Mkuu nimekumbuka hii stori yako ikabidi niitafute maana na mimi imenitokea leo.
Jioni hii mida ya saa mbili mbili nimekaa zangu sebuleni nacheki movie nimalizie easter, mara nikasikia panya anakukuruka ndani ya kochi nililokalia! Huyu panya ameshanisumbua mda mrefu hua namuona anakatiza spidi ila nikimtafuta ana dissappear katika mazingira ya kutatanisha. Zaidi ya mara tatu ameshaniponyoka. Sasa leo niliposikia kukuru kakara nikapigapiga kochi kwa pembeni mara namuona huyo kachomoka nduki kali sana. Kumuangalia vizuri nikaona kaenda kwenye sabufa na akatumbukia kwenye kale kashimo.... nikatabasam baada ya kukumbuka huu uzi!![emoji3][emoji3][emoji3]
Kwakua ni usiku nikaona nisifungulie muziki, nikaziba kile kitundu kisha nikabeba sabufa mpaka kwenye chumba kimoja ambacho hakina kitu ndani. Basi nilichofanya ni kuitikisa ile sabufa kwa nguvu kama dakika moja kisha nikaiweka chini nikafunua kale kashimo. Panya kachomoma nduki, lahaulaaa akakuta hana pa kujificha, yupo uso kwa uso na jitu linalotisha lenye fimbo ya ufagio mkononi! Kilichofuata hapo ni mtanange wa kukata na shoka, patashika nguo kuchanika na mpaka mwisho wa pambano, mimi 1 panya 0!
Nikamtoa na kumtupa nje kishujaa, nikarudi zangu kuendelea kucheki muvi kama vile hakuna kilichotokea. Hata dakika tano hazijapita, nikashangaa chini ya lile kochi kachomoka panya mwingine mkubwa mara mbili ya yule, nae nduki kali! Kumbe hua wako wawili!! Kumuangalia tena, nae akazama kwenye tundu lilelile la sabufa! Nikatabasamu tena, na mchezo ukawa ni ule ulee...!!! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Huyu wa pili kanipeleka mperampera balaa, panya anaruka anatembea kwenye ukuta kama bruce lee, almanusura anitoe knock out. Ila bahati haikua yake, kwani mpaka mwisho wa pambano, mimi 2 panya 0.