Mfano BOMBA SANA.
Tatizo si kuwa mtoto B hataki mtoto A anunuliwe shati.
Tatizo hapa ni kuwa pesa za kununulia shati la mtoto A lazima zitoke kwa baba, mtoto A na B. Pia baadaye sabuni za kufulia lazima zitoke kwa baba, mtoto A & B. Gharama za maji, umeme katika kufua na kunyoosha, lazima zitoke kwa baba, mtoto A & B.
Kama mtoto A anataka kununua shati, na yeye ni mtu wa makamu (naogopa kuandika mzima maana jando lilishafanya kazi yake) si aende tu Kariakoo au Posta akanunue hilo shati? Kuna mtu kamkataza?
Nauli ya kwenda na kurudi na ghalama ya kununua na kutunza, iwe kwake mtoto A. Kwani nyie watoto A hamna akili? Hamna mikono? Nyie ni viwete hadi kuwa mnasaidiwa kila siku na baba na mtoto B? Mbona usiku ukifika kwenye uwanja wa fundi seremala mwafaidi peke yenu na Abdallah bin Kichwa wazi wenu? Hapo hamjui baba au mtoto B.
Time is up. Kuweni na muache kulialia kama Wahindi kwenye film zao za Love in Goa au Kuchi kuchi hota hai.............