Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Swali la muhimu hapa...POLISI WATAKUBALI DEUS MALLYA AMTAJE MTU ALIYEMTUMA?
Je watauweka ukweli wazi?

Kama alikataliwa na MAKAO MAKUU...Ni kivipi Marehemu akawa rafiki wake?
Huyu kijana ni mtu hatari....Ila ametumiwa na amtaje aliyemtuma.

Tena tuanze na aliyemtuma atowe msisitizo wa umuhimu wa safari ya Wangwe.

Kwasababu Wangwe naye aliamka licha ya ugonjwa wake mara baada ya kuongea na Mallya...Basi na yeye alikuwa anaujuwa umuhimu wa safari yake...Na ili sisi tuweze kuujuwa umuhimu huo uliomfanya marehemu ashindwe kughairisha safari na kuikataa amri ya bwana mdogo Mallya...Ni wazi miadi ilikuwa mizito!Tunatakiwa tujuwe alikuwa na miadi ya kukutana na nani huko Dar.
Simu ziwe traced kuona ni nani marehemu aliwasiliana nao kabla ya ajali..Baada ya ajali ambapo ni kijana alifanya mawasiliano.
Haijalishi ni nani alikuwa na miadi naye lakini panaweza kuwa pazuri kuanzia.

Kwasababu kijana alifanya maamuzi kama vile alipewa amri na yeye...Kwani alipiga simu kwa watu muhimu muhimu sana na alipewa hayo maagizo..Maagizo ambayo ni vigumu kuyafuata kama kweli na wewe umepatwa na ajali.

Maneno makubwa haya mkuu, na yana clue kubwa ndani yake,

Kwani Kuja kuhudhuria msiba wa Bhoke kuna uhusiano gani na uhimizwaji wa safari na Malya?

Kwa jinsi hali ilivo kuwa ndani ya chama chake je ingewezekana aitwe na chama usiku usiku aende?

Je huenda huu wito hauna uhusiano wowote na chama chake ambacho hadi mauti yana mkumba walikuwa wakitofautiana kimtazamo?
 
Horace Kolimba alikuwa katibu mkuu wa CCM akagongana na wenzake na muda si mrefu akafariki, uvumi ulioenezwa ni kuwa wale aliogongana nao kimawazo ndani ya chama chake wamemkolimba, haikusemwa kuwa wapinzani wamemkolimba ilitizamwa kuwa kabla ya kufa Marehemu alikuwa na ugomvi na watu gani.

mfano wa pili wa kifo cha Marehemu Amina Chifupa hakikuusishwa na Chadema wala CUF, uvumi wote ni kuwa Amina alikuwa na nia ya kugombea uenyekiti wa CCM kundi la vijana mwaka huu na baadhi ya wana CCM wenzake hawataki agombee ndio wamemfupishia maisha yake.

hakuna aliyesema kuwa CUF wamehusika na kifo cha Amina,

kama alivyopania Marehemu Wangwe kuchukua uenyekiti wa Taifa Chadema,jee wamezima azima yake? kwani Wangwe alisema kuwa uamuzi wa mwisho juu ya hatima yake wanayo wanachama wa Chadema wa nchi nzima sio kundi la wahuni wa makao makuu ya Chadema, na uzoefu unaonesha kuwa Wangwe kwenye chaguzi ni ngumu kumzuia kama alivyopita kwenye umakamu wa Mwenyekiti na kwenye uenye kiti kulikuwa hakuna cha kumzuia.

Mfano wa tatu ni wa Junior Malecela aliyekuwa kwenye sakata la uchaguzi wa vijana na akapata ajali kama WANGWE,alipokufa kifo chake kilihusishwa na chama chake si vyama tofauti.

