Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Wewe unapinga au unaunga mkono.
Waache waanzishe ni haki yao ya mshingi,
Wamesema ni mahakama ambayo wakristo hiwahusu kabisa.
Wakati wa ukoroni waingereza walianzisha hii mahakama sisi ndio tulioifunga bila sababu yoyote
 
Si kila kitu tulichoachiwa na waingereza kilikuwa kizuri. Tuliamua kuondoa elements za divide and rule sasa tumeanza kuzirudisha wenyewe. Ni vigumu kuamini kama hii inatokea Tanzania.
 
Mimi nawambieni kuwa hivi vyote ni kampeni tu, maana sidhani kama jambo hilo litatokea hapa Tanzania, Mkapa angekuwa bado rais angewapa Mahakama ya kadhi na sio Jk, Sidhani kama litakuja kufanikiwa waseme pia watu toka Serikani ni wakina nani wapo kwenye mchakato huo,
 
Mbona kuna ubalozi wa Vatican, si tumeurithi toka kwa wakoloni! Ni kwa maslahi ya nani? Kwani umeathiri uislam? Kama siyo, kwa nini Mahakama ya Kadhi iwe Nongwa? Huyo balozi anapowasilisha nyaraka ikulu, kiprotokali mantiki yake ni nini? uhusiano wa serikali na Ukristo au ni mkorogo gani huo? Waacheni na wenzenu wajinome kama nanyi mnavyoingia ikulu kuwasilisha nyaraka za Vatican!
 
Wewe unapinga au unaunga mkono.
Waache waanzishe ni haki yao ya mshingi,
Wamesema ni mahakama ambayo wakristo hiwahusu kabisa.
Wakati wa ukoroni waingereza walianzisha hii mahakama sisi ndio tulioifunga bila sababu yoyote

Tatizo ni jaribio la kuvunja Ibara ya 19 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kinachosema 'Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini atakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na UENDESHAJI wa jumuiya za dini zitakuwa NJE ya shughuli za mamlaka ya nchi'. Kwa kuwa viongozi wetu wanatafuta kujaza matumbo yao kupitia kura wameamua kufumba macho na kuamua kutangaza na kuendesha dini ili mradi tu wao wabaki madarakani tusubiri mgogoro mwingine wa Kikatiba na kidini ndipo watakapojua kilichokuwa kinaishikilia amani ya Tanzania. Wamesahau kwamba amani ya Tanzania imetengenezwa, sio ya kuzaliwa nayo! Niliwahi kumsikia mtu mmoja anayejiita 'Profesa' Lipumba akidai kwamba watanzania ni watu wa amani! Pimeni alama za nyakati viongozi wetu! Historia itawahukumu!
 
Tatizo ni jaribio la kuvunja Ibara ya 19 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kinachosema 'Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini atakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na UENDESHAJI wa jumuiya za dini zitakuwa NJE ya shughuli za mamlaka ya nchi'. Kwa kuwa viongozi wetu wanatafuta kujaza matumbo yao kupitia kura wameamua kufumba macho na kuamua kutangaza na kuendesha dini ili mradi tu wao wabaki madarakani tusubiri mgogoro mwingine wa Kikatiba na kidini ndipo watakapojua kilichokuwa kinaishikilia amani ya Tanzania. Wamesahau kwamba amani ya Tanzania imetengenezwa, sio ya kuzaliwa nayo! Niliwahi kumsikia mtu mmoja anayejiita 'Profesa' Lipumba akidai kwamba watanzania ni watu wa amani! Pimeni alama za nyakati viongozi wetu! Historia itawahukumu!

Lakini si ilisha semwa hii mahakama ni ibada? sasa inakuwaje mnaweka huku jamvi la siasa? ipelekeni sehemu za ibada tafadhali!
 
Mbona kuna ubalozi wa Vatican, si tumeurithi toka kwa wakoloni! Ni kwa maslahi ya nani? Kwani umeathiri uislam? Kama siyo, kwa nini Mahakama ya Kadhi iwe Nongwa? Huyo balozi anapowasilisha nyaraka ikulu, kiprotokali mantiki yake ni nini? uhusiano wa serikali na Ukristo au ni mkorogo gani huo? Waacheni na wenzenu wajinome kama nanyi mnavyoingia ikulu kuwasilisha nyaraka za Vatican!

Ubalozi wa Vatican hauendeshwi na Serikali yetu, pia Vatican ni serikali kama zilivyo Iran, nchi ya Kiislamu ambayo ina ubalozi Tanzania. Tofauti iliyopo na ubalozi ni kwamba Mahakama ya Kadhi ni ibada ya Waislamu, ambayo waislamu wanataka Serikali iwaendeshee! Hili linahitaji kwenda shule? Wanaogopa nini kuiendesha wenyewe kwa maslahi yao? Kwani uendeshaji wa misikiti na BAKWATA vinaendeshwa na nani?
 
Mbona kuna ubalozi wa Vatican, si tumeurithi toka kwa wakoloni! Ni kwa maslahi ya nani? Kwani umeathiri uislam? Kama siyo, kwa nini Mahakama ya Kadhi iwe Nongwa? Huyo balozi anapowasilisha nyaraka ikulu, kiprotokali mantiki yake ni nini? uhusiano wa serikali na Ukristo au ni mkorogo gani huo? Waacheni na wenzenu wajinome kama nanyi mnavyoingia ikulu kuwasilisha nyaraka za Vatican!


Mbona kuna ubalozi wa ilani? Ni kwa faida ya nani? Unalinganisha ubalozi wa Vatican na mahakama ya kadhi? Kama vipi urudi shule, na acha ushabiki wa kina shehe ponda!!
 
Ni kweli watu wanachanganya vatikani na mahakama ya kadhi. Kwa nini WAISLAMU MSIENDESHE HIYO MAHAKAMA MNATAKA SERIKALI, HAMNA UWEZO NINI?? Kaane pembeni msiharibu nchi yetu.
 
Kuundwa kwa kamati ya kushugulikia hili suala kutokana na agizo la WAZIRI MKUU ni dalili tosha ya Serikali kunyoosha mikono na kukubali. Kwa nini serikali yetu haina misimamo kwenye maamuzi?? Kodi iliondoa baada ya kupata shinikizo hili nalo vile vile. Kweli tuna viongozi hapa.

Tanzania kuundwa kwa kamati si jambo geni hata kidogo mara zote zimeundwa kamati na zikafa hadi sasa mie sishangai na hili .Kura zinatafutwa
 
Tatizo ni jaribio la kuvunja Ibara ya 19 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kinachosema 'Kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini atakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi, na shughuli na UENDESHAJI wa jumuiya za dini zitakuwa NJE ya shughuli za mamlaka ya nchi'. Kwa kuwa viongozi wetu wanatafuta kujaza matumbo yao kupitia kura wameamua kufumba macho na kuamua kutangaza na kuendesha dini ili mradi tu wao wabaki madarakani tusubiri mgogoro mwingine wa Kikatiba na kidini ndipo watakapojua kilichokuwa kinaishikilia amani ya Tanzania. Wamesahau kwamba amani ya Tanzania imetengenezwa, sio ya kuzaliwa nayo! Niliwahi kumsikia mtu mmoja anayejiita 'Profesa' Lipumba akidai kwamba watanzania ni watu wa amani! Pimeni alama za nyakati viongozi wetu! Historia itawahukumu!


Sidhani kama serikali inavunja katiba ikiruhusu nahakama ya Kadhi, na ata kama, Katiba inaweza kurekebishwa kupisha maendekeo au freedom ya wananchi

Hakuna evidence inayo onyesha mahakama ya kadhi itavunja amani iliopo Tanzania, sanasana, kuktaliwa mahakma ndio kutavunja amani.

Evidence za kutosha zinaonyesha Mahakama ya kadhi haijavunja amani popote, mfano, Zanzibari, Kenya, Uganda, UK nakadhalika, zipo mahakama na bado jamii zao zinaishi kwa amani
 
Nahisi hutuhitaji hii kamati. Kwani serekali imekataa mahakama ya kadhi kuanzishwa? La hasha. Tatizo lipo, serekali kushinikizwa kuanzisha mahakama (ibada) kwa ajili ya waislam. Suluhisho ni waislam kuanzisha hiyo mahakani yao kulingana na taratibu na mafundisho ya uislam, ilimradi haikwaruzani na sheria za nchi.
 
Sidhani kama serikali inavunja katiba ikiruhusu nahakama ya Kadhi, na ata kama, Katiba inaweza kurekebishwa kupisha maendekeo au freedom ya wananchi

Hakuna evidence inayo onyesha mahakama ya kadhi itavunja amani iliopo Tanzania, sanasana, kuktaliwa mahakma ndio kutavunja amani.

Evidence za kutosha zinaonyesha Mahakama ya kadhi haijavunja amani popote, mfano, Zanzibari, Kenya, Uganda, UK nakadhalika, zipo mahakama na bado jamii zao zinaishi kwa amani

so, kuna evidence inayoonyesha kuvunjika kwa amani baada ya kukataliwa mahakama ya kadhi?
 
Sidhani kama serikali inavunja katiba ikiruhusu nahakama ya Kadhi, na ata kama, Katiba inaweza kurekebishwa kupisha maendekeo au freedom ya wananchi

Maendeleo ya wananchi yanaweza kuwepo hata kama Mahakama hizo wataziendesha wanaohusika nazo. Si walisema JOHN hawezi kuhukumu kesi ya mwislamu? Kwa nini JOHN huyo huyo agharimie IBADA yenu? Kwani mkishughulikia mambo yenu wenyewe kuna ubaya gani? Freedom ya wananchi ni kufanya mambo yao wenyewe kulingana utaratibu na sio kuingiliwa na serikali. Hiyo Freedom unayoizungumzia ni ipi?

Hakuna evidence inayo onyesha mahakama ya kadhi itavunja amani iliopo Tanzania, sanasana, kuktaliwa mahakma ndio kutavunja amani.

Evidence: Mbona Mahakama za Kadhi hazikuwepo na amani ilikuwepo tena kuliko za jirani zetu popote na sasa hivi amani inazidi kutoweka taratibu anapoingia huyu shetani aitwaye Kadhi?

Evidence za kutosha zinaonyesha Mahakama ya kadhi haijavunja amani popote, mfano, Zanzibari, Kenya, Uganda, UK nakadhalika, zipo mahakama na bado jamii zao zinaishi kwa amani


Evidence: Umesahau Nigeria, Somalia. Halafu ukumbuke kuwa hakuna mtu anayekataa Mahakama za Kadhi, ila ni kwamba Waislamu wenyewe WAIGHARAMIE NA KUIENDESHA kwa kuwa ni IBADA yao.
 
Wewe unapinga au unaunga mkono.
Waache waanzishe ni haki yao ya mshingi,
Wamesema ni mahakama ambayo wakristo hiwahusu kabisa.
Wakati wa ukoroni waingereza walianzisha hii mahakama sisi ndio tulioifunga bila sababu yoyote


Sababu dhaifu sana,hatuwezi kufikia maamuzi kwa kuwa eti wakoloni walikuwa nayo.ni bora tujadili na maamuzi yatokane nasi na si reference zisizo na maana.
 
Tatizo kubwa la serikali yetu ni KUTOSHIRIKISHA WADAU kwenye masuala nyeti yanayoigusa jamii moja kwa moja au UBABE WA SERIKALI.
kwanini serikali ikurupuke kufuta kodi kabla haijatoa taarifa rasmi kwa wahusika na kukaa nao kuona labda kuna namna ya kufidia mapato yaliyopotea...ni aibu kukurupuka bila kuwa na msimamo na mwisho kushindwa kusimamia uwamuzi wako...
vilevile kwenye suala la mahakama ya Kadhi, serikali bila kushirikisha wahusika imekaa ikataka kufanya inavyotaka yenyewe, kwanini, hata kama ilitaka zile sheria ziwe ndani ya sheria za nchi ingeweza kuongea na wahusika na labda kungepatikana suluhu...hizi ni dalili mbaya sana za UONGOZI SERKALINI. they have failed, hiki kipindi cha JK kimekuwa kigumu sana nahizi hata yeye atakuwa amekata tamaa...inafika hatua sasa serikali inataka kulazimisha mambo..angalia bajeti zinavyolazimishwa vipite???
 
Mahakama ya kadhi itakuwa kwa manufaa ya waislam peke yao, kuanzia ajira kwenye vitengo vyake zitakuwa ni za 'kibaguzi' sababu itatakiwa mwajiriwa awe muislam,mahakama hiyo itagharamiwa na kodi ya watanzania wote bila kujali dini yake. hilo linatosha kabisa kwa mwenye kufikiri ajue kwamba kwa mazingira ya nchi yetu mahakama ya kadhi ni kuleta mkanganyiko usio na umuhimu. Tatizo kubwa ni kwamba uislam hauwezi kuishi katika mazingira yenye matabaka tofauti na waislam hawataki kuliona wala kulielewa hilo,mamepumbazwa na kuamini juu ya haki zao bila kuangalia wengine...
 
Mbona kuna ubalozi wa Vatican, si tumeurithi toka kwa wakoloni! Ni kwa maslahi ya nani? Kwani umeathiri uislam? Kama siyo, kwa nini Mahakama ya Kadhi iwe Nongwa? Huyo balozi anapowasilisha nyaraka ikulu, kiprotokali mantiki yake ni nini? uhusiano wa serikali na Ukristo au ni mkorogo gani huo? Waacheni na wenzenu wajinome kama nanyi mnavyoingia ikulu kuwasilisha nyaraka za Vatican!

Balozi wa vatican hanainfluence yoyote katika jamii na hatumii kodi za walalahoi wa tanzania. Kuna nchi hazina balozi nchini haziathiriki lolote kulinganisha na zile zilizonazo. Mahakama ya kadhi itakuwa moja kwa moja inagharamiwa na serikali na ikishatolewa watataka kuwe na makadhi wa mikoa na wilaya. Swali la kujiuliza ni je ni waislamu wote wanaitaka mahakama hii au ni propaganda ya kikundi cha watu kutaka ulaji? nimeshapata kuongea na waisilamu kadhaa wala hawana habari na mahakama hiyo na wala hawajui utendaji wake ukoje. Ukitaka ujue hoja ina nguvu kiasi gani tuendelee kuhamasisha kutopigia kura CCM then muone kwenye kura ndio nmtajua BAKWATA mko peke yenu na kikundi kidogo cha watu

Na waislamu hatuoni huu utakuwa mwanzo wa migongano zaidi katika dini pale wale wa imani kali watakapotaka kuwa na kadhi wao tofauti na wa BAKWATA?

TAKBIR!
 
Balozi wa vatican hanainfluence yoyote katika jamii na hatumii kodi za walalahoi wa tanzania. Kuna nchi hazina balozi nchini haziathiriki lolote kulinganisha na zile zilizonazo. Mahakama ya kadhi itakuwa moja kwa moja inagharamiwa na serikali na ikishatolewa watataka kuwe na makadhi wa mikoa na wilaya. Swali la kujiuliza ni je ni waislamu wote wanaitaka mahakama hii au ni propaganda ya kikundi cha watu kutaka ulaji? nimeshapata kuongea na waisilamu kadhaa wala hawana habari na mahakama hiyo na wala hawajui utendaji wake ukoje. Ukitaka ujue hoja ina nguvu kiasi gani tuendelee kuhamasisha kutopigia kura CCM then muone kwenye kura ndio nmtajua BAKWATA mko peke yenu na kikundi kidogo cha watu

Na waislamu hatuoni huu utakuwa mwanzo wa migongano zaidi katika dini pale wale wa imani kali watakapotaka kuwa na kadhi wao tofauti na wa BAKWATA?

TAKBIR!

Ndugu yangu tafakari,mbona balozi za jamhuri za kiislam zipo pia ...sioni uhusiano wa balozi wa vatican unaohudumiwa na vatican Kulinganishwa na mahakama ya kiislam itayohudumiwa na serikali...Tatizo kubwa penye mapenzi uwezo wa kufikiri hufishwa watu hufikiri zaini kwa moyo kuliko vichwa vyao.
 
Back
Top Bottom