Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

panya wengine wameshindikana

ninao paka3 na wako full patrol daily eneo lote..

sasa shida panya wanatembea juu ya bati na darini,hawashuki chin

leo nawawekea nyanya,indocid,valium na piriton kupunguza machungu

Mlamu, panya wapo darini huko wewe unateseka na nini?
 
[emoji23][emoji23][emoji23]sisi tulkua kama wanne hv tumejifungia na panya ndani tunawawinda wawil tu wakachomoka speed kali kila mtu alitafta pakutokea
[emoji3]

Kuna siku panya kaingia kwenye kabati ya nguo niko na jamaa yangu tukaanza kupekura mule kabatini, pekenyua huku tunapigapiga bwana, yule panya si akatoka kwa spidi ya risasi.... Jamaa akaruka kwa mshituko [emoji3][emoji3] sasa kile kitendo cha kuruka ikawa ni kosa la jinai maana alimtimbatimba panya kapasukapasuka... Aisee siwezi sahau siku ile.
 
Dawa ya Panya ni nyoka tu hamna namna,kuna baaadhi ya nyoka unaweza kaa nao ndani bila ya shida yeyote kabisa tena unaweza tulia kwenye sofa unacheki tv na yeye akaja sebureni ila itapendeza zaidi ukiwa na mtoto mdogo ndani.

Maana watoto hupenda sana kucheza na nyoka na yeye kujisikia yupo comfortable.Ila angalia nyoka wa kubeba na sio kujibebea tu
 
Wiki iliyopita niliweka endocine na unga wa sembe panya walikufa wote kitu ambacho hakijawahi kutokea!
Ilikuwa nikiweka sumu za panya zingine hawafi wote ila safari hii nyumba imekuwa na amani
 
Panya hujificha juu darini na kushuka chini kupata misosi au kuzaa/kulea.

Ukiiziba dari vizuri kwa singibodi au jipsam unakuwa umekata mzizi wa fitna.

Hapo akibaki juu lazma afe kwa njaa au ahame na akishuka chini unamkamata kilaini.

**Penye panya wengi ni salama zaidi, hamna nyoka hapo mahali.
penye panya wengi hamna nyoka kivipi?
 
Je umekuwa ukisumbuliwa na panya sana?

Je umetumia pesa sana kununua sumu za panya bila mafanikio?

Kama jibu ni ndiyo basi soma na ufanye hivi;

Nenda duka la dawa nunua dawa inaitwa INDOCID (indomethacin 25 mg capsules) halafu katege kama unavyotegaga sumu nyingine za unga za panya. Baada ya siku 4-5 matokeo utakayoyapata naamini mwenyewe utaleta mrejesho.

Dawa hii hutumiwa na binadamu kama dawa zingine tu ila kwa panya ni sumu kwani wakishakula utaona siku ya nne panya wanakufa na wengine wanashindwa kutembea kwa kusagika sagika mifupa.

Kama una jirani yako mshauri naye atumie maana muda mwingine waweza kuta unahangaika kumbe wanahamia kutoka nyumba ya pili.

Dawa hii inaepusha gharama kwani pakiti ya buku (tembe 10) unaweza tega mara kadhaa bila kuimaliza pia ni salama kabisa wakati wa kutega kwani siyo sumu kwa binadamu.
Dawa ya panya ni paka tu
 
Mkuu una bahati hao wako mbona wastaarabu. Kuna wengine wanakuvizia usiku mwingi umelala wanakula tartiiiiibu ile sehemu nyeupe nene ya unyayo wako.

Kuna wengine wadogowadogo sana anaingia kwenye begi anatengeneza uchochoro wa ndani kwa ndani kwa kula nguo kutoka upande mmoja wa begi hadi mwingine. Siku unataka mtoko unakuta kila nguo unayoitoa humo ina shimo mahali fulani.
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] wakikung'ata wanakupulizia kabisa usiamke
 
Indocin haifanyi kazi mi nimewawekea vidonge v5 lakini hakuna matokeo
 
Mi panya wakizidi store,huwa siangaiki sijui na madawa Wala mapaka
Namkamata house brown snake namtupia huko nafunga store
Nikimkosa nachukua mpini wa jembe najifungia nao huko natembeza rungu

Ingawa wanaweza kukuuma
 
Leo nimewafungia kazi hawa jamaa baada ya kugundua maficho yao....
Nimekamata panya 8 physically nimewatanguliza kuzimu.....

Kuna haja ya kumuazima magawa aje awape semina....
IMG_20201016_142403_632.jpg
 
Back
Top Bottom