J'tatu hiyooo, Lema njeeee....

J'tatu hiyooo, Lema njeeee....

Heshima kwenu wajamvi.

Mheshimiwa G Lema anatarajiwa kutoka rumande leo tarehe 14/11/2011.

Mheshimiwa G Lema ni mbunge wa Arusha mjini alitarajiwa na wapiga kura wake wenye akili nzuri atimize wajibu wake wa kuhudhuria vikao vya bunge hasa kipindi hiki ambacho mchakato wa katiba mpya unajadiliwa mjengoni.

Sijui kama Mheshimiwa Lema alipokataa dhamana hakujua kikao cha bunge kingeanza wakati akiwa maabusu ?.Kama alijua hakika atakuwa amefanya kosa kubwa sana,atakuwa amewaangusha wapiga kura wake,atakuwa amewaangusha wapiganaji wenzake,atakuwa amewaangusha waTanzania wengi ambao walifurahia namba ya wabunge wa upinzani kuongezeka mara dufu mjengoni.

Binafsi nawalaumu sana wasaidizi/washauri wa mbunge,Viongozi wa CDM ngazi ya wilaya na mkoa ambao badala ya kumshauri mbunge wamemwacha pekee yake afanye atakavyo.Kitendo cha viongozi wa Taifa mwenyekiti,Katibu mkuu,Mwansheria wa CDM na viongozi wengine wengi kutaka kumtoa rumande Mbunge wa Arusha bila mafanikio.

Kitendo cha viongozi wa wa CDM ngazi ya taifa kushughulikia sakata la madiwani Arusha ilihali vingozi wa wilaya na mkoa wapo.Kitendo cha viongozi wa CDM taifa kulivalia njuga sakata la uchaguzi wa Meya Arusha utafikiri hawana shughuli nyingine za kufanya si tu kimezidi kushusha hadhi ya CDM na viongozi wake bali kimeacha maswali mengi miongoni mwa wananchi.

Viongozi wa CDM kwa maoni yangu wana wajibu mkubwa sana kwa taifa letu nilitegemea watajikita kwenye mambo ya maana kama katiba mpya,kukieneza chama vijijini [Rejea uchaguzi wa mwaka 2010 majimbo mangapi yalikosa wagombea ubunge na udiwani],kuhakikisha sera zake zinafahamika kuanzia mijini hadi vijijini.

Kupinga kwa nguvu zote kuingiza Tanzania katika siasa za udini,ukabila na ukanda hapa watatakiwa kuangalia upya sera yake ya majimbo.

kitendo cha viongozi wa CDM taifa kukesha uwanja wa NMC kwaajili ya kushinikiza mheshimiwa mbunge atolewe rumande huku wakijua wazi Mheshimiwa Lema alikataa mwenyewe dhamana kimenisononesha sana.Najiuliza mara mbili mbili kama viongozi wa CDM wanashindwa kuhandle suala dogo hivi je masuala makubwa na magumu wataweza ?.
 
Wakuu wangu tuweke ushabiki pembeni wala hapana haja ya kuitana majina mabaya lakini ukweli utabakia ukweli na utatuweka huru viongozi wa CDM laiti wangejiuliza na kutafakari hali ya siasa Tanzania nina uhakika suaala la katiba lingekuwa ajenda yao ya kwanza.

Ningekuwa na sababu ya kukesha NMC ikiwa kukesha huko kungekuwa ni kudai katiba ya waTanzania si kudai kuachiwa mbunge aliyekataa dhamana.


Vipi TLP wanasemaje?



magamba at work!

Hii ni njia nyepesi ya kutokea hasa maswali yanapokuwa magumu ahaaa aaa
 
Unajua kwanini alikataa mdhamana?

unajua kwanini tarehe 7 hakimu alikaaa kusaini removal order?...

Tatizo lako Ngongo unakurupuka sana hasa kwenye maswala ya lema yaani huwa unajifanya tahira wakati una akili timamu....

Kukataa kudhaminiwa kwa Lema ni ujumbe tosha na ujumbe umefika..............
 
Tatizo lako Crashwise Lema ni Mungu wako hakosei wanaokosea ni wakosoaji wake ?.Lema akigoma kula na wewe utagoma,Lema akimpatia talaka Neema na wewe utampatia Mama Crashwise ?.Lema hakuwa na sababu za msingi kukataa dhamana.

Unajua kwanini alikataa mdhamana?
unajua kwanini tarehe 7 hakimu alikaaa kusaini removal order?...
Tatizo lako Ngongo unakurupuka sana hasa kwenye maswala ya lema yaani huwa unajifanya tahira wakati una akili timamu....
kukataa kudhaminiwa kwa Lema ni ujumbe tosha na ujumbe umefika..............
 
Jibu hoja acha ujinga wa kuabudi mtu na chama.Lema kachemka ile mbaya.

Kuna Hoja gani ya kujibu? jina lako tu linanitia kichefuchefu

Wakuu wangu tuweke ushabiki pembeni wala hapana haja ya kuitana majina mabaya lakini ukweli utabakia ukweli na utatuweka huru viongozi wa CDM laiti wangejiuliza na kutafakari hali ya siasa Tanzania nina uhakika suaala la katiba lingekuwa ajenda yao ya kwanza.Ningekuwa na sababu ya kukesha NMC ikiwa kukesha huko kungekuwa ni kudai katiba ya waTanzania si kudai kuachiwa mbunge aliyekataa dhamana.







Hii ni njia nyepesi ya kutokea hasa maswali yanapokuwa magumu ahaaa aaa

Kwa mambo unayoandika inawezakana J3 umeamka na hangover za kutosha maana hapa hutumii akili yako
 
Wakuu wangu tuweke ushabiki pembeni wala hapana haja ya kuitana majina mabaya lakini ukweli utabakia ukweli na utatuweka huru viongozi wa CDM laiti wangejiuliza na kutafakari hali ya siasa Tanzania nina uhakika suaala la katiba lingekuwa ajenda yao ya kwanza.Ningekuwa na sababu ya kukesha NMC ikiwa kukesha huko kungekuwa ni kudai katiba ya waTanzania si kudai kuachiwa mbunge aliyekataa dhamana.







Hii ni njia nyepesi ya kutokea hasa maswali yanapokuwa magumu ahaaa aaa
Ngongo kimsingi anacho kilalamikia Godbless Lema ni unyanyasaji unaofanywa na jeshi la polisi zidi ya wananchi pamoja na chama chake...lakini ukiangalia kwa umakini utagundua tatizo ni katiba....viongozi wa polisi mahakama hawako huru ndiyo maana umeona juzi Mkuu wa Mkoa ana mwamru hakimu asimpe dhamana Lema ili kumsafishia njia boss wake kama angekuja Arusha tarehe 12.11.11
 
Vile viroba mlivyopewa NMC bado havijaisha kichwani.

Kuna Hoja gani ya kujibu? jina lako tu linanitia kichefuchefu



Kwa mambo unayoandika inawezakana J3 umeamka na hangover za kutosha maana hapa hutumii akili yako
 
wakuu nimeona breaking news ya ITV kwamba kamanda lema ametoka kwa dhamana,ni kweli tupeni update huko......
 
Ngongo kasema ajenda ya kwanza ya CHADEMA ingekuwa KATIBA mpya kaingia mnywa viroba mmoja kings of king anabwabwaja masabauri at work.

Ngongo kimsingi anacho kilalamikia Godbless Lema ni unyanyasaji unaofanywa na jeshi la polisi zidi ya wananchi pamoja na chama chake...lakini ukiangalia kwa umakini utagundua tatizo ni katiba....viongozi wa polisi mahakama hawako huru ndiyo maana umeona juzi Mkuu wa Mkoa ana mwamru hakimu asimpe dhamana Lema ili kumsafishia njia boss wake kama angekuja Arusha tarehe 12.11.11
 
Wakuu wangu tuweke ushabiki pembeni wala hapana haja ya kuitana majina mabaya lakini ukweli utabakia ukweli na utatuweka huru viongozi wa CDM laiti wangejiuliza na kutafakari hali ya siasa Tanzania nina uhakika suaala la katiba lingekuwa ajenda yao ya kwanza.Ningekuwa na sababu ya kukesha NMC ikiwa kukesha huko kungekuwa ni kudai katiba ya waTanzania si kudai kuachiwa mbunge aliyekataa dhamana.







Hii ni njia nyepesi ya kutokea hasa maswali yanapokuwa magumu ahaaa aaa

Mr green guard unastress. Mbunge wa jimbo lako ni nani???
 
Tazama huyu nae anajiita mchambuzi !.Suala la mbunge wa jimbo limetoka wapi ?.Acheni upuuzi wa kuifanya JF kijiwe cha CHADEMA watu wako huru kujadili na kutoa mawazo bila kujali itikadi za vyama.

Mr green guard unastress. Mbunge wa jimbo lako ni nani???
 
Sasa alichokuwa anakitaka jela kaishakipata?

Matthew 10:28
.....And do not be afraid of those who kill the body but cannot kill the soul; but rather be afraid of Him who can destroy both soul and body in hell (Jehanam).
 
Hili andiko linaingilianaje na mtu aliyekataa dhamana !.

Matthew 10:28
.....And do not be afraid of those who kill the body but cannot kill the soul; but rather be afraid of Him who can destroy both soul and body in hell (Jehanam).
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom