Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Hivi ibada ya kiislamu haikamiliki mpaka unapoamua maamuzi ya Ndoa? hasa hasa mirathi? au ndio janja ya wachache katika juhudi za kuwakweza akina mama? Kwa ninavyo jua Suala kama hili linaweza kuamuliwa kwenye mahakama za kawaida kwa kufuata sheria hizo hizo za kiislamu, maana sheria zinazo tambulika ni za kimila ikiwa umeamua ndoa yako iamuliwe hivyo, au hizi zinazopitishwa na bunge au za dini, inategemeana na ulivyo andikisha utashi wako au kama hukuandikisha , basi mahakama itaangalia ulikuwa unaishi kufuatana na misingi ipi? kwa mfano kuna waislamu wengine kutokana na experience or exposure ya maisha ya sasa kesi zao wasingependa kuamuliwa kwa misingi hiyo je hao watawekwa upande gani? Aidha Mwanaume au awe Mke.
Maana siku hizi ndugu wamekaa mkao wa kula na si kusimamia Mirathi wala nini?
Naomba rafiki yangu Mkandara na GT naomba mnieleweshe hapa na hata mwana zuoni yoyote mwenye ilimu na mambo hayo ya kadhi.
 
Sikonge,
Hapana mkuu wangu sheria zilizopo ktk Uislaam ni nzuri sana ktk sehemu nyingi za mirathi isipokuwa hofu yangu ilikuwa WATU na MAZINGIRA.

Nashindwa kuelewa kama mahakama hiyo itaweza fanya kazi kwa Ufasaha kwa sababu nyingi za kimsingi.. Watoto wa haramu hata ktk Ukristu hawatambuliwi ktk mirathi na mara zote ktk korti zetu wamekuwa wakipuuzwa..
Lakini Will inakubalika ktk Uislaam.. na bila shaka itakubalika kote kwa Wakritu, Waislaam na Wasiokuwa na dini isipokuwa muda wote imekuwa haina uzito kutokana na kutokuwepo sheria za kiislaam ambazo wengi wetu wanafikiria ni mbaya, mbaya, mbaya, kutokana na jina hili la Uislaam..

Pengine hii itawawezesha watu kuwapa elimu ya kuandika WILL kitu ambacho nchi za Ulaya kwa kupitia ma lawyer wanasisitiza sana.. WILL inaweza kusaidia sana inapofikia maswala kama haya isipokuwa tu kutokana na wananchi wengi kutokuwa na Elimu uandikaji wa Will ni kitu cha mwisho. Nakumbuka wakati sisi tukiwa wadogo wazee wengi walitumia Usia wa mwisho wakiwa mahtuti kitamdani na ukachukuliwa kama ndio WILL lakini uatamaduni huo ulikwisha baada ya sisi kuchukua mkondo mwingine wa sheria kuzizika sheria na tamaduni zetu.. Usia unakubalika ktk Uislaam na hata jadi za makabila yetu, hivyo bado mtoto wa haramu anayo nafasi kubwa ya kupewa haki yake..
Kumbuka tu ktk Uislaam Haramu ni kile kitendo sii mtoto aliyezaliwa.. Hizi hadithi nyingine watu tunaongezea tu katika kuupaka Uislaam..

swala la kuandika will, sheria law inakubali mtu aandike will ya quarter or one third ya mali yake, na sio mali yake yote. kwa hiyo mtu awezi kuigawa mali yake anavyotaka kwenye will kwa kutumia sheria law

swala la watoto wa nje labda mahaka ya kadhi iamue na kusema kesi zote za namna hiyo zipelekwe serikalini lakini sioni jinsi gani mtoto wa nje atambulike wakati wa kugawa mali na wakati kidini hatambuliki
 
Sikonge,
Hapana mkuu wangu sheria zilizopo ktk Uislaam ni nzuri sana ktk sehemu nyingi za mirathi isipokuwa hofu yangu ilikuwa WATU na MAZINGIRA.

Nashindwa kuelewa kama mahakama hiyo itaweza fanya kazi kwa Ufasaha kwa sababu nyingi za kimsingi.. Watoto wa haramu hata ktk Ukristu hawatambuliwi ktk mirathi na mara zote ktk korti zetu wamekuwa wakipuuzwa..
Lakini Will inakubalika ktk Uislaam.. na bila shaka itakubalika kote kwa Wakritu, Waislaam na Wasiokuwa na dini isipokuwa muda wote imekuwa haina uzito kutokana na kutokuwepo sheria za kiislaam ambazo wengi wetu wanafikiria ni mbaya, mbaya, mbaya, kutokana na jina hili la Uislaam..

Pengine hii itawawezesha watu kuwapa elimu ya kuandika WILL kitu ambacho nchi za Ulaya kwa kupitia ma lawyer wanasisitiza sana.. WILL inaweza kusaidia sana inapofikia maswala kama haya isipokuwa tu kutokana na wananchi wengi kutokuwa na Elimu uandikaji wa Will ni kitu cha mwisho. Nakumbuka wakati sisi tukiwa wadogo wazee wengi walitumia Usia wa mwisho wakiwa mahtuti kitamdani na ukachukuliwa kama ndio WILL lakini uatamaduni huo ulikwisha baada ya sisi kuchukua mkondo mwingine wa sheria kuzizika sheria na tamaduni zetu.. Usia unakubalika ktk Uislaam na hata jadi za makabila yetu, hivyo bado mtoto wa haramu anayo nafasi kubwa ya kupewa haki yake..
Kumbuka tu ktk Uislaam Haramu ni kile kitendo sii mtoto aliyezaliwa.. Hizi hadithi nyingine watu tunaongezea tu katika kuupaka Uislaam..
Mkandara nashukuru kwa kutufunua kidogo katika hili, lakini katika uelewa wangu mdogo, nilielezwa mahali kwamba kwa usia wakiislamu huwezi toa zaidi ya mafungu matatu 1/3 kwa mtu moja, hivyo tuseme Mimi Baba na watoto 6, kwa sheria ya kiislamu naweza kumwachia kwa usia huyo mtoto moja 1/3 si zaidi ya hapo na mali nyingine itagawanywa kufuatana na Sheria za Kiislamu ambapo kama na watoto wengine wakiume watapewa fungu lao, Mke nae atapewa fungu lake na kama nina wazee pia nao watapewa fungu lao, sasa tatizo la kisiku hizi, kuna wajomba amboa wamekaa mkao wa kula na kuna Mke ambaye labda ataolewa tena au hatoolewa lakini ana nafasi ya kuangalia mali aliyo acha Mume wake, hapo sheria inakuwaje katika kumlinda huyu Mama au watoto?
Na ninashukuru kwamba wazazi wako walikuwa na uelewa wa kuacha wasia, na ndio maana nasema kuna wazee wengi tu wa-hekima lakini wanabezwa wakati mwingine kutokana na kukosa elimu ya shule za kizungu lakini hapa si maanishi wazee wako please tusije tkatoka kwenye mada.
Halafu kuna issue kama Marehemu Balozi Hassan Diria nasikia alikuwa na watoto wa kike tu, kwenye hali kama hiyo inakuwaje? au ndio Ami anachukua kwa misingi kwamba Atakuwa ameolewa na Mtoto wa Mjomba ili mali isiende mbali?
 
Mkandara,
Nakubaliana na wewe kwa mengi. Ila hili neno MTOTO HARAMU, limeletwa na watu wa dini gani? Kumbuka kuwa katika Ukristo kumeandikwa kwamba "huwezi kukiita haramu, kitu kilichoumbwa na Mungu......." Kwa hiyo kama kuna watu walisema juu ya hili basi si Wakristo....... Mie yangu macho nasubiri nione.

Ila jambo moja. Kwenye Mahakama za serikali, kama mtoto ni wako basi inabidi umgharanie. Mtu kama Omary Mahita (POLISI) kusema huyu mtoto si wangu ilikuwa upupu wa hali ya juu. Ilitakiwa apimwe DNA na kuanzia hapo huyo mtoto atambuliwe kuwa ni wake. Mtoto hama kama utakuwa ulirithi, basi sheria zichukue mkondo wake.
 
Semilong, Mkuu nimesema zipo taratibu za kiislaam zinazoweza kumpa haki mtoto huyo pamojapo na WILL.Halafu nimesema mtoto huyo tunayemwita wa haramu ni maneno ya kiswahili tu kwa sababu kisheria kitanda hjakizai haramu il;a haramu ni kitendo. Ukisha elewa hilo nadhani utaelewa uzito wa sheria za kiislaam inapofikia maswala ya Urithi.. Hata Usia tu unaweza kumpa mrithi mtu asokuwa na nasaba nawe.

Pia kumbuka nimesema huko nyuma kwamba sheria nyingi za Kiislaam zinatakiwa jumuiya inayofuata dini, watu wanaofuata mafundisho ya dini. Sasa unapokuja TZ ukaona jinsi tusivyokuwa na dini kama katiba inavyosema ndipo hoja ya watu na Mazingira inapoingia. Watu huzaa hovyo hovyo kinyume cha ustaarabu wa ndoa za dini na mila zetu. Mtu ana wake ishirini kidogo, vimada, wengine ndoa za Halmashauri, Kanisani na misikitini haya yote ni matatizo ktk sheria zetu iwe ya kiislaam au sheria law tunayotumia..

Hivyo kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi sidhani kama ni suluhisho isipokuwa suluhisho ni kuwawezesha waumini wa dini hii wapate settlement zinazolingana na mikataba ya ndoa wanayoingia..iwe ktk Primary korti au Mahakama ya kadhi.. tatizo langu kubwa ilikuwa fikra za kwamba mahakama ya kadhi ndio solution badala ya sheria za kiislaam kuwa sababu ya hoja za Waislaam. hapo ingetusaidia zaidi kujadili hizo sheria na settlements zake badala ya kujadili mahakama ya kadhi kama chombo cha waislaam.

Pengine hii mahakama itawasaidia sana watu kupunguza Ufuska wakawa hawana budi kufuata vitabu kwani sheria itachua mkondo wake, but I doubt kufanikiwa kutokana na ukweli (reality) ya maisha ya wahusika pande zote..
Sii rahisi ktk society ambayo tumechukulia Nchi yetu haina dini kama vile sisi sii waumini wa dini yoyote hivyo kila mtu anaweza kupuyanga atakavyo..
 
Mkandara
naomba tuelimishane taratibu ktk hizi sharia maana ndiko tunaiingia tuwe na uelewa nazo .
1. mimi mtoto wbaba ni sheikh lakini mie nimebadirisha dini na kuwa mkristu sharia inasema nini kuhusu hatima yangu ktk urithi.?

2.Mimi baba nina fedha za kutosha nimefikisha miaka 65 hivi naamuwa kubadili dini nakuwa mkristu wkati watoto wangu wote ni masheikh, sharia inasema nini ktk hilo.?

3.Mimi ni shiekh ila kutokana nina matatizo ya kindoa na mke wangu naamuwa kuukana uislamu , hapa sharia inasema nini?
 
Mkandara,
Mahakama ya kadhi siyo kwamba ndiyo solution of every muslim problem, hata hivyo kuna society gani ambayo haina problem, naona mimi ni-sucesss then tuendelea kuisaidia iwasaidie wahusika
 
Mwana Kijiji,
Ukiwa German, unauliza wewe ni dini gani na ukishasema dini basi unakatwa hela kila mwezi kwa ajili ya kugharamia misikiti/kanisa/sinagogi tempo nk nk. Naungana na hili kwamba, Waislam waanzishiwe kodi yao maalumu na pesa wapewe viongozi wao ili kugharamia dini yao. Na hili liwe LAZIMA kwa Waislam wote. Asiyetaka basi atangaze kabisa yeye SI MUISLAAM. Mtoto akililia wembe...... Ila mie kodi yangu kulipia kadhi wala kanisa sitaki. Ntatoa tu pale ninataka na si lazima. Ikibidi basi ntatangaza kuwa SINA DINI..................

Kwani wao wanataka kukata kutoka kwenye ushuru wa mama anayeuza SUPU Ya Lonando?? sijaelewa hapo kidogo

Mkama,
Kwani serikali huko haikusanyi hela? Wananifurahisha Watanzania wanaojifanya HAWATAKI MASHOGA, ila hela za kodi kutoka UK zikija kuleta misaada wanapokea kwa shangwe huku wakiwa wamesahau kuwa UK inatoza ushuru hadi Madangulo (Manchestar Street), mashoga kama akina Elton John, George Michael nk. Mwapokea misaada kutoka kwa Waanglican. Mahakimu watapokea tu hizo hela bila kuuliza zimetoka wapi. Kupokea hela ya serikali mara nyingi ni kupokea hela baadhi yake zikiwa chafu. Heheeeeee hadi hela za kodi ya condom......

Wewe unafikiri kwamba kama vile waislamu hawataki kutoa kugharamikia dini ...hypothesisi yako ni "wrong" ni nguzo kufanya hivyo katika uislamu,
Lakini pesa za serikali (ambazo waislamu) wanachangia zisitumike kwaupendeleo kama kwenye MuO ya hila... kama haki bin haki mbona hatuna ugomvi na wakristo...
Maaskofu wenu wanakufanyeni tugombane wala christians have no problem "fedha mwanaharamu na maaskofu huyo ni mungu wao"

Tumain, soma ujumbe wangu hapo juu na nimeweka kwa maandishi mekundu na Blue. I don't give f.... iwe Kanisa au Msikiti. Wote hawa nawaita WALA VYA BURE. Ntatoa hela yangu kwao pale tu ninapotaka na si mtu mwingine aje achukue hela yangu na kuipeleka sehemu za ajabu ajabu. Ni sawa na tunavyolaani matumizi mabaya ya fedha za umma na viongozi wetu..... Hivyo kijana kabla hujaanza kujibu watu, soma kwanza misimimamo yao ujuwe wako upande gani na si kurukukia matrain yao ya umeme kwa mbele.......
 
Na Geofrey Nyang'oro

HAKUNA shaka kwamba utawala wa Rais Jakaya Kikwete sasa uko katika majaribu kutokana na mvutano uliopo baina ya taasisi kubwa mbili za dini, huku kila moja ikivutia kwake katika suala la uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi Tanzania bara.

Wakati Waislamu wakiwa wameweka msimamo wao wa kushinikiza suala hilo, Wakatoliki wamependekeza kinyume chake katika ilani yao ya uchaguzi iliyotolewa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) kwa kushirikiana na chama cha wasomi wa kanisa hilo (CPT).

Katika ilani hiyo iliyotolewa na idara ya Kichungaji, Tume ya Haki na Amani-TEC na kubatizwa kama 'Mapendekezo ya vipaumbele vya kitaifa', wameeleza kuwa wangependa katiba ya nchi iheshimu kanuni ya kuwa serikali haina dini na kutoruhusu taasisi za kidini kama vile Mahakama ya Kadhi na Uanachama wa OIC kuwa sehemu ya mfumo wa nchi.

Hoja za pande hizo mbili zinamweka kati Rais Kikwete na kumfanya akune kichwa kutoa maamuzi ya busara ambayo yataungwa mkono na pande zote.

Hali hii imekuwa tete zaidi baada ya serikali kupitia Wizara ya Sheria na Katiba kuanika bungeni mpango wake wa kutoanzisha mahakama hiyo inayodaiwa kuahidiwa kwenye ilani ya CCM mwaka 2005, badala yake ikataka kuhuisha sheria za kiislamu katika sheria za nchi kama inavyofanyika Afrika Kusini.

Lakini Waislamu ambao tayari wamekwenda mbali zaidi na kutishia kuinyima kura CCM katika uchaguzi mkuu ujao endapo mahakama hiyo haitaanzishwa bara, wanapinga kufuatwa mfano wa Afrika Kusini, badala yake wanataka ufuatwe mfano wa nchi za Kenya, Uganda na Zanzibar zilizopo Afrika Mashariki ambazo zina mahakama ya kadhi.

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba amesema kuwa Waislamu hawana sababu ya kukinyima kura chama hicho kwa kuwa kimeshatimiza ahadi yake inayodaiwa kuchangia Rais Kikwete kupata ushindi wa kishindo mwaka 2005.

Katika ahadi hiyo iliyopo kwenye ibara ya 108 (b), CCM ilipanga "Kulipatia ufumbuzi suala la kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi Tanzania bara", hatua ambayo Makamba anasema wameifikia, lakini Waislamu kupitia Baraza lao Kuu (Bakwata) na taasisi nyingine za dini hiyo bado wananung'unika.

Watu mbalimbali waliozungumza na gazeti hili na wengine kukaririwa na vyombo vingine vya habari nchini, wameonekana kwamba kila kundi linavutia kwake, Waislamu wanataka ofisi hiyo huku Wakristo wakiwa hawaoni umuhimu wake, hatua ambayo imelalamikiwa kuwa inahatarisha amani ya nchi.

Mkuu wa zamani wa Majeshi, Jenerali Robert Mboma amekaririwa na gazeti moja akionya hali hiyo na kushauri serikali kuwaruhusu Waislamu kuanzisha mahakama hiyo, na kujiwekea utaratibu wa namna ya kumlipa kadhi wa mahakama hiyo.

Mboma alifafanua kuwa kulihusisha bunge katika suala hilo ufumbuzi hautapatikana, kwani kila kundi litakuwa linavutia kwake, na kwamba kama mahakama hiyo itakuwa inajitegemea Wakristo wakizidi kulalamika watakuwa wendawazimu.

Mvutano huo umeibuka katika kipindi ambacho TEC kwa upande wake inasambaza Mpango wa Kichungaji Kuhamasisha Jamii kuelekea Uchaguzi wenye ilani inayoeleza vipaumbele vya kitaifa na mada za kuongoza maandalizi ya uchaguzi ujao, likiwamo suala la Mahakama ya Kadhi na Tanzania kujiunga na OIC na jinsi ya kupata kiongozi mwadilifu anayejali matatizo ya wananchi.

"Kiongozi, huduma kwa umma ni dhima muhimu kwa jamii yeyote ya wanadamu, ndio maana lazima pawepo uangalifu mkubwa kwa jamii yoyote katika njia na namna inavyochagua viongozi wake na namna inavyoweka taratibu za kusimamia na kudhibiti mienendo ya viongozi wao," inasomeka sehemu ya ilani hiyo.

Ilani hiyo inasisitiza kuwa mamlaka iliyopo mikononi mwa wanadamu inahitaji uangalifu ili pasiwe na madaraka yanayoegemea upande mmoja, yawe na uwiano na yasitumike vibaya na hata kuwa na rushwa.

Wakatoliki katika ilani yao wamezungumzia umuhimu wa kufanyika kwa mapitio ya mamlaka ya rais katika kuwateua mawaziri na idadi yao; pia uwezo na uhuru wa bodi za usimamizi wa mashirika ya huduma za umma na kuwaondoa wale wote wanaothibitika kutumia vibaya nafasi zao.

Pia wamekosoa sera ya uchumi ya sasa ambayo imeelezwa kuwa imelalia upande mmoja wa kuangalia matajiri na ikiacha maskini katika mazingira magumu.

Padri Baptist Mapunda amelieleza Mwananchi Jumapili kuwa ilani hiyo imelenga kukuza uelewa wa elimu ya uraia kwa Watanzania, kwa kuwa wengi wao hawajui maana ya demokrasia.

Alisema wamependekeza iundwe Tume Huru ya Uchaguzi ili kusaidia kuwepo kwa uchaguzi huru na wa haki kwa kuwa haiwezekani tume ikaundwa na kiongozi wa CCM halafu ikatoa maamuzi yasiyopendelea upande wowote.

"Tume yetu huru tunayopendekeza ivihusishe vyama vyote vya siasa hapa nchini,wanazuoni kutoka vyuo mbalimbali na hilo ndilo litakalowezesha Watanzania kuingia kwenye demokrasia ya kweli," alisema.

Padri Mapunda alisema mabadiliko ya katiba na Tume ya Uchaguzi hapa nchini ni muhimu katika kuleta demokrasia ya kweli.

Alisema ilani hiyo inapaswa kuibua mijadala miongoni mwa wananchi, kuhoji na kujua maana ya uraia na mapendekezo ya Tume ya aliyekuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, marehemu Francis Nyalali.

Kwa mujibu wa Mapunda serikali imelifumbia macho pendekezo la Jaji Nyalali kuhusu mabadiliko ya katiba.

Jambo jingine linalozungumziwa kwenye ilani hiyo ni upendeleo katika kuwaletea wananchi maendeleo, hali ambayo inaathiri mahusiano mema ya kibiashara na kikazi.

Pia wanadai wamebaini udhaifu mkubwa katika mfumo wa mahakama, na kuitaka serikali kuboresha mazingira ya mahakama ili kuzifanya ziweze kufanya kazi zake kutoa haki bila ya kuingiliwa.

Viongozi hao wa dini na wataalamu wao mbalimbali, wamekemea mchezo mchafu katika utoaji haki kama vile nyaraka muhimu kunyofolewa kwenye mafaili ya kesi na kuathiri mwenendo wake.

Wakizungumzia ufisadi, wameitaka serikali iongeze uwazi katika kuingia mikataba mikubwa, kwa kuwa si vyema mikataba hiyo kuendelea kuwa siri wakati inahusu Watanzania wote.

Vile vile wameonyesha kuchukizwa kwao na kasi ndogo ya kuchukua hatua na kutolea mfano wa kashfa za Buzwagi, EPA na Richmond, ambazo licha ya mapendekezo ya hatua za kuchukua mara moja, serikali ilitumia kanuni zuizi za bunge kudhibiti hali isichafuke zaidi.


Source: Mwananchi.

Nakubaliana na Mboma. Kama mahakama ya kadhi itaji tegemea na si sheria hizo kuingizwa kwenye katiba ya nchi then by all means they should go ahead. Cha muhimu ni ijitegemee na iwa affect wenye imani yao tu. Ila kama serikali itaamua kuingiza sheria hizi kwenye katiba basi hapo kutahitajika debate zaidi kujua namna itakavyo fanya kazi.
 
Tumain,
Mkuu sijakuelewa! nani kasema ndio solution..

MkamaP,
Vitu vyote ulivyoandika vimelenga kwamba wewe sii Muislaam sasa iweje utake settlement ifanyike na mahakama ya kadhi?

Nijuavyo mimi kutokana na elimu yangu ndogo, Mzazi (huyo mwenye mali na tuseme marehemu)ndiye mwenye amri ya nani apewe urithi kwa sababu alizichuma yeye na mkewe...hakuna mtu mwenye haki ya mali ile iwe serikali au mtu binafsi kutoa maamuzi ya mali ya mtu alochuma kwa jasho lake.
Hivyo unaweza kuwa mtoto wa kwanza ukaondoka mtupu ukiwa Muislaam au Mkristu na mtoto asiyefuata dini kabisa akaondoka na kisu kikubwa.. Settlement za kiislaam hazifuati kuchunguza dini ya wahusika (warithi) kutoa suluhu isipokuwa haki ya mhusika..Kuna vipengele vingi ambavyo mimi sina elimu navyo lakini anchofahamu utaratibu mzima haufuati dini za warithi bali Usia (Will) wa marehemu kutanguklia haki nyinginezo..
 
Tumain,
Mkuu sijakuelewa! nani kasema ndio solution..

MkamaP,
Vitu vyote ulivyoandika vimelenga kwamba wewe sii Muislaam sasa iweje utake settlement ifanyike na mahakama ya kadhi?

Nijuavyo mimi kutokana na elimu yangu ndogo, Mzazi (huyo mwenye mali na tuseme marehemu)ndiye mwenye amri ya nani apewe urithi kwa sababu alizichuma yeye na mkewe...hakuna mtu mwenye haki ya mali ile iwe serikali au mtu binafsi kutoa maamuzi ya mali ya mtu alochuma kwa jasho lake.
Hivyo unaweza kuwa mtoto wa kwanza ukaondoka mtupu ukiwa Muislaam au Mkristu na mtoto asiyefuata dini kabisa akaondoka na kisu kikubwa.. Settlement za kiislaam hazifuati kuchunguza dini ya wahusika (warithi) kutoa suluhu isipokuwa haki ya mhusika..Kuna vipengele vingi ambavyo mimi sina elimu navyo lakini anchofahamu utaratibu mzima haufuati dini za warithi bali Usia (Will) wa marehemu kutanguklia haki nyinginezo..

Mkuu
kwa maoni yako ama mawazo yako basi mimi naona hakuna umuhimu wa chombo hicho kwa TZ.

Mimi nafikiri BAKWATA wanatafuta pa kuvutia ngawila ama wazee wazima wanaweza pitishia huko DEEPGREEN na EPA jingine,kama wameweza kumtoa nishai KATAKSTA ndani ya chepo ,huko nako nafikiri wanatafuta ukwasi tu.
 
Mkandara nashukuru kwa kutufunua kidogo katika hili, lakini katika uelewa wangu mdogo, nilielezwa mahali kwamba kwa usia wakiislamu huwezi toa zaidi ya mafungu matatu 1/3 kwa mtu moja, hivyo tuseme Mimi Baba na watoto 6, kwa sheria ya kiislamu naweza kumwachia kwa usia huyo mtoto moja 1/3 si zaidi ya hapo na mali nyingine itagawanywa kufuatana na Sheria za Kiislamu ambapo kama na watoto wengine wakiume watapewa fungu lao, Mke nae atapewa fungu lake na kama nina wazee pia nao watapewa fungu lao, sasa tatizo la kisiku hizi, kuna wajomba amboa wamekaa mkao wa kula na kuna Mke ambaye labda ataolewa tena au hatoolewa lakini ana nafasi ya kuangalia mali aliyo acha Mume wake, hapo sheria inakuwaje katika kumlinda huyu Mama au watoto?
Na ninashukuru kwamba wazazi wako walikuwa na uelewa wa kuacha wasia, na ndio maana nasema kuna wazee wengi tu wa-hekima lakini wanabezwa wakati mwingine kutokana na kukosa elimu ya shule za kizungu lakini hapa si maanishi wazee wako please tusije tkatoka kwenye mada.
Halafu kuna issue kama Marehemu Balozi Hassan Diria nasikia alikuwa na watoto wa kike tu, kwenye hali kama hiyo inakuwaje? au ndio Ami anachukua kwa misingi kwamba Atakuwa ameolewa na Mtoto wa Mjomba ili mali isiende mbali?
Shuran kwa shule... taratibu tunaelimishana..
 
Mkandara,
Nakubaliana na wewe kwa mengi. Ila hili neno MTOTO HARAMU, limeletwa na watu wa dini gani? Kumbuka kuwa katika Ukristo kumeandikwa kwamba "huwezi kukiita haramu, kitu kilichoumbwa na Mungu......." Kwa hiyo kama kuna watu walisema juu ya hili basi si Wakristo....... Mie yangu macho nasubiri nione.

Ila jambo moja. Kwenye Mahakama za serikali, kama mtoto ni wako basi inabidi umgharanie. Mtu kama Omary Mahita (POLISI) kusema huyu mtoto si wangu ilikuwa upupu wa hali ya juu. Ilitakiwa apimwe DNA na kuanzia hapo huyo mtoto atambuliwe kuwa ni wake. Mtoto hama kama utakuwa ulirithi, basi sheria zichukue mkondo wake.

Aaaah! mkuu leo neno mtoto wa haramu linatoka kwingine!.. mbona nasikia Ismail mtoto wa kwanza wa Abraham (Nabii Ibrahim) mnawita mtoto wa haramu au?
 
Aaaah! mkuu leo neno mtoto wa haramu linatoka kwingine!.. mbona nasikia Ismail mtoto wa kwanza wa Abraham (Nabii Ibrahim) mnawita mtoto wa haramu au?

Hapana tunamwita mtoto wa kijakazi ,na tena ktk ukatoliki hatuna neno halamu,maana twaamini Mungu alisipendi aghalabu sekunde kadhaa kukifanya kuwepo sasa mwanadamu wawezaje kuita kitu halamu ,ambacho Mungu kasipendi mda wake??
 
Aaaah! mkuu leo neno mtoto wa haramu linatoka kwingine!.. mbona nasikia Ismail mtoto wa kwanza wa Abraham (Nabii Ibrahim) mnawita mtoto wa haramu au?
Ismail ni kizazi cha uislam hakuna muislamu anaweza kusema hayo?? ni mtume wa mungu! kama umesikia umesikia si kwa waislamu ila hao wenzako sijui wewe dini gani?
 
Wote mna-spin tu lkn bado sijasoma kutoka hata kwa mwana jamii mmoja akiwemo aliyeileta hii mada Masatu hasa hasa reliable source ya hii habari ya gvt kumeza maneno yake na kurudisha tena mahakama ya kadhi ameitoa/mmeitoa wapi?

kumbukeni tumewaomba sana chanzo ha habari hii ni kutoka wapi,lkn hadi sasa hamna aliyetuambia!We do need a concrete infos without reasonable doubt about this plz.
 
Wote mna-spin tu lkn bado sijasoma kutoka hata kwa mwana jamii mmoja akiwemo aliyeileta hii mada Masatu hasa hasa reliable source ya hii habari ya gvt kumeza maneno yake na kurudisha tena mahakama ya kadhi ameitoa/mmeitoa wapi?

kumbukeni tumewaomba sana chanzo ha habari hii ni kutoka wapi,lkn hadi sasa hamna aliyetuambia!We do need a concrete infos without reasonable doubt about this plz.
Itakuwepo hata kama siyo leo ...kwa hiyo ni vizuri JF kujadili "ikiwepo au isipokuwepo"
 
mimi ningomba tusifanya huu mjadala kama ugomvi kati ya watu wa dini tofauti, na namshukuru mkandra kwa kuwa na msimamo na mawazo mazuri ya kunga jamii pamoja na mahusiano yetu maana siku hizi kuoleana ni kama kazi muislamu/mkristo na mkristo/ muislamu nk.
 
Jamani wala msipoteze mda kuongea au kumuuliza masato sources, maana yawezekana wala hajua maana ya source........huo uamuzi wa jumapili usiku ni wa wapi....hoyo serekali ilikaa lini? Msiumize vichwa, katafuta namna ya kubadilisha alichokisema about biharamulo kuwa...."Chadema wakumbushwe kugomea kusign matokeo",,,je Ch....Cha....Mafisadi watagomea hilo?

I was excited to see CHADEMA win,,,,,and that HAS COME TRUE.....if other wishes were like this.....I am sure MASATU would ride on!"
 
Back
Top Bottom