Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

Voda wezi wa bando hao mie siku hizi nimeifanya simu ya mezani, hapa natafuta kitochi ikae tu nyumbani
 
Tatizo la Vodacom washajiona wana customer wengi,wamekua na kiburi,hakuna tena kujali wateja wao,wao ni kupandisha bei ya mawasiliano yao na kuwaibia wateja wao tu.hawa ni kuachana nao tu
 
Kwa hyo mitandao mingine ikiombwa hzo taarifa na serikali, huwa wanakataa?
Kuna kuombwa taarifa za MTU kwa kufuata sheria,SERIKALI LAZIMA IENDE MAHAKAMANI ILI KUPATA KIBALI,lakini kwa sababu serikali ndiyo inaongoza kwa kuvunja sheria Mara ngapi polisi wanapekua Nyumba za watu bila kibali cha mahakama wakati sheria inasema hivyo.
 
Kuna kuombwa taarifa za MTU kwa kufuata sheria,SERIKALI LAZIMA IENDE MAHAKAMANI ILI KUPATA KIBALI,lakini kwa sababu serikali ndiyo inaongoza kwa kuvunja sheria Mara ngapi polisi wanapekua Nyumba za watu bila kibali cha mahakama wakati sheria inasema hivyo.
Kumbe wa kulaumiwa sio network provider (vodacom). Tulaumu ubabe wa serikali yetu.
 
Kupitia mtandao wa twitter,kuna kampeni imeanza ya kuikataa kampuni fulani ya simu kwa tuhuma za kuvujisha siri za wateja wake.

Watu wameaandika jina la kampuni na nembo ya kiana na kisha kupiga mkasi wa mstari mwekundu.

Tutaeshimieni tu.

aisee wanavyojitetea sasa hadi huruma, ndo wakome.
 
Bahati mbaya siwezi kuhama voda pamoja na mspungufu yao internet yao ni bomba japo ni ghali sana.
Pigeni tu kampeni zitasaidia kuboresha huduma japo sihami voda nimewekeza sana
Bado tu unatumia voda?
 
Voda kwanza wezi sana. Me walishanipinguzia salio langu Mpesa almost Elfu 62400 Halafu nawaeleza ofisini kwao pale Kibo wananiambia miamala inachunguzwa na Selcom. Bora kuwahama
 
Unataka ushahidi gani?


Watu wanatekwa na serikali tuliyoipa dhamana yote kuhakikisha hawa watu wanashikwa hawashikwi,then wewe unategemea ushahidi gani?

Ninawashwa kwenda jela ya mama yako?

Hivi nini kinawapa kiburi namna hii mpaka unafikia kutoa hukumu eti natakiwa kwenda jela as wewe ni jaji tayari?

Kuna wadudu washaharibu bongo zenu!

dah mkuu umenifanya nmecheka kwa nguvu mpka wife kamshtuka
 
Kumbe wa kulaumiwa sio network provider (vodacom). Tulaumu ubabe wa serikali yetu.
Ni juu yao kukulinda mteja,wao wangedai kibali cha mahakama ilikuwa simple tu,kumbuka Kesi ya Max Melo walitaka kufanya kama walivyofanya kwa Vodacom,jamiiforum wakagoma sasa kesi iko mahakamani kila siku inaahirishwa,ni wajibu watu kuikumbusha serikali kutii sheria bila shuruti kama inavyotaka RAIA wafanye hivyo.
 
Mim nishahamia royal halotel bando mwez mzima unlimited kwa elf 10 tu. Bye voda ila siwez itupa maan watu wang weng wanaijua hio.. itakua ya kupokea call only
 
Mi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda
Basi hata benki zingefungiwa kwa kutoa siri ya viroba vya sandarusi na vijisenti vya mboga,kama kukataa kataa mwenyewe na siri gani hizo,kama unataka kuisaliti serikali utadukuliwa hata isipokuwa Voda,mara nyingi muovu huogopa hata kivuli,pia kudukuliwa mawasiliano si lazima yadukuliwe kutoka Vodacom tu hata kwenye kompyuta watu hudukuwa hao ndio hackers,kuwalaumu Vodacom ni kuwaonea
 
Utake usitake dunia ya leo kudukuliwa ni kitu cha kawaida,hata ukihamia sijui kampuni gani ya simu unaweza kudukuliwa na hii ni duniani kote,kumbukeni yaliyomkuta Ossama Bin Laden na yule muingereza mwarabu wa ISIS aliyekuwa anachinja watu kama kuku,karibu nchi zote zinadukuwa mawasiliano iwapo mamlaka zinakutilia shaka na mwenendo wako.Kipi kizuri mamlaka zidukue mawasiliano ili nchi ikwepe machafuko au iache kudukua watu walete machafuko?sijui hizo simu zenu mtasikilizia wapi kikiumana.
 
Back
Top Bottom