Je, Hatima (Destiny) Ni Kweli Ipo? Tujadili!

Je, Hatima (Destiny) Ni Kweli Ipo? Tujadili!

de Gunner

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2021
Posts
11,217
Reaction score
22,256
Tukijipumzisha kidogo na haya yanayo tokea nchini hebu tujadili hii issue kama kutafsiri kile kinacho endelea.

Katika kukuwa nilikuwa naskia huyu kijana, au huyu mtoto lazima aje aibadilishe hii familia, au huyu mtoto atakuja kuukomboa huu ukoo kutoka umaskini.

Au mzazi ana amua kuzaa watoto wengi ili kati yao mmoja aje kuwa msaada kwake. Utasikia anasema "mimi nimepambana sana, ila naamini kati ya watoto hawa huyu mmoja lazima aje kubadili hii familia na tutatoka katika umaskini.

Lakini pia katika biblia imeandikwa na ulisoma kuhusu Utabiri na kuzaliwa kwa Yesu, jinsi ambavyo nyota zili align na jinsi hakudhurika na kuuwawa mpaka alipofia msalabani.. Lakini pia jinsi Mungu alivyo mleta Musa kutoka katika uzao wa wamisri tena katika kipindi watoto waisraeli wa kiume waliuwawa.. Lakini Mussa aliyezaliwa na kutelkezwa mto Nile, akatokewa kupendwa na mtoto wa mfalme na kukuzwa na baadae kutoroka na kuja kuwa komboa wana wa Israeli.

Vivyo hivyo kwa wakina Isaka, Jacob na Daudi ni kama historia inatuambia kuwa kuna kitu kinaitwa destiny.. Watu ambao huja katika ulimwengu kwa ajili ya kufanya kitu fulani na kikatimia ndo wale wanaonekana kama wana destiny kwa sababu wao ndo wametimiza mazuri.

Lakini je, wale walikuwa kama pingamizi, watesi au maadui je? Na wale ambao walikuwa fuata upepo je? Binafsi naona wote hao walikuwa na destiny pia. Vile walivyo kuwa nayo pia ni destiny yao.

Je, katika historia ya maisha tukitoa dini, watu kama wakina Gandhi, kina Bob Marley, Martin Luther Jr, kina mother Theresa na wengine Je? Ukisoma historia vizuri uta gundua hakuna uongo kabisa.

Ni vile tu binadamu tunakuwa engrossed na maisha pasina kuangalia ni nini hasa kinaendelea. Ubaya na uzuri wote unaequa chanzes za destiny. Sema moja inaleta madhara nyingine inaleta manufaa.

Katika nature huwa kuna cyclical events kama El Nino, matetemeko, ghalika, au monsoon... Tunajua na yame tokea miaka na miaka. Ila je, kwa kawaida tunaweza kusema hizi ni destiny?

Je, kuna uwezekano pia ya kuwa sisi waafrika tuko destined kupitia umaskini na utumwa? Hasa kwa Karne hizi? Imagine unaambiwa ancient Egypt kule ndo ilikuwa matajiri wa ulimwengu. Walikuwa na majumba ya gold, zile pyramids zilikuwa na na wafalme ngozi nyeusi, na kulikuwa na watu wenye uelewa Mpana sana wa kifikra na kisayansi mpaka kuacha alama na lugha za kipekee ambazo zinazidi kupotezwa na kuficha na hao hao wazungu wanaocontro narrative ya ukweli kuhusu Africa.

Je, ndugu zangu nnaamini katika Destiny, ya kuwa vitu vipo jinsi vilivyo kwa sababu ni destiny na imejukuta iko hivyo tu. Kama msimu wa mvua na kiangnazi. Inaweza isiwe imeoangwa na mtu kama wengine watavyo fikiri ila ikawa ndo jinsi tu ulimwengu unavyo operate?

Nakaribisha mawazo yenu..

Nawatakia weekend njema pia.
 
Sijasoma maelezo yote, lakini hakuna mtu aliyepangiwa hatima.

Njia unazopitia, sehemu ulikozaliwa au kulia, familia uliyozaliwa, na mpambano ndivyo vitu vitakavyofanya uinuke au ubaki palepale.
Sawa sawa, na kwanini unazaliwa katika familia duni bila ridhaa yako? Au tuseme kwa nini hayo mazingira, watu, au malezi yawe tailored vyema kwa wengine vyema na kwa wengine vizuri.

Au nikuulize kwa nini tunasema wewe una bahati ya kuzaliwa sehemu fulani na mwingine awe na bahati mbaya?

Bila shaka point yako inamashiko pia
 
Sawa sawa, na kwanini unazaliwa katika familia duni bila ridhaa yako? Au tuseme kwa nini hayo mazingira, watu, au malezi yawe tailored vyema kwa wengine vyema na kwa wengine vizuri.

Au nikuulize kwa nini tunasema wewe una bahati ya kuzaliwa sehemu fulani na mwingine awe na bahati mbaya?

Bila shaka point yako inamashiko pia
Nadhani ni nature tu. Binadamu wawili (wa kiume na wa like) wakingonoka, bila kujalisha sehemu basi mimba hutungwa na mtoto akizaliwa.

Watu wote ni sawa tu tofauti tunaiona leo kwa sababu sehemu zingine zimeendelea kuli zingine ( mfano mijini na vijijini). Leo hii mtu anatamani angezaliwa sehemu fulani au katika familia fulani kwa sababu ya tofauti hizo, lakini hapo mwanzo kabla ya hizi tofauti kijitokeza huwezi kukuta mambo haya.
 
Nadhani ni nature tu. Binadamu wawili (wa kiume na wa like) wakingonoka, bila kujalisha sehemu basi mimba hutungwa na mtoto akizaliwa.

Watu wote ni sawa tu tofauti tunaiona leo kwa sababu sehemu zingine zimeendelea kuli zingine ( mfano mijini na vijijini). Leo hii mtu anatamani angezaliwa sehemu fulani au katika familia fulani kwa sababu ya tofauti hizo, lakini hapo mwanzo kabla ya hizi tofauti kijitokeza huwezi kukuta mambo haya.
Sawa mkuu
 
IMG-20260827-WA0092.jpg
 
unaambiwa ancient Egypt kule ndo ilikuwa matajiri wa ulimwengu. Walikuwa na majumba ya gold, zile pyramids zilikuwa na na wafalme ngozi nyeusi, na kulikuwa na watu wenye uelewa Mpana sana wa kifikra na kisayansi mpaka kuacha alama na lugha za kipekee ambazo zinazidi kupotezwa na kuficha na hao hao wazungu
Ufalme ukianguka unaanguka kweli unabakia historia tena mbaya au tajiri akifirisika watu wanabaki wanamshangaa. Wewe unashangaa dola ya Misri soma dola ya Ugiriki ndio utabakia kinywa wazi
 
Kama ni mzazi utaelewa, unaanza kuona hatma ya wanao tangia wakiwa watoto. Kama hujawahi kung'amua hilo anza kuwachunguza
Ndo maana tunapaswa kuwasiliza sana wazazi ni kama Mungu wetu wa pili... Japo pia yapaswa kuwa na discernment maana kuna muda wazazi wanaweza kugeuka kuwa mwiba nankimdumaza mtoto kufikia malengo...

Mimi naona kikubwa No kusikiliza wale wanaotutakia mema

Binafsi bado sijawahi mzazi, ila inshallah Mungu akijalia. Je wewe nini kina ku guide kutambua hatma ya wanao au mwanao? Ni nakuja automatic au unaangalia jinsi mtoto a navyo behave?
 
Ufalme ukianguka unaanguka kweli unabakia historia tena mbaya au tajiri akifirisika watu wanabaki wanamshangaa. Wewe unashangaa dola ya Misri soma dola ya Ugiriki ndio utabakia kinywa wazi
Hata siku soma kiundani zaidi, ila naambiwa ancient civilizations zilikuwepo na zikapita na nyingine kuibuka...
 

Hili jambo halina jibu la mkato, kwani mtazamo wake unategemea imani ya kidini, falsafa, na mtazamo wa mtu binafsi kuhusu maisha.

Upande mmoja wa kiroho na kidini unaamini kuwa hatima ipo na imepangwa kikamilifu na Mungu kabla hata mwanadamu hajazaliwa, huku kukiwa na dhana ya "wasaidizi wa hatima" wanaotumwa kuongoza njia ya mtu.

Kwa upande mwingine, wanafalsafa na wataalamu wa maendeleo binafsi wanasisitiza kuwa hatima haipo kama maandishi yaliyofungwa, bali ni matokeo ya ndoto, maamuzi, na nidhamu ya mtu mwenyewe, ambapo tabia mbaya zinaweza hata kuiharibu.

Hatimaye, mifumo ya unajimu na namba za kuzaliwa huona hatima kama mtiririko wa nishati na karma unaoamua changamoto za maisha.

Kwa ujumla, watu wengi hupata suluhu katikati kwa kuamini kuwa Mungu anatoa uwezo na fursa, lakini mwanadamu ana wajibu wa kuchagua na kufanya kazi kwa bidii ili kutengeneza mwisho mwema wa maisha yake.
 
Hili jambo halina jibu la mkato, kwani mtazamo wake unategemea imani ya kidini, falsafa, na mtazamo wa mtu binafsi kuhusu maisha.

Upande mmoja wa kiroho na kidini unaamini kuwa hatima ipo na imepangwa kikamilifu na Mungu kabla hata mwanadamu hajazaliwa, huku kukiwa na dhana ya "wasaidizi wa hatima" wanaotumwa kuongoza njia ya mtu.

Kwa upande mwingine, wanafalsafa na wataalamu wa maendeleo binafsi wanasisitiza kuwa hatima haipo kama maandishi yaliyofungwa, bali ni matokeo ya ndoto, maamuzi, na nidhamu ya mtu mwenyewe, ambapo tabia mbaya zinaweza hata kuiharibu.

Hatimaye, mifumo ya unajimu na namba za kuzaliwa huona hatima kama mtiririko wa nishati na karma unaoamua changamoto za maisha.

Kwa ujumla, watu wengi hupata suluhu katikati kwa kuamini kuwa Mungu anatoa uwezo na fursa, lakini mwanadamu ana wajibu wa kuchagua na kufanya kazi kwa bidii ili kutengeneza mwisho mwema wa maisha yake.
Hakika mkuu, Nashukuru kwa kuliweka hili jambo wazi.
Upande mmoja wa kiroho na kidini unaamini kuwa hatima ipo na imepangwa kikamilifu na Mungu kabla hata mwanadamu hajazaliwa, huku kukiwa na dhana ya "wasaidizi wa hatima" wanaotumwa kuongoza njia ya mtu.
Hakika, maana sio coincident unaona hili jambo likijirudia throughout scriptures and ancient texts.
Kwa upande mwingine, wanafalsafa na wataalamu wa maendeleo binafsi wanasisitiza kuwa hatima haipo kama maandishi yaliyofungwa, bali ni matokeo ya ndoto, maamuzi, na nidhamu ya mtu mwenyewe, ambapo tabia mbaya zinaweza hata kuiharibu.
Baada ya kufatilia kwa chache kuhusu astrology na numerology nilijikuta tu, naanza kuona link isiyo kwepeka kuhusiana na mambo haya... It is all aligning na maisha yangu, majina na tarehe za kuzaliwa.

Lakini pia kuna kitu kinaitwa synchronicity. Hiki pia imekuwa kama guidance kuniambia nina fanya kitu sahihi na nipo mahala ninapo paswa kuwa, repeating numbers, etc
Kwa ujumla, watu wengi hupata suluhu katikati kwa kuamini kuwa Mungu anatoa uwezo na fursa, lakini mwanadamu ana wajibu wa kuchagua na kufanya kazi kwa bidii ili kutengeneza mwisho mwema wa maisha yake.
Nakubalina nawe ya kuwa watu husubiri uwafikie mwisho wa safari ndo waanze kuona hiki kitu.
 
Mkuu Degu,@de Gunner,destiny ipo,hupangwa na Mungu,kila kiumbe ile siku anakuwa conceived,anakuwa ameishapangiwa destiny yake,ndio maana kwenye kila familia kunatokea mtoto mmoja anakuwa the choosen one,anaibeba hatma ya familia hiyo

Mara nyingi the chosen one huwa ni first born boy,lakini sometimes huwa ni mtoto mwingine yeyote hata mtoto wa kike.

Hata hiki kinachoendea nchini kwetu,kama the chosen one ndiye huyu anayekuwa persecuted,then Yeye huweza kulifanya lile jiwe lililokataliwa na waashi,kuwa jiwe kuu la pembeni!.

P
 
Mkuu Degu,@de Gunner,destiny ipo,hupangwa na Mungu,kila kiumbe ile siku anakuwa conceived,anakuwa ameishapangiwa destiny yake,ndio maana kwenye kila familia kunatokea mtoto mmoja anakuwa the choosen one,anaibeba hatma ya familia hiyo

Mara nyingi the chosen one huwa ni first born boy,lakini sometimes huwa ni mtoto mwingine yeyote hata mtoto wa kike.

Hata hiki kinachoendea nchini kwetu,kama the chosen one ndiye huyu anayekuwa persecuted,then Yeye huweza kulifanya lile jiwe lililokataliwa na waashi,kuwa jiwe kuu la pembeni!.

P
Mkuu umeongea ukweli mkubwa sana.

Na safari ya chosen one huwa ni ngumu sana. Naweza identify myself kwa hiyo identity na kile nimepitia naona kabisa I had no way I could do it on my own. Sometimes nilihisi kukata tamaa lakini kuna alignment ya matukio yanakuja kunifufua tena. So nlna pia kuna siku tulivyoenda kijijini kuna mshangazi mmoja ambaye ni mlevi sana, na hatujuani sana alisema, "Gunner wewe ndo umeubeba huu ukoo" maana nimechukua jina la babu yangu... Na ile kauli miaka ya hivi karibuni imekuwa ikijidhihirisha kupitia haya nayo yapitia
 
Back
Top Bottom