Kampeni ya kuikataa Vodacom

Kampeni ya kuikataa Vodacom

Nashauri Vodacom sasa waende hatua moja mbele,hasa kwa wale wanaowashambulia mitandaoni bila sababu

Tunajua wanatumia huduma zenu za SMS,mpesa na kupiga simu.

Basi kwa kasi ile ile mliyoanza nayo,anzeni kuwashikisha adabu wale wote wanaowaandama

Anzeni na wanandoa,halafu mnapanda polepole mpaka wanyooke
 
Vodacom soon itayumba.Imekuwa ya hovyo,na kumbe ni ya ccm!
 
Mi nawaomba kwa umoja kabisa tuanze kampeni hii ya kukataa kutumia vodacom labda akili itawarejea, haiwezekani sisi kama wateja siri zetu zinatolewa pasipo ruhusa ya mteja na kama haitoshi unafungiwa kupiga simu pasipo kutaarifiwa na kubwa zaidi tabia yao ya kupunguza vifurushi. Tuseme sasa inatosha voda wameota mapembe wakati sisi ndo tumewafikisha hapo.
# TuikataeVoda
# HawatufaiVoda
Naanza kutengeneza bango la tupa laini ya Vodacom Tanzania
 
Unakimbia Voda unaenda TTCL heheheh yale yale
 
Najiulizaga sAna wanaotumia voda wanamudu vip vifurushi vyao, kwani ni ghali sana
Afadhali ghali lakini BORA.. vifurushi vyao vya data vina speed ya hali juu. ukilinganisha na hayo mamitandao mengine, Tigo ndo kabisaa.Jana nilijaribu kutumia tigo kwenye YouTube, aisee nilikesha. Yaan kitu cha kuangalia dakika 10 nilitumia dakka 45.Ina play dakika moja, inaganda kwa dakika 5.Halafu inaplay tena.
Siwezi kuhama Vodacom Tanzania
 
Kwanza naomba kutoa interest yangu, mimi nina kesi mahakama kuu moja nchini lakini kuna siku mahakamani mlalamikiwa alikuja pembeni akasema anayo mawasiliano yangu ya simu na anaweza kuyaleta mahakamani, na kuna mpambe wake mimi niliongea nae somewhere akasema jamaa aliongea na mtu wa voda akampa na yeye alishayasikiliza....

Leo nakutana na hizi kitu kwenye attachment je ni kweli vodacom wanahisika kuvujisha siri za wateja....

20190730_201705.jpeg
20190730_201635.jpeg
 
Ona huu ujinga yani umeshabebwa na mazwazwa ya kisiasa tayari?

Wewe una siri gani Mpaka voda wahangaike kuliweka hadharani?

Pumbavu kabisa! Basi usitumie simu kabisa, maana kama una baya lolote utapatikana tu.

Mm siwezi kuhangaika eti nisuse mtandao kisa huo ujinga wenu wa siasa. Hivi kwa akili yako unafikiri kuna mtu anahangaika na kufuatilia kutongazana kwako kila siku na kina mwajuma.?
kila siku nasema ukimwamiini mwanasisa ni sawa sawa kabsa na .kumwamini shetani........

FB_IMG_1561740244400.jpeg
 
Ona huu ujinga yani umeshabebwa na mazwazwa ya kisiasa tayari?

Wewe una siri gani Mpaka voda wahangaike kuliweka hadharani?

Pumbavu kabisa! Basi usitumie simu kabisa, maana kama una baya lolote utapatikana tu.

Mm siwezi kuhangaika eti nisuse mtandao kisa huo ujinga wenu wa siasa. Hivi kwa akili yako unafikiri kuna mtu anahangaika na kufuatilia kutongazana kwako kila siku na kina mwajuma.?
Miye hata nikipigiwa simu kwa line ya VODA. SIIPOKEI
 
Back
Top Bottom