Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Kweli bwana namimi niliona hii isue na jamaa alikuwa anasisitiza kuwa kubwa ya walioamua ni uanzishwaji wa hii kitu. Sasa mimi sijaelewa vizuri hapa, hicho kikao mbona kinaonekana cha kimya kimya.... Anyways ngoja tusikie upande mwingine leo
 
Ni lazima kwanza ufahamu tofauti za mahakama na kazi zake, kisha jenga hoja inayohusiana. Mahakama ya kadhi inalenga ku settle tofauti baina ya waumini wa kiislaam, na Sharia law ni kwa ajili ya Utawala mzima hivyo haichagui mhusika na kwa kuelewa hivyo hawawezi kuomba ujinga huo..
Sheria za kadhi zinalenga waumini wa dini hiyo pekee na hawa wazee waislaam wameweka hoja hii kwa kupima uzito tofauti wa hoja hizi mbili kulingana na nchi yetu.
Inashangaza sana unapouliza swali kuhusu kukatwa mikono mwizi na stoning wakati ukijua wazi hutakubaliana na wazo hilo..Na kama wakiweka utasema sana kuhusu ubaya wa Uislaam hali wezi walikatwa mikono ma stoning zilifanyika toka wakati wa Nuhu..

Kukujenga kuhusu misingi ya post yangu ni hivi..Najadili misingi ya usilamu..hususan kuhusu SHARIA..sizungumzii wala kuongelea kuhusu application na interpretation..hizo nakuachie wewe maana we u msilamu na mimi hiyo hainihusu hata chembe. Kinachoni-bother hapa ni kwanini hatekelezi matakwa ya SHARIA? Kunani?

Kwa nini mnachagua tu zile sehemu rahisirahisi ? Kuhusu ndoa na mirathi? Why? Mnayafanyia kejeli maagizo ya mola wenu? Kama mtume Mwamedi aliamuru mama anayenyonyesha auliwe kwa kosa la uzinifu ni kipi leo kimebadilika mpaka hukumu ileile isitekelezwe kwa kosa lilelile? Kama mtume wa wasilamu aliamuru Mwivi akatwe mkono, mboni nyie hamuisimamii hiyo hukumu leo hii kwa kosa lilelile? Na wala hamuidai?Iweje leo 'wazee' wa kisilamu wawachagulie waja mambo ya kufanya? Lini wamepewa wahyi mpya? Taarifa tulizonazo ni kuwa Mwamedi ndiye mtume wa mwisho..hamna mjumbe mwingine baada yake?
 
ma lawayer waliosign mikataba ya kifisadi almost wote ni wakristo

waliofikishwa mahakamani kwa tuhuma za kifisadi almsot wote wakristo


make up our own conclusion

Naona sasa mkuu Game Theory, unakosa point na nidhamu kwenye kuheshimu dini za watu wengine, na hapa JF sio sehemu ya kudhalilisha dini nyingine. Hapa tunatoa arguments pekee. Tafadhali utashi wa mtu kwenye mambo anayoyafanya yasihusishwe na dini. Put respect before each other religion otherwise we can not tolerate this anymore.
 
naamini hiyo ni kamba,serikali haiwezi kuingilia uhuru wa dini hata siku moja maana katiba iko wazi ,kila dini iwe na mambo yake iyaendeshe kwa gharama zake.Vinginevyo patachimbika na kama hivyo itabidi wakristo nao waombe mahakama zao la sivyo wakatae kuiochagua ccm.Tuache ubabaishaji kwani waliotunga katiba na kuisimamia kwa dhati waliona mbali.
Tupeni habariza kweli jamani......
naamini nimesomeka......
Habari zinazoingia sasa hivi ni kuwa serikali imekubali kuanzishwa kwa mahakama za Kadhi na itazi gharamia
 
Naona sasa mkuu Game Theory, unakosa point na nidhamu kwenye kuheshimu dini za watu wengine, na hapa JF sio sehemu ya kudhalilisha dini nyingine. Hapa tunatoa arguments pekee. Tafadhali utashi wa mtu kwenye mambo anayoyafanya yasihusishwe na dini. Put respect before each other religion otherwise we can not tolerate this anymore.

Nitajie lawyer hata mmoja muislam aliyehusishwa na kesi za kifisadi

Kwani yule Mnkono ni Muislam?


hebu nipumzishe mie...mnataka sources from Masatu...vyenu mbona huwa hamtoi sources?

au ushasahau kuwa JF ni mabingwa wa exclusives?
 
Nitajie lawyer hata mmoja muislam aliyehusishwa na kesi za kifisadi

Kwani yule Mnkono ni Muislam?


hebu nipumzishe mie...mnataka sources from Masatu...vyenu mbona huwa hamtoi sources?

au ushasahau kuwa JF ni mabingwa wa exclusives?

Nadhani umeshajibiwa kuwa mambo ya wataaluma ndg zetu mliegemea kwenye madrasa..sasa huko taaluma za uanasheria, utabibu etc zitapatikana wapi?..teh teh teh..

Waambie jamaa zako nao wafute ujinga kwanza ili wakae karibu na 'jikoni'..
 
Chama tawala kazi yake ni kulinda maslahi ya chama, na pia kuhakikishia wananchi utawala bora. CCM haibagui wala haina hadaa ya dini yoyote katika nchi hii. Na ndio maana Serikali iliamua mahakama ya kadhi kutokuwa sehemu ya serkali ila iwe sehemu dini. Na kitendo cha baraza la viongozi wakuu wa dini kutokulitambua suala hili inaleta wasiwasi.
Kwa Mujibu huo inamaana serikali itakuwa inaongozwa kwa shinikizo na matakwa ya watu wachache na wala sio Maamuzi yake kama Serikali.

CCM Na Serikali Kwa Ujumla Ni lazima Tuwe na Msimamo ulio imara katika kushughulikia suala hili.
Thanks
 
Last edited:
Ummy Muya, Mwananchi, Julai 06, 2009.

MASHEIKH zaidi ya 400 jana walikutana kwenye Msikiti wa Mtoro wa jijini Dar es Salaam kuanza maombi maalum kwa siku arobaini mfululizo kumlilia Mungu ili atoe adhabu kwa wote walioshiriki kuwahadaa Waislamu.

Akisoma tamko mbele ya masheikh zaidi ya 400 waliowakilisha jumuiya mbalimbali za Kiislamu, Sheikh Mohamed Issa alisema Waislamu wamekerwa sana na kauli za viongozi wa serikali kuhusu kufuta hoja ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi, ikiwemo kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

"Kwa mujibu wa waziri mkuu, Mahakama ya Kadhi italeta kuvunjiku kwa amani, jambo ambalo si kweli kwa kuwa hakuna ushahidi wa kuvunjika kwa amani katika nchi tulizotaja na badala yake mahakama hizo zimeimarisha umoja, amani na upendo baina ya Waislamu na jamii nyingine," alisema.

"Natoa wito kwa Waislamu wote nchini kuondoa dhuluma hizo kwa mikono yetu wenyewe na njia moja wapo ni katika uchaguzi mkuu wa 2010 kwamba kura zetu zina thamani na ndio nguvu yetu dhidi ya dhuluma zinazofanywa na maadui wa Uislamu," alisema.


Sheikh Issa alisema kauli iliyotolewa bungeni na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe kuwa Waislamu ni wengi nchini Afrika ya Kusini ni uongo na ukweli ni kwamba kwa mujibu wa takwimu zilizofanywa mwaka 2007, Waislamu ni 772,678 kati ya watu 41,743,459. Alisema hiyo ni sawa na asilimia mbili.


Alisema waziri huyo ameacha kwa makusudi kutumia uzoefu wa nchi zinazofuata utawala wa sheria kama Tanzania na ambazo zina Mahakama za Kadhi na kutoa mfano Ethiopia ambayo alisema suala la Mahakama ya Kadhi lipo katika katiba ya mwaka 1994 kwa mfumo wa mahakama za mwanzo (Shariah) na mahakama za juu (Kadhi).

Wakati nchini Kenya mahakama ya kadhi iko katika kifungu cha 5 cha katiba ya mwanzo ya 1963 na ile ya 1967, nchini Uganda suala hilo limo kwenye katiba ya mwaka 1995 kifungu cha 129 na Gambia kifungu cha 120 (b). Alisema katika katiba ya Zanzibar ya 1997 suala hilo limo katika kifungu cha 100.

Sheikh Issa alisema kwa kuwa CCM imewahadaa Waislamu kwa kutumia ulaghai na ujanja wa maneno katika ilani yao ya uchaguzi ya 2005, wanalaani kitendo hicho.

Hata hivyo, kifungu namba 108 cha ilani ya CCM ya mwaka 2005 hakitoi ahadi ya kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi bali kinaeleza kuwa suala hilo litashughulikiwa na kutolewa ufumbuzi. Chikawe aliliambia Bunge kuwa serikali imeamua kuingiza baadhi ya sheria za Kiislamu kwenye sheria za nchi badala ya kuanzisha mahakama hiyo.

"Tunalaani ulaghai huu wa kisiasa wa CCM na tunaahidi kutolaghaiwa tena na tunadhamiria kuipa CCM adhabu inayostahili na wote wanaowafanyia Waislamu kejeli katika uchaguzi ujao 2010," alisema.

"Sababu tunayo, nia tunayo na uwezo wa kufanya tunao na siku zote Allah (SW) amewaahidi waumini ushindi," alisema.

Alisema kwa kuwa serikali ya CCM imeonyesha dharau kubwa kwa Waislamu watafanya maombi hayo maalum, yanayojulikana kama Qunut, katika misikiti yote nchini kumuomba Mungu awaadhibu wale wote waliofikia maamuzi ya kuzikijeli sheria zake kwa kutaka zichanganywe na kanuni za binadamu.

"Tunaitaka serikali ibadili msimamo wake haraka iwezekanavyo la sivyo tutaandaa maandamano ya amani nchini nzima kudai haki yetu na kwa kuanzia maandamano hayo ya tutafanya Ijumaa sambamba na kongamano kubwa litakalojumuisha misikiti, jumuiya na taasisi mbalimbali za kiislamu za Dar es Salaam na mikoa jirani," alisema.

Aliongeza kusema: "Kusudio la serikali kutumia sheria iitwayo 'Islamic law (restatement) Act 1964 (Re 2002) ambayo waziri anatakiwa kutangaza katika gazeti la serikali mara kwa mara, ni jaribio la ukarabati wa sheria za Allah (SW) jambo ambalo Uislamu na Waislamu hawakubaliani nalo kamwe."

haya ndio mambo ya uwafaya watu wajinga

sasa huyu waziri mzima wa katiba anaongopa mchana mchana...hivi kweli inahitaji shule kujua kama waislam in South Africa ni minority?

huyu MATHISA sijui MATAYO CHIKAWE alifikiri waislam hawajaenda shule au alifikiri kila mtu mjinga?

ngoja nitafute background yake huyu jamaa who knows usikute keshatoa kauli nyingi za kuongopa in the past maana kama anaongopa kwa hili lililowazi makes you wonder...
 
Nitajie lawyer hata mmoja muislam aliyehusishwa na kesi za kifisadi

Kwani yule Mnkono ni Muislam?


hebu nipumzishe mie...mnataka sources from Masatu...vyenu mbona huwa hamtoi sources?

au ushasahau kuwa JF ni mabingwa wa exclusives?

My point hizi, hakuna relationship kati ya lawyer kuwa mkristo na matendo yake na miiko ya au imani ya KIKRISTO yenyewe. Hakuna sehemu ya vitabu vya KIKRISTO palipoandikwa kuwa lawyer MKRISTO amtetee fisadi au kiongozi wa serikali au kampuni yeyote ile muumini wa dini ya KIKRISTO afanye ufisadi, hakuna, hakuna. Huu ni utashi na tabia ya mtu mwenyewe. Labda nikuulize na wewe kwenye hayo au haya matukio ya UGAIDI,amabapo wafanyaji au watuhumiwa wakubwa ni waislamu. Je waislamu wanaelekezwa kwenye imani yao kuwa wao ndio pekee wafanye vitendo vya kigaidi ikiwa ni pamoja na kujitoa mhanga kwenye hadhara ya watu na kuua mamia na maelfu ya watu. The point is tabia ya mtu au kikundi cha watu isiwekwe au ku-draw its legitimacy kwenye imani ya dini zao.
 
No two countries are the same. Sisi si Kenya, Ethiopia au Afrika ya Kusini. Si kila wafanyalo wao linatufaa sisi. Kwa mfano, Afrika ya Kusini ina lugha zaidi ya moja ya kitaifa. Sasa na sisi tuamue Kisukuma na Kichaga navyo viwe lugha za taifa? Afrika ya Kusini hawana Waziri Mkuu. Sasa na sisi tumfutilie mbali Mizengo Pinda? Kenya wana wagombea binafsi lakini sisi hatuna.


Kumwomba Mungu amwadhibu mwanadamu mwenzio ni inverse religion. Kumtakia mabaya mwezio ni kutompenda, na hicho ni kinyume cha sheria za Mungu! Sasa mkiombea Tanzania mabaya na ikapata mafuriko makubwa mtafurahi?

Kama mnaombea CCM mabaya mbona zaidi ya nusu ya CCM yenyewe ni Waislamu?


hilo la Waziri kuongopa na stats ziko wazi nalo vipi? tuliache on a side au?
 
kama ni kweli serikali imeridhia mahakama ya kadhi basi mwelekeo wa serikali yetu na watendaji wake sio mzuri
Serikari kama serikali ikiamua na kutangaza kitu ni vizuri ikawa na msimamamo kuhusu ilichokiamua.tumeona bungu likiondoa misaada ya kodi kwa mashirika ya dini,kelele zikapigwa na serikari ikasalimu amri na kurejesha misaada iyo.
Leo hii serikali inatangaza kuwa hapatakua na mahakama ya kadhi baada ya kelele inakubali,je tutafika wapi?
Kwa mtazamo wangu mimi,serikali isiwe inatangaza mambo bila kua na utafiti wa kina kama jambo ilo litakubalika kwenye jamii au la.Na ikitokea wameamua kutangaza basi wasimamie walichokitangaza kwani kwa mtindo huu serikali itakuja kua na wakati mgumu pale ikitangaza jambo la muhimu sana na wananchi wakalipinga kwani tumegundua kua watu wakipinga serikali inabadilika .ni hayo tu kwa leo.
 
Mimi nitawaomba hawa masheikh kuwa ktk hizo dua,ziwafikie mpaka hawa wa JF wanaoukejeli UISLAM..
 
Nadhani umeshajibiwa kuwa mambo ya wataaluma ndg zetu mliegemea kwenye madrasa..sasa huko taaluma za uanasheria, utabibu etc zitapatikana wapi?..teh teh teh..

Waambie jamaa zako nao wafute ujinga kwanza ili wakae karibu na 'jikoni'..

ili waibie taifa au vipi?
 
My point hizi, hakuna relationship kati ya lawyer kuwa mkristo na matendo yake na miiko ya au imani ya KIKRISTO yenyewe. Hakuna sehemu ya vitabu vya KIKRISTO palipoandikwa kuwa lawyer MKRISTO amtetee fisadi au kiongozi wa serikali au kampuni yeyote ile muumini wa dini ya KIKRISTO afanye ufisadi, hakuna, hakuna. Huu ni utashi na tabia ya mtu mwenyewe. Labda nikuulize na wewe kwenye hayo au haya matukio ya UGAIDI,amabapo wafanyaji au watuhumiwa wakubwa ni waislamu. Je waislamu wanaelekezwa kwenye imani yao kuwa wao ndio pekee wafanye vitendo vya kigaidi ikiwa ni pamoja na kujitoa mhanga kwenye hadhara ya watu na kuua mamia na maelfu ya watu. The point is tabia ya mtu au kikundi cha watu isiwekwe au ku-draw its legitimacy kwenye imani ya dini zao.


Yule advocate MKONO ni muislam?

jibu swali
 
kama ni kweli serikali imeridhia mahakama ya kadhi basi mwelekeo wa serikali yetu na watendaji wake sio mzuri
Serikari kama serikali ikiamua na kutangaza kitu ni vizuri ikawa na msimamamo kuhusu ilichokiamua.tumeona bungu likiondoa misaada ya kodi kwa mashirika ya dini,kelele zikapigwa na serikari ikasalimu amri na kurejesha misaada iyo.
Leo hii serikali inatangaza kuwa hapatakua na mahakama ya kadhi baada ya kelele inakubali,je tutafika wapi?
Kwa mtazamo wangu mimi,serikali isiwe inatangaza mambo bila kua na utafiti wa kina kama jambo ilo litakubalika kwenye jamii au la.Na ikitokea wameamua kutangaza basi wasimamie walichokitangaza kwani kwa mtindo huu serikali itakuja kua na wakati mgumu pale ikitangaza jambo la muhimu sana na wananchi wakalipinga kwani tumegundua kua watu wakipinga serikali inabadilika .ni hayo tu kwa leo.

Of course mwelekeo wa serikali utakuwa mbaya...kwa sababu kidogo walichokiomba waislam wamekipata sasa nyinyi hilo hamlipendi

Hivi waislam wanefanya MoU kama kanisa mngesemaje maana hili roho inataka kuwatoka!
 
kama ni kweli serikali imeridhia mahakama ya kadhi basi mwelekeo wa serikali yetu na watendaji wake sio mzuri
Serikari kama serikali ikiamua na kutangaza kitu ni vizuri ikawa na msimamamo kuhusu ilichokiamua.tumeona bungu likiondoa misaada ya kodi kwa mashirika ya dini,kelele zikapigwa na serikari ikasalimu amri na kurejesha misaada iyo.
Leo hii serikali inatangaza kuwa hapatakua na mahakama ya kadhi baada ya kelele inakubali,je tutafika wapi?
Kwa mtazamo wangu mimi,serikali isiwe inatangaza mambo bila kua na utafiti wa kina kama jambo ilo litakubalika kwenye jamii au la.Na ikitokea wameamua kutangaza basi wasimamie walichokitangaza kwani kwa mtindo huu serikali itakuja kua na wakati mgumu pale ikitangaza jambo la muhimu sana na wananchi wakalipinga kwani tumegundua kua watu wakipinga serikali inabadilika .ni hayo tu kwa leo.

Viongozi wetu wanakosa ile principle ya Machiavelli, that the prince once decide shouldn't hestate over his decision. Ila unajua tatizo ni nini, ni hii tabia ya kuambiwa kila kitu na wahisani ndio inayotutafuna, mwisho wa siku sis na serikali yetu tutakufa kwa cardiatic arrest
 
No two countries are the same. Sisi si Kenya, Ethiopia au Afrika ya Kusini. Si kila wafanyalo wao linatufaa sisi. Kwa mfano, Afrika ya Kusini ina lugha zaidi ya moja ya kitaifa. Sasa na sisi tuamue Kisukuma na Kichaga navyo viwe lugha za taifa? Afrika ya Kusini hawana Waziri Mkuu. Sasa na sisi tumfutilie mbali Mizengo Pinda? Kenya wana wagombea binafsi lakini sisi hatuna.


Kumwomba Mungu amwadhibu mwanadamu mwenzio ni inverse religion. Kumtakia mabaya mwezio ni kutompenda, na hicho ni kinyume cha sheria za Mungu! Sasa mkiombea Tanzania mabaya na ikapata mafuriko makubwa mtafurahi?

Kama mnaombea CCM mabaya mbona zaidi ya nusu ya CCM yenyewe ni Waislamu?
Wewe kama nani hasa useme kwamba mahakama halitufai? kama augustino mkatoliki au kama nani? ndugu
kenya, ethipia whetever? hakuna tofauti kwakuwa wote ni waislamu na sheria ya uislamu ni uniform accross the nations...kama wanaweza sisi tushindwe tuna nini?
 
Of course mwelekeo wa serikali utakuwa mbaya...kwa sababu kidogo walichokiomba waislam wamekipata sasa nyinyi hilo hamlipendi

Hivi waislam wanefanya MoU kama kanisa mngesemaje maana hili roho inataka kuwatoka!

Waislamu wangetoa MoU kama kanisa ingekuwa sawa tu, tatizo la waislamu wanashindwa kutetea hoja zao za msingi na kubaki kutumia nguvu kutetea imani yao. Imani inatetewa kwa hoja zenye mashiko, masuala ya kunyima kura 2010 sio point. Ilani ya CCM 2005 ilisema kuwa serikali ya CCM italishughulikia suala la MyK sio itaanzisha MyK. Leo hii watu wanalalama kuwa CCM ilihahidi kuanzisha, nani alisema hayo, kwahiyo ina maana waislamu waliichagua CCM 2005 ili waanzishiwe MyK pekee, haya mengine hayawahusu. Na sasa ndio nagundua kitu kumbe ndio maana hata kwenye vita ya ufisadi naona variations eeh!!
 
Dua ni utaratibu tuu nafikiri "actions baada ya dua will bring a real impact"
Ukweli ni kwamba mahakama itapatikana iwe leo, kesho au keshokutwa whoever is in govermenent whetever it takes..."No one can resist the power and will of Allah"
 
Hivi kwenye hili swala si linatakiwa kwnda kwenye katiba? Na mabadiliko ya katiba ni swala la wananchi wote? Sasa inakuwaje waziri mkuu anaweza kulitolea maamuzi kirahisi rahisi hivyo? au mimi ndo sielewi vizuri! Pse advise me.
 
Back
Top Bottom