Tumain
JF-Expert Member
- Jun 28, 2009
- 3,154
- 74
a) Argument zako zinaonyesha kama waislamu hawapiganii UFISADI au wananyamaza katika kulisemea hilo...sina uhakika na ukweli wake kila raia mwema nchini atafurahi kuona mafisadi wanashughulikiwa kisawasa mimi si msemaji wa bakwata lakini nadhani hawasupport mafisadi wote (weusi na weupe) bila kubagua hiyo ndiyo haki ya kweli!Ya mwanzo nimeshaandika vya kutosha na naona tutofautiane tu.
Nakuja kwenye suala la gharama:-
Ni rahisi sana kuandika kuwa ukianzisha hiki chombo basi kesi zitapungua. Ila unasahau kuwa tatizo ni PESA siku zote. Kama pesa ingelikuwepo basi kitivo cha sheria kingelipanuliwa, mahakimu wakasomeshwa wengi, mahakama zikajengwa..... naama jengo kubwa kuliko yote Tanzania linakuwa ni mahakama tu. Na haya yanakuwa kila mkoa. Huoni tatizo lingeliisha? Ila kumbuka Tanzania kwanza lazima wale mafisadi, lije jeshi likombe, Polisi, wizara ya afya, maji na umeme, wizara ya elimu, wanafunzi, nauli ya Muungwana kwenda nje, Washa, kongamano, ndege, shangingiS, misafara mikubwa ya Pinda na Muungwana na ................
Unafikiri hiyo pesa ya kuanza kulipia hao KADHI itatoka wapi?
Ndiyo maana Mwanakijiji akashangaa mwanzo kabisa kuwa wakati wengine tunalia na MAFISADI, wenzetu mwalilia KADHI. Haki ya nani, siku moja tukawaondoa MAFISADI na CCM yao, nione mtu anakuja kulialia hapa kuwa "ni sisi tulipigania uhuru..... sasa twadai pesa ya kadhi...." Tungeliungana Waislaam kwa Wakristo na kuwashughulikia MAFISADI na UCHUMI wa Tanzania ukisharudi mikononi mwetu, tukae chini tujadili juu ya hili maadamu pesa zipo, why not? So longer watu watapa ajirra.
b) Mahakama ya Kadhi huwezi kulinganisha na Ufisadi, in fact mtu yeyote anayemnyima mwenzake asipewe haki ya kuukumumiwa kwa haki kwa mujibu ya ibada yake amemnyima haki. kutokutoa haki ni UFISADI kwa MyK ni haki kwa waislamu tena ya iliyonyimwa miaka mingi 20+ ni ufisadi wa zaidi ya miaka 20 huu wa epa umeanza jana tu ndugu??
c) Issue ya gharama nafikiri tumeshakubaliana kwamba hata ingepanuliwa na mahakimu wakasomeshwa wakaongezeka lakini "BADO" waislamu watakuwa hawajapewa haki yao ya kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria zao..
d) MyK bila shaka ikianzishwa itapanuka, itahitaji pesa zaidi lakini ni swala la "pro-rata" kadiri inavyopanuka ndivyo inavyopunguza kesi kwenye mainstream kwahiyo itakuwa pesa zinatolewa kulingana na kesi unazoshughulika what is so difficult kuelewa hapo??