Sasa tatizo lipo wapi,naona kama Waislamu kuna mambo ambayo ni lazima yafuatwe na ili kuwakata makali wale wakaidi wanaokimbilia katika mahakama za serikali ili kukimbia mikono ya sheria za dini na haswa katika mambo ya kurithiana na kuowana ,talaka na engage inafaa kabisa kuwepo na mrengo ambao waislamu kwa baadhi ya mambo wangeweza kuruhusiwa kuyapeleka ndani ya mkondo wa sheria za dini yao,aidha kama itakuwa ngumu,labda kwa sababu binafsi za upande unaopinga,basi kungelianzishwa kitengo ambacho kingeruhusu kesi au madai yanayohusiana na waislamu yasikilizwe kwenye njia za Kiislamu ,na hii itapelekea zile kesi zinazozama zaidi katika mambo ya kiislamu ,mbona mabenki mengi siku hizi yanafuata muundo wa islamic bank tena huko huko maulaya kwenye wakirstu watupu walio wengi na hata wakiristo wamekuwa na afueni katika kukopa benki kwa kupitia njia hizo.Ni maamuzi tu na ubinadamu wa kuona wenzetu hawa jambo hili kwao ni muhimu.Na ndio watu wanavyoishi kindugu na mapenzi yanavyozidi baina yetu ,lakini sio kuekeana vigingi,maana kama walivyosema kuna uitalia kuna ukatoliki yote haya ni mariziano ya wananchi wenyewe kwani ukiangalia mambo hayo hayatakiwi kuwepo.Sasa ukianza kuona upande mmoja unalotaka kulifanya silo basi na wao watakuja juu na kukwambia basi na hili liondolewe.