Kauli ya Rais ni Sheria! Hii kauli ilitokea wapi?

Mpinzire

JF-Expert Member
Jan 18, 2013
7,223
12,943
Nimekuwa nikisikia mara nyingi kuwa kauli ya Rais ni sheria! NImejaribu kupekua Katiba yetu ya Tanzania ya mwaka 1977 na marekebisho yake ya mwaka 2008 sijaona ibara yoyote ya katiba yetu kuwa atakacho zungumza Mh Rais ni sheria!

Leo Waziri Mkuu anaibuka anakazia maneno ya Mh Rais kuwa TRA waachane na madeni ya malimbikizo ya kodi ya miaka ya nyuma kama Mh Rais alivyokasema huko nyuma! TRA wao wanapoenda kwa Wafanyabiashara wanadai madeni ya miaka ya nyuma bado! mfanya biashara akiuliza anajibiwa hizo ni kauli za majukwaani tu mi nafuata sheria.
TRA.jpg

Kwanini Serikali haioni haja ya kupeleka muswada Bungeni ili ipitishwe sheria ya kufuta malimbikizo ya madeni ya huko nyuma? Utawala Bora msingi wake si kufuata Katiba na Sheria?

Tamko la Rais linalindwa na sheria hipi au ibara hipi katika Katiba yetu?

Wanasheria kazi kwenu
 
Nimekuwa nikisikia mara nyingi kuwa kauli ya Rais ni sheria! NImejaribu kupekua Katiba yetu ya Tanzania ya mwaka 1977 na marekebisho yake ya mwaka 2008 sijaona ibara yoyote ya katiba yetu kuwa atakacho zungumza Mh Rais ni sheria!

Leo Waziri Mkuu anaibuka anakazia maneno ya Mh Rais kuwa TRA waachane na madeni ya malimbikizo ya kodi ya miaka ya nyuma kama Mh Rais alivyokasema huko nyuma! TRA wao wanapoenda kwa Wafanyabiashara wanadai madeni ya miaka ya nyuma bado! mfanya biashara akiuliza anajibiwa hizo ni kauli za majukwaani tu mi nafuata sheria.
View attachment 2622900
Kwanini Serikali haioni haja ya kupeleka muswada Bungeni ili ipitishwe sheria ya kufuta malimbikizo ya madeni ya huko nyuma? Utawala Bora msingi wake si kufuata Katiba na Sheria?

Tamko la Rais linalindwa na sheria hipi au ibara hipi katika Katiba yetu?

Wanasheria kazi kwenu
Wajinga wapumbavu ndio wanasema hivyo
 
Wanafananisha mambo ya kale ya uchifu na ufalme. Waziri mkuu atapiga porojo tuu ila hakuna wa kumfanya hapo tra aliyesema zilikua siasa. Maana ukija kwenye karatasi ni sheria inatakiwa kutekelezwa
 
Rais ni mtendaji mkuu wa serikali hao wengine ni wasaidizi wake kwahyo lazima watii maagizo yake otherwise watashindwa kwendana naye itabidi awaondoe ofsn.
 
Rais ni mtendaji mkuu wa serikali hao wengine ni wasaidizi wake kwahyo lazima watii maagizo yake otherwise watashindwa kwendana naye itabidi awaondoe ofsn.
Unaelewa nini ukisikia utawala wa sheria?
 
Rais ni mtendaji mkuu wa serikali hao wengine ni wasaidizi wake kwahyo lazima watii maagizo yake otherwise watashindwa kwendana naye itabidi awaondoe ofsn.
Hayo ni matamko ya kisiasa tu, bila sheria husika kubadirika! Mfano, lile agizo la JPM kuwa mkulima akiwa na mzigo chini ya tani moja asilipe ushuru. Kawaulize wakulima huko kama kuna hata mmoja aliyefanikiwa. Kuna DED mmoja wa Muheza aliwaambia, "Mimi nafuata WARAKA, unavyosema sio maneno ya majukwaani."
 
Wewe ni walewale wa Katiba Mpya tunataka blaah blaaah.
Katafute Ugali wa wanao.
Hayo mambo waachie wenyewe huko
 
Nimekuwa nikisikia mara nyingi kuwa kauli ya Rais ni sheria! NImejaribu kupekua Katiba yetu ya Tanzania ya mwaka 1977 na marekebisho yake ya mwaka 2008 sijaona ibara yoyote ya katiba yetu kuwa atakacho zungumza Mh Rais ni sheria!

Leo Waziri Mkuu anaibuka anakazia maneno ya Mh Rais kuwa TRA waachane na madeni ya malimbikizo ya kodi ya miaka ya nyuma kama Mh Rais alivyokasema huko nyuma! TRA wao wanapoenda kwa Wafanyabiashara wanadai madeni ya miaka ya nyuma bado! mfanya biashara akiuliza anajibiwa hizo ni kauli za majukwaani tu mi nafuata sheria.
View attachment 2622900
Kwanini Serikali haioni haja ya kupeleka muswada Bungeni ili ipitishwe sheria ya kufuta malimbikizo ya madeni ya huko nyuma? Utawala Bora msingi wake si kufuata Katiba na Sheria?

Tamko la Rais linalindwa na sheria hipi au ibara hipi katika Katiba yetu?

Wanasheria kazi kwenu

Ilitokana na dhana ya kwamba Bunge ni Rais na wabunge so wabunge wanatunga sheria kwa vikao vyao na Rais akitamka kwa sababu ni nusu ya pili ya bunge ni kwamba inakuwa katunga sheria! Dhana hii iliundwa zaidi kipindi cha awamu ya kwanza wakati nchi ilikuwa inaendeshwa zaidi kwa decrees, matamko ya mwalimu hadi kukaibuka dhana ingine kwamba fikra za mwalimu ni sahihi muda wote na zidumu! Kwa ujumla ishapitwa na wakati na imekuwa ikitumiwa vibaya muda mwingi sana.

So kwenye katiba utaipata kwenye tafsiri ya Bunge kwamba ni wabunge na Rais.
 
Back
Top Bottom