Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Ni bora kuwa na wanasiasa mafisadi wakivinjari kuliko wanasiasa mufilisi mbele ya vyombo vya habari......

Hawa jamaa wote waliletwa TARIME na ndege aliyokodisha MBOWE. Walipoifika msibani wakaachwa nyuma na kundi la mashabiki wa MBOWE kumuingiza katika eneo la shughuli ya mazishi.

Hawa ndio waliokuwa wakiimba RAISI, RAISI,...MPAKA KIELEWEKE....wakiwa na mabango lukuki yakihoji kifo cha WANGWE lakini hakuna hata moja lilikuwa likihoji uhusika wa CHADEMA au MBOWE. Hawa waliendelea kupiga kelele hata RC MAchibya am baye ni dui number moja wa wakazi wa TARIME alipopanda jukwaani na kuwataka wanyamaze. Hata kufikia kusema watulie ili waweze kumsikia RAIS wao...meaning MBOWE. RC Machibya aliendelea kuongeza lakini hakuna aliyemsikiliza huku vijana wawili wakiendelea kupiga kelele bila ya kutulia. Ni pale tu Zitto alipokuwa akiongea ndipo walitulia kidogo. Cha ajabu ni kuwa RC Machibya aikuwa hafurahishwi na hali hiyo kiasi cha kumnyang'anya Zitto MIC kila vijana hao wakiwa wanatulia na hivyo kuanzisha kelele nyingine. Mkumbuke kuwa MACHIBYA anaendesha operation ya kuzuia kusafirishwa chakula kwenda TARIME kwa madai kuwa wanatorosha chakula kwenda Kenya.

Cha ajabu zaidi ni kuwa Binamu wa Marehemu anayejulikana kama Mzee KEBA ambaye walikuwa na ushindani mkubwa kisiasa na Marehemu CHACHA WANGWE yeye akiwa kada na kiongozi wa CCM, alipanda jukwaani na kuwaonyeshea alama ya dole tupu waliokuwa wakipiga kelele hapo na hata kuchukua BANGO lilikuwa likiuliza kama Ni RISASI ama AJALI na kuliinua juu akilizungusha kwa kila mtu kuliona.

Hata hivyo vijana hao haswa wale wawili hawakuwa tayari kunyamaza hadi Zitto alipochukua MIC tena na kuanza kutumia slogans za CHADEMA ambazo ziliitikiwa kwa nguvu na kuanza kunyamaza ndipo alipomkabidhi MIC Prof Wangwe ambaye alitoa taarifa ya kuahirishwa kwa mazishi na kuwepo kwa uchunguzi mwingine wa mwili wa marehemu.

Baada ya hapo ndipo askari wa polisi na vijana wa ulinzi wa CHADEMA wakawachukua viongozi wote zaidi ya hamsini waliokuwepo plae na kuwaoonda mahala hapo kwa haraka kupitia chumba kilichokuwa na mwili wa marehemu ambacho kina milango miwili mmoja wapo ukiwa ni geti la chuma la kuingilia hala unatokea kwnye uwa wa nyumba kabla ya kupita mlango mwengie unaotokea mbel ya nyumba na kutoka nje kupanda magari.

Wakati wote huo hakuna waliokuwa wametoa silaha za aina yoyote na hata kutupa mawe. Kama ni kushambuliwa magari basi ilikuwa ni magari a serikali ambayo yalikuwa yakigongwa gongwa kwa mkono kama wafanyavyo wapiga debe wa daladala....

Ni kweli hapo nje kulikuwa na mtafaruku ambao ulisababishwa na panick iliyokuwepo miongoni mwa waheshimiwa wengi waliokuwepo hapo na kupelekea kukimbili katika magari yao na hata wegine kuingia katika magari yasiyo yao.

Ni wazi kuwa RC, RPC na watendaji wengine wa serikali walikuwa wamepanick na hata wakati mwengine kuonekana kuwa wanapenda kuonesha hali ya vurugu ipo.

