*
> Waislamu wanazungumzia kusitishwa uhusiano ulio rasmi na Vatikano yaani Serikali kuwa na uhusiano wa kiBalozi! sasa munaposema Kama Serikali itasitisha uhusiano na Kanisa Katoliki basi haina budi kusitisha uhusiano na Serikali za Saudia, Iran au Sudan!!!! POINTLESS!!!!!*
>
> I have seen spin in my life, sir this one is up there!!
>
>
> ---Quote---
> Kama serikali ya Tanzania haifai kujiunga na OIC, bila ya kuitisha kura ya maoni, eti kwa sababu OIC ni taasisi ya kidini; basi lazima tukubali kuwa kwa hoja hiyohiyo, serikali hiyo ya Tanzania itakuwa imefanya kosa kuanzisha uhusiano, tena wa kibalozi, na Vatikano, ambayo ni taasisi ya kidini, na siyo nchi yenye raia! kama vile Saudia na Iran!!
> ---End Quote---
> Ukichunguza utaona kuwa VAtican ni nchi kamili ambayo ilipata uhuru wake kamili 1929 kwa mkataba wa Laterani kati ya Papa na Mfalme wa Italia. Ni nchi kamili inayochagua kiongozi wake, yenye serikali yake kamili, nembo yake, bendera yake, sarafu yake, posta yake na hata jeshi lake! Siyo TAASISI ya kidini. Kanisa Katoliki ni taasisi, lakini Vatikani ni nchi.
>
>
> ---Quote---
> Uhusiano huo wa serikali ya Tanzania na Vatikano, ingawa ni uhusiano baina ya nchi hii na Kanisa Katoliki duniani, lakini jambo la kustaajabisha hakuna yeyote anayehoji juu ya uhusiano huo, si serikali wala makanisa ya Kikristo! tena na nyinyi wana Forum munaendeleza wimbo uleule wa kudai Vatikano ni nchi Kamili! *tangu lini Taasisi ya kidini ikawa nchi ndani ya nchi*!
> ---End Quote---
> unaendelea kujizungusha wewe mwenyewe. Saudi Arabi ni nchi na ndani yake kuna miji mitakatifu ya Maka na Medina. Sisi tuna uhusiano wa Kibalozi na Saudi Arabia, je Serikali yetu ina uhusiano na dini ya Kiislamu? Vatikani ni nchi kamili na haiko ndani ya nchi nyingine!!!! ina mipaka yake inayotambulika kimataifa. Na ndiyo nchi ndogo zaidi duniani.
>
>
> ---Quote---
> Wakiristo wa TZ inawahusu nini kuanzishwa mahakama za Kadhi? pilipili ziko shamba zawawasha nini? kama Biblia haina sheria za kuhukumia waumini wake kwanini Waislamu wasiruhusiwe kutumia baadhi ya sheria za Kurani kama vile mirathi na ndoa?
> ---End Quote---
> Sasa kama haiwahusu kwanini wanaitaka CCM itimize Ilani wakati ndani ya CCM kuna Wakristu au utakuwa ni mjadala wa Wana CCM waislamu peke yao? Na kule Bungeni ambako wanataka sheria ipitishwe watakuwa na kikao cha Bunge la Waislamu watupu na Wakristu hawatatakiwa kuchangia? Kama kuna ndoa yenye kuhusisha wakristu au wakristu hawana haki zozote kwenye hiyo Mahakama ya Kadhi na kama hawana kwanini wakubali wake zao wafuate maamuzi ya mahakama hiyo? Kama hawataki wakristu watolee maoni wajianzishie na waendeshe wenyewe nadhani hakuna mtu atakayelalamika.
> ************
> Re: Serikali isitishe uhusiano na Vatican mara moja!!
>
http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=97066#post97066
> Posted by: YournameisMINE
> On: 9th November 2007 03:20 AM
>
> Hovyoooooooooo na tena bure kabisa........hao waislam na wakristo wanaopiga makelele yasiyo na msingi wote ni "extremists" hawana tofauti na bin Laden, Pat Robertson au Marhum Jerry Falwell. Ndugu zangu WaTz mnatakiwa kuya-reject mawazo kama hayo huko juu kwa hii thread kwani ni pungumfu mno na primitive kushinda hata amoeba, watu wanatakiwa ku-concentrate kwenye vitu vya maana, issues za maendeleo kwa taifa zima regardless na imani zao za kidini!!!!. Uislam na Ukristo kwanza zote ni dini za KIFISADI, kikoloni na kufikirika..............tupeni kwenye trash udini!!!! Atheist wa Kibongo, yes sir, I said so. Nasubiri kuvurumishiwa kashfa na kubezwa, msipoteza muda kwani yatakuwa makelele ya chura.
> ************
> Re: Serikali isitishe uhusiano na Vatican mara moja!!
>
http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=97081#post97081
> Posted by: Mzee Mwanakijiji
> On: 9th November 2007 06:23 AM
>
>
> ---Quote (Originally by YournameisMINE)---
> Hovyoooooooooo na tena bure kabisa........hao waislam na wakristo wanaopiga makelele yasiyo na msingi wote ni "extremists" hawana tofauti na bin Laden, Pat Robertson au Marhum Jerry Falwell. Ndugu zangu WaTz mnatakiwa kuya-reject mawazo kama hayo huko juu kwa hii thread kwani ni pungumfu mno na primitive kushinda hata amoeba, watu wanatakiwa ku-concentrate kwenye vitu vya maana, issues za maendeleo kwa taifa zima regardless na imani zao za kidini!!!!. Uislam na Ukristo kwanza zote ni dini za KIFISADI, kikoloni na kufikirika..............tupeni kwenye trash udini!!!! Atheist wa Kibongo, yes sir, I said so. Nasubiri kuvurumishiwa kashfa na kubezwa, msipoteza muda kwani yatakuwa makelele ya chura.
> ---End Quote---
> kwa mtu ambaye ni atheist kuingia kwenye thread ya mambo ya dini nadhani ndiyo kelele za chura. Ila kuwa atheist nayo ni imani na una haki nayo, sawa sawa kabisa na mtu ambaye anaamini kuwa mwezi umeundwa kwa jibini!
> ************
> Re: Serikali isitishe uhusiano na Vatican mara moja!!
>
http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=97088#post97088
> Posted by: YournameisMINE
> On: 9th November 2007 07:22 AM
>
>
> ---Quote (Originally by Mzee Mwanakijiji)---
> kwa mtu ambaye ni atheist kuingia kwenye thread ya mambo ya dini nadhani ndiyo kelele za chura. Ila kuwa atheist nayo ni imani na una haki nayo, sawa sawa kabisa na mtu ambaye anaamini kuwa mwezi umeundwa kwa jibini!
> ---End Quote---
> Muungwana sana MKJJ,
> Kama nilivyotegemea....yakuwa kwamba utakuwa najibu, unanifanya nakuwa disappointed kwani upo predictable kupita kiasi. Kuna siku ulisema kwa kudhani kwamba nipo naive, nadhani tume-trade hiyo kitu......kumbuka haya ni mapambano ya kifkra. (hint, achana na huo mchezo wa umesema/ulisema.....ungekuwa mtu aliyesoma MUCHS ungeelewa, hiyo inaitwa SUMU. Kwa bahati mbaya inaonekawa tayari ni victim). Issues za kidini ziacheni!!!!.
> ************
> Re: Serikali isitishe uhusiano na Vatican mara moja!!
>
http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=97092#post97092
> Posted by: YournameisMINE
> On: 9th November 2007 07:45 AM
>
> Politics za nani Mslam au Mkristu ndizo ambazo Nyerere alizikandamiza kwa nguvu zake zote. Ktk mambo machache ninayokubaliana naye hilo mojawapo......leo nimepata lunch hooters, muhudumu mmoja wapo ni demu mzuri wa Kimorocco(tokana na jina lake). Nikamuuliza kama yeye ni mslam, akasema ndio!! nikauliza kama ana-practice, akasema ndio tena hamsa salawat......basi moyoni nikasema alaaaa, kumbe tupo kwenye globalization, watu wanapeta tu. Sasa ninyi jibunguzieni possibilities tu na udini ulopitwa na wakati.
> ************
> Re: Serikali isitishe uhusiano na Vatican mara moja!!
>
http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=97098#post97098
> Posted by: kweku
> On: 9th November 2007 08:19 AM
>
> Eeeh hii kali. Inabidi Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa ki mataifa aanzishe darasa.
> ************
> Re: Serikali isitishe uhusiano na Vatican mara moja!!
>
http://www.jamboforums.com/showthread.php?p=97122#post97122
> Posted by: Si Kitiyi
> On: 9th November 2007 10:59 AM
>
>
> ---Quote (Originally by Kadogoo)---
> JMUSHI1, MC na wengine:
>
>
> Wakiristo wa TZ inawahusu nini kuanzishwa mahakama za Kadhi? pilipili ziko shamba zawawasha nini? kama Biblia haina sheria za kuhukumia waumini wake kwanini Waislamu wasiruhusiwe kutumia baadhi ya sheria za Kurani kama vile mirathi na ndoa?
>
> Tuache udini na tujibu hoja!
> ---End Quote---
>
> Inatuhusu kwa sababu mnataka kutumia pesa zetu za kodi kuendeshea mambo yenu ya kidini na vilevile tunaiheshimu katiba yetu ambayo hairuhusu ubaguzi wa kidini, rangi wala kabila.
>
> Jambo linalotia shaka, kwa nini mnadai Mahakama ya Kadhi itashughulika n a baadhi ya sheria za Quran kama ndoa na Mirathi; Kwa nini isiwe zote? Kutakuwa na manufaa na tofauti gani kutekeleza baadhi ya sheria zenu kwenye mahakama ya Kadhi na zingine kuziacha kwenye mfumo wa Mahakama zingine za Serikali? Kwa nini mnataka hivyo? Mimi sipati picha.
>
>
>Shukran za dhati ziende kwa Mwanakijiji kwa kumwelewesha
kadogoo.Kusemakweli kadogoo ni vigumu sana kuificha nia yako hapa
kwenye mijadala ya wazi,maelezo yako kwa asilimia flani yana kamantiki
flani lakini nia yako haiwezi kujificha!Mwanakijiji ameshakueleza
kuhusu Vatican,Iran,Saudi nk,so sio nia yangu kurudia tena,ila mimi
sikuwa upande wowote ule!ila sikufurahishwa na madai ya kuvunja
uhusiano na vatican kwa sababu huo ndio mwanzo wa migawanyiko na ndio
maana nikasema wakristo nao wanaweza kudai ufutwaji wa uhusiano na
nchi hizo amabazo ofcourse zinatumia quran kama katiba yao!Mambo ya
Bush,Mtikila,na porojo nyinginezo ulizozitaja ndio zimeonyesha wazi
kabisa kwamba umetoka nje ya mstari kwa kuhusisha kauli zangu na
misimamo ya kina Bush amabayo hata mimi mwenyewe
sikubaliani!umeshindwa kujificha hapo!umeshindwa kuonyesha
ukomomavu!Kama unataka kujua msimamo wangu basi ungesoma baadhi ya
maoni yangu ambayo nimeshawahi kuposti humu ndani ya forum.Nilishawahi
kusema kwamba Waarabu na Wazungu walituletea dini zao ambazo
zilitugawanya na bado zinaendelea kututenganisha na
kutupiganisha!Lakini kwasababu tayari tumeshaingia kwenye huo mhezo
mchafu,hatuna budi kujadili mambo kama hayo hata kama hatupendi.Mimi
sijali kama kutakuwepo na mahakama ya kadhi,ila je ni kweli kwamba
itatekelezwa?na je wananchi walishaulizwa maoni yao kabla ya
utekelezaji huo?je mambo kama haya ya kupigania ni utamaduni gani kati
ya huo wa mzungu na huo wa muarabu ni wa maana zaidi utatusaidia vipi
kutuletea umoja na maendeleo ya kweli?Ni lini tutapata muda wa
kujadili ni kwa namna gani tutaweza kuja pamoja na kuiletea nchi yetu
maendeleo ya kijamii na kiuchumi?Je tutafika?
>
>