Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

Eti Tuikatae voda wewe na nani
Na mtandao upi Utumie labda hama nchi
Ukafanye kinyume na utaratibu lakini Hakuna sehemu utakimbilia ukawa salama kama wewe ni mvunjifu wa sheria na taratibu wa Nchi
Yeye na sisi tusio na PHD alizosema Musiba
 
Mi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda
Hivi kuna watu bado wanatumia voda?
Uko mkoa gani mkuu?
 
Mi niliacha kutumia baada ya kunifanyia uhuni zaidi ya mara tano kwenye kununua bando la elfu kumi,,,baada ya muda mfupi wanakutumia meseji kwamba bando lako la elfu tano limekwisha....pambaf kabisa
 
Customer privacy and cookies policies za makampuni ya simu zinasemaje kuhusu kutoa taarifa kwa third party? Mara zote matakwa yanayopewa na serikali kutekeleza yanakuwa ndani ya ile inayodaiwa ni sheria ya usalama ya nchi husika. Wao ni nani hata wakatae kutii "amri halali" waliyokubali kuitii walipoomba leseni? Vodacom wanajuaje kuwa nyuma ya amri hii kuna utekaji unaoenda kufanyika? Mnataka ku-victimize bure kampuni ya watu badala ya kupigia kelele matumizi mabaya ya sheria halali.
Umeongea la maana mkuu. ila watu hawaelewi,wanaendekeza siasa tu.
 
Hawa ni Vodacom waacha wafie mbali,wanashirikiana na watu wasiojulikana kuwateka watanzania hawa vodacom ni wauaji watatumaliza tuwaepuke hatuko salama.
Kwa hyo mitandao mingine ikiombwa hzo taarifa na serikali, huwa wanakataa?
 
Twende na simple logic, 1% ya 10M subscribers ni wateja wangapi? Kama kwa mwezi kila mteja akiweka vocha ya 1000 tuu ni pesa ngapi inaingiza hiyo 1%?
Hameni peke yenu, bila kutushawishi..
 
Nawaona vodacom wanavyosoma comments zenu kisha waone jinsi gani watajisafisha
Mi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda
 
Naanza na TTCL then Voda na wengine!

Makampuni ya kipumbavu sana!

Eti TCRA wamesema tufungie simu yako,yaani Vodacom inaongea hivi kabisa mbele ya mteja anaeenda kutekwa na regime hiyo hiyo!?

Yaani kampuni inasaidia utekaji??!

Kuna makampuni pia yalimsaidia Hitler,hii dunia tunaenda wapi?!
Una ushahidi au unawashwa kwenda jela tu?
 
Lazima mjue Rostam karudi nchini na ni mwanaccm.
Voda tanzania inamhusu.
La msingi ni kuomba msaada wa kisheria kuishtaki kampuni ya vada Tz kwa mmiliki mkuu kanda ya afrika.
Ni makosa sana kumwamini fisi kulinda bucha.
Uhalifu lazima ufatiliwe
 
Back
Top Bottom