Ni kweli pia katika hali kama ile ilikuwa ni busara kuwaondoa WAHEMSHIMIWA wale kwa haraka kwani eneo lile halikuwa na nafasi yoyote ya kuwalinda. Kilichofanya wao kupita katika kichumba ambacho ndipo mwili wa marehemu ulikuwepo ni kujaa kwa watu katika sehemu ya kuingilia katika eneo hilo ma tu baada ya MBOWE kungia na kundi la mashabiki ambao walijaa eneo lote la kuingilia kuelekea jukwaani na wengine wakijaribu kutoa mikono kwa waheshimiwa walikuwepo hapo haswa MBOWE na SLAA.

Zitto ndio alikuwa kiongozi wa mwisho kutoka eneo hilo na kuelekea nje ambak askari walimlazimisha kuingia katika gari la MHESHIMIWA MKONO akiwa na MESHIMIWA SARUNGI na mlinzi wake mmoja aliyepewa na IGP. Huyu alipewa baada ya yeye kukataa ulinzi wa FFU watatu ambao DC na KAIMU RPC wa MUSOMA walitaka aongozane nao MARA alipofika MUSOMA mjini........

Ukweli maizngira ya uwezekano wa vurugu kubwa na hatari yalikuwepo lakini si kweli kuwa siku ile kuna waliokuwa wakitishia maisha ya MBOWE. Na kama kuondolewa pale na askari hilo lilifanyika kwa wote walikuwa wamekaa kweny viti vya waheshimiwa wakiwemo wabunge zaidi ya 20, viongozi wa vyma zaidi ya 5, Viongozi wa CCM kadha ambao walikuja na mavazi yao ya chama kitu kilichopelekea hata MWenyekiti wa Moa aliyekuwa amekaa katika eneo la viongzi kutolewa na vijana wa CHADEMA na kuhamishiwa sehemu nyingine aliyopaswa kuwepo.

Wakina MREMA wao walichokuwa wakikifanya tangia wakati huo ni kuchochea sumu tu wakisaidiana na baadhi ya wanafamilia na kina MAMA KABAKA, Mzee GACHUMA na wengineo huko. Sumu yao pamoja na reporting ya kina GEORGE MARATO na mwenzake wa CHANEL TEN amao dio chanzo cha habari za kupotosha katika vyomb vingi vya habari ndio vilipelekea hali mbaya zaidi siku iliyofuata kwani hata baadhi ya watoto wake walianza kuamini kuwa marehemu aliuawa na risasi.

Mbaya zaidi ni kuwa hata wakati uchunguzi wa mwili ukiendelea TARIME MJINI kuna mtu alituma msg kijijini kuwa imethibitika kuwa kulikuwa na risasi mbili katika mwili wa marehemu....kitu ambacho kilifanya hata viongozi wengine wa CHADEMA kuamua kurudi TARIME mjini na wengine kuondoka hapo mara baada ya uchunguzi wa pili kwisha.

Kwa kweli sikuona ajabu kwa MREMAna MBATIA kufanya walichokifanya lakini ya Prof LIPUMBA yamenifanya kujiuliza zaidi kama nijiunge na siasa za vyama hivi ama laa. Iweje msomi kama yeye kutumia propaganda hovyo kama za kumhusisha MALLYA na UGAIDI eti kwa kuwa alikutwa na kikaratasi kikiwa na maandishi ya kiarabu ama aliwahi kwenda LIBYA. Hii haina tofauti na taswira iliyojengwa duniani kuhusu waislamu. Yaani hapa anahalalisha sumu hiyo dhidi ya uislamu na waislamu. Na yeye bado anajitambulisha yeye kama muislamu.

Na anaposema kuwa kichwa kilikuwa kimepondeka inabidi ajihadhari na hilo maana ukweli ni kuwa postmortem zote zinapaswa kufanywa na kurekodiwa na video. Nina uhakika wa hilo kwa uchunguzi wa TARIME maana alikuwepo mtaalamu wa ID wa polisi akirekodi zoezi zima.

