Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

Kama unasumbuliwa na panya pitia hapa

Panya hujificha juu darini na kushuka chini kupata misosi au kuzaa/kulea.

Ukiiziba dari vizuri kwa singibodi au jipsam unakuwa umekata mzizi wa fitna.

Hapo akibaki juu lazma afe kwa njaa au ahame na akishuka chini unamkamata kilaini.

**Penye panya wengi ni salama zaidi, hamna nyoka hapo mahali.
 
Je umekuwa ukisumbuliwa na panya sana?

Je umetumia pesa sana kununua sumu za panya bila mafanikio?

Kama jibu ni ndiyo basi soma na ufanye hivi;

Nenda duka la dawa nunua dawa inaitwa INDOCID (indomethacin 25 mg capsules) halafu katege kama unavyotegaga sumu nyingine za unga za panya. Baada ya siku 4-5 matokeo utakayoyapata naamini mwenyewe utaleta mrejesho

Dawa hii hutumiwa na binadamu kama dawa zingine tu ila kwa panya ni sumu kwani wakishakula utaona siku ya nne panya wanakufa na wengine wanashindwa kutembea kwa kusagika sagika mifupa

Kama una jirani yako mshauri naye atumie maana muda mwingine waweza kuta unahangaika kumbe wanahamia kutoka nyumba ya pili

Dawa hii inaepusha gharama kwani pakiti ya buku (tembe 10) unaweza tega mara kadhaa bila kuimaliza pia ni salama kabisa wakati wa kutega kwani siyo sumu kwa binadamu
Kuna kunguru wanakula vifaranga wangu nataka kuwatega je hii dawa inauwa wanyama jamii ya ndege kama kunguru
 
Fuga paka ndugu, tena tafuta breed inayowinda na kula panya.

Kero yake kuu ni pale panya watakapo kwisha ndani kwako ataanza kwenda kuwinda nje kisha anakuletea mizoga ndani.

Pia anavyozidi kukua ataanza kuwa jeuri na mwenye tabia za porini.

Mbali na hapo, hili ndilo suluhisho la kudumu. Panya wako very smart, wakijua nyumba hii kuna paka basi wanahama kabisa.
Leo ndio nilikuwa najiuliza kwanini kila paka ninaeleta alikuwa anakimbilia porini? Kumbe ni mipaka pori, ikikuwa inarudi kwao. Ahsante mkuu kwa kunijuza.
 
Usidanganywe indocide ni salama ikiwa kwenye capsule zake tu nje ya hapo ni sumu kama sumu zingine na hasa ikiingia mfano kwenye kidonda au sehemu ulipojikata hata uuzaji wake mpaka uwe na cheti cha dactari ndio unauziwa.

Ila ni sumu nzuri sana kwa panya na wakifa hawanuki
Yaani umeanza kwa kubisha lakini umehitimisha kwa kukubali hoja iliyoko mezani, kama ni kwenye debate club wewe umeshauza timu.
 
Mimi alikaa kwenye sofa, anatoka usiku mchana anakausha unamsikia anavyohangaika.

Muda ukaenda akatanuka nakuongezeka size..... Kunasiku anatembea kwenye sofa namsikia anavyojipenyeza..... Aiseee nilipiga ngumi, vipepsi na mateke lile eneo alipo hadi akaanza kupiga ukunga....

Aisee nilitandika ngumi za maana hadi akatulia baada ya siku mbili nikaanza kusikia harufu ya mzoga nikajua tayari....
[emoji1787][emoji28][emoji28][emoji28]
 
Mkuu aheri kutumia "Mouse glue traps " kuliko sumu ,mara inamfanya Kama Teja yaani anakufa kwa taabu tupu "Kuna nchi kuua panya bila kibali ni kosa Kama kuua mnyama wa porini bila kibali.
nchi gani hiyo?
 
Mkuu aheri kutumia "Mouse glue traps " kuliko sumu ,mara inamfanya Kama Teja yaani anakufa kwa taabu tupu "Kuna nchi kuua panya bila kibali ni kosa Kama kuua mnyama wa porini bila kibali.
nchi gani hiyo?
 
Yaani umeanza kwa kubisha lakini umehitimisha kwa kukubali hoja iliyoko mezani, kama ni kwenye debate club wewe umeshauza timu.
Mkuu nilichobisha ni hicho mtoa mada alichosema kuwa haina madhara kwa binadamu kitu ambacho sio kweli ila sijabisha kuhusu kuua panya, nisome katikati ya mistari utaelewa.
 
Mimi alikaa kwenye sofa, anatoka usiku mchana anakausha unamsikia anavyohangaika.

Muda ukaenda akatanuka nakuongezeka size..... Kunasiku anatembea kwenye sofa namsikia anavyojipenyeza..... Aiseee nilipiga ngumi, vipepsi na mateke lile eneo alipo hadi akaanza kupiga ukunga....

Aisee nilitandika ngumi za maana hadi akatulia baada ya siku mbili nikaanza kusikia harufu ya mzoga nikajua tayari....
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji477][emoji477][emoji477][emoji477][emoji477][emoji477][emoji477][emoji477][emoji477][emoji477]
 
Asante kwa hii mbinu, nitajaribu kumtega kwa nyanya... ila kama ana watoto namwonea huruma!
Kuna vile visumu vinauzwa barabarani vina pakti la rangi ya kijani, kimoja buku

Njoo home kata nyanya vipande vinne nyunyizia halafu vipange kila pembe, siku hiyo utasikia kitu kinajirusha na kujipigiza chini[emoji1787][emoji28]Mi nimemuua mmoja mkubwa huyo last month

NB hakikisha hizo procedure unavyozifanya hakuoni, akikuona hali ng'oo
 
Back
Top Bottom