Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Kasheshe,

Hao watu si ndio juzi walisema hawawezi kutoa hotuba ya shujaa wa taifa, Dr. Slaa, live kwa sababu za kiufundi? au?

Mkuu Field Marshall ES;

For those who knows what it takes to broadcast live, for sure they will agree with me that the success rate of TBC1 live broadcast is outstanding (99%) taking into consideration the level of ICT infrastructure and our people, these guys performance is superb.

Guys have showed that, what we are missing in the country is seriousness, consistency of whatsoever we are doing.
 
shahidi mmoja anasema watu 2 mwengine anasema kwenye gari kulikuwa na watu 3......na huyu anayesema kulikuwa na watu 2 ndie aliyekuwa na marehemu kwenye gari .....tushike lipi?
 
Manumba Adai Yoyote Mwenye Ushahidi Ajitokeze Kutusaidia

Umesaidiwa Na Kubenea Mpaka Acc/no Mwisho Ukaishia Kupiga Sachi Nani Akusaidie
Au Nani Anataka Kujeruhiwa Mapema Hivyo Chacha 52,,

Ama kweli watanzania wamechoka usanii wa polisi na serikali nzima. Hivi tutaendelea kuliajiri na kulilipa liserikali hili ambalo hatuliamini hado lini??

Hoja wa kifo cha Wangwe bado inamtaka Manumba atuonyeshe uwezo wake wa kazi aliyoajiriwa kufanya.

Wajamani bado naomba picha ya Deus Mallya!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
NINAITAKA SANA!!!!!

RIP Chacha Wangwe!!!
 
Nimechanganyikiwa kabisa. Sielewi chochote nahitaji scotland yard waje mana watatuambia a to z
 
I'm going to sleep.. I'll leave you with this:

a. Ni kweli huyo Malya alikuwa kiti cha nyuma
b. Ni kweli Chacha alikuwa abiria (kiti cha kushoto)
c.
d. Na aliyekuwa dereva aidha alikuwa anajulikana na Wangwe, au Malya au wote wawili na mtu wa kuaminika hadi kuachiwa gari la Mbunge.
e. Huyo/hao abiria wengine walipewa usafiri huo kati ya Dodoma na eneo la ajali.

Na mwisho kabisa: this is my biggest "what if of the night"

what if Chacha had no choice but to leave with those people and at that particular day or time hata kama alijua ni mgonjwa na familia walimtaka apumzike. What if that was not an option? Clue... one of my post earlier yesterday.

check KLHN for my own take.
 
I'm going to sleep.. I'll leave you with this:

a. Ni kweli huyo Malya alikuwa kiti cha nyuma
b. Ni kweli Chacha alikuwa abiria (kiti cha kushoto)
c.
d. Na aliyekuwa dereva aidha alikuwa anajulikana na Wangwe, au Malya au wote wawili na mtu wa kuaminika hadi kuachiwa gari la Mbunge.
e. Huyo/hao abiria wengine walipewa usafiri huo kati ya Dodoma na eneo la ajali.

Na mwisho kabisa: this is my biggest "what if of the night"

what if Chacha had no choice but to leave with those people and at that particular day or time hata kama alijua ni mgonjwa na familia walimtaka apumzike. What if that was not an option? Clue... one of my post earlier yesterday.

check KLHN for my own take.

I am with you mkuu.

Analysis yako na zingine za wakuu hapa bwana Manumba haziwezi.

Mimi pia nipo thousand of miles away (kutoka Dodoma) na nimeweza kujenga theory ambayo inaonekana Wangwe alikuwa na watu wawili kwenye gari yake.

Nnafikiria kuunda kampuni ya Richards Private Investigators.
 
hao viongozi wa chadema wasitafute mchawi wakati wao ndio wanahisiwa kuwa ndo wahusika kwani mwezi mmoja kabla walimpigia kura ya kutokuwa na imani na CHacha wangwe na kumvua madaraka kwa madai kuwa anatoa siri za chama. Na chacha wangwe akasema kuwa atazunguka tanzania nzima kuelezea maovu ya viongozi wa chadema pamoja na suala la ukabila katika chama.
 
... And how did it happen, Malya to come out without even slight injuries,
Did they kill and let the car drive itself to cover the accident? How did it happen? Someone tell us. HELP HELP!!!
 
Hii ni ajali kama ajali zingine na hakuna haja kabisa ya kumtafuta mchawi. Barabara zetu zinafahamika kwa ubovu na wembamba, na pia magari yetu mengi ni mabovu.

Gari lililopata ajali lilitoka gereji na bado lilikuwa halijatengemaa vyema, hivyo inawezakana kabisa ikawa pia ni gari ndiyo chanzo.

Huyu kijana Mallya bila shaka ndiye aliyekuwa dereva wa Chacha, kwa umri aliokuwa nao si rahisi kwamba walikuwa marafiki wa karibu. Na Marehemu amekutwa kiti cha mbele cha abiria kwani alikuwa haendeshi yeye bali alikuwa anaendeshwa.

Huyu kijana (Day worker aka dereva wa kukodishwa) alipata tenda hiyo ya kumpeleka Chacha Dar tokana na Chacha mwenyewe kuwa na malaria.

Jamani hii ni ajali kama zilivyo ajali nyingine zinazosababishwa na madereva vichaa wa Tanzania ama ubovu wa barabara zetu.
 
Waacheni polisi wafanye uchunguzi wao bila kuingiliwa na wanasiasa.Hiyo ni ajali tu na sidhani kama kuna mkono wa mtu yeyote.

Sijui kama hii inawezekana ndugu yangu. Kitu kama hicho hakitatokea Tanzania. Sioni kama kuna uwezekano wa polisi kuchuguza hii issue bila political interfearance. Hakuna historia hiyo Tanzania na huenda itachukua muda mrefu kabla ya kufika. Polisi wetu hawana mambo ya professionalism. Mfano mzuri upo kwenye kuvamiwa kwa ofisi ya Kubenea. Kupambana na ufisadi sasa hivi Tanzania ndio crime inayochunguzwa, lakini kuwalinda mafisadi ni kazi sahihi. Lakini issue zinazotakiwa kufanyiwa kazi kama vifo vye utata hazifanyiwi kazi, na usitegemee kama zitafanyiwa kazi. Wangwe amekufa baada ya wiki mbili tutasahau, tukamkubuka siku ya 40 and that will be it.
Tutadanganywadanganywa tu, kwa hiyo ni vizuri kama tukikaa kimya na kuendelea na mengine yanayoweza kufanyika.
 
kama polisi wanataka kufanya kazi yao sawa sawa basi
1) wangetupatia ripoti ya garage, na kujua gari ya kwanza ilikuwa na tatizo gani
2) wangembana huyo kijana kutueleza sababu za kumchukua mgonjwa kumpeleka safarini
3) kutueleza mtu wa tatu ni nani na ana uhusiano gani na yeye na wangwe?

lakini nionavyo mimi, polisi watakuja na maelezo kuwa ilikuwa ni ajali kama ajali nyengine tu.
 
hao viongozi wa chadema wasitafute mchawi wakati wao ndio wanahisiwa kuwa ndo wahusika kwani mwezi mmoja kabla walimpigia kura ya kutokuwa na imani na CHacha wangwe na kumvua madaraka kwa madai kuwa anatoa siri za chama. Na chacha wangwe akasema kuwa atazunguka tanzania nzima kuelezea maovu ya viongozi wa chadema pamoja na suala la ukabila katika chama.

Mkuu bado nipo, hii ndiyo sababu ya wauaji (if any) ili kuleta hoja/mawazo kama haya yako then mafisadi wawe washindi.
 
ndugu zangu wa chadema,

kwanza poleni sana kwa dhahama ambalo limewakuta maana katika dunia tunayoishi ni vigumu sana kuamini kama nyinyi leo mnaweza kuuliza maswali kama haya huku jamii ikijua wazi kuwa majibu mnayo.

kwa mshangao wa upeo wangu, maswali ambayo mh. mnyika ameomba serikali kupitia jeshi lake la polisi liyajibu, yanaleta utata mwengine hasa nikiangalia kwamba uelewa wake au kamati iliyokaa kujadili kuweka haya maandishi chini. kwa nini nasema hivyo........

ngoja niwaambieni ndgu zangua jamaa zangu, kifo ni kifo tu. mallya kwa maelezo yake alikuwa rafiki wa siku nyingi wa mh.chacha na hata kusema kuwa alikutana naye kwa mara ya kwanza makao makuu ya chadema pale kinondoni..(sijui kama ofisi zipo kinondoni) kwa hiyo ni aibu kuwa hamumjui huyu kijana ambaye ana fika sehemu ya hata kuingia gari moja na makamu mwenyekiti. kwa upande mwengine nashawishika kuamini kuwa huyu ni mtu aliyekuwa na umuhimu fulani katika maisha ya makamu mwenyekiti, mjumbe wa kamati kuu ya chama.