Hawa kina MREMA na MBATIA waace waendelee kkupalia moto hii chuki inayopandikizwa hapa wakidhani itakwisha kwa WACHAGA Mbowe na Mallya tu.....Hii inakwenda zaidi ya hapo. Hata hivyo sidhangai sana kwao kuvaa siasa hovyohovyo kama hizi kwani upeo wao unajulikana...Lakini la LIPUMBA linatisha....

Kwa mimi niliyekuwepo TARIME kuanzia mwili ulipoingia hadi siku ya kuzikwa nashukuru wengi wenu hapa jinsi mnavyochemsha kwani mnaniwezesha kujielimisha mambo mengi ikiwemo hili suala la kujenga imani kwa misingi ya hisia zilizokosa chembe ya ujuvi......

Tanzanianjema

unatumia nguvu nyingi sana kuuzima moto huu ..tatizo umebeba mafuta ya petrol kwenye ndoo hiyo unayodhani imejaa maji ya kuuzima moto huo..
 
Sioni sababu ya kukuza sana mambo, ati jasusi!

Huyu alikuwa mhangaikaji tu wamjini, akitafuta order za kusuply tona za photocopy, cabon paper, printing etc. akisikia tenda fulani hata waziri atamzoea tu ili apate connection.

Ukweli ile corolla ilikuwa mkangafu, uwezekano ilikuwa na tube zenye viraka vilivyozibwa kwa patex na engine kuchemsha ni mkubwa. Haiwezi tembea mchana toka dom hadi dar, magari ya mtindo huu hutembea usiku kwa usiku.

mh. aliwahi kuwa rastafarian siku za nyuma, hivyo uwezekano alikuwa mtu wa dope ni mkubwa, ndo maana washkaji zake nimajanki, kama walilipuliza ndo wakaanza safari? kama alipata balimi mbili na dope uwezekano wa mzinga ni mkubwa, hakuna aliyempima alcohol baada ya ajali.

Kama dogo angekuwa kamanda asingepiga kelele kuomba msaada, angetambaa kwani alitoka fiti, madereva wangapi wanapiga mzinga na kulala mbele.
 
Yaani awe SPY ndani ya Jamhuri! Halafu awe anawafanyia kazi watu wengine na sio Jamhuri?.... Thats not normal!

So our government trains assassins kuua raia wake...?
Si umeambiwa ana urafiki wa karibu na Ghaddafi he could be a double agent, anaweza kuwa ni rogue agent vile vile...kuna possibilities nyingi tuu.....Kwa hiyo kuexpose jina lake kunaweza kuwa na manufaa kwa taifa.

Kama alijifunzia Libya atakuwa ni mwanafunzi wa Musa Kousa..
 
Sioni sababu ya kukuza sana mambo, ati jasusi!

Huyu alikuwa mhangaikaji tu wamjini, akitafuta order za kusuply tona za photocopy, cabon paper, printing etc. akisikia tenda fulani hata waziri atamzoea tu ili apate connection.

Ukweli ile corolla ilikuwa mkangafu, uwezekano ilikuwa na tube zenye viraka vilivyozibwa kwa patex na engine kuchemsha ni mkubwa. Haiwezi tembea mchana toka dom hadi dar, magari ya mtindo huu hutembea usiku kwa usiku.

mh. aliwahi kuwa rastafarian siku za nyuma, hivyo uwezekano alikuwa mtu wa dope ni mkubwa, ndo maana washkaji zake nimajanki, kama walilipuliza ndo wakaanza safari? kama alipata balimi mbili na dope uwezekano wa mzinga ni mkubwa, hakuna aliyempima alcohol baada ya ajali.

Kama dogo angekuwa kamanda asingepiga kelele kuomba msaada, angetambaa kwani alitoka fiti, wangapi wanapiga mzinga na kulala mbele.

And what are you trying to say here?
 

...ama kwa hakika, huu msiba na hii ajali imenifungua mawazo kuhusiana na mambo mengi. Kuanzia Contradiction statements za mhusika kwenye ajali, washuhuda wa eneo la ajali, waandishi wa habari, ndugu jamaa na marafiki, vyombo vya dola na maoni ya wanasiasa pamoja wananchi kwa ujumla.

Mwenyezi Mungu amsamehe madhambi yake Marehemu, ndugu jamaa na marafiki zetu wote walokwisha tutangulia mbele ya haki.

Ameen.
 
Anatoa maelezo chini ya kanuni ya 50 ya bunge, anasema kuwa kanuni zinaelekeza masuala ya kufanyika pindi inapotokea kuwa mbunge amefariki, na anasema kuwa yeye aliteuliwa na Mheshimiwa spika kuwa mwenyekiti wa ujumbe aakiwa na Wanyancha, mkono, john chetyo,sarungu,hamad ,mnyaa,slaa,juma kilimba ,zitto,kabaka,masunga joyce,jaeth masaburi.suzan lyimo ,james nsekela ,vedastus manyinyi .

waliondoka saa mbili na nusu asubuhi na kuwasili saa tano kamili asubuhi,na kupokelewa na mkuu wa mkoa akiwa pamoja na viongozi wengine wa kisiasa.

waliondoka na masafara wa magari ya serikali, na ujumbe ulipofika ulibaini kuwa mambo sio shwari kwani vijana wengi walikuwa wanarandaranda na mabaongo na kuonyesha kuwa palikuwa na mtafaruku, na walipodadisi kwa viongozi wa serikali waliambiwa kuwa mazishi hayatafanyika siku hiyo kutokana na ndugu kuwa na wasiwasi juu ya msiba husika , na baada ya hapo walijadiliana na ndugu hao wakiwa na mkuu wa mkioa wa mara na kwa kuwa ujumbe wa spika ulikuwa ni kwa ajili ya kusoma risala na kukabidhi mchango wa rambirambi .

wakataka wasome risala na ujumbe uweze kuondoka ,ila ilipofika saa nane na dakika 30 mtafaruku ulianza na wananchi walisema kuwa wako tayari kiumchagua mwingienwakamuue tena , na katika hali waliyoiona hawakuwa na njia nyingine ila ni kwa ujumbe kuondoka na kuelekea musoma na kurejea dodoma .

kabla ya kuwasilisha maelezo hayo ,walipata taarifa za uhakika kutoka kwa viongozi wa mkoa wa mara kuwa uchunguzi ulifanyika na ndugu kukubaliana na uchunguzi huo,na tayari alishazikwa.

Kwa kuwa mazishi yalishafanyika, wanaandaa utaratibu wa kuwasilisha mchango wa rambirambi ya bunge kwa familia ,anashukuru bunge kwa kuwapa heshima ya kuliwakilisha ,na jukumu lilikuwa zito na nyeti na lenye utata mkubwa.

mwisho anaushukuru kwa dhati uongozi wa mkoa wa mara kwa ushirikiano mkubwa na pia anawashukuru wabunge wenzake kwa uadilifu na pia ushirikiano kwa kipindi chote ,pia anampongeza spiaka kwa kuwezesha TBC kuweza kushiriki shughuli za mazishi na pia kwa wao kuweza kuonyesha mazishi hayo live.

amemaliza.

swali;mbona hakuna cha mapanga, sime,mishale, marungu .n.k?

yeye anasema kuwa waliona mabango na vijana wakiimba kwa uchungu,

hasemi kuwa walisindikizwa chini ya ulinzi mkali wa polisi ,

sasa jadilini wenyewe,

hakutaja mapanga ila amekiri kuwa hali haikuwa shwari na wabunge walihisi amani kuweza kuvunjika wakati wowote..
bado ngoma ipo pale pale
 
Hivi kuna waatu mpaka sasa hivi wanaamini kuwa wachunguzi wetu wameshindwa kujua nani alikuwa anaendesha gari, nini kimetokea, Wangwe aliikuwa amekaa kiti gani?

Kama ni hivyo nini maana ya kutumia hela nyingi kusomesha watu wa crime scene na maswala ya evidence collecting? Kitakuwa kitu cha ajabu sana!!

Ina maana serikali haijua nani alikuwa anaendesha gari? No way si walishachukua fingerprints mapema au?
 
Was a normal accident, then what are the possible causes, may be mechanical falts or alcohol influence.
 
Mkuu MK,

Kwanini kama Mbowe hakutishiwa kukatwa mapanga na kukatwa mapanga,kuna tatizo gani?Je inampunguzia nini Mh. Mbowe?Hoja imekuwa mbowe hakutishiwa kukatwa mapanga,kwa kuwa wanampenda sana au?

Kama wanampenda,

1.Kwanini hakuhudhuria Mazishi kama ilivyo kwa Mhe. Kabwe na viongozi wengine?

2.Mhe. Shelukindo mtu mzima na ndiyo maana kasema haya kwa kifupi,Suala la Mbowe kutishiwa kukatwa Mapanga siyo suala la kitaifa,liko kichama zaidi ndiyo maana kwenyeripoti yake hakusema ammbo ya CCM wala CHADEMA
 
hakutaja mapanga ila amekiri kuwa hali haikuwa shwari na wabunge walihisi amani kuweza kuvunjika wakati wowote..
bado ngoma ipo pale pale


Kila mtu anakiri kuwa hali ya usalama ilikuwa mbaya. Nahisi hata Mbowe na Zitto ukiwauliza watadhibitisha. Swali la msingi walibeba mapanga, mishale nakadhalika? Je, walimfukuza Mbowe peke yake au wote?

Any way turudi kwa mafisadi mana wamepumua vya kutosha

Asanten
 
Mkuu MK,

Kwanini kama Mbowe hakutishiwa kukatwa mapanga na kukatwa mapanga,kuna tatizo gani?Je inampunguzia nini Mh. Mbowe?Hoja imekuwa mbowe hakutishiwa kukatwa mapanga,kwa kuwa wanampenda sana au?

Kama wanampenda,

1.Kwanini hakuhudhuria Mazishi kama ilivyo kwa Mhe. Kabwe na viongozi wengine?

2.Mhe. Shelukindo mtu mzima na ndiyo maana kasema haya kwa kifupi,Suala la Mbowe kutishiwa kukatwa Mapanga siyo suala la kitaifa,liko kichama zaidi ndiyo maana kwenyeripoti yake hakusema ammbo ya CCM wala CHADEMA

Wanamuogopa sana
 
Kichuguu na Mkandara.

Nauliza swali, Mbowe alituma press R nyingi kwenye vyombo vya habari kueleza kwanini Wangwe kasimamishwa nafasi yake ya umakamu wa mwenyekiti na hawezi kufanya nae kazi, lakini sijaona tamko lake au rambi rambi kwa ndugu wa marehemu,wana Chadema au marafiki wa Wangwe ameshindwa hata kwenda kuitembea familia ya Wangwe na kuongea nao,yaani hajatoa kauli yeyote juu ya kifo cha WANGWE na amemuachia mtoto mdogo Mnyika kuandika barua kwa IGP,

kwanini hakumuachia Mnyika kuandika juu ya Wangwe kusimamishwa Umakamu?

kitu kingine wazee wa Chadema kama MTEI,Ndesamburo,Ngaiza,Baregu au kundi la wabunge wanawake wa Chadema kama Suzan Lyimo,Grace Kiwelu,Anna Komu na mtoto wa Ndesamburo(Lucy) hawakwenda kwenye msiba hata mmoja kati yao, kama angekuwa kafa Mbowe wasingekwenda? mzee Mtei au Bob Makani kama Mbowe angekuwa amefariki wasingekwenda?

Akifa Pius Msekwa ambaye ni makamu wa Mwenyekiti wa CCM,watu kama mzee Mwinyi,Kawawa na Malecela hawatakwenda kwenye msiba? jee wazee wa Chadema wamejiingiza kwenye ugomvi wa marehemu Wangwe na Mbowe na wao kuwa upande wa Mbowe kiasi cha kususia kwenda kuiaga maiti?

naomba jibu, naona Wangwe hakupewa hadhi yake na watu wa Chadema.
kumtuma Mnyika kwenda kutoa tamko la Chadema ni sawa na Muafaka wa DR.Salmini Amour na Seif Shariff Hamad walipoitwa na jumuiya ya Madola chini ya Chifu anyauko, pande hizo mbili ili kupata suluhu ya muafaka kwa mara ya kwanza, ambapo DR.Salmin hakuhudhuria na badala yake akamtuma sheha(mjumbe wa nyumba kumi) kuwakilisha upande wa CCM. ilikuwa kama dharau kwa Seif Hamad,
jee kitendo cha Mbowe kutotoa kauli hadi sasa na kumtuma Mnyika(sheha wa Chadema) ni dharau kwa Wangwe?

maneno yako yamejaa hekma kubwa na yakini ndani yake..natamani kama yangechapishwa kwenye magezeti yale ya mfanyakazi na mzalendo na nipashe sijui..
 
Mwacheni Alale Salama Wangwe Wa Watu Jamani

Huyo Mallya Ata Kama Amemuuaa Imeshatokea Afanyiwe Kazi
 
Lakini pamoja na moyo wote wa Wangwe kwa wananchi hakuwa na bahati kwani huko Chadema ndio kapata masimango mengi toka kwa Mbowe aliyesema kuwa hawezi kufanya kazi na Wangwe, Kitila Mkumbo alisema kuwa Wangwe ni mzigo mkubwa ndani ya Chadema na hana INTERPERSONAL SKILLS, swali kama hakuwa na INTERPERSONAL SKILLS aliweza vipi kukubalika na wananchi wake?

Misukosuko waliyompa Wangwe hawa jamaaa wa Chadema ni mingi sana, na cha ajabu Mwenyekiti wa Chadema hajatuma wala kuandaa salamu za rambirambi kwa familia au wanachadema, pia wazee wa Chadema hakuna aliyekwenda kuzika kama Mtei,Ndesamburo,ngaiza,baregu,wabunge wanawake wa chadema hawakwenda kuzika.

Mbowe alituma barua nyingi wakati wa Wangwe kusimamishwa lakini kwenye msiba hajatuma salamu za rambi rambi wala pole kwa wana Chadema wala ndugu wa Wangwe ameshindwa kupeleka hata ubani kwa wafiwa.
Mkubwa unachanganya sana mambo mpaka wakati mwingine utahisiwa kuwa unatumika katika hili na sii mawazo yako.
Marehemu Wangwe alikubalika hata naviongozi wa Chadema kuwa ni shujaa mpiganaji. Lakini Chadema kama taasisi ya Umma inataratibu zake za uendeshaji ambazo zimewekwa eitha ndani ya katiba yao au kwa kanuni walizojiwekea. Kiongozi au mwanachama anayekwenda kinyume na kanuni za uendeshaji ni lazima aadhibiwe.
La ajabu hapa adhabu ya kiongozi ndani ya Chadema CCM eti ndio wanalivalia njuga suala hilo na kulikuza kiasi cha kusambaza waraka mikoani kama vile wana uchungu mkubwa kwa yeye alivyosimamishwa. Uchungu unatoka wapi wakati Marehemu alikuwa mwiba kwao?
Sasa ndio wanaunganisha mambo ya kifo na kusimamishwa uongozi, ajabu kubwa hii.
Binafsi nina imani sana na viongozi wa juu wa Chadema na ninaimani kuwa watatulia na huu upepo unaopulizwa makusudi ili kuwatoa kwenye mstari wa mapambano kamwe hautawaweza na utashindwa.
Chadema msiba ndio huo,msichangwanywe na maneno ya maadui zenu,kazi ya kuchunguza chanzo cha ajali ile waachieni wanaohusika ninyi mubaki na ajenda yenu kuu MAPAMBANO DHIDI YA MAFISADI MPAKA KIELEWEKE
 
Vikao vya Marehemu Chacha Wangwe na Katibu Mkuu wa CCM luteni ussu Yusuph Rajabu Makamba, haswa pale Wangwe alipoenda ili kutafuta fedha kwa ajili ya kufanya kazi za kukiumiza CHADEMA, ILA NINAJUA KUWA ALIPEWA ASSIGNMENT FULANI KABLA YA KUPEWA FEDHA HIZO.

Wangwe alikutana na Mawaziri mbalimbali nyumbani kwao usiku na kupanga hatua za kuchukua.

Kitendo cha CCM kuanza kuusambaza waraka wa Wangwe kwenda mikoani siku moja kabla ya ajali husika kutokea ,hili linapaswa kuchunguzwa kwani waraka huo umekuwa ukitumwa kutokea Lumumba na Makao makuu ya CCM huko Dodoma.

Kitendo cha CCM kupanga kumdhalilisha Mbowe akiwa huko Tarime kiliposhindwa magazeti yakawa tayari yameshaandika kuhusiana na suala hilo.

RA kupiga simju yake ya kwanza ndani ya dk 15 baada ya ajali ya Marehemu hili linapaswa kufanyiwa kazi na kufuatioliwa kwa kina sana , kwani alikuwa yupo nje ya Nchi na bila kutafuna maneno huyu alikuwa Jijini Nairobi Kenya.

RA kusambaza milioni moja kwa baadhi ya wahariri waliopotosha habari ile , nasema kwa uhakika kuwa alisambaza milioni moja kwa kila mhariri ama mhariri wa habari aliyeweza kuwepo kwenye kikao chake na wengine ilibidi wakapelekewa fedha hizo wakiwa news room.

Kitendo cha numba za FAX ZA CCM kutumika kusambaza waraka unaoitwa wa WANGWE kwenda nchi nzima na mpaka ngazi za chini ,kinaonyesha kuwa kuna jambo lilikuwa limeandaliwa mahususi na kwa makakati maalum.

Mpango kazi uliokuwa umeandaliwa kwa ajili ya Wangwe kufanya ziara nchi nzima kuanzia mwezi September na bajeti yake ambayo tayari ilikuwa imeshaanza kuandaliwa, mpango kazi huo utachapishwa na gazeti mojawapo kama makala ,ila utalipiwa na mtu mmoja ambaye amekuwa akifadhili mkakati mzima.

Mke wa Wangwe Mariam kutaka familia iamini kuwa CHADEMA inahusika ,huku akiwa yeye ndio alikuwa anaenda kukutana na wakina Rostam Azizi haswa pale Kempinsik kwa ajili ya kufanya mipango na hata kumfanya mumewe kuwa na ukaribu na MAFISADI HAO.
Mariam amekuwa sasa na mkakati wa kuhakikisha kuwa mtoto wa marehemu yule wa kiume mkubwa Zakayo anatumika kisawasawa kutoa kauli kuwa CHADEMA wanahusika ,japo watu wengine kwenye familia hiyo wamekuwa wakipingana na mawazo hayo,na haswa baada ya kujua na kuona mbinu na hila za huyu mke mdogo ambaye alikutana na Wangwe baada ya kuwa Mbunge na hata kumfanya Wangwe kuishi naye.

Familia mpaka sasa wanaugomvi na huyu mke mdogo kwani wanataka kujua mali za marehemu kama vile nyumba na shamba la ekari sita lililonunuliwa huko Dodoma liko wapi na hati zake ziko kwa nani ,hii ilipelekea juzi usiku kukaa kikao mpaka asubuhi.

Mke mdogo akishirikiana na mke wa kwanza wameamua kumtenga mke wa kati yaani yule wa pili ,sasa huyu ndio alikuwa na marehemu wakati wote wa kampeni na hata alipokuwa amefungwa huyu alikuwa naye bega kwa bega.

Namalizia hapa kwa leo.
 
Kuna watu wanaijua profile yake lakini naona wanabana! Baadhi ya maelezo yaliyotolewa juu ya Malya(kama ni ya kweli) yanaonyesha huyu si mtu wa kawaida. We need more details about the guy.
 
Hivi kuna waatu mpaka sasa hivi wanaamini kuwa wachunguzi wetu wameshindwa kujua nani alikuwa anaendesha gari, nini kimetokea, Wangwe aliikuwa amekaa kiti gani?

Kama ni hivyo nini maana ya kutumia hela nyingi kusomesha watu wa crime scene na maswala ya evidence collecting? Kitakuwa kitu cha ajabu sana!!

Mkuu Icadon,

Mbona polisi tayari wamemshitaki Mallya kwa kuendesha gari bila leseni. Ina maana polisi tayari wana ushahidi wa kuonyesha nani alikuwa anaendesha gari.
 
Wanamuogopa sana

Kwanini wamuogope Mbowe,Na hiki kitu kwa sisi wakruya huwa hatukitaki,na ndiyo maana walimchukia Chacha Wangwe sababu hakutaka kubeba mambo ya ukabila.

Kwa hili la kifo cha wangwe niilishatoa onyo zamani sana,ole wao CHADEMA....

Dr. Slaa yupo Nchini,maanda haongelei kabisa suala la Mbowe,wamemuachia Zitto na Mnyika.Na hapa natoa ujumbe kwa mnyika,kama jana alisikiliza hotuba ya Mzee Mandela hapa SA nilipo kwa sasa katika kituo cha kulelea Yatima Basi atakuwa ameupata vizuri.Without Education you can not be a good leader..Rudi shule na ujiendeleze kwanza na ambao mengine baadaye,ungana kina Kitila Mkumbo
 
lazima mtambue mantiki ya uhusika wa ROSTAM hapa sio tu kuwageuzia kibao WASEMA MAFISADI bali pia kuhakikisha kuwa ifikapo 2010 kina MWAKYEMBE na wenziwe wapatao 70 ndani ya bunge hawana upenyo wa kutokea CCM wakihsalimwa vichwa kama ilivyokuwa kwa wakina KITINE 2005. Wanaamini kuwa endapo hakutakuwa na chama mbadala cha kukimbilia wakati huo ambao utakuwa mchache kwa kuanzisha chama kipya na kujijenga basi ni wazi "USHUJAA" wao utakwisha na kelele dhidi ya UFISADI itapungua kama sio kwisha kabisa....

Kwa mimi niliyekuwepo TARIME kuanzia mwili ulipoingia hadi siku ya kuzikwa nashukuru wengi wenu hapa jinsi mnavyochemsha kwani mnaniwezesha kujielimisha mambo mengi ikiwemo hili suala la kujenga imani kwa misingi ya hisia zilizokosa chembe ya ujuvi......

Tanzanianjema

Tanzania Njema, unaelekea kuukaribia ukweli ,
 
unatumia nguvu nyingi sana kuuzima moto huu ..tatizo umebeba mafuta ya petrol kwenye ndoo hiyo unayodhani imejaa maji ya kuuzima moto huo..

Kwa hiyo ndugu yangu ulitaka ninyamaze kimya niache upotoshaji huu ukiendelea? Naipenda Tanzania yetu na chuki hii inayosambazwa, siasa hovyohovyo na uhuni wa WADAU WA UFISADI ni hatari kubwa kwa taifa letu. Siwezi kunyamaza na kwa hilo naomba samahani kwa nitakao wakwaza.

Nimeifuatilia sana ART ya siasa ya nchi yetu na kosa kubwa tulifanyalo wengi ni kuogopa kusema yale ambayo tunapaswa kuyasema lakini hayatakiwi kusemwa...

Tanzanianjema
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom