Heshima kwenu wajamvi.
Mheshimiwa G Lema anatarajiwa kutoka rumande leo tarehe 14/11/2011.
Mheshimiwa G Lema ni mbunge wa Arusha mjini alitarajiwa na wapiga kura wake wenye akili nzuri atimize wajibu wake wa kuhudhuria vikao vya bunge hasa kipindi hiki ambacho mchakato wa katiba mpya unajadiliwa mjengoni.
Sijui kama Mheshimiwa Lema alipokataa dhamana hakujua kikao cha bunge kingeanza wakati akiwa maabusu ?.Kama alijua hakika atakuwa amefanya kosa kubwa sana,atakuwa amewaangusha wapiga kura wake,atakuwa amewaangusha wapiganaji wenzake,atakuwa amewaangusha waTanzania wengi ambao walifurahia namba ya wabunge wa upinzani kuongezeka mara dufu mjengoni.
Binafsi nawalaumu sana wasaidizi/washauri wa mbunge,Viongozi wa CDM ngazi ya wilaya na mkoa ambao badala ya kumshauri mbunge wamemwacha pekee yake afanye atakavyo.Kitendo cha viongozi wa Taifa mwenyekiti,Katibu mkuu,Mwansheria wa CDM na viongozi wengine wengi kutaka kumtoa rumande Mbunge wa Arusha bila mafanikio.
Kitendo cha viongozi wa wa CDM ngazi ya taifa kushughulikia sakata la madiwani Arusha ilihali vingozi wa wilaya na mkoa wapo.Kitendo cha viongozi wa CDM taifa kulivalia njuga sakata la uchaguzi wa Meya Arusha utafikiri hawana shughuli nyingine za kufanya si tu kimezidi kushusha hadhi ya CDM na viongozi wake bali kimeacha maswali mengi miongoni mwa wananchi.
Viongozi wa CDM kwa maoni yangu wana wajibu mkubwa sana kwa taifa letu nilitegemea watajikita kwenye mambo ya maana kama katiba mpya,kukieneza chama vijijini [Rejea uchaguzi wa mwaka 2010 majimbo mangapi yalikosa wagombea ubunge na udiwani],kuhakikisha sera zake zinafahamika kuanzia mijini hadi vijijini.
Kupinga kwa nguvu zote kuingiza Tanzania katika siasa za udini,ukabila na ukanda hapa watatakiwa kuangalia upya sera yake ya majimbo.
kitendo cha viongozi wa CDM taifa kukesha uwanja wa NMC kwaajili ya kushinikiza mheshimiwa mbunge atolewe rumande huku wakijua wazi Mheshimiwa Lema alikataa mwenyewe dhamana kimenisononesha sana.Najiuliza mara mbili mbili kama viongozi wa CDM wanashindwa kuhandle suala dogo hivi je masuala makubwa na magumu wataweza ?.