Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kwa ninayo yasikia ni bora kujihami mapema, hivyo nimeachana kabisa na kutumia laini ya Vodacom na nitatumia mitandao mingine nayo ikishindikana basi nitaanza kutumia Email kuwasiliana.

VODACOM sio salama kwa mawasiliaona kabisa labda tuwaachie Makada waendelee kutumia.
Acha tu, ukisusa....?
 
Afadhali ghali lakini BORA.. vifurushi vyao vya data vina speed ya hali juu. ukilinganisha na hayo mamitandao mengine, Tigo ndo kabisaa.Jana nilijaribu kutumia tigo kwenye YouTube, aisee nilikesha. Yaan kitu cha kuangalia dakika 10 nilitumia dakka 45.Ina play dakika moja, inaganda kwa dakika 5.Halafu inaplay tena.
Siwezi kuhama Vodacom Tanzania
Halotel GB1 na mameseji kibao na dakika kwa 1000 week nzima, halafu speed ya kufamtu... GB 1 voda unanunua shngap?
 
Voda ni Kama ccm. Bado hawana mbadala pamoja na usumbufu wao wote
 
Mi voda ipo kama pambo siwezi kununua hata muda wa hewani wa sh 500
 
Ona huu ujinga yani umeshabebwa na mazwazwa ya kisiasa tayari?

Wewe una siri gani Mpaka voda wahangaike kuliweka hadharani?

Pumbavu kabisa! Basi usitumie simu kabisa, maana kama una baya lolote utapatikana tu.

Mm siwezi kuhangaika eti nisuse mtandao kisa huo ujinga wenu wa siasa. Hivi kwa akili yako unafikiri kuna mtu anahangaika na kufuatilia kutongazana kwako kila siku na kina mwajuma.?
Wewe siyo jua kwamba huchangamani na wengine, wakimaliza na wao, watarudi kwetu.....think nje ya Box!!
 
Una ushahidi au unawashwa kwenda jela tu?

Unataka ushahidi gani?

Watu wanatekwa na serikali tuliyoipa dhamana yote kuhakikisha hawa watu wanashikwa hawashikwi,then wewe unategemea ushahidi gani?

Ninawashwa kwenda jela ya mama yako?

Hivi nini kinawapa kiburi namna hii mpaka unafikia kutoa hukumu eti natakiwa kwenda jela as wewe ni jaji tayari?

Kuna wadudu washaharibu bongo zenu!
 
Jambo baya sana kwa mitandao yetu hii tuliyokua tunaiamini. Hatua za kufanya;-
KWANZA wataarifu ndugu, jamaa na marafiki kwamba unaifunga line yako ya voda(hii itakusaidia wasipatwe na mshtuko maana tunasikia matukio hayo ya line kublokiwa).
PILI piga simu Huduma kwa Wateja wataarifu wakufungie line yako.
TATU hamisha namba zilizopo kwenye line yako hiyo, mwisho kaitupe kusikojulikana.
 
Kwa ninayo yasikia ni bora kujihami mapema, hivyo nimeachana kabisa na kutumia laini ya Vodacom na nitatumia mitandao mingine nayo ikishindikana basi nitaanza kutumia Email kuwasiliana.

VODACOM sio salama kwa mawasiliaona kabisa labda tuwaachie Makada waendelee kutumia.
Unadhani ni voda tu, acha kabisa kutumia simu maana pamoja na makelele mengi google bado wanalalamikiwa kukusanya taarifa ambazo wanazihandle kwa serikali ya marekani sasa ije kuwa Tanzania - Marekani nayo inaibana china kwa kuhofia yale yale ambayo yenyewe inayafanya hahaha no where to run bro labda utumie apps ambazo zina end to end encription kwa matumizi ya kupiga na kupokea ila jiulize wangapi wanatumia apps hizo? huko kwenu kwa mababu na ndugu hata wanazijua? ni hatari sana mkuu
 
Nilikuwa natafuta chanzo cha kuachana nao nimepata issue ya jana imenirahisishia, kwanza ni wezi wa bando na airtime. Kuna hash tag imeanzishwa #JiondoeVodacom itazinduliwa rasmi hivi karibuni.
Kwanini wadukuliwe wao na sio wewe
 
Back
Top Bottom