Insurgent,
Nakubaliana na theory yako. Naamini Mallya alikuwa anaendesha gari na Wangwe alikuwa kiti cha nyuma na most likely hakufunga mkanda. Atakuwa alichoka na kuamua kujipumzisha.
Kuumia alikoumia ni dalili ya mtu ambaye hakufunga mkanda. Ukifunga mkanda ni ngumu sana kupasuka kichwa labda ugonge mwamba au mti.
Duniani kote, wanaosababisha ajali husingizia waliokufa. Siamini kwamba kulikuwa na mtu wa tatu.
Mtanzania, huyu ni Malya akiingia hospitali baada tu ya ajali
Gari lilipopelekwa Gereji:
KIFO cha Mbunge wa Tarime Chacha Wangwe, kimezidi kugubikwa na giza nene baada ya fundi magari katika gereji iliyoko eneo la Sido mjini hapa kusema kwamba, mtu anayedaiwa kuwa dereva wa gari iliyopata ajali na kuumua mbunge huyo, Deus Mallya, ndiye aliyeendesha gari la marehemu hadi gereji kabla ya safari siku ya ajali.
Maelezo hayo ya fundi huyo Israel Remen, ambayo yanashabihiana na ya watoto wa marehemu, yanapingana na kauli ya Mallya ambaye alikuwa katika gari moja na marehemu Wangwe, lakini (Mallya) anadai kwamba hajui kuendesha gari.
Akizungumza na gazeti hili katika gereji hiyo iliyopo karibu na ofisi za Shirika la Sido, Remen alisema, awali
marehemu alipita na Mallya na kusema gari lingerudishwa na rafiki yake huyo kutengenezwa.
Alizidi kusimulia kwamba, baadaye Mallya alilifikisha gari hilo gereji hapo akiwa analiendesha na likafanyiwa matengenezo mbalimbali Remen alitaja matengenezo hayo kuwa ni pamoja na kumwaga mafuta machafu (oil) na matengenezo mengine madogodogo. (Gari lilipelekwa hapo mara mbili; ya kwanza na Malya, na ya pili angalia hapa chini).
Hata hivyo, alisema baadaye mnamo saa 12.00, Mallya alirudi tena safari hiyo akiwa na marehemu na kutakiwa kukaza sukrubu za tairi la kulia la nyuma.
"Alivyokuja, alikuwa na mheshimiwa (marehemu)
ambaye alikaa kiti cha mbele akiwa amekilaza, mimi nikamwambia mheshimiwa usipate tabu kushuka kaa hapo hapo, basi nikakaza kisha wakaondoka Mallya akiwa anaendesha," alisisitiza.
Fundi huyo alipoulizwa kwamba aliwahi kumwona Mallya akimwendesha marehemu kabla, alijibu: "Si mara moja, nilimwona sana, hapa mjini ndiye alikuwa akimwendesha, hata siku chache zilizopita niliwakuta mjini na wakanipungia mkono."
Kwa mujibu wa Remen, tayari yeye amehojiwa na polisi na alipelekwa hospitali mkoani hapa kwa ajili ya kumtambua Mallya, na kuongeza kwamba alithibitishia polisi kwamba ndiye aliyefika na gari hiyo akiwa anaendesha.
"Nashangaa anaposema hajui kuendesha gari, alikuja hapa na gari akiwa ndiye anaendesha, na si mara ya kwanza,
hata mjini alikuwa akimwendesha mheshimiwa," alifichua siri.
Kauli hii ya fundi gereji huyo inazidi kuibua mjadala na utata kuhusu mazingira ya kifo cha Wangwe ambaye alikufa Jumatatu usiku, eneo la Pandambili, Wilayani Kongwa akiwa safarini kwenda Dar es Salaam kuwahi mazishi ya mbunge wa kwanza wa Tarime, Bhoke Munanka.
My Take:
Pale lilipoletwa gari mara ya kwanza na Malya peke yake ni muhimu kweli kujua ni matengenezo gani yalifanyika na kwanini suala la kukaza screws za tairi la nyuma hakukufanywa wakati huo hadi baadaye na yeyote aneyejua magari anajua wazi kuwa kukaza sukurubu za tairi unless hauna zile spana huitaji kwenda gereji.
Ina maana tangia mwanzo wa safari Wangwe alikuwa amejilaza chali... drugged? Kwa sababu ningependa kujua huyo fundi alipomwambia Mheshimiwa kaa tuu hapo hapo, Wangwe alionesha ishara ya kujibu au kuitika?