pamoja na hayo, tujikumbushe siku za mwisho za marehemu. kabla mahuti hayajamkuta bwana wangwe, kumekuwa na migogoro ya mara kwa mara ndani ya chama. ambayo kwa namna moja au nyengine inatokana na siasa za ukanda zinazotawala maendeleo ya chama. sintoshangaa watu wakija juu na kusema kuwa chadema au kundi la wanasiasa wa upande fualani wamemuuwa chacha.ni jambo la kawaida ambalo mnatakiwa kulikabili.

polisi kwa upande wao kama wafanya kazi wa sekta hii lazima watafanya uchunguzi wao. kuweka ripoti adharani au kutoweka ni juu yao. wewe unataka ripoti iwekwe hadharani kwa jambo gani haswa. unafikiri hii ndiyo njia ya kujisafisha? ndugu yangu angalia maana unaweza kuja tafuta njia ya kukimbilia maana jamii inataka maelezo zaidi maana hawata elewa kusikia kwamba hamjahusika. wangwe alikuwa akiongelea sauti ya umoja. alikuwa anaubiri siasa ya ukweli ambayo kwa ushujaa wake aliweza isimamia, sio tu ndani ya chadema bali pia bungeni. alipenda sana kupanua wigo wa siasa.

ZITTO ZUBERI KABWELUKA...........kaka pole sana. maana umepoteza mpiganaji aliyekuwa anakupa raha na uelekeo katika mitizamo. ni imani yangu umepwaya ndani ya harakati zako. umepoteza muhubiri wa mtazamo wako wa kutanua demokrasia ndani ya chadema, toka machame hadi tanzania. usikonde mungu atakusaidia. mnyika ni hajui alitendalo.

mwisho elewa maswali kama haya haustahili kuuliza...ongea na watu wa karibu watakuambieni.najua mnataka kuanzisha kuwa huyu mallya alitumwa na mtu fulani. hapana naibu katibu....endelea fanya kazi zako na achana na haya.

sijui alienda dodoma kufanya nini....ina maana yeye ndiye alimwambia chacha twende dar kuzika au unafikiri ni rahisi kwa mtu ambaye hamjui kumpa gari alipeleke garage. haiwezekani bro.huyu ni mtu aliyeaminiwa na chacha na ndiyo maana hata alisafiri naye.

mungu ibariki tanzania.
 
Jamani hivi picha za gari lililopata ajali ziko wapi?[/QUOTE]

mkuu picha hizi hapa
View attachment 1891
Na hii nyingine
10.JPG
 
Jamani huyu Deus Mallya huyu hapa.
3.JPG
Kama kuna mtu atakuwa anamtambua tunaomba data zake kamili.
 
GB,
Maandishi yako mbona yanajaa utoto? watu wanajadili vitu serious, by the way wewe mtu mzima unaweza kweli kutumia nick name hii? kweli huu ndo ulimbukeni wa ajabu kabisa.
 
sio ulimbukeni..............

naomba uniambie jambo moja zuri tu.ni nani kati yetu mwenye uwakika ya yaliyotokea. sisi sote tunaongea kwa kufuatilia tetesi. utakuwa mchache wa kufikiri kama utaanza kurusha makombola kwa watu.

maswali mengi yameulizwa lakini hakuna mtu ambaye amefikiria upande mwengine wa shilingi.nini busara ya mawazo kama watu wote mnafikiri kwamba mallya kamuuwa huyu mzee..........kwa nini isiwe mbowe na chadema yake au kwa nini isiwe ajali ya kawaida kama nyengine............

weka fikra sawa, muungwana.
 
kuhusu matumizi ya nick name usiwe na shaka, ni vijimambo tu. kubwa na linatakiwa hapa ni mawazo unayotoa.

elimika.
 
Kuna watu wanamchukia George Bush kiasi kwamba hawatasoma maoni yako ust because of the nic name!!!!! chunga sana.
 
Kijana wa Wangwe alitambulishwa kuwa Malya ni mtu aliyekuwa akifanya kazi fulani na baba yake. Kazi hiyo inaonekana kuwa nyeti kiasi cha kulazimisha safari ya Dar wakati hali ya Wangwe kiafya haikuwa nzuri. Kwa mujibu wa kijana, Malya ndiye angeendesha gari kwani alitahadharishwa kuendesha kwa uangalifu kwa kuwa abiria alikuwa mgonjwa. Maswali mazito ni hiyo kazi nyeti Wangwe aliyokuwa anafanya na Malya ni ipi, na huyo dereva mwingine ambaye inaelekea ndiye aliyetokomea na vitu vya marehemu ni nani?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom