter Kivuyo, (kulia).
* Adai Mbunge Wangwe hakuendesha gari lililopata ajali

Na Faraja Jube, Dodoma


UTATA umejitokeza iwapo marehemu Chacha Wangwe aliyefariki katika ajali ya gari Jumatatu usiku alikuwa akiendesha gari hilo ama la.


Kwa mujibu wa mtu aliyefika katika eneo la tukio dakika chache baada ya ajali hiyo, Mwiguni George, alimkuta marehemu Wangwe akiwa katika kiti cha mbele cha abiria huku sehemu ya kichwa chaki kikiwa kimebanwa ubavuni mwa kiti hicho na mlango wa nyuma.


Akizungumza juzi mbele ya Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishina Msaidizi wa Polisi, Peter Kivuyo, Kamanda wa Usalama Barabarani wa Mkoa wa Dodoma, Vitus Nikata na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kongwa, Ramadhan Kalowa, Georgr alieleza kwamba alikuta mwili wa marehemu Wangwe ukiwa umebanwa ubavuni mwa kiti na mlango wa nyuma huku mkanda wa usalama katika gari hilo ukiwa bado upo mwilini mwake.


''Nilikuwa nyumbani nasikiliza kipindi cha michezo, muda ya saa mbili na nusu usiku, nikasikia kishindo kikubwa, nikakimbilia eneo la ajali. Nilipofika katika eneo la ajali nilimkuta kijana mmoja akiwa analizunguka gari huku akipiga kelele za kuomba msaada,'' alieleza George.


Hata hivyo, mtu huyo alieleza mashaka yake kuwa kulikuwa na watu watatu katika gari hilo na siyo wawili kamba ambavyo ilitangazwa katika vyombo vya habari.


Juzi Deus Francis Mallya alikaririwa mara mwili wa marehemu ulipofikishwa katika hospitali ya Mkoa ya Dodoma, akisema kwamba walikuwapo wawili katika safari hiyo na kwamba marehemu Wangwe ndiye aliyekuwa akiendesha gari.


''Nilisikia katika taarifa ya habari kuwa walikuwa wawili. Marehemu ndiye aliyekuwa akiendesha gari na kwamba mmoja amepona. Mimi nina mashaka, kwani nahisi kuwa na mtu wa tatu na kwamba marehemu hakuwa anaendesha gari wakati wa tukio,'' alisema George na kuongeza.


''Nilipofika katika eneo la ajali kulikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa akiwatawanya watu walioanza kufika kwa ajili ya kutoa msaada wasilikaribie gari. Hata hivyo, tulianza kuutoa mwili wa marehemu uliokuwa katika kiti cha abiria upande wa mbele,'' alieleza George.


''Nilimvua mkanda wa usalama katika gari ambao bado ulikuwapo mwilini mwake, kisha tukamtoa kupitia mlango wa dereva kwani mlango upande aliokuwa amekaa haukuweza kufunguka,'' alisema.


Kwa mujibu wa Goerge, mtu huyo wa tatu alielekeza kutolewa kwa fedha alizokuwa nazo marehemu ndani ya mfuko wa koti, jambo ambalo lilimfanya shuhuda huyo kuhisi kuwa alikuwa pamoja nao.


''Tulianza kutoa vitu vya marehemu na mtu huyo alielekeza kuwa kuna fedha ndani ya mfuko wa koti,'' alieleza na kuhoji: ''Sasa mie nikajiuliza kama hakuwa nao alijuaje kuwa marehemu aliweka fedha ndani ya mfuko wa koti?''


Hata hivyo, shuhuda huyo alieleza kuwa wakati pilikapilika zilipokuwa zikiendelea, hakuweza tena kumuona mtu huyo wa tatu, ambaye alitoweka.


Maelezo hayo ya George yalipelekea Kamanda Kivuyo kuagiza askari waliokuwapo katika eneo hilo kuchukua maeleo ya shuhuda huyo kwa

ukamilifu.


''Kwanza nakupongeza sana kwa ujasiri wako na moyo wa kizalendo wa kutoa msaada kwa marehemu,'' Kamanda Kivuyo alimweleza shuhuda huyo.


Maelezo hayo yanaleta mkanganyiko kutokana na taarifa za awali kuwa marehemu Wangwe alikuwa akiendesha gari na kwamba walikuwapo watu wawili katika gari hilo.


Haya tusubiri atakachosema huyu Malya
 
Tunashukuru sana kwa reference na hatimaye picha kabisa kutoka mpoki.blogspot...., Huyu anaonekana kijana mwadilifu kwa sura lakini kisaikolojia hakuna nyoka mwenye sura mbaya. Hata hivyo kwa dataz ziloletwa hapa recently huyu Bwana mdogo ana maswali mengi ya kujibu kwa wananchi, sio kwa polisi maana msitegemee lolote kutoka kwa hawa vibaraka wa wakoloni weusi walioko Tanzania. They have never done a good job over these kind of issues.

Kama PM alisema huyu kijana alifanya mengi kwenye muda wa wiki hadi mwezi kabla ya msiba huu, mfano kutafuta namba za simu za viongozi wa Chadema na kuwazuzua, kuongea na RA wiki moja kabla... na mengine. Kisha huyu kijana kihistoria alishawahi kujifanya "Invisible" wa JF...??? Why??? akapigwa mkwara akatulia, kisha tumeambiwa ni CCM na Chadema at the same time...??? HUU NI MTANDAO...!!!

Sura yake haionyeshi wasiwasi na mshituko wa ajali mbaya kama iliyotokea na kumuua Wangwe "On the Spot"...??? Sura yake inaonyesha ujuzi wa matukio. Simhukumu ila namsoma sura kwa namna niijuayo. Majibu yake yanaonyesha alifundishwa kupanga majibu lakini akayachanganya, kwahiyo ukiunganisha unapata pumba, ukizitoa unabaki ukweli kwamba anahusika na jambo fulani mahala fulani.

Swali langu kubwa ni kwamba, yeye ndio alimlazimisha Marehemu kusafiri na alimwamsha kwa nguvu wakati mtoto wa marehemu alipokataa kumwamsha, Marehemu alioga na akaamua kuondoka lakini akiwa bado mnyonge tena ndani ya dozi ya malaria...!!! Bw. Mallya ndio alitengeneza gari ambalo mbele ya safari lilionekana lina tatizo kisha kurudi tena garage...!!! Wakaondoka kutoka nyumbani saa 1 jioni, IWEJE SAA 2.55 Marehemu (ambaye alikuwa hoi) ndio alikuwa shupavu kama dereva na Bw. Mallya alikuwa nyuma kama mgonjwa aliyezidiwa na usingizi...??? Nimeona baadaye amekubali kwamba alikuwa anaendesha yeye, je kama haya yote ni kweli..., nani atahakikisha huyu kijana anabanwa kusema NANI SOURCE YA HAYA YOTE...? Kisha kutupa ukweli wa mambo nasi tukajihadhari huko mbeleni...? ikiwa pamoja na kumhukumu mhusika...???
 
cha Wangwe: Shuhuda atoa taarifa mpya polisi





Mkazi wa eneo la Pandambili, Mwiguni George, aliyefika dakika chache katika eneo la Pandambili baada ya kutokea ajali iliyosababisha kifo cha Mbune Chacha Wangwe, akieleza hali ilivyokuwa kwa Kamanda wa Polisi, Peter Kivuyo, (kulia).
* Adai Mbunge Wangwe hakuendesha gari lililopata ajali

Na Faraja Jube, Dodoma


UTATA umejitokeza iwapo marehemu Chacha Wangwe aliyefariki katika ajali ya gari Jumatatu usiku alikuwa akiendesha gari hilo ama la.


Kwa mujibu wa mtu aliyefika katika eneo la tukio dakika chache baada ya ajali hiyo, Mwiguni George, alimkuta marehemu Wangwe akiwa katika kiti cha mbele cha abiria huku sehemu ya kichwa chaki kikiwa kimebanwa ubavuni mwa kiti hicho na mlango wa nyuma.


Akizungumza juzi mbele ya Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishina Msaidizi wa Polisi, Peter Kivuyo, Kamanda wa Usalama Barabarani wa Mkoa wa Dodoma, Vitus Nikata na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Kongwa, Ramadhan Kalowa, Georgr alieleza kwamba alikuta mwili wa marehemu Wangwe ukiwa umebanwa ubavuni mwa kiti na mlango wa nyuma huku mkanda wa usalama katika gari hilo ukiwa bado upo mwilini mwake.


''Nilikuwa nyumbani nasikiliza kipindi cha michezo, muda ya saa mbili na nusu usiku, nikasikia kishindo kikubwa, nikakimbilia eneo la ajali. Nilipofika katika eneo la ajali nilimkuta kijana mmoja akiwa analizunguka gari huku akipiga kelele za kuomba msaada,'' alieleza George.


Hata hivyo, mtu huyo alieleza mashaka yake kuwa kulikuwa na watu watatu katika gari hilo na siyo wawili kamba ambavyo ilitangazwa katika vyombo vya habari.


Juzi Deus Francis Mallya alikaririwa mara mwili wa marehemu ulipofikishwa katika hospitali ya Mkoa ya Dodoma, akisema kwamba walikuwapo wawili katika safari hiyo na kwamba marehemu Wangwe ndiye aliyekuwa akiendesha gari.


''Nilisikia katika taarifa ya habari kuwa walikuwa wawili. Marehemu ndiye aliyekuwa akiendesha gari na kwamba mmoja amepona. Mimi nina mashaka, kwani nahisi kuwa na mtu wa tatu na kwamba marehemu hakuwa anaendesha gari wakati wa tukio,'' alisema George na kuongeza.


''Nilipofika katika eneo la ajali kulikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa akiwatawanya watu walioanza kufika kwa ajili ya kutoa msaada wasilikaribie gari. Hata hivyo, tulianza kuutoa mwili wa marehemu uliokuwa katika kiti cha abiria upande wa mbele,'' alieleza George.


''Nilimvua mkanda wa usalama katika gari ambao bado ulikuwapo mwilini mwake, kisha tukamtoa kupitia mlango wa dereva kwani mlango upande aliokuwa amekaa haukuweza kufunguka,'' alisema.


Kwa mujibu wa Goerge, mtu huyo wa tatu alielekeza kutolewa kwa fedha alizokuwa nazo marehemu ndani ya mfuko wa koti, jambo ambalo lilimfanya shuhuda huyo kuhisi kuwa alikuwa pamoja nao.


''Tulianza kutoa vitu vya marehemu na mtu huyo alielekeza kuwa kuna fedha ndani ya mfuko wa koti,'' alieleza na kuhoji: ''Sasa mie nikajiuliza kama hakuwa nao alijuaje kuwa marehemu aliweka fedha ndani ya mfuko wa koti?''


Hata hivyo, shuhuda huyo alieleza kuwa wakati pilikapilika zilipokuwa zikiendelea, hakuweza tena kumuona mtu huyo wa tatu, ambaye alitoweka.


Maelezo hayo ya George yalipelekea Kamanda Kivuyo kuagiza askari waliokuwapo katika eneo hilo kuchukua maeleo ya shuhuda huyo kwa

ukamilifu.


''Kwanza nakupongeza sana kwa ujasiri wako na moyo wa kizalendo wa kutoa msaada kwa marehemu,'' Kamanda Kivuyo alimweleza shuhuda huyo.


Maelezo hayo yanaleta mkanganyiko kutokana na taarifa za awali kuwa marehemu Wangwe alikuwa akiendesha gari na kwamba walikuwapo watu wawili katika gari hilo.


Haya tusubiri atakachosema huyu Malya

Nimesoma habari hii ikanishangaza sana.
 
Kuhusu huyo mtu wa tatu ni utata mkubwa kuliko yote maana haiwezekani kumpa lifti mtu usiyemjua tena usiku, hata hivyo ilikuwaje mtu huyo kuwa ni mzima kabisa baada ya ajali maana kwa shahidi mzee wa jirani alimkuta huyo mtu wa tatu eneo la tukio na yeye ndio alimwelekeza mwokoaji kutoa pia hela kwenye mfuko wa Marehemu. Kwanini hakuonekana baada ya hapo...??? Sio swali la kujiuliza kwamba Deus Francis Mallya anamfahamu, Deus anaonekana kuwa kijana mjanja mjanja sana na issue yake mtasikia itaishia hivi hivi kimya kimya, nina hakika asilimia kubwa Deus hatajiua kwa ajili ya hili, sio mtu mzima wa akili ya kujitoa roho kwa hili maana kwa ujumla haonekani kushtuka wala kuumia kuhusu msiba wa ghalfa uliomhusisha moja kwa moja kama huu, sana sana hatari niionayo anaweza kutolewa roho kwasababu anachanganya maelezo na kutoa nafasi kubwa ya kumtambua mhusika kirahisi.

Nimesikia fununu kwamba waandishi watapewa nafasi ya kuongea naye, hana akili ndefu huyo. Ni kama robot, akikosa maelekezo anapotea. Kwahiyo ninyi waandishi mkimbania kidogo sana kwenye kona mtapata majibu bila kutoa jasho hata kidogo.

Nasema tena, sijamhukumu. Lakini majibu kuhusu kila kitu anayo yeye. Aulizwe tena kwa utaratibu lakini mapema iwezekanavyo kabla Mafia hawajafanya kazi yao.
 
tusimshuku huyu kijana kuwa alihusika moja kwa moja.. ila ni mtu pekee ambaye akiulizwa vizuri atakuwa ni ufunguo wa kuelewa nini kilichotokea.

MKJJ Mimi nashangaa sijui ni kwanini watu wengine wanakuwa wagumu kuelewa halafu wana rush kwenye judgement.
 
Nimesoma habari hii ikanishangaza sana.

Hili linaibua mapya kabisaa,nadhani huyu mzee ni mkweli maana ni shuhuda tu kama by stander na kama kuna mtu alikuwa akimpa maelekezo na hajamtambua kama ni malya sasa huyo mtu ni nani?na huyu anathibitisha marehemu hakuwa anaendesha gari kwani yeye ndio kamfungua seat belt sasa nani aliendesha wakati malya anadai alikuwa siti ya nyuma hakugusa usukani?
mmh,it leaves many to be desired
 
Najua mtashangaa kwamba nimeenda moja kwa moja kwenye judgement lakini ni maoni ya uchunguzi wangu baada ya kupitia magazeti, umbea, minong'ono, vituo vya televisheni, redio na mwisho post zote za JF kuhusu hili, hata hivyo nimesisitiza kwamba hapa mimi bado sijahukumu mtu.

La msingi, huyu Deus ndiye majibu yote kuhusu lililotokea na nasikitika sana kwamba polisi hawataleta judgement yeyote yenye kuleta sura. Sijui...??? Nitashangaa kama kwenye hili watakuwa wanyoofu..., NAKUBALI KUWASUBIRI TUONE...!
 
Malya.. ana historia kidogo na viongozi wa Chadema; historia pekee inayokosekana ni uhusiano wake na Wangwe, hili linaonekana ni la siku za karibuni sana. Ka nzi ka KLHN ambako kamepeperuka kwa muda maeneo ya DDM na Dar kanaeleza pasipo shaka kuwa Malya amejaribu kujiweka karibu na viongozi wa Chadema kwa muda sasa na amefika makao makuu kama mjasiriamali akatolewa nje. Baada ya kutolewa nje akawa ameandika barua kadhaa za malalamiko kwa kiongozi mmoja wa juu wa Chadema.

Siku chache zilizopita alimkaribia kiongozi mwingine na kutoa wazo kuwa angependa kuandika biograph yake;

inatosha kwa usiku huu: ka nzi kameenda kulala.

one more.. siku moja aliwahi kujitokeza akiwa amebadili rangi za nywele zake akidai kuwa alikuwa ameigiza kwenye mchezo mmoja wa luninga..!!
 
Wangwe alishauwawa na ajali inaweza kuwa set up..Inawezekana walimlima risasi ya kichwa...Kwani wakifanya uchunguzi watajuwa...Pia hiyo damu ya passengers side nayo ni ya Wangwe...Sidhani kama damu ya kijana itakutwa kwenye gari.
Pili kijana inaelekea alikuwa hajui kinachoendelea kwa undani ila amepewa maagizo.
Ni muhimu kujuwa ni nani alimwambia kijana atowe msisitizo wa safari ya Wangwe..Imean UMUHIMU WA SAFARI VS UGONJWA WA MAREHEMU...Je ni kwsababu ya msiba ama alikuwa na miadi mingine?
Kwasababu kama kulikuwa na mambo ya siri za serikali kutolewa..Ni lazima watu wenye kula pande mbili wakawa target ya either side...Ama conspiring...Lakini ukweli unaweza kuwekwa bayana...Ama tukansema tuje pamoja na kuudai UHURU WETU.
 
Hili swala limechukua sura nzuri sana baada ya yule mwanakijiji (siyo wewe MZEE MWANAKIJIJI wa JF teh!!! teh!!! teh!!!) kutoa ushahidi wake.

