Mkuu Waberoya tupo pamoja. Nadhani CCM ilipoingiza hoja hii kwenye ilani yao ya uchaguzi mwaka 2005 hawakuwa na nia ya kuianzisha hiyo mahakama ya kadhi bali janja ya kupata kura. Inasemekana kipengele hiki kiliingizwa kwenye ilani na Kingunge - hana dini na Mang'ula - mkristo. Kwa maneno mengine kiliingizwa na wanasiasa. Wanasiasa wakati wote first priority yao ni "votes". Ustawi wa taifa kwao ni second priority iwapo tu utaelekea kuwadanganya raia kuwachagua tena kuwa viongozi. Kwa kuingiza kipengele hiki kwenye ilani yao ya uchaguzi kwa uroho wa kupata kura, CCM hawakujua kuwa wanajipalia makaa. Sasa imefika wakati kuwa hata Waziri mkuu anapewa siku 14 na waislamu kufuta kauli ya serikali bungeni iliyotolewa na waziri wa katiba! hapa TULIPOFIKA NI HATARI. Kumbuka, waislamu ni sehemu tu ya watanzania, na kwa bahati mbaya mchango wao katika ustawi wa taifa kielimu na kiafya ni mdogo sana! Shule zao za sekondari (kama Waberoya alivyosema) zinazoongoza kwa kufanya vibaya (hata pamoja na kuzibadilisha jina eti nazo ziitwe seminari!! kumbe tatizo si jina!). Chuo chao kikuu walichopewa bure na serikali ya Mkapa (Majengo ya Tanesco Morogoro) wanashindwa kukifanya kitoe taaluma bora inayokusudiwa. Si siri kuwa hata lecturers wao wanawachukua tutors wa chuo cha ualimu kigurunyembe kinachotoa diploma na sasa wafundishe undergraduates!!!!. Sasa iwapo wakristu nao wakija juu na kuipa serikali ultimatum ya kufuta wazo la mahakama ya kazi la sivyo nao wafunga vyuo vyao vikuu ambavyo ni bora sana kama SAUT, BUCHS, MWENGE, RUCCO, TUMAINI, etc pamoja na hospitali zao bora sana (tena za rufaa!! zenye madawa na vifaa) kama BUGANDO, KCMC, na sekondari zao bora sana kama MARIAN GIRLS -Bagamoyo, ST. FRANCIS-Mbeya, KIFUNGILO-Lushoto nk, achilia mbali zahanati zao zilizotapakaa nchi nzima! Je serikali hii ya CCM bado itasimama! Si nchi nzima italipuka! Tafadhali CCM, msitupeleke kusiko kwa uroho wa "votes". Heshimu katiba ya nchi ambayo inasema wazi kabisa kuwa serikali haina dini bali raia wake wana dini. Waacheni raia wake wenyewe waanzishe mahakama yao ya kadhi (mradi hawapingani na katiba) kwa gharama za dini yao na wala si kwa kodi za raia ambao wengine si waislamu. Mambo yao ya ibada - kama wanavyodai juu ya mahakama ya kadhi - basi isiwe gharama kwa wengine wanadaiwa kuwa makafiri katika upeo wa dini yao. Nao waislamu wenyewe wang'amue ni kwanini ibada yao iwahusishe makafiri katika kuamua, kuanzisha na hatimaye kuigharamia!!!!! something must be wrong in their heads!