Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Jk hayuko tayari kuvunja katiba ya nchi kwa ajili ya kuwafavour waislamu wenzake. Serikali kulazimishwa kuunda mahakama ya kadhi ni kutowatendea haki wananchi wengine ambao si waislamu,umuhimu wa waislamu kuwa na mahakama yao hakuna anayepinga kinachopingwa ni kwa mahakama hiyo kuundwa kwa sheria za nchi wakati nchi yetu haina dini,sheria ni lazima iwe na saini ya president hivyo ndio kusema inakuwa ni sheria ya nchi,suala la kuwa mashehe au wahudumuaji mahakama hizo watagharimiwa na BAKWATA si hoja kwa kuwa hoja ya msingi ni mahakama hiyo kuwa kwenye sheria za nchi,gharama za serikali mfano kuchapisha muswada na hatimaye kuchapisha sheria zenyewe kwa ajili ya kusomwa na waislamu au wanasheria for that matter ni kodi za wananchi wote. Ni kweli kuwa waislamu hawawezi kuunda mahakama yao isiyokuwa na nguvu za kisheria ndio maana wanataka iwe sheria ya nchi,pamoja na kudai kuwa ni haki yao lakini haki gani ambayo haitambuliwi kisheria? kwani waislamu wamekatazwa kusali?Sheria tayari inatambua kuwepo kwa misikiti na makanisa pamoja na suala zima la uhuru wa kuabudu kwanini basi waislamu wasiendelee na uhuru wao huo ikiwa ni pamoja na kuunda mabaraza yao ya kutatua migogoro ambayo yataheshimiwa na waumini wote? Ingawa kuna barukta na Bakwata? misimamo inaweza tofautiana lakini hilo ni juu yao kwa nini serikali iwe moved kufanya kwa niaba ya dini fulani? Ni haibu kwa waislamu kutoelewa hilo


Kwahiyo unataka kusema nchi ambazo zinamahakama hii ya ki-islam kama vile kenya wananyanyasa raia wengine wasio kua waislam? nawakati wanaaihidi kuanzisha mahakama wakati wa uchaguzi, hawakuiona katiba ya nchi? Hebutoweni blabla zenu, wakati umefika we need changes
 
Hivi mie ngoja niulize swali wakristo peke yao ndio walipa kodi kwanza wafanyabiashara wengi tanzania ni waislamu na ndio walipa wakubwa kama hutaki kachukue daftari la walipa kodi wakubwa TRA ujiangalie mwenyewe. Kuanzia Bakhressa, Zakhem, Zakaria etc je nao hawa wakihoji kodi yao inaenda wapi tutaishi na tutafika. Pili kama kigezo ni kodi mbona kuna hospitali za missionary serikali inazisaidia kujenga tena wakitoa na mchango wao kwa kigezo eti zitasaidia watu swali laja je mahakama ya kadhi haitasaidia watu tanzania if not waislamu si watu katika jamii.

Acheni kuwa biased wachangiaji wa humu ndani ya forums kama mna chuki yenu dhidi ya uislamu semeni lakini hii kitu hailali tunaisubiria kwa hamu ikwame tuone kama hii nchi ya wakristo au yetu sote. Msidhani waislamu wa sasa hivi ni kama wale waliokuwa wakikaa madrasa tumesoma wote shule hizo hizo tujibiwe kwa hoja na uwazi wapi na wapi na sio eti walipa kodi wa kikiristo watachukia kodi zao zinazoenda katika mahakama ya kadhi kwani waislamu hawalipi kodi?????
 
Mimi dini yangu ni tofauti na ukristo wala uislam ni budha hivyo kuunda mahakama ya kadhi kwa kuwalipa pesa za taifa hili ni dhuluma kwa taifa hivyo . Mimi nasema kuwa Waislamu wana haki ya kuunda mahakama ya kadhi na pia waunde bila ya kushirikishwa serikali katika Jambo hili
 
Nadhani unajua Kenya, Uganda, UK nanchi nying kama hizi waislam wapepewa fursa kuanzisha Mahakama na serikali inalipia kulikoni Tanzania? hii isue imeshaelezwa kirefu tu, kinachotokea hapa niwakristo na serikali kuwafanya waislam kama second class citezen, we need changes, now is camming. kaa mkao wa kula.

Kwanini mahakama za Kiislamu ndo zilipiwe? mbona dini zingine wanazo mahakama zao na serikali haizilipii?

Sijawahi ona mtu anaye dai upendeleo uwe ni haki yake!
 
Maaskofu labda waanzishe chama chao. Kuanzisha mahakama ya kadhi na Tanzania kuingia OIC ni sera rasmi za CCM. Sasa mnapinga nini? Haya mambo yamo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM na lazima watekeleze ahadi zao. CCM wanaamini walipata kura kwa sababu ya sera hizo!! Sasa ukipinga, unamaana unawazuia CCM kutekeleza sera zao? think again. Hizi ni sera rasmi za chama tawala na hazina budi kutekelezwa!!
 
Wewe Bull usituletee mambo ya Uganda na Kenya. Hii ni Tanzania, na tumeshasema hatutaki suala la KADHI sio la serikali bali la BAKWATA. Period. Na hilo la Waislamu kufanywa kuwa second class citizens linatoka wapi Yarabi! Jiepushe na maneno ya uchochezi.
 
Mashekh kazeni buti, kazi rasmi ikianza tufahamisheni na wale vijana wetu kule Toraborapia wakotayari wanasubiri vianze, pia Sheik Bin yuko aware na hii stuation. Tunahitaji changes, walishatuburuza vyakutosha. Sheikh Simba (Bakwata) pia wamechoshwa na tabia inayoendelea hapa nchini.

Hii tena haiitaji fat'wa iko very clear, We are on our way.

Mmmmmmmmmmm!! Torabora, your "Child" training to kill fields!! Real satanic!! So your Sheikh also is involved? Will better inform FBI on this also!! I was wondering why Mr. Mkapa endorsed this Law "act"of terrorism; he knew in advance of our brothers who are trained to kill!!

But mind you; don't send children do that, try by yourself, they are painful!!
 
Hebutoweni blabla zenu, wakati umefika we need changes

Sasa ndugu yangu, mabadiliko tunayahitaji Tanzania au Waislamu? Mimi nadhani kuna mabadiliko ambayo tunayahitaji kama taifa na hayo yanatuhusu sote, ila yale ambayo yanahusu taasisi fulani mfano kanisa au islamu, basi yanazihusu hizo taasisi na wafuasi wake tu! Nadhani hapo ndipo inapokuwa vigumu wengi kukubaliana.
 
Maaskofu labda waanzishe chama chao. Kuanzisha mahakama ya kadhi na Tanzania kuingia OIC ni sera rasmi za CCM. Sasa mnapinga nini? Haya mambo yamo kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM na lazima watekeleze ahadi zao. CCM wanaamini walipata kura kwa sababu ya sera hizo!! Sasa ukipinga, unamaana unawazuia CCM kutekeleza sera zao? think again. Hizi ni sera rasmi za chama tawala na hazina budi kutekelezwa!!

Kipima pembe naona hapa hujapima vyema!
Kama sera ya chama ni kuuwa watu wote watakakamatwa kwa kosa la wizi, je ni haki kutekeleza hukumu ya aina hiyo kwa kigezo kuwa walipata fursa ya kuongoza? Ni muhimu sana kutekeleza ilani ya chama, lakini ni muhimu zaidi kuilinda na kuitetea katiba ya nchi!, sio rais wala kiongozi yeyote wa serikali anaeapa KUILINDA ILANI (shoping list) ya chama chake, ila ni KATIBA! Hapa ndipo ngoma ilipo.

Mimi nadhani hapa ndipo tunapopelekana pabaya Watanzania. Watu wamekuwa wakiweka kwenye ilani za uchaguzi mambo mengi ambayo utekelezaji wake ni mgumu. Mimi ninaziita ni ankara za kuwadanganya wananchi wawape kura! Nakumbuka hata Mkapa aliwahi kusema kuwa ilani zingine hazitekelezeki, na sio yeye tu, jiulize hata JK ametekeza ngapi? Mambo ya msingi hasa kama haya yanayohusu imani za watu yanatisha sana, na ni bora wanasiasa wakawa-wanayachukulia kwa umakini mkubwa, matokeo yake yanaweza kuwa mabaya kweli kweli!
 
Nadhani unajua Kenya, Uganda, UK nanchi nying kama hizi waislam wapepewa fursa kuanzisha Mahakama na serikali inalipia kulikoni Tanzania? hii isue imeshaelezwa kirefu tu, kinachotokea hapa niwakristo na serikali kuwafanya waislam kama second class citezen, we need changes, now is camming. kaa mkao wa kula.

serikali ya UK hailipi mahakama ya kadhi
haya ndio ya uk
The Islamic Sharia Council is listed as a charity but people seeking a divorce, or talaq, must fill in a form and pay a fee. For a man it is £100; for women, it is £250 because the imams say it takes more work to process a woman's application as her word has to be corroborated.
 
Nadhani unajua Kenya, Uganda, UK nanchi nying kama hizi waislam wapepewa fursa kuanzisha Mahakama na serikali inalipia kulikoni Tanzania? hii isue imeshaelezwa kirefu tu, kinachotokea hapa niwakristo na serikali kuwafanya waislam kama second class citezen, we need changes, now is camming. kaa mkao wa kula.
Katiba ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kuwa, serikali haina dini. Sijui kuhusu katiba za hizo nchi ulizozitaja zinasemaje kuhusu suala la dini na serikali. Ila katiba ya Tanzania inasema bayana kuwa haijihusishi na haiegemei kwenye dini yoyote...fullstop. Vinginevyo, ili kutokea mabadiliko yoyote kuhusu masuala yanayohusu dini, itabidi katiba ifanyiwe marekebisho!

Sijasikia hata siku moja Wakristo wakiomba wapewe mahakama zao. Sijasikia hata siku moja Wakristo wakidai haki tofauti. Kama Waislamu wanajiona kuwa wao ni second class citizens, waeleze kinaga ubaga kuwa ni katika maswala yepi ambapo wamefanywa kuwa hivyo, na kutokana na ushahidi utakaodhihirika hapo ndipo mtu anaweza kueleza dukuduku zake.

Lugha unayotumia ni ya vitisho mno. Hivi hayo unayoyafikiria yakiibuka utayaweza wewe au unasikia na kuangalia mambo kwenye TV?
 
Kweli kumbe dini mara nyingi hutumika kujenga chuki badala ya upendo, kwenye maswala ya dini hata asiyejua msikiti wala kanisa atajifanya kusimama ngangali kupiginia dini, waumini wengi wanafiki na viongozi wengi wa dini pia niwanafiki tu.....

Tanzania imetumia pesa nyingi kutetea ama kupagania haki za waganda, wa comoro, wamsumbiji, wa south, wakongo n.k, lakini hakuna wa kulalamikia fweza, kwetu ni sifa, sasa linapokuja suala la watanzania wenyewe, eti kwa sababu ya tofauti za dini, linakuwa gogoro...

Misamaha ya kodi kwenye tasisi za dini haina uwiano,wala quota, kwa hiyo dini ama madhahebu mengine yananufaika zaidi kwa kuingiza bidhaa zaidi ya wengine, sehemu ndogo ya misamaha hiyo hutumika kutoa huduma kwa jamii, lakini sehemu kubwa hutumika kuimarisha miundo mbinu ama biashara ya baadhi ya madhebu ama dini.....lakini tukiamua kubalance kila kitu , je tutafika?

Hapa sioni kama cost ya mahakama ya kadhi ni tatizo kwasababu hakuna hata ambaye ameshawahi uliza hata hizo extra cost za mahakama ya kadhi, SO tatizo hapa ni udini, na Tanzania uduni unakuwa, tena kwa kasi....

Viongozi wetu wa dini kwa unafiki wao wanaweza kufanya hata damu ikamwagika kwa suala dogo kama hilo...baada ya damu ndio sasa watajifanya kukaa mezani kutafuta suruhu.

Dini hizi kubwa mbili in one way or another zinatumia pesa wa walipa kodi, hata Rais au waziri mkuu anapokwenda kwenye shughuli za kidini kama vile kuchangisha fedha, kufungua shule au jengo la taasisi ya dini, atatumia hela za walipa kodi, itafikia wakati haya nayo yatakuwa mgogoro.

Viongozi wa dini wawe ndio mfano wa upenda na uvumilivu, siyo ukipigwa kofi la kushoto, wewe unachomoa kisu....naamini viongozi wengi wa dini ni watu wazima, matamshi yao lazima yawe ya busara, ukisha jenga chuki kwenye mioyo ya vijana you will never reverse it, wafanye mambo kwa kuangalia vizazi vijavyo, otherwise wao na osama kuna tofauti gani? Mungu awape hakima wazee wetu ili tupate muafaka.
 
Hili ni Suala la CCM na Serikali yake, To be honest man wakristo hawezi kukubali kwa kutoa pesa za wakipa Kodi kwenye Taasisi za dini nyingine
 
Hili ni Suala la CCM na Serikali yake, To be honest man wakristo hawezi kukubali kwa kutoa pesa za wakipa Kodi kwenye Taasisi za dini nyingine
Sio swala la Wakristo kukubali au kukataa. Hili ni swala la taifa ambalo linaendeshwa na katiba. Jambo la kufanya hapa ni kuweka mswada bubgeni, ujaliwe, kama ukipita utungiwe sheria kikatiba. Uendeshaji wa serikali unafuata taratibu maalumu zilizowekwa (katiba), na sio kundi la watu fulani kukataa au kukubali. Pale amabapo katiba itasema kuwepo kwa mahakama ya kadhi, ukatae usikatae itakuwepo. Jambo muhimu hapa ni kuweka kipengele hicho katika katiba.
 
Nchi inakwenda pabaya sasa, hivi hawa CCM walipoweka hili katika ilani yao ya uchaguzi hawakujua kama wngepingana na katiba ya nchi? Najua kwa wakati ule iliwasaidia kweli kwa sababu ya uchaguzi lakini wajitahidi wawe wanaona mbali basi!!madhara yake ndio haya sasa, MUNGU atusaidie watanzania.

Rabin

Mkuu tuna mangapi yanayokiuka katiba kwenye Ilani ya CCM. Kuna mangapi yanayofanywa na viongozi wetu yanayokiuka katiba. Chama kinayumba, na kitaendelea kuyumba kama juhudi za makusudi hazifanyika. Na kinaweza hata kuyumbisha nchi yetu. Miaka mitano hili lilikuwa linazungumzwa tu, lakini sasa inaonekana ni zaidi ya kulizungumza.
 
Tatizo kubwa ni kwamba Watanzania wengi hawaielewi katiba ya nchi yetu. Hata wale walioiandaa ilani ya uchaguzi mwaka 2005 hawakuwa wanaielewa sawasawa au walipuuzia tu kuisoma kwanza kabla ya kuipitisha hiyo ilani.

Mtazamo wangu ni kuwa hii yote inazidi kuonyesha jinsi ambavyo CCM imelewa madaraka kiasi kwamba hata kimefikia mahali ambapo ama kimeshindwa kuheshimu wananchi wake au kimeshindwa kufanya mambo kwa makini kwani jambo linalohusu Taifa zima siyo jambo la kufanya kimzaha mzaha au kibabe babe, "without been seriuos". Kimezoea kushinda kwa udanganyifu danganyifu kiasi sasa kinaanza kuumbuka.

Inashangaza kuona wapo wanaotishia wenzao hapa- torabora nk. Inaonyesha wazi kuwa hawajijui hata ni wananchi wa nchi gani. Tanzania kama nchi haina dini! Rudi nchini mkuu! uwasiliane na wazalendo wa bongo wakuelimishe.

Ukiona huelewi waombe wahenga wakusaidie ile risala ya Baba wa Taifa aliyofafanulia jambo hili. Na kwa taarifa yako aliwafafanulia Mashekhe halafu Maaskofu na kwa kumalizia kwa Taifa zima. Kwa taarifa yako pande zote zilimshangaa alipotamka mara ya kwanza kuwa Tanzania haina dini, Maaskofu wakasema "Yesu Wangu" Mashekhe wakatoa "Astakafur laah!" lakini baadaye ilielekweka. Sasa Mkuu ulikuwa wapi wakati huo? Ulikuwa hujatoka nini?? Bado hujachelewa ila utachelewa ikiwa hutapenda kujielimisha kuhusu katiba ya nchi yako, kama ni yako kweli lakini!
 
Back
Top Bottom