(a)Ametoa ukweli kuwa gari lilikuwa linaendesha na mtu mwingine kwa vile marehemu alikuwa kwenye kiti cha abiria huku amefunga mkanda wake. Dereva yule anaweza kuwa aliangusha gari makusudi.

(b) Amedhihirisha kuwa kulikuwa na mtu wa tatu kwenye gari lile ambaye alikuwa anafahamu fika kuwa marehemu alikuwa ameweka hela kwenye koti lake. Kitendo cha mtu huyu wa tatu kujificha kinatia wasiwasi sana kuhusu uhusika wake kwenye ile ajali.

(c) Deusi Mallya alianza kwa kueleza kuwa gari lilikuwa linaendshwa na marehemu. Ushahidi ulitolewa na George unaonyesha vinginveyo: ama Mallya hakuwa na uhakika kuwa ni nani alikuwa anaendesha gari au anajua mambo yote ila anafisha tu. Inawezekana gari lilikuwa na watu zaidi ya hao watatu.

(d) Shahidi pekee aliyepo ambaye anaweza kutupa ukweli zaidi ni huyu Deusi Mallya.

(e) Kama kweli kuna conspiracy katika ajali hii basi huenda hata huyu Deusi Mallya na yule shahidi Mwiguni George wakawa hatarini ili kuficha ushahidi. YAANI KAMA KWELI KUNA CONSPIRACY
 
Malya.. ana historia kidogo na viongozi wa Chadema; historia pekee inayokosekana ni uhusiano wake na Wangwe, hili linaonekana ni la siku za karibuni sana. Ka nzi ka KLHN ambako kamepeperuka kwa muda maeneo ya DDM na Dar kanaeleza pasipo shaka kuwa Malya amejaribu kujiweka karibu na viongozi wa Chadema kwa muda sasa na amefika makao makuu kama mjasiriamali akatolewa nje. Baada ya kutolewa nje akawa ameandika barua kadhaa za malalamiko kwa kiongozi mmoja wa juu wa Chadema.

Siku chache zilizopita alimkaribia kiongozi mwingine na kutoa wazo kuwa angependa kuandika biograph yake;

inatosha kwa usiku huu: ka nzi kameenda kulala.

one more.. siku moja aliwahi kujitokeza akiwa amebadili rangi za nywele zake akidai kuwa alikuwa ameigiza kwenye mchezo mmoja wa luninga..!!

Swali la muhimu hapa...POLISI WATAKUBALI DEUS MALLYA AMTAJE MTU ALIYEMTUMA?
Je watauweka ukweli wazi?

Kama alikataliwa na MAKAO MAKUU...Ni kivipi Marehemu akawa rafiki wake?
Huyu kijana ni mtu hatari....Ila ametumiwa na amtaje aliyemtuma.

Tena tuanze na aliyemtuma atowe msisitizo wa umuhimu wa safari ya Wangwe.

Kwasababu Wangwe naye aliamka licha ya ugonjwa wake mara baada ya kuongea na Mallya...Basi na yeye alikuwa anaujuwa umuhimu wa safari yake...Na ili sisi tuweze kuujuwa umuhimu huo uliomfanya marehemu ashindwe kughairisha safari na kuikataa amri ya bwana mdogo Mallya...Ni wazi miadi ilikuwa mizito!Tunatakiwa tujuwe alikuwa na miadi ya kukutana na nani huko Dar.

Simu ziwe traced kuona ni nani marehemu aliwasiliana nao kabla ya ajali..Baada ya ajali ambapo ni kijana alifanya mawasiliano.
Haijalishi ni nani alikuwa na miadi naye lakini panaweza kuwa pazuri kuanzia.

Kwasababu kijana alifanya maamuzi kama vile alipewa amri na yeye...Kwani alipiga simu kwa watu muhimu muhimu sana na alipewa hayo maagizo..Maagizo ambayo ni vigumu kuyafuata kama kweli na wewe umepatwa na ajali.
 
Swali la muhimu hapa...POLISI WATAKUBALI DEUS MALLYA AMTAJE MTU ALIYEMTUMA?
Je watauweka ukweli wazi?

Kama alikataliwa na MAKAO MAKUU...Ni kivipi Marehemu akawa rafiki wake?
Huyu kijana ni mtu hatari....Ila ametumiwa na amtaje aliyemtuma.

Inategemea na interrogation techniques wanazotumia wapelelezi wetu; ila wasitumie zile za Guantanamo Bay.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom