Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Huyo ni mtaalamu wa mambo ya uchumi, zamani kidogo alikuwa mwenyekiti wa bodi ya madirectore wa ESRF, kisha akateuliwa kuwa mwenyekiti wa kuongoza tume ya kuratibu maoni ya watanzania kuhusu kuharakishwa kwa shirikisho la afrika mashariki, of which watanzania waliukataa huo mchakato, na nadhani ile tume inafahamika zaidi kama tume ya Wangwe...walau kwa juu juu

Lakini si mtu mdogo kitaaluma yuko juu sana...sina hakika kama naye si mmoja wao.
Asante sana, huyu hawezi kuwa tofauti na wao akapewa majukumu aliyopewa. Ni mmoja wao. Hata hivyo simaanishi alishiriki kum-kolimba kaka yake kama mtandao wao utakuwa unahusika.

Hata hivyo kidogo kuna utata pale inaposemekana Prof. Samwel Wangwe anaandaliwa kuchukua jimbo badala ya ndugu yake aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha.
 
Mode, why hizi thread za Wangwe zisiunganishwe?
 
Katibu Tarafa sitaki kukupinga moja kwa moja. Ila ujue kuwa wengine tuna machungu na tunataka maelezo ya kina kuhusu msiba huu.

Ninamsubiri sana Halisi atupe yaliyotolewa na pathologists huko Tarime.
 
Nimesoma mwanzo mpaka mwisho sijaona zaidi ya aftermath ya ajali yenyewe ,na watu kukimbizana kwa habari ambazo naziona ni zile zile kwa uhusiano unaoelezewa.
Labda hadi hapa nilipofikia sijaona namna ajali ilivyotokea,kwa mfano ,je gari ilipasuka mpira au mipira,Je iligonga mti ,Je ilibingiria na kubiruka biruka , bado sijaona maelezo kuhusu na ajali yenyewe kiasi nashindwa kutoa hitimisho ,aidha kama abiria alikua mmoja wawili au watatu ,kwa jinsi nilivyoiona ile gari na abiria mmoja kufariki basi na abiria mwengine kwa hali yeyote ile asingekosa michubuko au mipasuko ,hata hivyo sio hoja inawezekana mtu akatoka bila ya mkwaruzo wowote ule.
Ila tukumbuke tu kama kuna ishu imejulikana basi ni bora ikaanikwa hapa la si hivyo siku ukija kuandika utakuta watu wameshafunga kazi na ofisi hazina tena nguvu ya kuifuatilia hoja yako kwani hii ni Tanzania.
Mkuu majibu kuhusu ajali ilivyotokea anayo Bw Mallya maana usiku huo hakuna mwingine aliyedai kuwa shuhuda wakati inatokea.

Bw Mallya sasa yeye alilala wakati ajali inatokea ili asione ilitokeaje, samahani maana siundi hoja. Alisema alisikia tu kishindo, kisha akaona ameenea vumbi na kichwa cha marehemu kimelala miguuni pake kikitoka damu nyingi. Kwahiyo hajui ilitokea vipi...!
 
Kuna taarifa kwamba familia ya Marehemu Chacha Wangwe imetaka kufanyike kwa posmoterm mpya leo na sasa anasubiriwa daktari, na hivyo mazishi huenda yakachelewa kwa muda wa saa kadhaa. Habari zaidi baadaye

Hapo familia imenena. Itasaidia kuondoa utata inagawa inabidi wamtafute Daktari wao kwa kazi hiyo..
 
suala la prof wangwe kusimama tarime kugombea halina mjadala baada ya msiba wa mdogo wake. CCM ndo karata yao pekee ya kulichukua jimbo hilo kwani yule mama naibu waziri elimu KABAKA itabidi ameze mate tuuuu. ila prof wangwe alikuwa na mpango wa kugombea kibaha 2010 na maandalizi yalishapata baraka ya wenye maamuzi juu.

ni mchumi mtaalamu ila kama ujuavyo bongo hata kama umeelimika bado ili heshima uifurahie yabidi uwe nao. ni mwenzao hata ile tume ya maoni ni alama tuu na anahusika kwenye mambo mengi ya kiushauri kwa sasa. itabidi asaliti usomi wake kwa kuanza siasa zisizo na tija kwenye hyo taasisi yao[ccm].

ikumbukwe aligombea uwakilishi wa afrika mashariki akadondoka na inasemekana wakuu walimpa pole kwa kumwabia umefungua njiaa vemaaaa. TUJADILII.
 
ni kitu kizuri, lakini sina imani sana na madaktari wetu.....
sitegemei kama iwapo serikali inahusika na akaambiwa aseme inachotaka serikali aseme kama anaweza kwenda kinyuma na kusema ukweli ....
 
kunakipindi pale dar ulienea uvumi kuwa kuna mtu kageuka chatu maeneo ya buguruni,na alikuwa ameifadhiwa pale buguruni polisi,basi watu waliminika kwa wingi kwenda kushuhudia hayo maajabu.lakini mwisho wa siku waliambuliwa patupu.
Sipendi nieleweke vibaya kwa ndugu wa marehemu lakini ni ukweli usiopingika kuwa marehemu amefariki ktk ajali ya kawaida tu,kama ajali zingine.
Hebu tujiulize kidogo
1,ni kitu gani ambacho marehemu alikuwa anatarajia kukifanya au hata ni mabadiliko gani kuanzia kwenye chama,jimbo,hata serikali ambayo yange kuwa kikwazo kikubwa ktk nchi.
2,au ni siri gani ambazo alikuwa nazo kiasi kwamba watu waliona kuwa ni tishio kwao mpaka wafikie kumuondolea uhai wake.
Tumeshuhudia mengi makubwa tena mazito na yamepita au yanapita na wahusika wanakula na kunywa bila wasiwasi,kama vile hakuna kilichotokea.

Inawezekana wewe unaishi dunia ya peke yako. Kwanza maswali unayouliza majibu yake ni baada ya huo uchunguzi. Kwamba ni kitu gani na siri gani, ni mpaka uchunguzi ufanyike, ambao wewe unaupinga.

Lakini pia, ujue Wangwe alikuwa mbunge na anatoka katika chama na jimbo lenye mazonge mengi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Ujue Wangwe ni binadamu, na sheria za Tanzania binadamu anapofariki hata katika ajali ya kawaida kabisa, ni lazima uchunguzi ufanyike tena hata kwa zaidi ya mara moja. Sasa wewe ndugu yangu fikiria mara mbili kabla ya kuandika au kujadili mada inayohusu kifo cha mtu
 
Mimi naomba familia isimamie huo uchunguzi na serikali isiwaingilie kabisa maana hao wanasifa ya kupindisha habari, halisi tunakungoja utumwagie habari. Mwenyezi Mungu isimamie familia ili ipate ukweli.
 
Maoni yangu, hakuna conspiracy. Kulikuwa na watu wawili tu kwenye gari. Huyo Malya ndio alikuwa dereva sasa anaogopa sheria pengine hana leseni au kwa sababu nyingine.
 
Deus Malya ndie yule yule Ramadhani Musa (1 anayedaiwa kuingia Dar es Salaam akitokea Mtwara, na kunaswa akiwa na kichwa cha mtoto mdogo



Huyu watu ndiye David Sawe au alikopi message ya David?
His/her first message here!



.
 
kunakipindi pale dar ulienea uvumi kuwa kuna mtu kageuka chatu maeneo ya buguruni,na alikuwa ameifadhiwa pale buguruni polisi,basi watu waliminika kwa wingi kwenda kushuhudia hayo maajabu.lakini mwisho wa siku waliambuliwa patupu.
Sipendi nieleweke vibaya kwa ndugu wa marehemu lakini ni ukweli usiopingika kuwa marehemu amefariki ktk ajali ya kawaida tu,kama ajali zingine.
Hebu tujiulize kidogo
1,ni kitu gani ambacho marehemu alikuwa anatarajia kukifanya au hata ni mabadiliko gani kuanzia kwenye chama,jimbo,hata serikali ambayo yange kuwa kikwazo kikubwa ktk nchi.
2,au ni siri gani ambazo alikuwa nazo kiasi kwamba watu waliona kuwa ni tishio kwao mpaka wafikie kumuondolea uhai wake.
Tumeshuhudia mengi makubwa tena mazito na yamepita au yanapita na wahusika wanakula na kunywa bila wasiwasi,kama vile hakuna kilichotokea.

Katibu Tarafa,

Naikumbuka hii, nilikuwa mlimani, yaani ilikuwa balaa tupu.

Mimi nimeanza kukataa haya mambo ya uchawi siku nyingi. Kuna mpaka wanafunzi wakasema wamemwona kabisa kumbe yalikuwa yale yale ya hearsay, unasikia kwa mtu na baadaye na wewe unajifanya umeona.

Familia wamefanya vizuri kuomba postmortem nyingine ili wapate ukweli kamili na kuridhika.
 
Maoni yangu, hakuna conspiracy. Kulikuwa na watu wawili tu kwenye gari. Huyo Malya ndio alikuwa dereva sasa anaogopa sheria pengine hana leseni au kwa sababu nyingine.
Unayosema yanawezekana lakini historia ya huyu jamaa alivyojihusisha na Chadema inatatiza kidogo, watoto wa marehemu wanasema alikuwa nyumbani tangu juzi (yaani kama siku 2 au 3 kabla ajali haijatokea). Hajulikani na Chadema kiundani ila alishawafuata kwa style za ajabu ajabu wakamtolea nje, iweje alijitolea kukaa na marehemu kwa karibu kiasi hicho bila sababu za msingi...? kuna nini hapo...? iweje amlazimishe marehemu kusafiri hali akijua hali yake wakati huo...?

Kama kweli yeye ndiye aliyekuwa anaendesha, basi utata unaongezeka maana picha inaonyesha kwamba baada ya ajali Deus alifungua mlango wa dereva akatoka, kisha akaufunga, akafungua mlango wa nyuma akahamia siti ya nyuma, akafunga mlango wa nyuma, akanyanyua kichwa cha marehemu akaweka miguuni pake, kisha akafunga mkanda na kulala hadi raia wema walipofika kusaidia...!!!??? alipata wapi hiyo akili...???
 
Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni, siasa za Tanzania jamani....
 
Wanapoteza Muda Mwisho Watazika Tu Hao Wanasubiri Tu!!!wagawane Mali Kabla Ya Kuzikwa!!!wamefanyiwa Sokoine Ije Kakayangu Wangwe Wapi Iliishia
R.i.p Wangwe
Tafadhalini Naombeni Mpumnzisheni Braza Wetu Msijejiundia Tume Kula Ulaji Kwa Jina La Marehemu
Ulale Pema Peponi
 
Ni haki ya kila familia kuomba uchuguzi wa maiti (Post-mortem examination) iwapo wanahisi kuna kuna utata katika kifo hicho.

Watanzania wengi hawalifahamu hili, na kuwa hii huduma ni bure, iwapo utatoa taarifa polisi na kuomba maiti ifanyiwe uchunguzi kutokana na kuhisi kuna mkono wa mtu! Unapotoa taarifa ya namna hii, inachukuliwa kama "police case", na wizara ya mambo ya ndani ndio inayogharamia hizo police case "post-mortem".

Wana-familia wengi wanabaki wakilia kuwa ndugu yetu alilishwa sumu ama .. lakini hawafahamu wana haki ya kuomba uchunguzi wa maiti wao, ili kujilidhisha na chanzo cha kifo ama kumpata mchawi wao!
 
I'm going to sleep.. I'll leave you with this:

a. Ni kweli huyo Malya alikuwa kiti cha nyuma
b. Ni kweli Chacha alikuwa abiria (kiti cha kushoto)

Kuna jambo nimekuwa najiuliza na nadhani baada ya muda ntapata jibu langu na kuridhisha nafsi, maneno yako Mkuu hapa yananiongezea maswali na kufikiri kusiko na mwisho. Natumai yote yatafunuliwa hapa.

what if Chacha had no choice but to leave with those people and at that particular day or time hata kama alijua ni mgonjwa na familia walimtaka apumzike. What if that was not an option? Clue... one of my post earlier yesterday.

Kama ambavyo inasemekana kwamba Malya alikutwa akiwa na Bastola, ingawa hakuna ripoti hata moja ambayo imesema kwamba hiyo silaha inamilikiwa kihalali na kisheria na Malya ama la. Pia hakuna ripoti kuhusiana na silaha hiyo kama kama ilikuwa Discharged at any time.

Hili ni swali limenijia tena baada ya kusoma hapo juu, kama he had no choice, na kupumzika was not an option ina maana ya kwamba alilazimishwa. Na kama nipo sawa katika hilo, waliokuwa na CW mmoja alikuwa anaendesha gari na abiria aliekuwa na Silaha (Malya)alikuwa seat ya nyuma... Nachoka zaidi.!

Hapo nadhani kama ni hivyo Dots za Mwanakijiji zitaungika tu...
 
Haya sasa,

Jambo limezua jambo. Yanayosemwa Tarime ni mengi sana kuhusiana na kifo cha mbunge wetu Chacha Wangwe. Tetesi zimekuwa nyingi na washukiwa ni wengi hadi inatia simanzi zaidi kuliko faraja.

Wengine wanasema:

1. Serikali imehusika
2. Rostam Azizi amehusika
3. Chadema wamehusika
4. CCM wanataka jimbo la Tarime.
5. Makampuni ya kuchimba madini
6. Wakereketwa wasiompenda Wangwe
7. Kifo ni cha kawaida kama vifo vingine

Ombi kwa wakazi wa Tarime, tusikubali kugawanywa na vyombo vya habari - TBC hadi vile vya habari corporation ambao wanataka kuleta mgawanyiko wa kikabila na kikoo Tarime.

Tuwe na nguvu na tumalize maombolezo kwa amani na turudi kujenga taifa na jimbo letu ambalo liko nyuma sana kimaendeleo.



May the almight loard rest his soul in enternal Peace.. We will Miss U Mpiganaji ''CHACHA WANGWE''.... naandika haya nikiwa na uchungu mkubwa moyoni..na nikiwa bado siamini yaliyotokea..na sasa ni siku tatu zimepita......''Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la bwana Lihimidiwe''
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom