BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,377
- 8,120
Serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani na Utawala wa Nchi imetangaza kuwa Novemba 13, 2023 itakuwa Siku ya Mapumziko kwa Nchi nzima ambapo Wananchi wote watatakiwa kushiriki katika Upandaji Miti.
Taarifa ya imesema hatua hiyo ni mpango wa Serikali kurejesha na kulinda mazingira ambapo inatarajiwa Miti Bilioni 15 itapandwa katika mpango huo.
Takriban Kaunti 47 zinatarajiwa kutenga maeneo yatakayotumika kupanda Miti.