X-PASTER,
Mkuu huwezi kushindana wala ku reason na watu walojaa hasira.. Haikusaidii kitu wala hutamsaidia kitu kwani kisha pigwa mhuri..
Kitu kikubwa wasichofahamu ni kwamba dini zote zilianza na mahakama ndogo za kadhi kusaidia jamii zilizopo kupata haki zao. Ni katika kuleta haki na usawa baina ya jamii ndipo watu walianza kujenga imani ya dini hizo ambazo leo hii ni tawala na wamejenga mfumo ambao tunautumia.
Tatizo letu wengi hatufahamu historia za dini zetu zaidi ya kusoma Biography ya mitume na jina kubwa la MUNGU, bila kuelewa kwamba moja ya mission kubwa ya dini ni kuongoza jumuiya hizo ktk misingi ya haki na ni hizi dini zilizoangusha falme kubwa kubwa..Haki ni part of Ibada hata ktk lugha ya UN ndioo maana tuna haki za wanawake , watoto na kadhalika.na haki hizi hazikpatikani chumbani ila mahakamani kwenye sheria.
Mahakama zipo kwa sababu kuna watu kama hawa wanaofikiria kwamba hukumu ni mbinguni tu, halafu utawasikia Mafisadi wanatakiwa kufungwa Jela, kwa nini tusiwaachie hadi mbinguni wakahukumiwe!