Wangwe alikuwa na mgongano wa kimawazo na wana Chadema wengi hadi wengine wakasema kuwa afutwe uanachama, wengine wakasema apigwe risasi humu humu JF,wengine wakasema ni Pandikizi la CCM kupitia kwa Rostam na alinunuliwa akiwa Movenpick hotel.

kama CCM walimnunua kwanini wamuue? kama kipimo cha kumpimia Kolimba kilikuwa alikolimbwa na wana CCM wenzake kwa kugongana kimtazamo kama alivyogongana Wangwe na wana chadema wenzake,kwanini tusihusishe kifo chake na mgongano wa kimawazo na wenzake ndani ya chama chake?

katika vita ya ufisadi anayesema kauli hiyo ni Slaaa sio Wangwe basi wangemuua Slaa,lakini Mwanakijiji ana msemo wake kuwa kipimo kiwe kimoja nakubaliana nae,kuwa kipimo cha Kolimba aliyekuwa na mgongani wa kimtazamo na kimawazo na wanaccm,kinafaa kutumika kwenye kadhia hii ya Wangwe, alipofariki DR.OMAR ALI JUMA haiukuhusishwa CUF ni wana CCM wenzake ndio waliovumishiwa ubaya na hilo hadi kwa marehemu Sokoine. mchawi siku zote ni jirani au mtu wako wa karibu hamlijui hilo?
Huo ndio ukweli kama ni kumtafuta mchawi CHADEMA tutawashuku kwa 99% na CCM 1% Maana hali inajionyesha kama kwa Kolimba n.k
 
Hivi mtu hawezi kufa kifo cha kawaida?Mie nadhanin tuamini Mhe. amkufa kwa kifo cha kawaida kwa kuwa hamna ambaye yuko tayari kusema nini chanzo cha habari.Hata MWanakijiji anaendelea kufanya Speculation ila hataki kueleza anachokijua kuhsu Ajali hiyo

IGP Mwema kaomba mwenye ushahidi aupeleke,Na mie ningependekeza Mnyika Apeleke Ushahidi kwa yale aliyoyasema na maswali aliyonhayo kichwani.Kwa maelezo yake anajua Menngi sana kuhusu hili.Na kama CHADEMA wasipokuwa Makini hili suala linaweza likaharibu kabisa Credibity ya Chama chao
 
Ni kwa nini mara nyingi ikitokea ajali kama hii utasikia kulikuwa na mtu mmoja ambaye hakutambulika.Ile ya marehemu Mbatia kulikuwa na mtu ambaye mpaka leo hajulikani ni nani,hii pia tunaambiwa kuwa kulikuwa na mtu wa tatu ambaye hajulikani.
 
