Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,240
- 44,487
Kwani waarabu na waajemi si wasilam?
Ama wakisema wakristo humaanisha ni wazungu tu?
duh.. nina kazi!
Kwani waarabu na waajemi si wasilam?
Ama wakisema wakristo humaanisha ni wazungu tu?
Mushi,
Hili la uarabu wa mke wa marehemu kulihusisha na uarabu wa mume aliyeachana naye sidhani kama ni issue. Binafsi nashindwa kuamini kuwa huyu Mariam alikuwa hafahamiani na huyu Malya. Mariam ndiye mke aliyekuwa karibu na marehemu, na kwa mujibu wa kijana mkubwa wa marehemu kuwa Malya alikuwa akifanya kazi fulani na marehemu, bila shaka Mariam anaifahamu hiyo kazi waliyokuwa wakiifanya kwa ubia. Huyu mama anafahamu mengi sana tatizo ni kuwa, akitakiwa kueleza yote anayoyafahamu atakuwa tayari? Naanza kuhofia usalama wake.
duh.. nina kazi!
duh.. nina kazi!
kwa nini uchanganye kabila zima kwa ajili ya kasoro ya mtu mmoja? kama damu itamwagika nchi hii kwa ajili ya vita ya kikabila, basi mwanzilishi na mfadhili wa hii vita ni rostam azizi kupitia magazeti yake ya new habari corporation, na fedha za wizi alizoiba. pia kupitia vikaragosi kama wewe na akina balile
Mengine yote nakubaliana na wewe 100%, lakini nililo-bold hapo juu!!! nasita kusema kumbe tayari mnafanya vizuri sana... kumbe tuna makengeza wengine... mimi nilidhani ndio munahitaji kusimama imara kumbe already ndio muko imara...
Oooh... maskini nchi yangu.
Mimi nafikiri tumechanganya mambo mengi kwa sababu wengi wetu tumechangua upande. Ukitaka kuwa objective utagundua mambo haya:
- Ni wazi kwamba kulikuwa na tafrani kwenye msiba kutokana na ukweli kwamba kifo cha marehemu kilikuwa na utata mwingi. Ningeshangaa sana mimi kama msiba huu ungekuwa wa amani kama misiba mingine.
- Hata hivyo, kwa sababu za kisiasa, tafrani zilizotokea zimekuzwa ili kuonyesha kwamba kulikuwa na fujo, na fujo hizi zilielekezwa kwa chadema.
- Kwa sasa kuna kila dalili kwamba CCM watatumia msiba huu kama njia ya kutokea, maana kwa kweli wamebanwa sana.
- Sababu za chadema kunyoshewa kidole katika msiba huu zinaeleweka na zinapaswa kutarajiwa: i) ndio chama kinachotishia uhai wa CCM kwa sasa, ii) mbunge aliyefariki alikuwa ni mbunge wa chadema na hivyo wapinzani wa chadema wangependa kutumia msiba huu kuhakikisha kwamba chadema haichaguliwi tena huko Tarime iii) marehemu alikuwa na mgogoro na viongozi wake, na kwa kiasi kikubwa alijaribu kuonyesha kwamba mgogoro huu ulikuwa kati yake na Mwenyekiti wa chadema.
- Kwa maoni yangu, maelezo ya Zitto kwamba hapakuwa na fujo huko Tarime yalilenga zaidi kukanusha madai kwamba hasira za wananchi zilielekezwa kwa Mwenyekiti Mbowe, na kwamba hapakuwa na mapanga wala mishale. Pengine alichokosea Zitto ni kukanusha madai ya fujo kwa jumla jumla. Angeweza kukiri kwamba, yes, kulikuwa na aina fulani ya tafrani au fujo lakini sio kweli kwamba fujo hizi zilielekezwa kwa mwenyekiti Mbowe, na wala sio kweli kwamba fujo hizi zilifikia kiwango cha wananchi kubeba mapanga, mishale kama ilivyoripotiwa. Nafikiri ile kamati ya wahariri itaweza kufafanua hili vizuri. Nahisi kwamba kamati itakiri kuwepo kwa aina fulani ya fujo, ambayo inaeleweka kutokana na mazingira ya kifo na umaarufu wenyewe wa marehemu. Lakini nahisi pia kwamba kamati itakanusha madai ya kufanyiwa fujo kwa Mweneyikiti Mbowe, na wala wananchi kubeba mapanga na mishale.
Ni wazi kwamba CHADEMA tumetikiswa. Ama tutaanguka au la, itategemea tutakavyo-handle matukio baada ya msiba huu. Kwa maoni yangu njia pekee ya kusimama ni kuwa wa kweli, na inabidi tuwe wa kweli katika mambo makubwa manne yafuatayo:
(a) Tukiri kwamba, yes, kulikuwa na mgogoro kati ya marehemu na viongozi wenzake katika chama. Baada ya uchunguzi uliofanyika, Kamati Kuu ya CHADEMA iliona kwamba marehemu alikuwa amekiuka baadhi ya kanuni za chama ,na hivyo ikaona ni vyema kumsimamisha uongozi
(b) Tukiri kwamba, yes, baada ya kusimamishwa, marehemu hakuridhika na maamuzi yale, na alikuwa akifanya utaratibu wa kukata rufaa katika vikao vya chama, na hata mahakamani
(c) Tukiri kwamba, yes, baada ya msiba huu, wapinzani wetu, na hasa CCM, wamekuwa wakijaribu kuhusisha kifo cha marehemu na mgogoro huu ili ionekane kwamba kifo cha marehemu kimetokana na mgogoro huu.
(d) Tukemee njia chafu wanazotumia CCM kujaribu kufifisha nguvu za upinzani na kujipatia umaarufu kupitia kifo cha marehemu. Tuweke wazi kwamba huu ni ushetani, na sio jadi ya watanzania kutumia msiba wa mwenzako katika kujipatia umaarufu. Na wala sio jadi ya watanzania kujaribu kumjeruhi ng'ombe aliyekwishajeruhiwa. Katika hali ya kawaida ya utanzania wetu, ilitarajiwa kwamba CCM wangekuwa wanawapa CHADEMA pole na rubani kwa kufiwa na mwanachama, kiongozi na mbunge wa chama chao. Badala yake hawa wenzetu wapo busy kujaribu kutumia msiba huu kujinufaisha kisiasa. Kwa maoni yangu tukijenga hoja hii vizuri kwa wananchi, ndio itakuwa mwisho wa ghiliba za CCM kuendelea kutumia msiba huu kama njia ya kutokea. Hili jambo halihitaji danadana.
Kwani waarabu na waajemi si wasilam?
Ama wakisema wakristo humaanisha ni wazungu tu?
Mimi nakuonea huruma maana mambo naona yanakupita kushoto. Udhaniavyo sivyo. Mbowe ndiye kiboko ya sisisemu sasa na mikakati ya sisiemu inajulikana dhahiri.Oooh... maskini Kasheshe
Mushi bwana saa nyingine mambo yako ya ajabu sana! Sio kila mwarabu ni muislamu, waajemi si waarabu, sio kila muajemu ni muislamu....kuna waarabu wengi tu ambao ni wakristo hasa Lebanon, Egpty, Palestine na sehemu za Syria!! Pia waajemi kuna kundi la kutosha wana dini yao inaitwa Bah'ai. Anywayz hiyo ni issue nyingie..tatizo langu kule juu sehemu nimeona una-introduce udini ktk sakata hili!! Ushindwe na ulegee.
bado ni rafiki yangu, though..
eazy.
Kuna mambo mengi sana ya kujifunza kwenye mjadala huu, na haswa baada ya Kiranja kuweka post zake ,naona kuna baadhi ya watu wameloose control mpaka inafika mahali wanajitambulisha kuwa wao sio A bali ni B wakati siku zote walikuwa wanajionyesha kama ni Neutral.
Heri walio upande fulani na maandishi yao yanasema hivyo kuliko walio upande fulani halafu wanaona aibu kutetea misimamo yao, naamini kuwa baada ya siku zinavyokwenda patachorwa mstari na nani ni nani kujulikana ama kwa matendo au kwa maandishi yake.
Huo mstari nani atauchora?? Hakuna atakaye chora mstari huo kwa kizazi hiki cha nyoka .Labda Mbiguni tu.
Kizazi hiki cha faa kuangamizwa kabisa maana chote ni cha kinafiki na kikifuata sera za yule MWOVU.
Mwanasia aliyevaa hilizi kiuononi ama kua na kababu akiamini ndio mlinzi wake ama vibuyu ktk kona ya nyumba zake AMINI NA KUAMBIA KAMWE hatachora mstari wa haki BALI atachora mstari wa dhuluma ,unyanganyi,UONGO,WIVU,UZINIFU,UUWAJI,UTAPELI,UFITINISHI.
Hapa tayari kuna jibu kuwa yawezekana marehemu alikuwa na kadi mbili. Ya Chadema na ya sisiemu.Hii ni mara ya kwanza kwa CCM kujitokeza wazi kusambaza waraka wa Chadema, ikiacha maswali kama ilipewa waraka huo na Wangwe au ndiyo ilikuwa ikishirikiana naye katika kuendesha harakati zake ndani ya chama hicho cha upinzani.
Alipofariki Wangwe nilichangia katika thread iliyohusu kifo chake kwa kuandika misitari miwili tu, na baada ya hapo sikuchangia tena kwa sababu my gut feeling was telling me that the man was assassinated!
Mistari miwili pekee niliyochangia katika kifo cha Marehemu Wangwe ni hii hapa na baada ya hapo nilifumba mdomo wangu:
1. RIP Wangwe.
2. Police should thoroughly investigate the cause of the eccident.
Kutokana na hali inavyoendelea, ambapo sisiem na chadema wanaonekana kutoa kauli mbalimbali za ama kuchafuana au kujisafisha, ninalazimika kusema kitu kimoja tu nacho ni kwamba: kama ni kweli kwamba kifo cha wangwe kina mkono wa mtu basi huo mkono lazima uwe umetoka ama csiemu au chademo. Na ndomaana wanatumia muda mwingi kujisafisha na kuchafuana.
Nataka nimalizie kwa kusema hivi: Kujisafisha au kuchafuana kunakoendelea, kuhusiana na kifo cha Wangwe ni kazi bure! Kwani it is just the matter of time before tanzanians can know what real is behind Wangwe's death or assassination if proved! Kila kitu kitakuwa wazi. Tusubili muda, ukifika either csiemu or chadema wataumbuka. Believe me they won't get away with it! Hakika Mungu atawaumbua!
RIP Wangwe.
Uoza na uvundo wa Gembe:wink:Nini kinakutapisha tena ? Nimeshindwa kukuelewa unaposema kuwa umeshatapika mara mbili ,kuna kitu gani?