Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

swalikwa the so called GREAT THINKERS

where are te so called arguments kwa nini its wrong ku incorporate sharia laws kwenye sheria za kawaida

swali zuri; sharia law zipi ambazo zinaweza kuwa incoporated katika sheria za kawaida? La pili nalo ni kuna tofauti gani ya sharia laws na sharia za "kawaida"? Kwanini hizi nyingine na hizi nyingine si za kawaida?
 
Kama wewe umeona gharama tu, basi kwa taarifa tu, waislamu, kuhusiana na mazungumzo yetu hapa, maana waislamu wa Tanzania, wakishikama tu na mafundisho ya Qur-ani na Sunna za Mtume Muhammad (S.A.W) wanaweza kuendesha sio hizi mahakama tu za kadhi, bali nchi yetu nzima, tena kwa uadilifu, haki, usawa na heshima. Lijue hilo na usiwe brain-wash na hawa wanaotandaza hofu na utawala wao wa vyombo vya uongo.

Wewe unajibana mwenyewe hapa. Kuwa waislamu waendeshe wenyewe hizi mahakama bila ya serikali kuidhinisha sio kujitenga na kuigawa nchi huko?? yaani waislamu na wasiokuwa waislamu. Na hili pia waislamu wanaliweza, unayo habari hiyo? Lakini je una maana kwako wewe ndio busara hiyo?

Ni wasiokuwa waislamu ambao hapa wanaonyesha kiburi na kutojali. Watanzania msiwe kama watu na serikali zisizo huru za magharibi. Au nanyi mmetiwa mikononi na Uzayuni. Wakistro wa Tanzania, mmelala??? wakati hata hao wenzenu wa magharibi wanaamka. Hebu angalia unavyoishi na huyo jirani yako hapo Manzese au Temeke, na hali ya kuwa dini zenu mbali mbali, sio ubinadamu huo?

Ulimwengu unabadilika, na Mahakama ya kadhi, kama independent body kudili na masuala ambayo purely ni ya kidini ni muhimu hata kwa hao waislamu ambao kutokana na ufinyu wao wa ilmu ya dini, au uhadaa wa dunia hawalioni hili. Waislamu hawaombi hili kwa wasiokuwa wasiokuwa waislamu bali ni haki yetu. Au ndio mmeshatiwa pomu mnapenda kuona waislamu loose control, sio busara ni upumbavu huo.

Nato hoja
 
Kama John hawezi kuamua kesi ya Ramadhan inakuwaje John huyo huyo aweze kutoa hela yake kumlipa Ramadhan?
 
swali zuri; sharia law zipi ambazo zinaweza kuwa incoporated katika sheria za kawaida? La pili nalo ni kuna tofauti gani ya sharia laws na sharia za "kawaida"? Kwanini hizi nyingine na hizi nyingine si za kawaida?

the answer to your question is embedded in the first paragraph of my post in which you quoted...weird that you havent quoted the whole post
 
A Muslim, devout or otherwise, is certainly free to submit a family dispute to a Muslim cleric. Who is preventing it? Start such courts if they do not exist.

You complain that Christians are able to take family disputes to their religious leaders. Instead of complaining and waiting for the government to start a court for you, go ahead and do it yourselves.

Wow...how me where i complained...come on now you can do better that this

The pragmatic one is as follows: Tanzania is home to at least 15m Muslims. Many of them choose to run their lives, like followers of other faiths, in accordance with religious law. They want to marry, divorce, lend, borrow and generally conduct their affairs in accordance with sharia. But there is no mechanism in British society for recognising in public law the decisions they have made in private.

Such mechanisms do exist for other religions. So fairness dictates that it should be technically easier for Muslims to get state recognition for their faith-based judicial rulings, as long as the choices sanctioned by sharia do not contravene the law of the land.


what's wrong with that?
 
Hivyo Sisi Watanzania Tunakwenda wapi ndugu zangu

Watanzania wameshachoka na Amani tunakoelekea sio kuzuri!Kukizuka fujo na uvurugaji wa amani siye tulioyopo nyumbani ndiye tutakaye pata shida wale waliomo nje ya nchi wapo salama!
 
Hivyo Sisi Watanzania Tunakwenda wapi ndugu zangu


what a quote from a "GREAT THINKER" resident but then again its strange reading intolerant contributions to the debate and I am flabbergasted that I am reading them in the so called "HOME OF GREAT THINKERS" aka JAMII FORUMS rather than, say, DARHOTWIRE FORUMS...
 
Watanzania wameshachoka na Amani tunakoelekea sio kuzuri!Kukizuka fujo na uvurugaji wa amani siye tulioyopo nyumbani ndiye tutakaye pata shida wale waliomo nje ya nchi wapo salama!

mhhh are you another "GREAT THINKER"?
 
Nafiiri Wadau wengi hapa hawajajua kinachoendelea.Sidhani kama waislam wanahitaji hiyo mahakama iwe inagharamiwa na Serikali,Wanachokitaka ni IDHINI kwamba ianzishwe au isianzishwe.Maana kama maswala ya mishahara mimi sioni kama hilo ni jambo kubwa litakalowashinda waislam.Kama kuna za wakatoliki,na hawalipwi na serikali basi kuna uwezekano wa kuwepo za kislam na zisilipwe na serikali.Jambo linalohitajika hapa ni je iundwe au isiunde?Huo ndiyo mjadala.Serikali ikubali kuanzishwa lakini ikatae kugharamia tuone kama waislam wataweza kuianzisha au la.
 
nafikiri ugumu upo kwenye
1. ku execute hizo kesi zao, kwa kawaida mtu akihukumiwa, geshi la polishi/magereza wanakuwepo ili kumpeleka gerezani au kukata kiganja (somalia)nk sasa kwao itakuwaje? je mtu akiona upepo unaelekea kubaya akaenda kubatizwa kwa kakobe pale watafanyeje? ile hukumu itakuwa na uzito tena? nk
2. ndoa nyingi ni za mseto waislamu wameoa na kuolewa na wakristo hawa watahusika vipi na hizo mahakama?
3. Je mahakama za juu za nchi zinauwezo wa kubatilisha hukumu ya mahakama ya kadhi? mf. inavunja sheria za nchi au inavunja haki za binadamu? (wengi wanasema mahakama ya kadhi huwa inawanyima haki wanawake na watoto) then what will be next? maandamano?
nk nk

1:Kaulize South Africa wanavyo-execute.
2:Kaulize South Africa
3:Kabla ya kuundwa lazima serikali itapitia sheria zote zitakazokuwa zinafuatwa ili kujua km zitaenda kinyume na sheria za nchi au la au zitakuwa zinaenda kinyume na haki za binaadam.Kama itakuwa ni kinyume na matakwa ya serikali sidhani km itaundwa.Fuatilia za South Africa.
 
Nafiiri Wadau wengi hapa hawajajua kinachoendelea.Sidhani kama waislam wanahitaji hiyo mahakama iwe inagharamiwa na Serikali,Wanachokitaka ni IDHINI kwamba ianzishwe au isianzishwe.Maana kama maswala ya mishahara mimi sioni kama hilo ni jambo kubwa litakalowashinda waislam.Kama kuna za wakatoliki,na hawalipwi na serikali basi kuna uwezekano wa kuwepo za kislam na zisilipwe na serikali.Jambo linalohitajika hapa ni je iundwe au isiunde?Huo ndiyo mjadala.Serikali ikubali kuanzishwa lakini ikatae kugharamia tuone kama waislam wataweza kuianzisha au la.
Kwani wakatoliki walipokuwa wanaanzisha mahakama zao waliomba kibali kutoka kwa serikali?? Hebu acheni hiyo bana. Waislamu wanasema mahakama zao ni sehemu ya ibada kwa Mungu. Ibada kwa Mungu inahitaji ruhusa kutoka kwa serikali? Si ni swala hiyo? Kwa nini katika kuswali kwao waombe ruhusa ya serikali? Mbona serikali ilishatoa uhuru kwa kuabudu miaka nenda-rudi. Waseme wanachokitafuta serikalini wote tukijue!
 
1:Kaulize South Africa wanavyo-execute.
2:Kaulize South Africa
3:Kabla ya kuundwa lazima serikali itapitia sheria zote zitakazokuwa zinafuatwa ili kujua km zitaenda kinyume na sheria za nchi au la au zitakuwa zinaenda kinyume na haki za binaadam.Kama itakuwa ni kinyume na matakwa ya serikali sidhani km itaundwa.Fuatilia za South Africa.

Nani afuatilie sasa? Si heri ukae kimya tu?
 
Kwani wakatoliki walipokuwa wanaanzisha mahakama zao waliomba kibali kutoka kwa serikali??

Hebu fafanua hapo..maana naona cheap shots zimezidi humu jamvini kila kukicha zinazidi tu.. Over 90 % ya wachangiaji wanasema chochote kinachowajia kama vile tupo kwenye kilabu cha dengerua..


Yaani unaweza ukasoma thread weeee wala usipate jambo la maana hata moja...aaarrghh
 
mhhh are you another "GREAT THINKER"?

Mhhh, Mzee NAONA umepata moto mno!! usijeliingiza sana moyoni hili baba, utapasuka!! Yako mengi mno hayako kama tunavyotaka na hata tukiishi miaka elfu hatuta yamaliza!!
Pole sana,.....
 
Hebu fafanua hapo..maana naona cheap shots zimezidi humu jamvini kila kukicha zinazidi tu.. Over 90 % ya wachangiaji wanasema chochote kinachowajia kama vile tupo kwenye kilabu cha dengerua..
Yaani unaweza ukasoma thread weeee wala usipate jambo la maana hata moja...aaarrghh
Wakatoliki wana mahakama zao zinazoshughulika mambo mbalimbali yakiwemo mambo ya ndoa katika majimbo yao. Uko hapo?
 
Kama wewe umeona gharama tu, basi kwa taarifa tu, waislamu, kuhusiana na mazungumzo yetu hapa, maana waislamu wa Tanzania, wakishikama tu na mafundisho ya Qur-ani na Sunna za Mtume Muhammad (S.A.W) wanaweza kuendesha sio hizi mahakama tu za kadhi, bali nchi yetu nzima, tena kwa uadilifu, haki, usawa na heshima. Lijue hilo na usiwe brain-wash na hawa wanaotandaza hofu na utawala wao wa vyombo vya uongo.

Wewe unajibana mwenyewe hapa. Kuwa waislamu waendeshe wenyewe hizi mahakama bila ya serikali kuidhinisha sio kujitenga na kuigawa nchi huko?? yaani waislamu na wasiokuwa waislamu. Na hili pia waislamu wanaliweza, unayo habari hiyo? Lakini je una maana kwako wewe ndio busara hiyo?

Ni wasiokuwa waislamu ambao hapa wanaonyesha kiburi na kutojali. Watanzania msiwe kama watu na serikali zisizo huru za magharibi. Au nanyi mmetiwa mikononi na Uzayuni. Wakistro wa Tanzania, mmelala??? wakati hata hao wenzenu wa magharibi wanaamka. Hebu angalia unavyoishi na huyo jirani yako hapo Manzese au Temeke, na hali ya kuwa dini zenu mbali mbali, sio ubinadamu huo?

Ulimwengu unabadilika, na Mahakama ya kadhi, kama independent body kudili na masuala ambayo purely ni ya kidini ni muhimu hata kwa hao waislamu ambao kutokana na ufinyu wao wa ilmu ya dini, au uhadaa wa dunia hawalioni hili. Waislamu hawaombi hili kwa wasiokuwa wasiokuwa waislamu bali ni haki yetu. Au ndio mmeshatiwa pomu mnapenda kuona waislamu loose control, sio busara ni upumbavu huo.

Nato hoja

Hapo hukufikiria sana sijui kwanini??
Ziko nchi nyingi tu za hiyo dini moja na zina hali mbaya sana kiusalama,

Tabia yenu mnapenda vya kuiga! Ungesema turudi kwenye imani zetu za jadi ningeona sawa, imani ambazo japo tulikuwa tunatembea bila mavazi likini tulikuwa hatubakani!!
 
Maisha bila Kadhi atakayebebwa mgongoni mwa Serikali yanawezekana!
 
Sasa sheria za waislamu ziingizwe kwenye katiba ya nchi ina maana hata wasio waislamu wata hukumiwa na sheria hizo hizo? Na Tanzania si tunadai ni secular state sasa sheria za dini zitageuzwaje kuwa sheria za nchi? Na je wakianzisha mahakama ya kiislamu hiyo haitaonekana na upendeleo iwapo itagundulika adhabu za moja wapo ya mahakama(aidha ya nchi au ya kiislamu) ni nzito au nyepesi kuliko ya mahakama nyingine? Kuna ulazima wa waislamu kuwa na mahakama yao wenyewe na wata hakikisha vipi sheria zao hazitaingiliana na sheria za nchi? Tatizo watanzania tuna kimbilia kujiingiza kwenye mambo. Hapa kuna baadhi ya watu watakuja na kusema oh mbona nchi fulani wana mahakama ya serikali na ya kiislamu?! Tusi kimbilie kuingiza vitu ambavyo haviendani na hali yetu kwa ajili ya kuridhisha tu baadhi ya makundi ambao wao kila siku wanaona tu kuwa wanaonewa au wenzao wana pendelewa.



Nakuunga mkono 100% . Ni kwanini waislamu wasifanye mambo yao bila kuhusisha serikali,kwani wao ni special sana au vipi? Serikali imefanya vizuri mahakama ziendelee kutumia sheria za kiislamu. Tanzania ipo mtegoni kwani kuna mataifa ya kiislamu yanachochea hiyo mahakama huku kwao
mkristu hatambuliki, Mimi nafikiri waislamu wanaweza kuweka wao wenyewe mfumo wa kutatua migogoro yao ambao utaheshimika kwa waislamu wote ila ukiangalia walivyo utakuta kuna ambao hawamtambui mufti au Bakwata, sasa unapata maswali mengi je hata kama mahakama hiyo itaundwa hakuna ambao wataipinga? Tunachoomba sisi ni salama tu isije ikaanza hoo hatujatendewa haki basi tuidai kwa mabomu.
 
Kumekuwa na upotoshwaji mkubwa sana wa dhana nzima ya mahakama ya kadhi. Watu wengi wamepotoshwa kuwa mahakama ya kadhi itakuwa ikihukumu criminal cases. Ukweli wa mambo ni kuwa itakuwa inajihusisha na civil cases pekee na katika civil cases hizo ni katika masuala ya ndoa (talaka) na mirathi pekee. Hivyo hakuna kumkata mtu mkono.

Zanzibar ni sehemu ya muungano wa Tanzania kuna mahakama ya kadhi, je katiba imevunjwa? Tanganyika ilikuwa na mahakama za kadhi na baadaye nyerere alizivunja, je nyerere alivunja katiba? Kenya na Uganda wana mahakama hizo, je kuna mtu kakatwa mkono?
 
Back
Top Bottom