Kama uzuri wa sura, umbo, ngozi na mguu ndiyo vigezo vyako muhimu kwa kuoa basi umepotea sana

Mkuu kama hujaoa nakupa pole, na kama umeoa na unadhani uko smart kwa wachawi unajidanganya na hujui kitu. Wachawi ni genge hatari na familia chache sana ziko free.

Inabidi nifunguke kidogo ili watu wengine wasiingie mkenge. Mimi mama (RIH) yangu alikuwa mchawi hiyo ni " rot in Hell".

Matatizo niliyopata hakuna sababu ya kuweka hapa.

Kilichonisaidia ni mimi kuwa mlokole na kuoa mke mlokole wa kumaanisha.
Sasa Mama alipokuja kuwanga kama kawaida yake siku hiyo yeye alimuona yaani walionana macho kwa macho.
Ila shida ataniambiaje mimi kwa mama mkwe mchawi. Ilichukua muda sana. Mimi na jirani yangu kulikuwa na kutoelewana ķuhusu mpaka na ikafika hatuongei mwaka mzima.
Sasa rafiki yake wife akaniambia anaeniletea matatizo ni mama yangu sio huyo jirani. Sikukubali wala kukataa. Niliamua kufuatilia kimya kimya.

Sasa mama alikuwa anakaa mbali na sisi, ila akija nyumbani lazima amchukue binti yangu anaenda nae kuoga. Yaani wanaoga wote uchi bafu moja. Mi nilikuwa sijui nakuwa kazini. Ndipo wife akanitonya kinachoendelea.

Mimi nilienda kwa wakubwa ambao hawamjui mama na nikatoa stori kama mhusika sio mimi wala faimilia yangu kutaka ushauri. Nikaambiwa huyo mama yangu sababu ameshakuwa mtu mzima alikuwa anatafuta mrithi. Hivyo mtoto mdogo akishazoea wakubwa kuwa uchi baadae akienda nae hatashangaa.

Sio hivyo tu alipata mama matatizo mengine ilibidi aende kwa siri kwa mganga alipelekwa na rafiki yake ambae sio mchawi. Akaja akagombana na huyo rafiki yake akimtishia kumpeleka polisi kwa wizi, kumbe aliyeiba ni ndg yake mama.
Sasa huyo rafiki yake ndio akatoa stori kwamba mganga alimwambia mama kwamba ajibu maswali ya ramli kama ni kweli ndio apate tiba.
Baadhi ya maswali ni pamoja na kula nyama za watu na viungo vya albino, ambapo mama alikubali.

Naishia hapo ila niko Free sasa mchawi mama ameshakufa.

Hakuna cha fununu mkuu.

Ila baada ya kushindwa kunitoa kafara ilibidi afe yeye mwenyewe kabla hajafa alimjia wife kwenye ndoto kumuaga kwamba anakufa. Wife baada ya kuota ile ndoto alimwendea mama nyumbani kwake na kumuambia ameota anamuaga. Mama akajibu ni kweli atak7fa muda sio mrefu.

Mama alikufa muda mfupi baada ya kuanguka akitokea chooni.

Kaa vizuri na Mungu wako Mkuu from experience ni vigumu kuwakwepa hawa watu. Tatizo wanaloga kote kote.
Ok mkuu nakubaliana na wewe asilimia 100%. Naomba nitangulize hofu ya Mungu kama kigezo cha kwanza , then IQ na vingine. Ila kuhusu uchawi ukichunguza zaidi kwa majirani na ndugu wa karibu wa binti wanaweza kukupa hint.
 
Ok mkuu nakubaliana na wewe asilimia 100%. Naomba nitangulize hofu ya Mungu kama kigezo cha kwanza , then IQ na vingine. Ila kuhusu uchawi ukichunguza zaidi kwa majirani na ndugu wa karibu wa binti wanaweza kukupa hint.
Mi nakushauri uokoke na uwe serious na wokovu.

Mi nimeona watu wamelazwa muhimbili na waliokuwa wanatoa msaada sana na kupeleka chakula na kumsaidia sana mgonjwa ni wachawi waliomloga. Wanamsindikiza afe haraka, sasa we fikiria kama kuna dokta mchawi humo pia inakuwaje. Wodi za wazazi ndio zaidi sasa.

Naona wewe bado umri mdogo changamoto za dunia hii huzijui.

Unadhani wachawi ni mafala hawana elimu.

Kwenye kundi hilo wapo pia wachungaji, ma injinia, wazungu,walimu wakurugenzi, wabunge na wafanya biashara n.k.

Uchawi ni " spirit" inayofanya kazi kupitia ndani ya mtu. Hivyo kupitia milango mitano ya fahamu ambayo ni " physical faculties" huwezi kumbaini mchawi. Wapo wachawi wadogo "wanga" ambao mara nyingi utasikia kadondoka sehemu fulani. Hao unaweza kubahatika kupata stori zao.

" Spirit" ya uchawi unaweza kuisambaratisha na " Holy Spirit" ambayo inatokana na Mungu. Sababu Mungu amekuumba wewe na huyo mchawi nguvu ya Mungu ni Super Power ambayo mchawi au majini hayafui dafu. Ndio maana walokole tunatamba sana. Ila mchawi ana uwezo wa kujua mlokole feki na genuine.
Mchawi pia ana uwezo wa kujua kuna kijana ana piga piga "chabo" anataka apate hint anataka kuoa ila anaogopa wachawi anapita pita hapa. Basi utakuta unasetiwa unaungia mzima mzima, kichwa na miguu.

Hii kwenda kwa waganga kupata kinga ni kujidanganya sababu kwa waganga nao ni ma witch, hakuna super kinga ambayo hio ukiwa nayo basi wachawi watakimbia, inakuwa ya muda tu ina expire.

Kinga ambayo ni 100% na hakuna ku expire ni Jesus.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom