Hata misupu ameweka hewani, Hakuna cha marekani wala wapi. Dr Batilda izi in Dar, na sioni mimba yoyote...
MICHUZI
Alikuwa Wazo, wana progamu ya mazingira walikua wanaizindua na yeye alikuwa mgeni rasmiHata misupu ameweka hewani, Hakuna cha marekani wala wapi. Dr Batilda izi in Dar, na sioni mimba yoyote...
MICHUZI
Awali ya yote, mimi siko Arusha na hata huyu dada tunayemzungumzia simjui. Mimi hapa najibu mada kama ilivyoletwa kuwa wananchi wa Arusha hawamtaki kwa sababu mbalimbali mojawapo ikiwa ya kuolewa na mzanzibari. Ninachokisema ni kuwa, kama hivyo ni kweli, basi ile sumu ya lugha za kibaguzi zinazotalwala uhusiano wetu na Zanzibar imewasili bara! Ndio maana nikasema kuwa inaelekea hao wapiga kura wanaiona Zanziba kama nchi adui hadi kuona yeyote mwenye mahusiano nako ni adui. Sidhmchango mkubwa katika kukataliwa kwake kama hilo la kuolewa na mtu kutoka nchi isiyo kubalika. Mimi nimeongelea dini kujibu hoja ya Kanda2 kuhusu Ana Komu ambae sikujua kuwa ni mngazija au mtu aliyeritadi.
Sikubaliani na wewe kuwa kisa cha wakristu kuwa adimu katika uongozi Zanziba ni kutokana na demographics peke yake! Na hata huko Rombo, Peramiho, Moshi vijijini hivyo hivyo. Ukweli ni kuwa watu wengi wanapiga kura kwa kuangalia dini ya mtu hasa inapokuja kwenye local politics. Nawajua wakristu wengi tu ambao wako tayari kupigia kura jiwe kuliko huyo ambae wanamuona kuwa ni "mswahili". Zanzibar nako ukweli ni kuwa wengi hawako tayari kumpigia kura "kafir". Ukweli huu, ndio unaofanya wale wanaotoka kwenye minority religions kutojisumbua kugombea nafasi za uongozi katika sehemu wanazoishi. Hizo hesabu zako zina mushkel kidogo maana hakuna connection kati ya idadi ya watu na mwamko wao kisiasa. Wayahudi wako wachache marekani lakini mbona wanamwamko wa kuongoza na wanakubalika. Kama mtu kugombea kunategemea wingi wa kundi analofanana nalo basi hiyo ni dalili ya ubaguzi kuwepo.
Kuacha kuzungumzia udini, ukabila, ubaguzi wa rangi na maovu mengine yaliyo nchini yetu kwa kisingizio cha kuangalia "big picture" ni kuwa kama ostrich anaye fukia kichwa chake kwenye mchanga ili asionekane. Ingekuwa vizuri sana kama kila mgombea angeweza kupimwa kutokana na uwezo wake au ushawishi wake lakini bahati mbaya si hivyo. Jinsia ( uja uzito wa huyu dada ni moja ya ishu zilizoletwa hapa!), rangi, dini, uzawa bado zinachukua sehemu kubwa katika jamii yetu hata kama haipendezi. Kama alivyoandika Cornell West, " Race Matters". It still does. And religion and gender and all the rest of it!
Amandla.........
Hauwezi kuwazungumzia watu wote wa Arusha. Ushahidi ni wa huyu aliyeleta mada hii hapa ambayo anadai ni matokeo ya mazungumzo yake na watu wa Arusha. Ingawa si kitu tunachopenda kusikia lakini bado katika jamii yetu kuna wengi tu ambao watapiga kura kutokana na muangalio wa jinsia, dini, kabila na rangi. Si Arusha peke yake bali nchi nzima. Tunachoweza kufanya ni kuhakikisha kuwa mambo ya muhimu zaidi yanapewa kipaumbele lakini kujidanganya kuwa haya ya kipuuzi hayapo ni hatari mno. Hivi kweli, Mkuu, unataka kuniambia kuwa wabunge wote wanaokubalika ni kutokana na utendaji wao tu na hakuna chembe ya huyu ni wa kwetu? Huyu dada si the worst of the lot lakini bahati yake mbaya mambo mengi yamekutana kwake!
Amandla.........
Sasa mimi nikajiuliza, kumbe mama akiwa mjamzito hafai kuwa mbunge? Lakini baadae nikagundua si suala la ujauzuto tuu, mama huyu wengi wa Arusha hawamtaki kwa sababu zifuatazo
1. Wanasema hawawezi kuongozwa na mtu aliyeolewa zanzibar
2. wengi kutokana na athari za mila hawataki kuongozwa na mwanamke
3. Tatu kuna habari zinazosambazwa kwamba mama huyu hafai kwa sababu si mtu aliye na historia ya kuwasaidia watu kama lowassa, na kuna upepo flani tuu unaolenga kuonesha mama huyu hafai.
Hiki ndio chama cha Demokrasia kinachoshikilia hoja za kibaguzi. Hii ni aibu. Tangazeni sera zenu-mtawafanyia nn Wanaarusha na sio kumkashifu mama wa watu. Kwani wewe mama yako asingeshika mimba ungezaliwa?Acheni mfumo dume.Hii inatufanya tufikiri mara mbili kuwapa kura niyi wahuni. Subirini mshangao Octoba 31.
Napata wasiwasi sana, na najiuliza mbona kama Tanzania tunaendekeza upuuzi namna hii? Watu wanauana Tarime kila siku hatuoni hata wanajeshi wakisema neno. Nakumbuka ulipoongezeka uharamia katika msitu uliopo kati ya Biharamulo na Kigoma wanajeshi walisema kazi yao si kulinda usalama wa raia bali mipaka ya nchi na waingilia kati kama jeshi la polisi litawaomba. sasa swali langu kwa sasa wameombwa na nani kuingilia mabo ya uchaguzi? yaani mwema na vibaraka wenzake wameshindwa kabisa? hata Tossi nlimuona amejikalia pembeni tuu anakodoa macho