MKJJ Hapo ndipo penye utata wenyewe...Kwangu binafsi nafikiri huyo kijana ni shahidi mzuri sana tu.
Kwanza kabla ya kuanza kuzungumzia haya...Ni bora tuanze na wale ambao wanaweza kunufaika na kifo chake.
Kama huyo kijana alidai kuwa kazi zinalala...Ni kazi gani zilizokuwa zinalala?
Si walikuwa wakienda msibani?
Je ni nani mwingine aliyekuwa akijuwa kuhusu kazi yake ya huko msibani?
Alikuwa akienda kumwakilisha nani kwenye msiba wa Bhoke?
Chama,ama familia ama ni yeye binafsi?
Pia inabidi tuzungumzie issue ya yeye kupambana na Barrick huko kijijini kwake...Hivi mnaijuwa Barrick nyie watu?
Huyu mtu ni kweli alikuwa mpambanaji...Tatizo ni tamaa ya madaraka...Na kutokuwa mwangalifu kwenye siasa zetu...Sasa anaweza akawa ameuwawa na mafisadi kwa namna ambayo italeta vurugu kwenye jamii...!
Marehemu Wangwe ni kweli alikuwa akiyapigania maslahi ya wananchi wake wa jimboni...Na alihamia chadema kwani wananchi walishachoshwa na ccm.
Sasa na yeye huo ukaribu wake na ccm bila kuwa mwangalifu halafu akiwa anawapinga tena kuhusiana na Barrick?
Si alikuwa kinyume kabisa na mkuu wa Polisi wa mkoa na kuu wa mkoa mwenyewe?
Yeye kama mbunge alikuwa tishio...Lakini at the same time...Tamaa ya madaraka ilimponza na hakuchukuwa maamuzi ya busara licha ya nia nzuri aliyokuwa nayo!
ccm wasilete UNAFIKI kabisa kwani huyu mtu alikuwa akipinga sana unyanyasaji wa serikali huko kwenye migodi kwa kuwatumia polisi na hata hoja yake aliyokuwa akitaka kuiwakilisha ilizimwa kwa kila namna na wakati akikaribia kuiwakilisha ndio akafa.
Na ili kumuenzi wabunge wanadai kuwa hoja yake hiyo ya mapigano hayo ya koo ifanyiwe kazi na isomwe bungeni.
Hoja hiyo ikisomwa pia tutapa clues nyingi sana.
Na ndio maana nikasema makabila mengine jamani tujifunze kuishi kama watanzania...Sasa unaweza kukuta labda hizo koo huko mara zinagombea ardhi yenye madini..Sasa dunia ya sasa ukoo wa kiafrika unamiliki madini ya Wananchi...wapi na wapi.
Hizo ardhi wanazogombea huko hao wanaojiona ni machifu si ni za Tanzania?
Tunataka mtuletee issues hapa na si kuletea assumptions ambazo hazina kichwa wala miguu!
Kwanza hizo tairi unaweza kuta zilipigwa risasi.
Na kwa uzoefu wangu mimi...Marehemu Wangwe nayeye inanishangaza sana alipoamuwa kuendelea na safari licha ya dalili zote hizo!
Ni wazi alijuwa ana mess na something BIG!
Lakini inaonyesha alijitowa MUHANGA!
Kitendo cha nuts kulegea kwenye gari yake kilitosha kumfana ajiulize maswali mengi kwani si kitu cha kawaida kuwa na nati zisizofiti na ama kutight kama kweli gari hilo ni lake na analitumia kila siku!
Na huyo kijana na historia ya jinsi walivyojuwanan iwekwe hapa!
Huyo kijana kule Kilimanjaro huwa wanaitwa NYOKA.
Hawa Nyoka kazi yao ni kuhakikisha mambo yote ni sawa ikiwa na uzima wa gari na kila kitu!
Sasa ika vipi NYOKA akalala nyuma na Bosi kuendesha?
Tena MH MBUNGE?
Pana UTATA HAPO!
Wangwe alikuwa akienda kukutana na nani?
Nani mwingine aliyekuwa akijuwa ratiba yao?
Kabla ya ajali na safari na mara baada ya ajali...Hizo namba zote za simu zilizopigwa na nyoka kwa kutumia simu yake na ya Wangwe zichunguzwe.
Nyendo zao wote zichunguzwe
Kwa sasa tuanzie hapo.
INASIKITISHA SANA!
MACHOZI YA MAMBA YA ccm YATAWACOST kama haki isipotendeka kwani wao ndio wanao miliki dola na wananchi wanataka majibu.

jMushi,
Mbona hujaeleza kuwa Wangwe alitofautiana na Mwenyekiti wa CHADEMA na aliahidi kugombea nafasi hiyo kurekebisha mambo.

Iliandikwa kuwa Wangwe apigwe risasi, kisa mtafaruku wa CHADEMA, hili mbona hujaliandika au kuna ukweli mahali sasa unataka kupoteza lengo?

Huenda wewe kama anavyoshukiwa Deus na wewe unajambo ambalo unataka kujikosha hapa, tulia uchunguzi uendelee
 
Kifo cha Bwana Wangwe kilipangwa na Mungu tusianze kutafuta mchawi we ukiambiwa huyo Deus alikuwa rafiki yake kubali. Utata huo tunajizulia wenyewe na hapa serikali itakuwa ina mkono wake let hear about those pezzonovantes from the system on what have to say. To be honest these are merely conspiracy theories the guy is already dead let them make an inquiry about how he died instead of cleaning their own shit before the bublic.
 



3.jpg

mallya, Jamaa Aliyekuwa Na Chacha Katika Gari Lililopata Ajali.​




mallya Malya Malya Tuambie Ukweli
 
Kwa historia iliyoletwa hapa JF kuhusu Deus, sio kijana mjinga aliyechanganyikiwa kama muonavyo. Ni kijana mjanja ajuaye anachokifanya, tatizo lake upeo wake wa kupanga hoja za uongo kama alivyoelekezwa sio mkubwa kwahiyo anachanganya na matokeo zinaonekana kama pumba. Mkimpa nafasi baadaye ataongea mambo ambayo hamtayaamini hata kidogo.

Sasa yenyewe anaonekana kuwakana watoto wa marehemu, lakini kuna ukweli mkubwa kwamba yeye ndio aliondosha gari nyumbani maana walipoondoka ni Deus alilazimisha kwakuwa Marehemu alikuwa hoi tena mnyonge na alikuwa ndani ya dozi. Isingewezekana Marehemu aendeshe halafu Deus ndio alale tena siti ya nyuma.

Deus angekuwa amechanganyikiwa angejikuta anasema ukweli kwa asilimia kubwa, hajachangikiwa ila hana upeo wa kupanga hoja za kukwepa ukweli.


..you'll be disappointed!
 
5.JPG


Gari lililohitimisha maisha ya Chacha likiwa
limeharibika vibaya, watu wanajiuliza kumbe
huyu mtu hakuwa Fisadi alitumia tu kataksiii
wakati wengine wana mashangingi!!!!!!!!

3.JPG

Mallya, jamaa aliyekuwa na Chacha katika gari lililopata ajali.​

2.JPG

Gari alilokula nalo mzinga likiwa linaondolewa
barabarani maeneo ya Pandambili, Dodoma jana.

1.JPG

Chacha enzi za uhai wake baada yakunyoa rasta!

Pictures Credit: http://mpoki.blogspot.com/
Malya atueleze kilichotokea
 
sio ulimbukeni..............

naomba uniambie jambo moja zuri tu.ni nani kati yetu mwenye uwakika ya yaliyotokea. sisi sote tunaongea kwa kufuatilia tetesi. utakuwa mchache wa kufikiri kama utaanza kurusha makombola kwa watu.

maswali mengi yameulizwa lakini hakuna mtu ambaye amefikiria upande mwengine wa shilingi.nini busara ya mawazo kama watu wote mnafikiri kwamba mallya kamuuwa huyu mzee..........kwa nini isiwe mbowe na chadema yake au kwa nini isiwe ajali ya kawaida kama nyengine............

weka fikra sawa, muungwana.
Sehemu kubwa inatia shaka kwamba Mallya katumika, kubwa hapo ni nani kamtumia...???
 
Siisemei CHADEMA wala Zitto wala Slaa wala Mnyika wala Mpaka Kieleweke bali natoa hisia zangu mwenyewe kuhusu kifo cha Wangwe.

Ni ukweli usiofichika kuwa kuna dalili za zengwe kwenye kifo hiki. Nazo zimejikita kwenye nafasi ya:
1. Kijana huyu Deus ambaye sijajua kwa nini alisafiri na Chacha, ana
uhusiano gani naye na ni uhusiano wa muda gani? Kwenye uhusiano wao
ni lipi Chacha anajua na ni yapi yaliyo siri dhidi ya Chacha. Kwa taarifa
tulizo nazo huyu kijana ndiye aliyeshawishi safari ifanyike.

2. Ni nguvu gani ilikuwa nyuma ya Chacha ya
kumlazimisha/kumharakisha/kumshawishi Chacha kwamba kwa lazima
aende DSM siku ile ile licha ya kuugua sana na familia yake kumzuia
kusafiri. Najua kuwa kesho yake alikuwa ahudhuria mazishi ya Mzee
Munanka. Lakini bado sijajiridhisha kuwa hilo lilikuwa na ulazima na
umuhimu kiasi cha kuweka mbali vikwazo vyote vya safari vilivyotokea
kwake siku hiyo.

3. Niliwasikiliza TBC1 wakicover habari ya kifo cha Chacha Wangwe jana
asubuhi. katika mzungumzo yao walikuwa wakiconclude kuwa Kifo hiki
kimetokea siku chache baada ya Wangwe kuwa na mgogoro na chama
chake. NIliwaelwa vibaya sana TBC 1. Kwani inaonekana wazi kuwa nia ya
yao ilikuwa kuhusianisha kifo hicho na mgogoro wa chama. Sentensi hiyo
haikuwa na umuhimu wowote katika kumtambulisha Chacha kwa umma.

Mambo haya yameniweka mimi kwenye wasiwasi wa haki kwenye kifo cha Wangwe.
All in all nakubaliana na wote kuwa hiki ni kifo cha kawaida kabisa kilichotokana na ajali ya barabarani ingawaje naamini kuwa uchunguzi wa kina ukifanyika tutaweza kupata kahabari ambako kataonyesha kuwa vita ile ile ya kupambana na WM Pinda, Sayeed Kubenea na Spika Sitta na wakweli wengine wote ndani na nje ya bunge inaendelea kwa namna hii.

Mathalan itamsikitisha yeyote mwenye utashi wa kiutu na akili ya kawaida ya kiwango cha kupembua mambo ya kisiasa kwamba eti CHADEMA wanahusishwa na kifo hiki. Huu ni utoto, upotoshaji, uvivu wa kufikiria, ushambenga na kwa hakika ni dhuluma kubwa kwa umma wa watanzania.

Jukwaa hili haliwezi kujicontradict kiasi hicho. Eti para hii inaelezea kuwa CHADEMA ni mtambo wa kupambana na mafisadi halafu para nyingine inaelezea kuwa CHADEMA ni kinyongeo cha wapambanaji. Please people be fair. Take more time to swim in reality.

The war against graft is not that much easy. It takes a lot of risk to combatants. And I admit this is just one of them. The corrupt are as brave and smart. they know how to smash any move against them. They are also very smart in creating implications against their enemies. Discussants in JF be watchfull.

Haya!!!!!!!!


Huu si wakati wa kujitetea, kila mtu au kundi linaweza kuwa mtu / watuhumiwa endapo kama kulikuwa na umafia ndani yake. Usiusemee moyo wa mwenzio kwani hujui nini anachokifikiria
 
Kuna taarifa kwamba familia ya Marehemu Chacha Wangwe imetaka kufanyike kwa posmoterm mpya leo na sasa anasubiriwa daktari, na hivyo mazishi huenda yakachelewa kwa muda wa saa kadhaa. Habari zaidi baadaye
 
Deus Malya ndie yule yule Ramadhani Musa (1 anayedaiwa kuingia Dar es Salaam akitokea Mtwara, na kunaswa akiwa na kichwa cha mtoto mdogo
 
Tupe baba: Tunaisubiri happa hapa. Hatoki mtu hapa mpka tujue kulikoni
 
Kuna taarifa kwamba familia ya Marehemu Chacha Wangwe imetaka kufanyike kwa posmoterm mpya leo na sasa anasubiriwa daktari, na hivyo mazishi huenda yakachelewa kwa muda wa saa kadhaa. Habari zaidi baadaye
Thanks very much for the current nyuz, tutashukuru Mungu kama familia yake haijaingiliwa na mdudu Sirkali maana tunaweza kupata ukweli kwa namna moja au nyingine. Vinginevyo yawezekana yote hiyo ni janja ya nyani kusafisha anga kupitia mkono wa familia maana nijuavyo serikali inahusika moja kwa moja na mazishi ya huyu Kamanda, sio rahisi sana familia kuingilia kirahisi kudai uchunguzi mpya katikati ya mambo.

By the way, naomba kumfahamu vyema huyu ndugu yake na Chacha Wangwe aitwaye Prof. Samwel Wangwe. Wanaomjua vizuri watupe data tafadhali.
 
Deus Malya ndie yule yule Ramadhani Musa (1 anayedaiwa kuingia Dar es Salaam akitokea Mtwara, na kunaswa akiwa na kichwa cha mtoto mdogo
duh...hizi kwangu mpya mkuu, kwahiyo huyu Deus sio tu mjanja mjanja fulani bali pia kwenye ndumba yumo. Au unamaanisha nini mkuu? tupe data tafadhali...
 
Thanks very much for the current nyuz, tutashukuru Mungu kama familia yake haijaingiliwa na mdudu Sirkali maana tunaweza kupata ukweli kwa namna moja au nyingine. Vinginevyo yawezekana yote hiyo ni janja ya nyani kusafisha anga kupitia mkono wa familia maana nijuavyo serikali inahusika moja kwa moja na mazishi ya huyu Kamanda, sio rahisi sana familia kuingilia kirahisi kudai uchunguzi mpya katikati ya mambo.

By the way, naomba kumfahamu vyema huyu ndugu yake na Chacha Wangwe aitwaye Prof. Samwel Wangwe. Wanaomjua vizuri watupe data tafadhali.


Huyo ni mtaalamu wa mambo ya uchumi, zamani kidogo alikuwa mwenyekiti wa bodi ya madirectore wa ESRF, kisha akateuliwa kuwa mwenyekiti wa kuongoza tume ya kuratibu maoni ya watanzania kuhusu kuharakishwa kwa shirikisho la afrika mashariki, of which watanzania waliukataa huo mchakato, na nadhani ile tume inafahamika zaidi kama tume ya Wangwe...walau kwa juu juu

Lakini si mtu mdogo kitaaluma yuko juu sana...sina hakika kama naye si mmoja wao.
 
Nimesoma mwanzo mpaka mwisho sijaona zaidi ya aftermath ya ajali yenyewe ,na watu kukimbizana kwa habari ambazo naziona ni zile zile kwa uhusiano unaoelezewa.
Labda hadi hapa nilipofikia sijaona namna ajali ilivyotokea,kwa mfano ,je gari ilipasuka mpira au mipira,Je iligonga mti ,Je ilibingiria na kubiruka biruka , bado sijaona maelezo kuhusu na ajali yenyewe kiasi nashindwa kutoa hitimisho ,aidha kama abiria alikua mmoja wawili au watatu ,kwa jinsi nilivyoiona ile gari na abiria mmoja kufariki basi na abiria mwengine kwa hali yeyote ile asingekosa michubuko au mipasuko ,hata hivyo sio hoja inawezekana mtu akatoka bila ya mkwaruzo wowote ule.
Ila tukumbuke tu kama kuna ishu imejulikana basi ni bora ikaanikwa hapa la si hivyo siku ukija kuandika utakuta watu wameshafunga kazi na ofisi hazina tena nguvu ya kuifuatilia hoja yako kwani hii ni Tanzania.
 
kunakipindi pale dar ulienea uvumi kuwa kuna mtu kageuka chatu maeneo ya buguruni,na alikuwa ameifadhiwa pale buguruni polisi,basi watu waliminika kwa wingi kwenda kushuhudia hayo maajabu.lakini mwisho wa siku waliambuliwa patupu.
Sipendi nieleweke vibaya kwa ndugu wa marehemu lakini ni ukweli usiopingika kuwa marehemu amefariki ktk ajali ya kawaida tu,kama ajali zingine.
Hebu tujiulize kidogo
1,ni kitu gani ambacho marehemu alikuwa anatarajia kukifanya au hata ni mabadiliko gani kuanzia kwenye chama,jimbo,hata serikali ambayo yange kuwa kikwazo kikubwa ktk nchi.
2,au ni siri gani ambazo alikuwa nazo kiasi kwamba watu waliona kuwa ni tishio kwao mpaka wafikie kumuondolea uhai wake.
Tumeshuhudia mengi makubwa tena mazito na yamepita au yanapita na wahusika wanakula na kunywa bila wasiwasi,kama vile hakuna kilichotokea.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom