Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Wakatoliki wana mahakama zao zinazoshughulika mambo mbalimbali yakiwemo mambo ya ndoa katika majimbo yao. Uko hapo?

Nipo wapi? kwenye upotofu wako? HAPANA!

Mimi ni mkatoliki na nakuhakikishia kuwa hakuna mahakama..Mambo yote ya kisheria yanayowahusu waumini yanaamuliwa na dola ktk taratibu tulizokubaliana waTz wote. Hakuna popote utakaposikia kanisa limemlipisha mtu faini au kumtia mtu jela muumini awaye yote kuhusiana na kadhia za jinai au madai popote pale.

Sasa labda utuambie kama wewe Babuyao umeanzisha dhehebu jipya linaloitwa ukatoliki..ambalo lina mahakimu na kuhukumu watu.
 
Tatizo wengi hatuelewi kuwa hii ni sera rasmi ya CCM. Piga ua, mahakama ya kadhi itaingia kwa mtindo wowote ule. Hii ni sera ya chama tawala. Sera za chama chochote na jinsi kinavyopanga kuzitekeleza utaziona kwenye ilani yao ya uchaguzi. CCM wameshaiweka hii kitu kwenye ilani yao ya uchaguzi. Kelele zitapigwa, lakini hii ndi sera ya CCM lazima waitekeleze. Suala sasa ni dini zingine vile vile kupenyeza mambo yao kwenye vyama wanavyoamini vitawasaidia. Tume ya uchaguzi ilishindwa kukemea mambo haya. Sasa ikishakuwa sera rasmi ya CCM ni kuhakikisha waislam wanapata special treatment na CCM ndo chama tawala mtafanya nini?
 
Nafiiri Wadau wengi hapa hawajajua kinachoendelea.Sidhani kama waislam wanahitaji hiyo mahakama iwe inagharamiwa na Serikali,Wanachokitaka ni IDHINI kwamba ianzishwe au isianzishwe.Maana kama maswala ya mishahara mimi sioni kama hilo ni jambo kubwa litakalowashinda waislam.Kama kuna za wakatoliki,na hawalipwi na serikali basi kuna uwezekano wa kuwepo za kislam na zisilipwe na serikali.Jambo linalohitajika hapa ni je iundwe au isiunde?Huo ndiyo mjadala.Serikali ikubali kuanzishwa lakini ikatae kugharamia tuone kama waislam wataweza kuianzisha au la.


Ukishasema mahakama maana yake imeingia kwenye ule muhimili yaani Judicialy hivyo basi watakao kaa katika mahakama hizo wako kwenye utumishi wa umma hivyo wana haki ya kulipwa mishahara na serikali,iwapo tu wazee wa baraza ambao wanaalikwa kusaidia kesi za kislamu mahakamani wanalipwa iweje isiwe hivyo kwa mashehe? Mahakama ya kazi hata kama itaundwa kitakachofuatia ni kukataliwa na baadhi ya waislamu hasa ambao hawatambui BAKWATA,watataka kuwepo mahakama nyingine inayowahusu wao tu kutokana na msimamo wao.Kuwepo kwa mahakama ya kadhi kwenye nchi za kiislamu ni sawa kwa kuwa serikali zao zina dini,suala la kusema uingereza mbona ipo na south Afrika si hoja hata kidogo,kila nchi ina nama yake ya kuendesha mambo, nafikiri nchi yetu ni mfano wa kuigwa kwani nchi za kiislamu ukatiri uko mbele sana mtu kubadiri dini adhabu ni kuuawa je ikiundwa hiyo mahakama haitakuwa hivyo hivyo? suala la kusema sheria itashughulika na mirathi na mambo ya ndoa si kweli,kwani usishangae mtu akahukumiwa na jina humo ukiuliza unaambiwa hii ni mahakama ya kadhi inashughulika na sheria za kiislamu utajibu nini hapo?Chonde ndugu zangu waislamu tuendelee na ustaarabu huu huu ndio uliofanya mpaka sasa tuna amani nchini,waislamu wanaoa wakristu lakini hakuna tabu na wakristu wanaoa waislamu mambo yanakwenda(ingawa ndugu wa mwanamke wengine usoma hitma lakini ndoa zinadumu).
 
Kwani wakatoliki walipokuwa wanaanzisha mahakama zao waliomba kibali kutoka kwa serikali?? Hebu acheni hiyo bana. Waislamu wanasema mahakama zao ni sehemu ya ibada kwa Mungu. Ibada kwa Mungu inahitaji ruhusa kutoka kwa serikali? Si ni swala hiyo? Kwa nini katika kuswali kwao waombe ruhusa ya serikali? Mbona serikali ilishatoa uhuru kwa kuabudu miaka nenda-rudi. Waseme wanachokitafuta serikalini wote tukijue!

Wakuu labda niulize, waislamu wana kitu kinaitwa "talaka tatu/talaka rejea"
na wamekuwa wakifanya hivyo siku zote Je? huo utaratibu na mengineyo si ndio moja ya hizo sheria za kiislamu maana hakuna talaka tatu au talaka rejea kwa mkristo.Serikali imewahi kuwanyima huo uhuru wa kuzishughulikia hizo tataribu zao au hizo zinatafsiriwa kama mila za kiislamu na si sheria.
 
Wow...how me where i complained...come on now you can do better that this

The pragmatic one is as follows: Tanzania is home to at least 15m Muslims. Many of them choose to run their lives, like followers of other faiths, in accordance with religious law. They want to marry, divorce, lend, borrow and generally conduct their affairs in accordance with sharia. But there is no mechanism in British society for recognising in public law the decisions they have made in private.

Such mechanisms do exist for other religions. So fairness dictates that it should be technically easier for Muslims to get state recognition for their faith-based judicial rulings, as long as the choices sanctioned by sharia do not contravene the law of the land.


what's wrong with that?


Niliposoma maneno yako yalinikumbusha article niliisoma mwaka jana kwenye the Guardian. Inasema hivi:
The pragmatic one is as follows: Britain is home to at least 1.6m Muslims. Many of them choose to run their lives, like followers of other faiths, in accordance with religious law. They want to marry, divorce, lend, borrow and generally conduct their affairs in accordance with sharia. But there is no mechanism in British society for recognising in public law the decisions they have made in private.

Such mechanisms do exist for other religions. So fairness dictates that it should be technically easier for Muslims to get state recognition for their faith-based judicial rulings, as long as the choices sanctioned by sharia do not contravene the law of the land.

Nikaogopa kudhania kitu fulani.
 
Kumekuwa na upotoshwaji mkubwa sana wa dhana nzima ya mahakama ya kadhi. Watu wengi wamepotoshwa kuwa mahakama ya kadhi itakuwa ikihukumu criminal cases. Ukweli wa mambo ni kuwa itakuwa inajihusisha na civil cases pekee na katika civil cases hizo ni katika masuala ya ndoa (talaka) na mirathi pekee. Hivyo hakuna kumkata mtu mkono.

Zanzibar ni sehemu ya muungano wa Tanzania kuna mahakama ya kadhi, je katiba imevunjwa? Tanganyika ilikuwa na mahakama za kadhi na baadaye nyerere alizivunja, je nyerere alivunja katiba? Kenya na Uganda wana mahakama hizo, je kuna mtu kakatwa mkono?

Usitudanganye hii mahakama ya kadhi ni kiingilio cha kuifanya nchi kuwa ya kiislamu! Baada ya kufikia lengo hilo ndipo upigwaji mawe, ukataji mikono, uchapaji bakora, ugaidi, nk vitakavyoanza. Uislamu sio dini ngeni, usitupumbaze na maneno yako 'matamu'. Haijaandikwa kwenye Quran kwamba mwanamke atakayefumaniwa akifanya uzinzi apigwe mawe mpaka afe? Huko kufanya uzinzi sio swala linalohusu ndoa? Na hiyo adhabu sio kwa criminal offence? Suala linaweza kuwa civil katika dini ya kiislamu lakini likawa criminal kwa sheria za nchi! Kwa hiyo sio upotoshwaji kama wewe unavyotaka tuamini. Swali: kwa sasa mashekhe wakiletewa suala la talaka huwa hawaligusi kabisa kwa sababu hakuna mahakama za kadhi ili kufanya hiyo mnayoiita ibada? Kama waislamu hawapendi mambo yao yaingiliwe vipi wataishije na wenzao? Km Ijumaa ni siku ya kazi Tz na wao wanatakiwa waende kuswali. Kwa ujumla sioni kitakachowaridhisha waislamu zaidi ya watu wengine wakubali kila kitu wanachotaka wao! Hii mahakama ya kadhi ni stepping stone tu. Mimi siipingi lakini waislamu waiendeshe wenyewe kwa gharama zao. Si wamesema JOHN hawezi kuamua suala linalohusu waislamu? Mbona wanamhitaji JOHN huyo huyo kuwaamulia mambo yao Dodoma? Elewekeni pls!
 
Nipo wapi? kwenye upotofu wako? HAPANA!

Mimi ni mkatoliki na nakuhakikishia kuwa hakuna mahakama..Mambo yote ya kisheria yanayowahusu waumini yanaamuliwa na dola ktk taratibu tulizokubaliana waTz wote. Hakuna popote utakaposikia kanisa limemlipisha mtu faini au kumtia mtu jela muumini awaye yote kuhusiana na kadhia za jinai au madai popote pale.

Sasa labda utuambie kama wewe Babuyao umeanzisha dhehebu jipya linaloitwa ukatoliki..ambalo lina mahakimu na kuhukumu watu.

Tunapozungumzia mahakama haimaanishi siku zote kwamba kuna hakimu, polisi mwendesha mashtaka, nk. Wewe niambie, ikiwa Padre ameenda nje ya masharti ya upadre huwa haitwi na maaskofu kuonywa na ikishindikana huwa suala lake linafikishwa kwa Papa? Mara nyingi mkosaji anakaa peke yake katika eneo lake huko Rome kwa ajili ya kutafakari na kujutia makosa yake. Kwa upande wa waumini wengine huwa wakitenda dhambi huwa wanaitwa na chombo husika kuonywa. Adhabu nyingine inaweza ikawa ni kufungiwa kupokea komunyo kwa muda au milele. Kwa masuala ya ndoa nako kuna utaratibu wa kuyashughulikia kikanisa na kuna adhabu zake, japo sio kupiga mawe. Kwa hiyo mahakama ipo kwa mtindo huo, pole kama hujaiona. Mahakama yenyewe sio harsh ndio maana haionekani kama inastahili kuitwa hivyo.
 
Habari zinazoingia sasa hivi ni kuwa serikali imekubali kuanzishwa kwa mahakama za Kadhi na itazi gharamia
 
Last edited by a moderator:
Habari zinazoingia sasa hivi ni kuwa serikali imekubali kuanzishwa kwa mahakama za Kadhi na itazi gharamia

Hapo nilipokandamizia wino pananishangaza, kwani hoja ya ilikuwa ni gharama? CCM inadanganya tena kwa mara nyingine ipate kura! 2010 tutasikia mengi
Mkuu Masatu weka ushahidi wa habari ndio tuwaze zaidi
 
Habari zinazoingia sasa hivi ni kuwa serikali imekubali kuanzishwa kwa mahakama za Kadhi na itazi gharamia

We Masatu umeshahama Simba SC na kuanza andika habari ambazo hazina kichwa wala miguu!? Kama una hakika tupe source ya infor na siyo unaandika kama mafinyufinyu. Karibu kwetu Yanga Sc.
 
Confirmed...mwenye wivu ajinyonge

Source pls!

zimeingia kutoka wapi?!

Hapo nilipokandamizia wino pananishangaza, kwani hoja ya ilikuwa ni gharama? CCM inadanganya tena kwa mara nyingine ipate kura! 2010 tutasikia mengi
Mkuu Masatu weka ushahidi wa habari ndio tuwaze zaidi

chanzo tafadhali!

Nyama-lize the story plz

We Masatu umeshahama Simba SC na kuanza andika habari ambazo hazina kichwa wala miguu!? Kama una hakika tupe source ya infor na siyo unaandika kama mafinyufinyu. Karibu kwetu Yanga Sc.

Imekubali au vipi?? wewe umepata wapi habari hizi



Mwanzo mlidemand kuona MoU ya kanisa na serikali mkasema wee ohh uzushi ohhh uzandiki sasa kiko wapi!!

On a flipside kuna mu aliniambia kuwa waislam wasilalamike...wenzao Kanisa walikuwa sharp na wajanja sasa what waqislam wanachokifanya ni same thing...u sharp tuu kama watu wakanisa walivyofanya


We HUSTLE in different ways
 
Hiyo Nyama-lize ndio nini? Huyu Masatu atupatie data kamili ili tuchangie tafadhali!
Maana yake stori haijajitosheleza ipo mifupa mifupa (skeleton), hivyo inahitaji kuongezwa taarifa za ziada (nyama) au (nyama-lization).
 
Back
Top Bottom