Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

Panya wa Dar wengi wanaijua mitego, baada ya kuligundua hilo huwa nanunua visamaki halafu nachanganya na sumu baada ya hapo nafunga kama nimeficha.

Hapo akili yao inajua nimeficha chakula changu ndo navyowapukutisha, uswahilini ukitega panya wengine watakufa huko nyumba ya 5.
 
Huenda huko darini wanaunda UKAWA wakishuka huko lazima paka wahame hiyo nyumba.
panya wengine wameshindikana

ninao paka3 na wako full patrol daily eneo lote..

sasa shida panya wanatembea juu ya bati na darini,hawashuki chin

leo nawawekea nyanya,indocid,valium na piriton kupunguza machungu
 
Mimi alikaa kwenye sofa, anatoka usiku mchana anakausha unamsikia anavyohangaika.

Muda ukaenda akatanuka nakuongezeka size. Kuna siku anatembea kwenye sofa namsikia anavyojipenyeza. Aiseee nilipiga ngumi, vipepsi na mateke lile eneo alipo hadi akaanza kupiga ukunga.

Aisee nilitandika ngumi za maana hadi akatulia baada ya siku mbili nikaanza kusikia harufu ya mzoga nikajua tayari.

Hahahahah Nguvu yote hiyo kuua panya tu
 
Ahhh aseeh kwenye sabufa yangu pale kweny lile tobo aliingia nikiwa namuona kabisa ilikuwa mchana basi ilikuwa on nikaweka bluetooth nikatafuta nyimbo yenye mdundo wa maana alafu nikaongezaaaa sauti volume hadi mwisho nikapita kinyuma nyuma nikaziba kwa haraka lile tundu na nguo kisha nika play [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] nilimchangamsha niliplay nyimbo tano zenye mdungo mkubwa kisha nikatoa tambara alitoka anatembea kama mlevi nikamalizia kuua saafi

Ila we jombi ni mafia sana 😂😂😂
 
Dawa ya panya ni paka tu. Lipaka litawakamata ndani ya wiki moja wote anawafyeka.
 
Nimehamia mtaa na makazi mapya, nilipofika siku ya kwanza ilikuwa shwari kabisa. Baada ya week nikaanza kuona panya mmoja. Nikamwinda nikamuua. Baada ya miezi miwili miaka tena panya.

Hadi tunapoongea ndani kuna panya kama sita. Nimejaribu kuwatega na sumu Sanasana anakufa mmoja afu ananuka nyumba nzima.

Week mbili zilizopita nikiwa na jirani yangu nikamwambia napita dukani ninunue Dawa ya panya. Akanambia yeye amekaa mitaa hii miaka kumi sasa akiwa anaishi na panya ndani Wala hawaishi. Akanitajia na majirani wote walia na Hili tatizo la panya.

Mwenye msaada wa dawa tafadhali naomba.
 
Huku kijijini kwetu wanasema ukiwa na panya kwako ina maana hauna njaa ndani kwako, kama huwezi kufuga paka azima kwa aliyefuga aje alale kwako hata usiku mmoja then umrudishe kwa mwenye naye.
 
Wakamate hao panya uwalete huku lab, we need all of them. We will pay you kwa effort za kuwakimbiza na kuwakamata, tutamnunua pia kila panya.
 
Kuna dawa huwa tunatumia ni ya binadamu lakini tunaulia panya inaitwa (Indosidi) sijui inaandikwaje kitaalam ila inatamkwa hivyo. Ipo kama zile rangi mbili. Unafumua vile vi tube na kuweka kwenye mnofu.

Panya wakila wanalegea hata kutembea hawawezi unawakamata na kuwatupa nje.
 
Kuna dawa huwa tunatumia ni ya binadamu lakini tunaulia panya inaitwa ( Indosidi) sijui inaandikwaje kitaalam ila inatamkwa hivyo. ipo kama zile rangi mbili. Unafumua vile vi tube na kuweka kwenye mnofu.

Panya wakila wanalegea hata kutembea hawawezi unawakamata na kuwatupa nje
Usiue mkamate tuletee
 
Panya wanategemea sana usafi wa nyumba na mpangilio wa vitu. Mie toka nihamie kwangu karibia muhongo mmoja sijawahi ona panya. Kwanza atakimbia vipi kwenye tiles ya mspaniola.
 
Back
Top Bottom