Kama kuna kosa kubwa mabalo Nyerere alililea ni lile la dhana potofu ya kuwa Utajiri ni sumu (Ubeari ni Unyama)!
Watanzania tumeendeleea kuwa vipofu na wagumu kukubali kuwa hata misahafu yazungumzia kuhusu jamee na falme zilivyokuwa na Utajiri. Tulichoshupalia kutoka misahafu na hasa biblia ni lile la yesu kuonyesha kuwa maskini ana nafasi kubwa kwenda Mbinguni kuliko tajiri. Hivyo basi kwa mafunzo ya kidini na itiadi tulizokuwa nazo za kijamaa zinatufanya tuhofie kuwa na mali, kuhofia kuwa matajiri eti tutaungua jehanamu.
Masaki umezungumzia kuwa Mbowe kuwa na kuishi kitajiri huku wananchi wanakufa na malaria, sijui ulitaka Mbowe aishi kimasikini au agawanye utajiri wake kwa kila mtu kwa kutoa chloroquine au chandarua?
Mbowe kakopa pesa, kaweka gumba na sahihi katika mkataba alipokopa. je kukopa ni uhalifu? je kuwa na mali au kuishi kwa fahari ni kosa la jinai? kwa mujibu wa katiba na vipengele vya sheria gani?
Mnaodai kuwa Mbowe kafeli elimu, sawa kafeli, yeye ni wa kwanza? Mnaodai kuwa mbowe anaishi maisha ya Anasa, je yeye ni wa kwanza? Mnaomuita mbowe mwizi, kaiba wapi?
Kwa wale mnaotuhumiwa kuwa makuwadi wa mafisadi, msifananishe mtu kukopa na mtu kuiba au kujipatia pesa kwa njia a udanganyifu!
mafisadi wenu walitengeneza kampuni hewa na kujichotea fedha; Uhujumu na Wizi! Mbowe kakopa, Lowassa kazembea kampuni hewa ikaingingia nchini na kuhujumu je mambo haya yanafanana?
Ni mawazo ya kidumavu na ambayo yanaturudisha nyuma kwa watu kuona kuwa kila mfanyabiashara mwenye mali ambaye kapata halali na kwa jashi lake, basi twamuona mwovu au fidhuli.
Ikiwa kuna mmoja wenu ana ushahidi kuwa Mbowe alijipatia utajiri wake kwa kuiba au kuhujumu, leteni huo ushahidi.
Hili la NPF-NSSF kutoa mkopo tayari mshatamka kuwa ni mkopo. ikiwa Mbowe atashindwa kulipa, kitakachomsibu kikubwa ni kufilisiwa mali za kampuni na si mali binafsi.
Hao mafisadi wenu wameiba na kujipatia fedha kwa udanganyifu BOT kupitia EPA. Waliosafi na wakopaji wazembe kama Mbowe walikwenda BOT wakakopa zile pesa za CIS kutoka Japan.
People! get your facts together!