Jana usiku (Tar.5 Julai) nilikuwa nikitazama TV, Channel 10, kipindi kinachoitwa Arrisaalah. Kabla ya mzungumzaji kuendelea na mada yake aliongea kwa kifupi kuhusu Mahakama ya Kadhi. Alisema ya kuwa kulikuwa na kikao kilishofanywa na Mhe. Pinda, Mhe. Chikawe, Mhe.Lukuvi na Wah. Masheikh zaidi ya 20. Matokeo ya kikao hicho ni kuwa Serikali imeridhia uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi.
Lakini, masuala vipi Mahakama hiyo itaendeshwa, na nani watakuwa Makadhi, na pia kuhusu malipo/mishahara kwa hao Makadhi bado haijaamuliwa. Haya yatatafutiwa ufumbuzi katika vikao vitakavyokuwa vikiendelea kufanyika kati ya Serikali na Kamati itakayoundwa na Mhe. Mufti. Ndio habari hiyo niliyoisikia.
Mimi binafsi, sioni haja ya kuwazuia waislamu wasifanye tendo la ibada, kwani itakuwa ni kuwaindilia katika uhuru wao wa dini. Lakini, Serikali ya Tanzania isijihusishe kwa lolote, kwani Serikali haina Dini. Mhe. Mufti aunde tu kamati yake, na waanze utekelezaji hakuna mtu wa kuwazuia watu katika ibada zao. Serikali isijihusishe na mambo haya, isiingilie kamati itakayoundwa, na pia kamati hiyo isiingilie Serikali, labda tu kama itaonekana kuna uvunjaji wa sheria fulani fulani za nchi.