Awali ya yote, mimi siko Arusha na hata huyu dada tunayemzungumzia simjui. Mimi hapa najibu mada kama ilivyoletwa kuwa wananchi wa Arusha hawamtaki kwa sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ya kuolewa na mzanzibari. Ninachokisema ni kuwa, kama hivyo ni kweli, basi ile sumu ya lugha za kibaguzi zinazotalwala uhusiano wetu na Zanzibar imewasili bara! Ndio maana nikasema kuwa inaelekea hao wapiga kura wanaiona Zanziba kama nchi adui hadi kuona yeyote mwenye mahusiano nako ni adui. Sidhmchango mkubwa katika kukataliwa kwake kama hilo la kuolewa na mtu kutoka nchi isiyo kubalika. Mimi nimeongelea dini kujibu hoja ya Kanda2 kuhusu Ana Komu ambae sikujua kuwa ni mngazija au mtu aliyeritadi.
Sikubaliani na wewe kuwa kisa cha wakristu kuwa adimu katika uongozi Zanziba ni kutokana na demographics peke yake! Na hata huko Rombo, Peramiho, Moshi vijijini hivyo hivyo. Ukweli ni kuwa watu wengi wanapiga kura kwa kuangalia dini ya mtu hasa inapokuja kwenye local politics. Nawajua wakristu wengi tu ambao wako tayari kupigia kura jiwe kuliko huyo ambae wanamuona kuwa ni "mswahili". Zanzibar nako ukweli ni kuwa wengi hawako tayari kumpigia kura "kafir". Ukweli huu, ndio unaofanya wale wanaotoka kwenye minority religions kutojisumbua kugombea nafasi za uongozi katika sehemu wanazoishi. Hizo hesabu zako zina mushkel kidogo maana hakuna connection kati ya idadi ya watu na mwamko wao kisiasa. Wayahudi wako wachache marekani lakini mbona wanamwamko wa kuongoza na wanakubalika. Kama mtu kugombea kunategemea wingi wa kundi analofanana nalo basi hiyo ni dalili ya ubaguzi kuwepo.
Kuacha kuzungumzia udini, ukabila, ubaguzi wa rangi na maovu mengine yaliyo nchini yetu kwa kisingizio cha kuangalia "big picture" ni kuwa kama ostrich anaye fukia kichwa chake kwenye mchanga ili asionekane. Ingekuwa vizuri sana kama kila mgombea angeweza kupimwa kutokana na uwezo wake au ushawishi wake lakini bahati mbaya si hivyo. Jinsia ( uja uzito wa huyu dada ni moja ya ishu zilizoletwa hapa!), rangi, dini, uzawa bado zinachukua sehemu kubwa katika jamii yetu hata kama haipendezi. Kama alivyoandika Cornell West, " Race Matters". It still does. And religion and gender and all the rest of it!
Amandla.........