The Khoisan
Platinum Member
- Jun 5, 2007
- 18,639
- 18,270
Mimi ni mkristo na niko bega kwa bega na waislamu wanaotaka mahakama yao, ila hiyo mahakama isigaramiwe chochote na serikali wala kingizwa kwenye katiba ya nchi na isivunje sheria za nchi kama ni hivyo ianzishwe haraka. Na iwe mahakama inayotatua matatizo yanayohusiana na Dini tu bila kupingana na sheria zilizopo za nchi.
Mimi ninavyoona hiyo mahakama itakuwa ya kusuluisha ndoa zilizofungwa kiislamu tu pamoja na ugomvi wa kwenye misikiti kama uliotokea Morogoro wa kugombea kumiliki msikiti wa Kilakala Bong'ola kati ya waislamu wenye msimamo mkali na waislamu wa kawaida.
Lakini ukianza kusema wanawake wasivae suruali na vimini na kuifanya ni sheria, au mwizi akatwe mkono au aliyezaa bila ndoa apigwe mawe hadi kufa hapo patakuwa hapatoshi. Mwanamke ndio anapigwa mawe mwanaume wala!!!
Kama wanataka mahakama ya kidini basi wafanye kwelikweli kama Mahakama za Nigeria hapo ndiyo nitaona waislamu wote wanaounga mkono wako serious. Kwa nini wachague kesi fulani fulani tu. Kama ni sharia na iwe sharia ila isituguse sisi tusio na dini halafu tuone kama watu hawatabadili majina.