J'tatu hiyooo, Lema njeeee....

J'tatu hiyooo, Lema njeeee....

mimi niko mbali niambieni basi kama katoka au bado, sijui chochote, thread niliyoiona inaelzea mambo ya polisi lakini haielezei kama katolewa
 
samahani, sijaangalia habari.. ila natamani kupata picha kamili ya kilichotokea Arusha leo ndipo niendelee kuchangia.... tafadhali

In short lema alipoachiwa kwa dhamana wafuasi wake wametoka mahakamani kwa maandamano mpaka ofisini kwa lema na maandamano hayakuwa na kibali pia hakuna aliyeumia kwa vile polis hawajaingilia inaonyesha vurugu zote zinasababishwa na polis
 
Mwema mwenyewe anayatamani hayo mapinduzi ila anahofia kutemwa kazi
 
Kila siku watu wanafanya mikesha ya sala tena kwa makelele sana maana wanatumia speakers. Mbona Mwema hajasema lolote kuhusu hilo? Au wakati Kakobe na wafuasi wake walipoamua kukaa nje ya kanisa lao kwa zaidi ya mwezi wakipinga uwekaji wa nguzi za kupitasha umeme karibu na kanisa, Mwema alikuwa wapi?
 
Mwema ni neno tu kama neno ujinga aua upumbavu,lakini haiakisi na matendo,uelewa na dhamira ya kutambua ya kuwa anaowapiga ni watu kama yeye alivyo,ila naseama Mungu haja lala acha aendelee na uonevu wake,iko siku ataisoma kondoo kwa kirundi kwamba inaitwa kontro ng'aasi,na dalili imejionyesha juzi kule Mbeya maana mbwa wake walielemewa na ikabidi kuita masodaa.hivyo iko siku ataisoma tu wacha waendelee na dhuluma na uonevu wao.
 
Wanajamvi: Hivi inakuwaje pale Polisi wasipoingilia maandamano/mikutano ya CDM huwa hakuna uvunjifu wa amani na hakuna anayepoteza maisha au kuumia?

Mara mbili hilo limetokea hapo Arusha – kwanza ni mapema mwaka huu siku ile ya kuiaga miili ya marehemu wanaChadema waliokufa kutokana na risasi za polisi. Hafla yote ile kubwa haikuingiliwa na polisi hata mmoja na hakuna hata mtu aliyechubuka.

Pili ni tukio la leo pale Mh Lema aliposhindikizwa kwa maandamano makubwa kutoka mahakamani baada ya kupewa dhamana. Polisi hawakuingilia na hakuna aliyechubuka. Halafu hapa hapa kuna swali, je maandamano yale ya kumshindikiza Mh Lema leo yalikuwa na ‘kibali’ cha polisi? Nauliza tu.

Kwa hivyo conclusion ni kwamba polisi ndiyo huanzisha vurugu – kuzuia mikutano/maandamano bila ya sababu ya msingi, kwani sababu hiyo wanayoiimba kila siku ya eti kuzuia uvunjifu wa amani huwa ni uwongo mtupu. Wakubali kwamba wanatumika tu kisiasa – kuwapaka matope wapinzani kuwa daima ni watu wa vurugu, kitu ambacho siyo kweli kabisa.


Kitu kingine: Leo hii IGP Mwema kazungumza lakini alionekana kubadilisha hoja ya kwa nini hasa polisi huzuia maandamano/mikutano kwa sababu eti hii huwanyima watu kufanya kazi zao za kila siku za kujitafutia riziki.

Hii inawezekana ni kweli kwa asilimia flani, lakini siyo suala la polisi kamwe. Mimi nikiamua kwenda kwenye maandamano haiwi shauri la polisi kutaka kujua kwa nini nilitelekeza kazi yangu inayonipatia riziki. Mie najua mwenyewe ninachokifanya.

Inawezekana kuna wengine ambao hawataki maandamano lakini yakitokea inabidi wasimamishe biashara zao kwanza. Hii sababu pia haina mashiko sana kwa sababu kama ni hivyo, basi maandamano yote yapigwe marufuku kwa sababu inawanyima haki wengine kufanya kazi zao.

Ningependa kujadili suala hili.
"Natoa hamasa kwa wanaarusha na watanzania kwa ujumla kuwa popote mtakapomuona polisi yeyote kadondoka barabarani, naomba mumsaidie kumuinua na mumpatie maji anywe kwani hawa askari wote wanapata msoto kama raia wengine wanavyonyanyaswa na serikali legelege" By Mh. God Bless Lema.
 
Kama unandugu arachuga mwambie akupe story,hakuna bendera ya magamba nji waliyopita pipo pawa,mji ulisimama kwa muda mpaka mheshimiwa raisi lema alipo fika kwenye ofisi ya chama.polisisiemu waliku wapo tu wakishuhudia bendera za magamba zikishushwa chini na nguzo zikivunjwa.pale ngarenaro kuna kona ya nairobi kuna sehemu inaitwa kibanda umiza ilifanywa hakuna,watu walikula kichapo kimtindo na bendera zote kupigwa chini.kwa ujumla waswahili hakuna rangi waliacha ona.
 
baada ya fundisho la arusha, mbeya naona polisi na wana siasa wameisha jifunza,nchi hii ilikuwa iingie kwenye matatizo haya toka awamu ya alhaji, waka mtumia mrema kupoza hasira za watu, sasa huyu jk wa sasa anataka kuturudisha kwenye hayo matatizo lakini naona sasa somo limeisha fika mahali pake
 
Ukisoma maelezohayo hapo chini (chanzo: gazeti mwananchi) hii inathibitisha polisi ndio chanzo cha vurugu. Kwa mapokezi ya Mh. Lema yaliyogeuka kuwa maandamano ya amani na kuishia kwa mkutano wa amani inaonyesha sababu ambazo huzitoa kuzuia maandamano mbalimbali eti kulingana na taarifa za kiintelejensia kutakuwa na uvunjifu wa amani ni uzushi mtupu. Mapokezi ya jana ya Lema yaliyogeuka kuwa maandamano na polisi hawakuwakamata pia hiki ni kioja na kwa maana hiyo na kesi wanayomshitaki mahakamani ni kioja haina maana yoyote.

Habari ifuatayo ni kama ilivyoandikwa na Mwananchi:

SHUGHULI mbalimbali za kibiashara na kijamii katika Jiji la Arusha jana zilisimama kwa muda kupisha mapokezi ya Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema baada ya kutoka rumande katika Gereza la Kisongo alilokaa kwa siku 14.Oktoba 31, mwaka huu, Lema na wenzake 18 walifikishwa mahakamani wakidaiwa kufanya kusanyiko lisilo halali na kukaidi amri ya polisi iliyowataka watawanyike yeye na wenzake. Walikamatwa na kufikishwa mahakamani na kudhaminiwa lakini Lema akikataa dhamana akisema ameamua kutangulia gerezani kudhihirisha kwamba haogopi gereza.Lema alitoka kwa dhamana na kuandaliwa mapokezi makubwa ya wafuasi wa Chadema ambayo yaligeuka kuwa maandamano ya amani.Shamrashamra za mapokezi hayo zilisababisha kusimama kwa muda kwa shughuli kadhaa kama huduma za kibenki hasa zile zilizo katika Barabara ya Sokoine.

Wakati wa maandamano hayo wafuasi hao wa Chadema walikuwa wakipeperusha majani na matawi ya miti.
Mahakimu, mawakili na makarani wa mahakama nao walilazimika kuacha shughuli zao kwa muda na kutoka nje kushuhudia mapokezi ya mbunge huyo yaliyokuwa yakipambwa kwa nyimbo mbalimbali nje ya mahakama hiyo.

Sehemu ya nyimbo hizo zilimgusa Mkuu wa Polisi Wilaya hiyo ya Arusha, Zuberi Mwombeji ambaye hivi karibuni aliingia kwenye mvutano mkubwa na chama hicho cha upinzani akituhumiwa kutumia nguvu kuwadhibiti viongozi wake.Waliimba: “Tunamtaka….panya wetu… tunamtaka mbunge wetu… Zuberi (OCD), aondoke. Mlituvizia usiku, leo sasa ni mchana hapatatosha. Hatuandamani, tunampokea shujaa wetu.”

Shamrashamra hizo pia ziliambatana na mabango mbalimbali huku pia kukiwa na fulana maalumu zilizokuwa zimevaliwa na baadhi ya mashabiki zikiwa na maneno yaliyosomeka: “Lema kaonyesha njia mbadala ya kudai haki. Jela ni mahali pa kuishi kama sababu ya kwenda huko ni vita
dhidi uonevu, ukandamizaji wa haki na utu wa binadamu.”

Mahakamani
Lema aliyefika mahakamani Saa 3:20 asubuhi akiwa ndani ya gari maalumu ya polisi, alipewa dhamana na Hakimu Mkazi, Judith Kamara baada ya kukamilisha masharti ya kuwa na wadhamini wawili wenye vitambulisho na barua za utambulisho ambao walisaini hati ya dhamana ya Sh5 milioni kila mmoja.

Alidhaminiwa na Sarah Mohamed na Mwajuma Manonge na kutoka eneo la Mahakama Saa 5:15 asubuhi akiwa amebebwa juujuu na wafuasi wake baada ya juhudi zake za kutaka kuondoka kwa kutumia gari lake kushindikana.Wafuasi hao walimzuia kuingia katika gari lake na kumtaka atembee kwa miguu hadi eneo la Ngarenaro ziliko Ofisi za Chadema Mkoa wa Arusha.
Mbunge huyo hakuwa na budi kukubaliana na agizo hilo la wafuasi wake kuongozana hadi Ngarenaro lakini aliwasihi wamruhusu apande na kusimama juu ya gari lake, ombi lililokubaliwa.

Licha ya mashabiki hao wa Chadema kulazimisha kumbeba Lema juujuu na kuanza kutoka naye eneo la Mahakama huku wakiimba, Kamanda wa Operesheni Maalumu za Polisi Mkoa wa Arusha, Peter Mvulla aliwaamuru askari wake waliokuwa wakilinda amani eneo hilo kutowaingilia.

“Waacheni waandamane na mbunge wao, msiwapige mabomu. Subirini tuangalie kitu gani kitatokea. Kama hawafanyi vurugu msiwaingilie hadi nitakapotoa amri nyingine. Muhimu hakikisheni mmejipanga sawasawa kila eneo,” alisikika Mvulla akitoa maelekezo kwa simu.
Busara za Mvulla aliyekuwa mkuu wa kikosi cha ulinzi katika shughuli ya jana, zilisaidia kuepusha vurugu katika mapokezi hayo yaliyoishia kwa Lema kuwahutubia wafuasi wake nje ya ofisi za chama hicho mkoa huku amani na utulivu vikitawala.
 
Hongera kamanda Lema, mission complete, rudini bungeni tupachimbe swala la katiba kama hawataki ni non stop maandmano mpaka m.kwere an'goke. We are tired of him
 
Ni kosa kisheria kukataa dhamana na kama mahakama ikiamua inaweza kukuacha ndani kama adhabu kadri itakavyoona inafaa. wale wenzetu watatuambia ni mkono wa CCM

Wewe Kipepeo,

Ulisoma sheria wapi zinazosema kukataa dhamana ni kosa la kisheria? Acha kulaghai watu wewe. DHAMANA NI HAKI YA KILA MTU KAMA YUKO TAYARI KUDHAMANA NA WADHAMINI wawepo. Kuna watu chungu nzima wako mahabusu kwa kukosa dhamana,je unataka kutuambia kuwa kwa vile wamekosa dhamana basi wamefanya kosa la kisheria???Acha uzezeta mazee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom